Madai ya Polisi kuwabambikia kesi watuhumiwa yamejithibitisha katika kesi ya Kabendera

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Nilistushwa na mabadiliko ya msimamo wa waendesha mashitaka, ambao ni Polisi katika kesi ya Kabendera hapo jana.

Nimewasikia waendesha mashitaka hao wakieleza kuwa upande wa mashitaka hauna nia ya kuendelea na kesi hiyo na hivyo wamekubali kuwa mazungumzo ya upande wa mashitaka na mtuhumiwa yafanyike ili mtuhumiwa aachiwe huru!

Nimejiuliza hivi hatua hii imefikiwa baada ya Rais Magufuli kutoa kauli kali siku chache zilizopita akiwatuhumu Polisi hao kuwa wanaowabambikia kesi za uhujumi uchumi na utakatishaji pesa ili watuhumiwa hao waendelee kusota magerezani kwa lengo la kuwakomoa watuhumiwa hao?

Rais aliendelea kufunguka kwa kusema kuwa walaaniwe waendesha mashitaka hao ambao wanawabambikia kesi watuhumiwa hao kwa lengo tu la kuwakomoa ili wakae magerezani kwa kipindi kirefu sana.

Nimejiuliza hivi hii kesi ya Kabendera si imefikishwa mahakamani hapo zaidi ya miezi 6 iliyopita, na wakati wote huo waendesha mashitaka hao wamekuwa wakiendelea "kukomaa" kuwa ushahidi hawajaukamilisha?

Sasa iweje hivi sasa, baada ya kumsotesha Kabendera zaidi ya miezi 6 jela, ndiyo hao waendesha mashitaka waone hakuna haja ya kuendelea na kesi hiyo?

Hao waendesha mashitaka, ambao ni Polisi si wamekuwa wakidai, katika kipindi chote hiko cha miezi 6 kila kesi inapoenda kutajwa mahakamani, wanaomba kesi iahirishwe kwa madai kuwa ushahidi haujakamilika?

Kama ni hayo majadiliano kati ya mtuhumiwa na upande wa mashitaka, si huyo Kabendera alishayafanya zaidi ya miezi 4 iliyopita na akaeleza kuwa yeye hana hatia kwa makosa hayo wanayomtuhumu nayo hapo mahakamani?

Kama alivyosema Mheshimiwa Rais na Mimi niunge mkono kuwa walaaniwe waendesha mashitaka wote ambao ni Polisi, kwa kuwabambikia kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji pesa kwa watuhumiwa na hivyo kuleta usumbufu mkubwa kwa mtuhumiwa kukaa gerezani kwa kipindi kirefu sana.

Ningependekeza kwa hao Polisi wenye tabia hiyo, ili na wao waweze kuona hayo matendo wanayoowafanyia Watanzania wenzao kuwa siyo mazuri, mahakama iweze "kuwageuzia kibao" na wao waweze kukaa magerezani kwa kipindi kirefu sana.

Kama hayo ni "maigizo" anayotufanyia Jiwe na yeye ndiye anayewaagiza hao Polisi wafanye unyama huo na yeye anawaruka hivi sasa, basi laana hiyo imgeukie yeye mwenyewe
 
Hata kama yeye Rais ndiye "anawaagiza" kutenda vitendo hivyo vya kinyama, hivi sasa keshawaruka futi elfu 10!

Inabidi na nyinyi Polisi mjiongeze na mfanye kazi yenu kwa weledi wa hali ya juu, mkizingatia pia usemi wa Rais mstaafu wa awamu ya 4 aliposema kuwa, ya kuambiwa, changanya na akili yako.........................
 
Ningependekeza kwa hao Polisi wenye tabia hiyo, ili na wao waweze kuona hayo matendo wanayoowafanyia Watanzania wenzao kuwa siyo mazuri, mahakama iweze "kuwageuzia kibao" na wao waweze kukaa magerezani kwa kipindi kirefu sana.
Mkuu Mystery, kwanza naunga mkono hoja kuhusu kulaaniwa wale wote wanaosababisha mateso kwa wenzao.

Mimi ni muumini wa kitu kinachoitwa karma, hivyo kwa mujibu wa karma, watakao laaniwa sio polisi wala waendesha mashitaka, bali aliyewatuma. Hao polisi huwa hawaamki tuu na kumbambikia mtu kesi, bali hutumwa!. Polisi na waendesha mashitaka wao wanatumwa tuu, hivyo wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa ajira zao za kutii mamlaka, ni sawa tuu na wale waliomshambulia Tundu Lissu, kama ni utekelezaji wa amri halali, kwa mujibu wa sheria ya karma, hawana kosa lolote, na hawatapata laana yoyote, bali aliyewatuma.

Kwenye hili la Kabendera, kwa vile na mimi nimetajwa kuwa eti ndiye niliyemchomea kupitia makala zangu humu, jf, kama kweli lengo la makala zile lilikuwa kumchongea mtu au kumchomea, kwenye karma ya Kabendera, nitakuwa na sehemu yangu, lakini kama niliziandika genuinely for informative porpoises only na sio kuchomea mtu, hata kama ni kweli makala hizo ndizo zilizochochea kumkuta yaliyomkuta, I'll be totally innocent and no karma reprisals will befalls me.



P
 
Hata kama yeye Rais ndiye "anawaagiza" kutenda vitendo hivyo vya kinyama, hivi sasa keshawaruka futi elfu 10!

Inabidi na nyinyi Polisi mjiongeze na mfanye kazi yenu kwa weledi wa hali ya juu, mkizingatia pia usemi wa Rais mstaafu wa awamu ya 4 aliposema kuwa, ya kuambiwa, changanya na akili yako.........................
Polisi wetu (baadhi si wote) akili zao wanazijua wenyewe wakishatumiwa wanabwagwa huku wakibeba laana zote na mikosi ya waliowatuma!!
 
Pascal Mayalla,
Binafsi huwa naamini kuna kitu Marehemu Mengi alikuwa anakifahamu kumuhusu Kabendera, baada ya mgogoro ule kati yake na wale wazungu, Kabendera alimruka muajiri wake na kuwatetea wazungu(Hermitage), nadhani alimuwasha.

Hizi ni hisia zangu sina ushahidi wala uhakika wowote. Maana lile saga nalo lilimchafua Marehemu Mengi kimataifa, nadhani naye aliamua kumlipua jamaa kiaina.
 
Not at all, a big NO! haya yote yanafanyika kwa maagizo ya Jiwe! Believe it or not!
Kuna shinikizo kubwa la kimataifa kuhusu haki za Kabebdera! and this is confirmed information!
Hilo shinikizo linataka nini au linasemaje?
 
Binafsi huwa naamini kuna kitu Marehemu Mengi alikuwa anakifahamu kumuhusu Kabendera, baada ya mgogoro ule kati yake na wale wazungu, Kabendera alimruka muajiri wake na kuwatetea wazungu(Hermitage), nadhani alimuwasha. Hizi ni hisia zangu sina ushahidi wala uhakika wowote. Maana lile saga nalo lilimchafua Marehemu Mengi kimataifa, nadhani naye aliamua kumlipua jamaa kiaina.
Not necessarily ni lile, na hata kama ni lile, Eric Kabendera alianza kupata matatizo baada ya kuutoa ushindi ule uliomgaragaza Mengi, ukitofautiana na Mengi, ni kweli yanakukuta ya kukuta and not necessarily the cause ni Mengi.

P
 
Not necessarily ni lile, na hata kama ni lile, Eric Kabendera alianza kupata matatizo baada ya kuutoa ushindi ule uliomgaragaza Mengi, ukitofautiana na Mengi, ni kweli yanakukuta ya kukuta and not necessarily the cause ni Mengi.
P
Hata kama siyo lile naamini kuna watu hawakufurahi jamaa kuwatetea wale wazungu, sijui kwanini lakini nafahamu hata kama Marehemu Mengi hakufanya kitu, some one somewhere in the system hakupenda au kufurahishwa na utetezi wa kabendera kwa wazungu, na kumtosa muajiri wake na aliye aminika ni mzalendo number one. Hili huwa na lihisi ingawa ni ngumu kulitolea maelezo, ila my gut has always thought, all this could be associated with that.

Huyu jamaa anaonekana siyo mzalendo kwa kumruka Mengi, na mbaya zaidi alikuwa muajiri wake.
 
Mystery, Wewe hujitambui bora ukae kimya. Tafakari yafuatayo:-

1. Kabendera alikamatwa kwa kosa gani?
2. Nani walimkamata?
3. Nani mlalamikaji? Yaani aliyetoa taarifa za kabendera kuanzisha kesi dhidi yake?

Then...
1. Unajua kuna tofauti ya ofisi ya ddp na dci?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
42 Reactions
Reply
Back
Top Bottom