Madaktari fungueni mashataka haraka -Arusha UN au Uswis

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Nafikiri kunahitajika kwa Chama cha Madaktari kuripoti story nzima wakianzia kwenye vyombo vya Ubalozi ,bila ya kuchelewa wafungue mashtaka pale Arusha ,huyo alietorokea S/Africa inawezekana kutrace tarehe alizoondokea nchini na siku ya tukio.
Washtakiwa wengine waliopo mikoani waorodheshwe na huyo alietambulika hapo hospitali awe nambari one ,kama kuna ushahidi wa kutosha ,hakuna cha kungojea.
 
Hata mimi naona that is the best way wanaweza kufanya. Tahadhari asitekwe mwingine wakati wa kufuatilia hizo taarifa. Mfano-mtu atakwenda immigration kufuatilia akitoka kabla hajafikisha taarifa pengine tutaambiwa amekutwa hotelini amekufa---kwa hiyo ingawa ni jambo la busara umakini mkubwa sana wahitajika,na ni kazi ngumu kwelikweli
 
Jamani mbona hamkutushauri nasi wananchi tuwashitaki madaktari wakati nasi tunaendelea kuwapoteza wapendwa wetu au nyinyi hampotezi wa kwenu didnt you depend on their services? au nyinyi mnatibiwa india? vip kuhusu wakina mama wanaosubili kuleta watoto wao duniani au uchungu nao usubilie mgomo upite ni wangapi watakufa?
 
Jamani mbona hamkutushauri nasi wananchi tuwashitaki madaktari wakati nasi tunaendelea kuwapoteza wapendwa wetu au nyinyi hampotezi wa kwenu didnt you depend on their services? au nyinyi mnatibiwa india? vip kuhusu wakina mama wanaosubili kuleta watoto wao duniani au uchungu nao usubilie mgomo upite ni wangapi watakufa?
Aloo mbona unakuwa mpotevu ,hao madaktari sio wa kujitolea hapo kwenye mahospitali ,kwanza unatakiwa ulifahamu jambo hilo ,sawa ! Sasa kama kiliniki ina doctor mmoja na wasaidizi watatu ,wagonjwa wafikao hapo kwa siku ni zaidi ya mia ,kuwahudumia wagonjwa ,kuwapoza maana vifaa vya kuwapima hamna ,dawa hamna na hata kama zipo havitoshelezi ,jamaa anaingia asubuhi hadi usiku wa manane na saaingine anapelekewa mgonjwa nyumbani au anapigiwa simu ,akipima matatizo hayo na mshahara anaopewa inaonekana hautoshi kwani anaweza kufa yeye kabla hajamaliza kuwatibu wagonjwa.

Hao wameajiriwa hawakujitolea wana kila sababu ya kudai nyongeza toka kwa muajiri wao ya mshahara wachilia mbali vifaa au vitendea kazi.
 
Nchi hii ni ya kibepari mbona watu wana mawazo ya kuhurumiwa hurumiwa nani anamuhurumia mtu wa kwaida , mbona mmeficha mabilion ulaya
Madaktari wamegoma kutoa huduma yao cha kufanya ni kama serikali ina ubavu iwafukuze , sio kuwavizia kiharamia na kuwadhuru.Madaktari kukataa kutibu sio kwamba wamekwenda kudhuru watu mitaani. Wewe kama huna pesa kafie mbali acha kulahumu hawa watu.Huwezi kuwashikia bunduki kutibu, watu hawa wametumia muda mwingi na akili nyingi na zaidi wengine tumewasomesha kwa pesa yetu mpaka wakawa Madr, Wewe kama umempleka mwanao madrasa ndiye huyo sungusungu wako Msangi muua watu eti usalama wa taifa wauaji wakubwa. Usalama wa Magamba sio wa raia
 
Ndugu yangu Kitintunu mbona hawa akina mama wakilala chini huko wodini hujawaonea huruma?Au mgonjwa huyo akifa sababu tu CT-Scan mbovu?Tuhurumie hao akina mama tunao lala chini sakafuni badala ya kitanda wakati unasubiri kujifungua.System inayoshurutisha mama huyo alete na vifaa ambavyo haki yake kuvikuta hospitali.
Badala ya kulaumu madaktari tulaumu viongozi wetu,kwanini keki ya taifa tusigawane sawa?Wao waendelee kwenda Appola basi na siye watupatie huduma stahiki mahospitalini.
Wakijilipa vizuri wahakikishe vifaa vinapatikana kwenye hizo hospitali.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom