Unauliza vibao Polisi Mkuu?
Hapa nazungumzia ukandamizaji wa Tanganyika wa kuivamia Zanzibar.
Kama mnakandamizwa na Watanganyika, na mmekandamizwa kwa miaka 47 kama unavyodai, mnasubiri nini kutoka? Na mlikuwa wapi kufanya hivyo huko nyuma? Hudhani kuwa baada ya miaka 47 mmekwishazoea kukandamizwa? Kama ni kweli mmekandamizwa kwa miaka 47, unaaminije sasa kuwa mnaweza kukaa kwa usalama bila mkandamizo mliouzoea? Au mnataka kukandamizwa na mtu mwingine?
Katika kukandamizwa huko, Tanganyika imefaidika na nini?
Acha mawazo ya kitwana ya kulalama lalama. Zanzibar haijakandamizwa. Usitawaliwe na hisia zako ukataka kujumuisha na wengine kwenye mawazo yako ya kitwana. Wanzanzibar wamekuwa watu huru siku zote na tumefurahi nao sote pamoja na tumeshirikiana kwa hali na mali kama watu huru na tulioungana kwa hiari, tena kwa majadiliano na kalamu.