fullcup
JF-Expert Member
- Jun 21, 2016
- 806
- 2,182
Wanabodi poleni na mihangaiko ya kila siku na hongeleni kwa ushindi wa Bidden. Leo ningependa niwaletee kisa cha mapepo ninachokifananisha na madai ya wizi wa kura.
Mwaka 2002 kulikua na mdada ambae alikua na mapepo mtaani tuliyaita mashetani. Kila siku jioni baada ya chakula cha usiku badala ya taarifa za habari na mambo mengine sisi tulikua tunaenda kupata burudani huko.
Yaani walikua wanaandaa ubani yeye anafunikwa na kuvukizwa (kupigwa nyungu) ili kumpandisha mashetani. Mashetani yakipanda yakiume alikua makorofi sana lakini yakike tuliimba na kucheza pamoja nayo.
Kuna siku moja kiti sijui alifanya upuuzi gani na aliyefanya nae huo upuuzi alikuwepo kwenye mduara wakati tukisubiri yapande. Sasa yalipopanda alikua ni jini wa kiume na aliunguruma kwa sauti nzito na kudai kuwa amekuja kwa kazi moja tu kutoa adhabu kwa kiti na huyo jamaa.
Kwakua hatukujua kua limefanyika kosa gani na nani kafanya. Sasa kwakua wengi tulikua karibu na huyo kiti, tulikaa attention kwa lolote. Baada ya muda kidogo kuna jamaa aliyekua kwenye mduara alitandikwa bonge la fimbo. Sasa ile sauti ya fimbo tukajua majini yamekuja mengi kutoa adhabu, tukaanza kukimbia hovyo kila mmoja na njia yake.
Kesho yake stori ikawa ni nguvu ya majini katika kisa kilichopita. Stori zikawa nyingi kwamba majini huwa yanaitana na ndio maana Jana yake kila mtu alikua na jini linalomfukuza. Kila mtu alitoa ushuhuda kuwa alifukuzwa na jini. Swali likawa jini yupoje.
Katika kutoa ufafanuzi wa kila mmoja ikaja kufahamika kuwa hakuna cha jini aliyefukuza mtu wala nini. Maana kiti miguu haikufanya kazi na kifua kilibanwa baada tu ya jini kutoka. Hata tuliokuwa tunakimbia tulikua tunakimbiana wenyewe kwa wenyewe na aliyepiga fimbo ni binadamu sio jini.
Baada ya kubaini hayo tukajiridhisha kuwa jini tulimuumba wenyewe na vurugu zote zilijengwa na akili zetu tu na hakukuwa na uhalisia.
MADAI YA WIZI WA KURA
Mwaka huu kulikua na uchaguzi ambao umeisha kwa kila chama kupata matokeo yake. Uzuri ni kuwa chama cha Demokrasia na maendeleo kiliweka mawakala sehemu kubwa nchini. Mchakato mzima ulishuhudiwa na mawakala hao na fomu za matokeo wanazo.
Sasa baada ya kushindwa zimekuja stori za wizi wa kura. Lakini kama stori ya majini tu hakuna mwenye uhakika na jambo husika. Kila mtu ukimuuliza imetokea wapi? Anajibu sehemu nyingi tu nchini, majina hataji au hatà jina la mtaa tu.
Kuna walioenda mbali zaidi na kudai kuyashika masanduku ya kupigia kura lakini ukiwauliza yako wapi? Hawajui au wanakuambia wamechoma! Yaani ushahidi mkubwa kama huo unachoma ili iweje? Kwa jinsi jamaa wanavyopenda kuonekana wangeyapata kweli wangechoma?
Aliyepigwa fimbo anajua amepigwa na nani lakini wengine wanakimbia kimbia tu bila kujua wanakimbia nini. Yaani wanachojua kura zimeibwa, lakini ukiuliza *Zimeibwa wapi?, Kituo gani? Kura ngapi? Walioiba wako wapi? Hatà wao hawajui.
Aliyeibiwa alete ushahidi wa maandishi ili tumalize mgogoro. Chadema kwakua wana nakala za matokeo nchi nzima wajumlishe wao wenyewe au ikiwezekana watuletee vituo vilivyoibwa kura maana kila kituo ilikua ni watu chini ya 450. Mbona kwenye serikali za mitaa walionesha mpaka majina ya wenyeviti wa mitaa waliokatwa na makosa waliyofanya. Hapa wanakwama wapi?
Halafu yule aliyepigwa fimbo amejitoa kwenye zikiri eti ametishiwa maisha! Nani akutishie maisha wewe leo huna cheo chochote hatà cha ubalozi wa nyumba kumi?
Serikali toeni ajira za ualimu bhana nikafundishe shuleni mada ya How CHADEMA failed to organize protests in Tanzania.
Mwaka 2002 kulikua na mdada ambae alikua na mapepo mtaani tuliyaita mashetani. Kila siku jioni baada ya chakula cha usiku badala ya taarifa za habari na mambo mengine sisi tulikua tunaenda kupata burudani huko.
Yaani walikua wanaandaa ubani yeye anafunikwa na kuvukizwa (kupigwa nyungu) ili kumpandisha mashetani. Mashetani yakipanda yakiume alikua makorofi sana lakini yakike tuliimba na kucheza pamoja nayo.
Kuna siku moja kiti sijui alifanya upuuzi gani na aliyefanya nae huo upuuzi alikuwepo kwenye mduara wakati tukisubiri yapande. Sasa yalipopanda alikua ni jini wa kiume na aliunguruma kwa sauti nzito na kudai kuwa amekuja kwa kazi moja tu kutoa adhabu kwa kiti na huyo jamaa.
Kwakua hatukujua kua limefanyika kosa gani na nani kafanya. Sasa kwakua wengi tulikua karibu na huyo kiti, tulikaa attention kwa lolote. Baada ya muda kidogo kuna jamaa aliyekua kwenye mduara alitandikwa bonge la fimbo. Sasa ile sauti ya fimbo tukajua majini yamekuja mengi kutoa adhabu, tukaanza kukimbia hovyo kila mmoja na njia yake.
Kesho yake stori ikawa ni nguvu ya majini katika kisa kilichopita. Stori zikawa nyingi kwamba majini huwa yanaitana na ndio maana Jana yake kila mtu alikua na jini linalomfukuza. Kila mtu alitoa ushuhuda kuwa alifukuzwa na jini. Swali likawa jini yupoje.
Katika kutoa ufafanuzi wa kila mmoja ikaja kufahamika kuwa hakuna cha jini aliyefukuza mtu wala nini. Maana kiti miguu haikufanya kazi na kifua kilibanwa baada tu ya jini kutoka. Hata tuliokuwa tunakimbia tulikua tunakimbiana wenyewe kwa wenyewe na aliyepiga fimbo ni binadamu sio jini.
Baada ya kubaini hayo tukajiridhisha kuwa jini tulimuumba wenyewe na vurugu zote zilijengwa na akili zetu tu na hakukuwa na uhalisia.
MADAI YA WIZI WA KURA
Mwaka huu kulikua na uchaguzi ambao umeisha kwa kila chama kupata matokeo yake. Uzuri ni kuwa chama cha Demokrasia na maendeleo kiliweka mawakala sehemu kubwa nchini. Mchakato mzima ulishuhudiwa na mawakala hao na fomu za matokeo wanazo.
Sasa baada ya kushindwa zimekuja stori za wizi wa kura. Lakini kama stori ya majini tu hakuna mwenye uhakika na jambo husika. Kila mtu ukimuuliza imetokea wapi? Anajibu sehemu nyingi tu nchini, majina hataji au hatà jina la mtaa tu.
Kuna walioenda mbali zaidi na kudai kuyashika masanduku ya kupigia kura lakini ukiwauliza yako wapi? Hawajui au wanakuambia wamechoma! Yaani ushahidi mkubwa kama huo unachoma ili iweje? Kwa jinsi jamaa wanavyopenda kuonekana wangeyapata kweli wangechoma?
Aliyepigwa fimbo anajua amepigwa na nani lakini wengine wanakimbia kimbia tu bila kujua wanakimbia nini. Yaani wanachojua kura zimeibwa, lakini ukiuliza *Zimeibwa wapi?, Kituo gani? Kura ngapi? Walioiba wako wapi? Hatà wao hawajui.
Aliyeibiwa alete ushahidi wa maandishi ili tumalize mgogoro. Chadema kwakua wana nakala za matokeo nchi nzima wajumlishe wao wenyewe au ikiwezekana watuletee vituo vilivyoibwa kura maana kila kituo ilikua ni watu chini ya 450. Mbona kwenye serikali za mitaa walionesha mpaka majina ya wenyeviti wa mitaa waliokatwa na makosa waliyofanya. Hapa wanakwama wapi?
Halafu yule aliyepigwa fimbo amejitoa kwenye zikiri eti ametishiwa maisha! Nani akutishie maisha wewe leo huna cheo chochote hatà cha ubalozi wa nyumba kumi?
Serikali toeni ajira za ualimu bhana nikafundishe shuleni mada ya How CHADEMA failed to organize protests in Tanzania.