Madai ya waalimu

Ziltan

JF-Expert Member
Aug 20, 2011
2,649
6,832
Salama ndugu zangu,
mwenzenu naandika thread hii nikiwa na ghadhabu juu ya hii serikali yetu inayotunyanyasa waalimu, nina madai mengi ninayodai lakini nimeishia kusikia ahadi zao kwenye vyombo vya habari tu kwamba wanalipa lakini wapi,
ndugu zangu hii serikali imejaa ulaghai ulionivunja moyo wa kuwasaidia hawa watoto,
 
Mi naona kuwa kama serekali itashindwa kutekeleza madai ya walimu basi hamna haja ya kuingia madarasani mpaka pale madai yatakapotekelezwa! Zike porojo y kuwa ingieni tu madarasani madai yenu yanashughulikiwa tucyakubali, mimi naona akuambiae hivyo anakuona kama kindagateni, na anaogopa tu kukutusi moja kwa moja!
Ndimi mwl hapa Udsm.
 
Salama ndugu zangu,
mwenzenu naandika thread hii nikiwa na ghadhabu juu ya hii serikali yetu inayotunyanyasa waalimu, nina madai mengi ninayodai lakini nimeishia kusikia ahadi zao kwenye vyombo vya habari tu kwamba wanalipa lakini wapi,
ndugu zangu hii serikali imejaa ulaghai ulionivunja moyo wa kuwasaidia hawa watoto,

Mwalimu hebu acha kutudanganya hapa, una madai mengi yapi? je ni likizo, uhamisho, kujikimu au marekebisho ya mshahara? Hebu niambie mwaka 20004, 2007,2008,2009 serikali ililipa madeni ya walimu je wewe hukulipwa? Navyo jua mimi walimu wengi wamelipwa madai yao ya likizo, uhamisho na kujikimu. marekebisho ya mishahara yanalipwa na hayawezi kwisha kwani kila mwezi walimu wanapanda madaraja. je wewe unadai nini?

Nachukia sana viongozi wa CWT kukomalia migomo bila ya kushughulikia suala la msingi la mishahara midogo ya walimu
 
Muungwana ukiona mkubwa analia jua kuna jambo lamkuna, angekuwa mwongo huyu basi kelele za walimu tusingezisikia, sio walimu wote wenye madai wamelipwa, ana haki ya kusema "ana madai mengi" kwani wingi wa kitu huanza na mbili kwa hiyo hata kama anadai madai mawili tu bado ni mengi hayo, wasipotekelezewa ni kufanya kazi wakiwa na vinyongo na matokeo ya hizo kazi tunayaona.
 
Da wajinga ndiyo waliwao walimu mna tatizo gani kwemye madai yenu ya msingi wanawaletea siasa.Huyu mnayemuita Mwenyekiti wa chama cha walimu very techniquer kwa maslai ya yeye na serikali kwa hiyo kashawafanya walimu majuha.Anatangaza mgomo ili kuwapumbaza kuwa yupo pamoja na nyinyi wakati huo huo lazima mjue yupo na serikali bega kwa bega.Serikali inatangaza tunalipa walimu yeye anafuta mgomo kwa madai serikali imesema inalipa kwa hiyo hapo ni danganya toto ya nguvu.Walimu mpo wengi lakini umoja wenu si chochote si lolote mmezaliwa masikini,mnafanya kazi kimasikini,mnastaafu kimasikini na mtazikwa kimasikini Ok mtalipwa mbinguni kama mnadhani haki ipo huko because no one back after death.Na serikali ishadharau hii field wanaweza wafanya chochote msifanye lolote na sasa walhitimu wapo wengi wanaweza fukuza na kuajiri kwa hiyo wanahitajika viongozi wa kujitoa mhanga siyo hawa wa sasa wanawatumia walimu kama mtaji wao wa kimaslai.WALIMU HAMKENI HMUWAONI WAZEE WALIO KWENYE HII FIELD WALIVYOCHOKA KWA AJILI YA KUDHULUMIWA HAKI ZAO KILA WAKATI.
 
Back
Top Bottom