nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Monday, 06 June 2011
NA NJUMAI NGOTA
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imetoa amri ya kuondolewa kwa kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Fred Mpendazoe.
Hatua hiyo ya Mahakama Kuu inatokana na sababu kwamba baadhi ya mambo katika hati ya madai ya Mpendazoe kuwa yamejificha.
Mpendazoe alifungua kesi ya msingi mahakama hapo, akipinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk. Makongoro Mahanga. Walalamikiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo.
Jaji wa Mahakama hiyo, Profesa Ibrahim Juma alitoa uamuzi huo jana baada ya kupitia hoja zilizowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mlalamikaji na walalamikiwa. Alisema ametoa amri ya kuondolewa kwa kesi hiyo mahakamani kwa sababu baadhi ya aya katika hati ya madai ya Mpendazoe ina mambo yaliyojificha ambayo yangeweza kuwasaidia upande wa walalamikiwa kuandaa utetezi wao.
Jaji alisema anaiondoa kesi hiyo na kutoa siku 14 kwa upande wa mlalamikaji kufanya marekebisho katika hati hiyo.
Wakili wa Serikali, David Kakwaya katika hoja zake aliiomba mahakama iifute kesi hiyo na kwamba katika hati ya madai ya Mpendazoe kulikuwa na dosari, kwani kuna baadhi ya mambo yaliyojificha ambayo yangeweza kuwasaidia katika utetezi wao.
NA NJUMAI NGOTA
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imetoa amri ya kuondolewa kwa kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea, Fred Mpendazoe.
Hatua hiyo ya Mahakama Kuu inatokana na sababu kwamba baadhi ya mambo katika hati ya madai ya Mpendazoe kuwa yamejificha.
Mpendazoe alifungua kesi ya msingi mahakama hapo, akipinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk. Makongoro Mahanga. Walalamikiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo.
Jaji wa Mahakama hiyo, Profesa Ibrahim Juma alitoa uamuzi huo jana baada ya kupitia hoja zilizowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mlalamikaji na walalamikiwa. Alisema ametoa amri ya kuondolewa kwa kesi hiyo mahakamani kwa sababu baadhi ya aya katika hati ya madai ya Mpendazoe ina mambo yaliyojificha ambayo yangeweza kuwasaidia upande wa walalamikiwa kuandaa utetezi wao.
Jaji alisema anaiondoa kesi hiyo na kutoa siku 14 kwa upande wa mlalamikaji kufanya marekebisho katika hati hiyo.
Wakili wa Serikali, David Kakwaya katika hoja zake aliiomba mahakama iifute kesi hiyo na kwamba katika hati ya madai ya Mpendazoe kulikuwa na dosari, kwani kuna baadhi ya mambo yaliyojificha ambayo yangeweza kuwasaidia katika utetezi wao.