Madai ya mgomo Chuo kikuu Dar hayana upeo mkubwa

Ili tuweze jadili vizuri hii hoja, ingesaidia kama tungepata mchanganuo wa mahitaji ya wanafunzi ya "lazima" na gharama zake halisi kwa sasa halafu tulinganishe na pesa wanayopewa kwa siku.
 
Ni jukumu la serikali kuwasomesha watoto wa walalahoi na ni pamoja na kuhakikisha wanapata hela ya kula na accomodation, hata wao walisoma hivyo hivyo, lakini kitendo cha kugomea POSHO/boom/mshiko/allowance kila siku kwa Wanavyuo hamta ungwa mkono na watanzania, Vyuo vina matatizo mengi uhaba wahadhiri, mazingira mabovu ya kusoma etc etc ambayo yanawaathiri wanavyuo lakini hayafanyiwi maandamano wala migomo, hali ya SIASA na UCHUMI ya nchi nayo pia itazamwe na wasomi siyo kudai posho binafsi tu, posho mkipata na mazingira ya kusoma mabovu mtafanyia nini!
 
Wewe hujasoma Tanzania. Tanzania hakuna mabox ya kubeba au wazee wa kuwaangalia wakati wa likizo kama mnavyofanya huko "majuu".
Sijasoma Tz wewe ndie ulienisomesha? watu wengine bana..

Wenzenu Kenya wanapiga mabox?
 
"Kiwango cha posho ya Tsh 5000 kwa siku kwa mwanachuo kwa mazingira ya sasa kwa Tanzania, ni kiwango kinachoweza msaidia kama anaakili ya kupanga vizuri bajeti yake. Kama wanachuo wanataka kuishi kwenye hoteli za gharama au kifahari ni jukumu lao na wazazi wao kuongeza pesa za kujikimu kifahari. Kiwango cha Sh laki moja na nusu kwa mwezi kama yuko makini na kufikiria zaidi future yake anaweza panga vizuri bajeti na akaishi bila tatizo kubwa. Ila kama anataka awe anakwenda kula Hamburgers McDonalds ni juu yake na familia yako kuongeza matumizi".

Ndg yangu mtoa mada pole sana hasa kwa kutoijua Tanzania uizungumziayo. Unapaswa kuelewa kuwa tofauti na zamani wanafunzi wengi katika elimu ya juu nchini wanatakiwa kujilipia ada. Kujilipia kwenyewe kunafanyika katika sehemu mbili yaani Mkopo (ambao huwa katika asilimia) na malipo ya moja kwa moja kutoka mfukoni mwa wanafunzi.

Mfano. Kama ada ni 1,500,000 na mwanafunzi analipiwa 80% ya ada hiyo, anatakiwa kulipa 260,000/= yaani asilimia 20. Kufatia ukweli kuwa wanafunzi wengi wanatoka katika familia duni, mwanafunzi analipa ada hiyo kutoka sh. 5000 ya mlo na kulipia malazi.

Pili, vyuo vingi (tena vya umma) havina hostel za kutosheleza wingi wa wanafunzi uliopoko kwa sasa. Hivyo wengi/baadhi wanapanga mitaani. Akiwa mtaani hana ruzuku katika kodi ya nyumba, maji na umeme ambazo pia zimeongeza sana. Thamani ya 5000 inaendelea kupungua namna hivyo.

Tatu, mfumuko wa bei unaonekana kukua kwa kasi kubwa tangu mwaka 2005 ni sababu nyingine inayopunguza dhamani ya hiyo 5000 ambayo kwa mtazamo wako unaina inatosha sana.

Unapaswa kutambua kuwa ni wazazi wachache wenye uwezo wa ku-finance watoto wao katika elimu ya juu. Ninatambua kuwa wapo watanzania wengi wanaoishi chini ya dola moja na pia kuna matatizo mengi yanayo hitaji ufumbuzi. Lakini baba asipoacha nyumbani ugali kwa kisingizio cha kukosa pesa na katika pitapita wanae wakamuona hotelini akijichana kuku, watamuelewa? Kwanini serikali iseme haina hela wakati kuna misamaa ya kodi isiyokuwa na tija kwa taifa? Kwa nini viongozi wetu watoe vipaumbele katika safari za nje bila kujari athari zake kwa uchumi? Kwa nini tuendelee kuagiza mashangingi wakati hakuna dawa mahospitalini? Kwa nini tuilipe Dowans wakati hatuwezi kulipa madai ya walimu? kwanini viongozi waendelea kujilipa posho, kuingia mikataba yenye utata bila kuchukuliwa hatua wakati watanzania wanakosa huduma?

Wewe katika hili umekimbilia kuona selikali ina mambo mengi ya kufanya na si wanafunzi tu! Kwa nini usifikilie chanzo cha serikali kushindwa kufanya hayo?
 
hao graduates tu hawana kazi, na kwa bahati mbaya likizo wanayoweza kutafuta hizo pesa unazowaambia watafute ni wiki tatu maana most of them likizo ndefu huwa wanakuwa field...
If u r looking for excuses u will always find them..hivi kuingiza hela lazima uajiriwe?
 
Yaani wewe inaelekea elimu uliopata bado haikusaidii, unadai serikali mbali na elimu ina mengi ya kufanya kama afya, mawasiliano na huduma za jamii, nabado unasisitiza serikali haiwezi kuwapa posho ya 10,000 a day. Inamaana hiyo pesa ya dowans ambayo bila pingamizi ingeshalipwa siku nyingi, serikali ingezipata wapi kwa siku moja? Hivi kama serikali ingedhibiti kwa ukamilifu mambo kama Dowans,EPA, Richmond, Deepgreen, meremeta, Kiwila, Loliondo, Bulyanhulu, Geita Gold etc. Unadhani hiki ambacho wanafunzi wanakidai kisingekua historia. Leo unaambiwa chenge ana mabilioni ya Dollars huko Uswiss, tumeambiwa na SFO, yeye anadai ni vijicent, Je kama kwake ni vijicent vipi walio na vyeza? je kama vyote hivi vingedhibitiwa kikamilifu, si ingekua ni history? Mbona unaongea kama si msomi? Wanafunzi wanajua serikali yao ina pesa za anasa nyingi , kwa hiyo nawao wanaona kuliko pesa nyingi za walipa kodi kutumiwa hovyo na wachache basi wazipate ziwasaidie.Hata kama ni wewe baba anamiliki Filling station kila siku unamkuta baa anakunywa bia na chips, kesho ukimwambia pesa ya daftari na kalamu(vitu vya msingi) anakwambia sina pesa, utamwelewaje? jadili hili afu unipe jibu sio kukurupuka na kujadili fikra ambazo si zako.
YOU HAVE TO EMANCIPATE YOURSELF FROM BEING A MENTALLY SLAVERY NONE BUT YOUSELF SHOULD FREE YOUR MIND. STOP BEING A PUPPET OF THIS PUPPETIC sisim. blood idiot.

Kiwango cha posho ya Tsh 5000 kwa siku kwa mwanachuo kwa mazingira ya sasa kwa Tanzania, ni kiwango kinachoweza msaidia kama anaakili ya kupanga vizuri bajeti yake. Kama wanachuo wanataka kuishi kwenye hoteli za gharama au kifahari ni jukumu lao na wazazi wao kuongeza pesa za kujikimu kifahari. Kiwango cha Sh laki moja na nusu kwa mwezi kama yuko makini na kufikiria zaidi future yake anaweza panga vizuri bajeti na akaishi bila tatizo kubwa. Ila kama anataka awe anakwenda kula Hamburgers McDonalds ni juu yake na familia yako kuongeza matumizi.

Tumepitia vyuo vya Tanzania na tumepitia vyuo vya mataifa makubwa, kwa ulinganifu katika masuala ya posho naweza sema kumbe Tanzania ni bora mwanafunzi anaweza pata posho hiyo kuliko vyuo vya nchi tajiri. Watu hatukulala usingizi ni darasa na kazi. Uwapo kazini wakati wa mapumziko ndo unafanya homework, hakuna kulaza damu.

Tusiwe watu wa kulaumu serikali katika kila kitu, tulaumu yale ya msingi lakini katika hili mimi binafsi nasema hapana.

Watanzania tuko wavivu mno wa kujituma na kufikiri. Mazingira yako huru mno kujishughulisha Tanzania kuliko mataifa yaliyoendelea.

Utakuta walimu wanakimbilia kufundisha shule za mijini, kumbe shule za vijijini zina nafasi zaidi kwa kujiongezea pato kwa kujishughulisha na kilimo au kufungua biashara ndogo ndogo kusaidia wanavijiji kupata bidhaa ambazo wanapata taabu kuzifuata mbali. Mshahara wake ungezalisha zaidi kuliko mijini anamalizia kwenye starehe na gharama kubwa ya maisha.

Athari wanazopata wanachuo katika migomo yao ni kubwa kwao wanafunzi kuliko viongozi wanaowanyooshea vidole wakati wanaishi maisha ya starehe, na waendapo vyuoni ni kwenda kuwapiga msasa wa kisiasa tu. Kinachofanyika sasa vyuoni ni kama cheer ambayo ni kufuata mkumbo tu na kulazimisha wasiotaka lazima wafanye vinginevyo watadhurika, huku ni kuwanyima wengine uhuru wao wa kujiamulia wanavyotaka. Haki ya uhuru ni uamuzi wa dhamira safi baada ya upembuzi yakinifu.

Serikali ina mengi ya kufanya si wanafunzi tu, elimu, mawasiliano, afya, na huduma nyingine za jamii. Hata Chama kingine kikitawala hakitamaliza matatizo hayo kwa siku moja.
 
Anasa zipo saana vyuoni, lakini je madai yao yanamsingi kimahitaji wawapo vyuoni?
Ama ni agenda fulani nyuma ya pazia?

Naomba kuuliza tu ili nijue.

Swali zuri tu. Zamani watu walikuwa wanaona busara kujibanabana ili pesa zitumike kuhudumia wengine.

Lakini siku hizi wizi umezidi. Ukiangalia kwa upande mmoja unaona kuwa kuna mabilioni yanaenda kwa mafisadi na sio kuendeleza nchi au kuwasaidia masikini. Kama pesa zipo kwanini wanafunzi wasipate, au ni halali kwa wanasiasa tu kuzipata na wanafunzi wasipate
 
Swahilian!!! umeiangalia Elimu kwa ufinyu sana na wale ambao tuna thubutu kuwa ita wasomi, kwanza, binafsi nawaona wanafunzi kuwa wabinafsi mno, kwahiyi kwa mantiki yako kila gharama za maisha zinapo panda basi na boom ipande? hivi unajua hilo ndilo linalo fanywa na serikali yako? kila mwaka wafedha kodi inapanda? hakuna hata dalili ya kutafuta vyanzo mbadala vya mapato au kutatua mfumoko wa bei ambao sasa tupo kwenye troting iflation, serikali inategema Hydro electric power only, wakati tuna vyanzo chungu nzima, ngoja nikuchekeshe ndo uone hapa kwetu TZ ni Wehu na hawa watoto mi nawaita watoto wanao andamana nio wehu! kuna wasomi walichukuliwa kufanya utafiti (research) ktk bonde linalo peleka maji bonde la mtera, mi si mzuri kijografia lakini ninayo hii documentary yote! nia ya kufanya uchunguzi ilikuwa ni hili kuruhusu TZ kuingia mkataba wa kuzalisha mpunga na wazungu, research results zilionu=yesha mahali pale panafaa na hapata kuwa na athari na kilimo kitakuwa productive, mkataba ukaingiwa, kilimo kika anza, kwakifupi matokeo yake, Maji katika bomde lile la mto yamekauka, mpunga uliokuwa unazalishwa pale ni ghali kuliko unao toka nje, alafu maji yale yale ndo yalikuwa yanapelekea chanzo cha umeme, sasa..! mpunga hakuna, umeme hakuna, hawa ndo watafiti wetu TZ walio tupelekea huku, swali! HIVI UNAFIKIRI MAMBO KAMA HAYA YA KINA CHENGE, NA HAWA WANAFUNZI WA VYUONI WANALETA CONTRIBUTION YOYOTE KTK TAIFA HILI AU NI SHIDA TU?
 
Inshu siyo kuwekewa mezani kila kitu!! ni mfumo wenyewe ulivyowekwa. vipindi vinapigwa hadi saa 2 usiku utapata muda wa kufanya ndugu yangu? Hata hayo mashule ya kata yangekuwa yanawatumia hawa jamaa yasingekuwa yanapata zero hata moja, lakini kwa vile hakuna " The called Coordination ya Elimu kuanzia chini hadi vyuo vikuu au vya elimu basi ni bora liende". Kila mtu anataka anavyoona, nchi haina mipango ya maana kiutekelezaji katika nyanja yeyote zaidi ya mipango kwenye karatasi.

My take:
1) Hawa jamaa wawwape muda wa wao hata kutafuta kazi mitaani japo kufundisha kwa masaa mawili mashule ya kata inapunguza matatizo kibao. Nchi inatatizo na walimu wakati ni kiasi cha kutwist some parameters na kujikuta wanasolve mengi.
2) Kama ni kumwagilia bustani za barabarani, wanalipwa nako poa ni sera tu. Wanaweza kukataa mara ya kwanza baadae watakubali.

shoprite+game ni maeneo ambayo wanafunz wanaweza kufanya kaz kwa shift!so waliosaini mikataba wangeweka kipengele hcho
 
jamani kuna mfumuko wa bei,maisha yamepanda sana......huwezi sema wajilipie wenyewe kwakuwa huo mfumo haupo na hawawezi uanzisha wao....mi kweli,sioni kama inatosha.....wengi wanakosa vyumba na jioni badala ya kula vyakula vya bei ya chini vinavyopatikana chuoni wanakula mtaani wanakoishi ambako vyakula ni ghali, walipie kodi na nauli za kurudi mitaani walikopanga, bado dispensary ya chuo ukienda mara dawa hamna,mara wakupe referral uende kwa Kariuki...jamani,lets be realistic......

mtu ana vipindi asubuhi hadi saa moja usiku vinapishana tu masaa mawili au moja,kazi atafanya wapi?? biashara ataanzisha na nini kama hela ya mlo hana???Serikali iwaangalie wanafunzi......:coffee:
 
Mi nafikiri swala sio kiwango cha pesa, bali tufanye nini hili ikibidi hata hicho kiwango cha 5000/- kiwe ni cha kusaza, maana ukiangalia kweli 5000/- haitoshelezi lakini swala si kudai nyongeza kila kuna kucha, na ndomana hawa wapo huko vyuoni!!! serikali imeshindwa kubuni mbinu mbadala hata wa kuongeza tu bajeti, ndo mana kila siku bidhaa zinapanda bei, sasa hiyo niserikali, wanafunzi ambao tunathubutu kuwaita wasomi hawana mapendekezo ya tija kwa taifa zima na sio suluhisho la muda mfupi kama wanavyo dai? let say wamepewa hiyo nyongeza, the what???? huko chuoni wata kaa milele?? wangali wana nafasi yakutumia yaliyomo kitabuni kuishinikiza serikali katika ku impose policy zake na ku priortise mambo yake kielimu haya mambo yanwezekana na ndo mana wanaendelea kuwemo huko chuoni, hawasomi wakaja kupata hajira tu, ni pamoja kutatua matatizo ya kitaifa, ni vipi kama wange andamana kwanini serikali imeshindwa kutumia rasilimali katika kuliletea taifa maendelo, au kwanini serikali imeshindwa kutumia vyanzi vingine kuzalisha umeme wakati tuna rasilimali za kusaza? mambo ya jinsi hiyo yangweza kutataua matatizo sio tu ya boom bali hata wazazi wao ambaa hata kama wao wangalipewa hiyo boom haitoweasaidi na jamii kwa ujumla, ni lini msomi atatumia elimu yake sawa sawa??? Basi kuweni na sababu ya kuandamana kupinga kupanda kwa gharama za umeme, ambazo zimepelekea hata hiyo 5000/- kuto kutosha kwani gharama za uzalishaji zimekuwa kubwa, bidhaa zimepanda bei sana, nk

hayo ni magumu kuyafikri???? au kianzishwe kitengo maalumu chenye mtaala wake pia?
 
jamani kuna mfumuko wa bei,maisha yamepanda sana......huwezi sema wajilipie wenyewe kwakuwa huo mfumo haupo na hawawezi uanzisha wao....mi kweli,sioni kama inatosha.....wengi wanakosa vyumba na jioni badala ya kula vyakula vya bei ya chini vinavyopatikana chuoni wanakula mtaani wanakoishi ambako vyakula ni ghali, walipie kodi na nauli za kurudi mitaani walikopanga, bado dispensary ya chuo ukienda mara dawa hamna,mara wakupe referral uende kwa Kariuki...jamani,lets be realistic......

mtu ana vipindi asubuhi hadi saa moja usiku vinapishana tu masaa mawili au moja,kazi atafanya wapi?? biashara ataanzisha na nini kama hela ya mlo hana???Serikali iwaangalie wanafunzi......:coffee:

Michelle, serikali iangalie mfumo wa elimu na mambo mengine sio wanafunzi peke yake! Wakiongeza pesa ya kujikimu na walimu je? Manesi? Polisi? Tatizo si wanafunzi peke yake! We have a bigger problem and that is what we shuld address and solve!

Kuwaongezea wanafunzi hela peke yake haitoshi.
 
shoprite+game ni maeneo ambayo wanafunz wanaweza kufanya kaz kwa shift!so waliosaini mikataba wangeweka kipengele hcho

Asante, umeona mbali saaaaaaaaana, hivyo ndivyo ambavyo ilipaswa kuwa hivyo, lakini unaweza kukuta kaka/dada yako ndo anafanya kazi hapo na ndo huyo tena nakupa mahitaji ya chuo.

Kuna mambo mengi saana ya kubadilisha mfumo wetu wote wa elimu sio mzuri, mazingira ya vyuo vikuu ni aibu kabisa, hakuna tofauti na sekondari. Mwalimu aliyenifundisha elimu ya Msingi ndiye nilikutana naye chuo kama mhadhiri msaidizi kilichoongezeka kwake ni maneno ya kiingereza na uwezo wake wa kukariri lakini uwezo wa bongo yake (IQ) haukuwa tofauti sana na aliponifundisha msingi

Tsh 5,000 haitoshi kabisa, kwani si kuna watz wanaishi kwa anasa, je TZ sio maskini? kama kuna wanafunzi wanaishi kwa anasa haiondoi ukweli kuwa TSh 5,000 ni ndogo. Kama hujasoma bongo huwezi kuona hii pesa ni ndogo.
 
mi ninaamini hiyo 5000 kwa siku haitoshi! haswa kwa jinsi gharama zinavyopanda! na kama hizo hela za kujikimu ni mkopo kwanini kuwe na ubahili wa kuzitoa?
 
Umaskini unatuua na mwisho kuuana. Kumnyooshea kidole baba yako kila unachoona hakiendi sawa ni upeo finyu. Kaa na baba yako uone bajeti ilivyo ndo utaelewa vipaumbele alivyoweka baba yako. Kisha utatambua kwamba kumbe natakiwa nini nimshauri baba afanye ili kuoongeza kipato na kupanga vizuri bajeti.

Nilipokuwa shule ya msingi awamu ya kwanza ya utawala wa nchi hii nilikuwa nafanya kazi siku za likizo ili kupata mahitaji ya shule kuwasaidia wazazi wangu. Nilipokuwa sekondari vivyo hivyo. Nilipokuwa chuoni serikali ilikuwa na utaratibu wa wanafunzi wakati wa likizo kwenda kufundisha shule za msingi na kupata posho. Na wengine walikuwa majaribio viwandani na idara za serikali au mashirika binafsi.

Utaratibu huo ingefaa pia ufanyike siku hizi.
Ratiba vyuoni isiwakabe mno wanafunzi, ili wapate muda wa kuhangaikia riziki.
Tatizo la walimu shule za kata lingeweza tatuliwa kwa wanachuo kuwa part time instructors.
Vyuoni ratiba za wanachuo ugawanywe katika vipindi viwili, ili kuwepo na wahudhuriaji wa kipindi cha asubuhi na wahudhuriaji wa kipindi cha alasiri. Muda ambao wanafunzi wako huru ndio wanatakuwa wanafanya kazi kujikimu kama kufundisha mashuleni nk.

Hatima wanachuo waweke kando starehe ili kupunguza gharama za maisha zisozolazima ili kupanga vizuri bajeti ya chuoni
 
Umaskini unatuua na mwisho kuuana. Kumnyooshea kidole baba yako kila unachoona hakiendi sawa ni upeo finyu. Kaa na baba yako uone bajeti ilivyo ndo utaelewa vipaumbele alivyoweka baba yako. Kisha utatambua kwamba kumbe natakiwa nini nimshauri baba afanye ili kuoongeza kipato na kupanga vizuri bajeti.

Nilipokuwa shule ya msingi awamu ya kwanza ya utawala wa nchi hii nilikuwa nafanya kazi siku za likizo ili kupata mahitaji ya shule kuwasaidia wazazi wangu. Nilipokuwa sekondari vivyo hivyo. Nilipokuwa chuoni serikali ilikuwa na utaratibu wa wanafunzi wakati wa likizo kwenda kufundisha shule za msingi na kupata posho. Na wengine walikuwa majaribio viwandani na idara za serikali au mashirika binafsi.

Utaratibu huo ingefaa pia ufanyike siku hizi.
Ratiba vyuoni isiwakabe mno wanafunzi, ili wapate muda wa kuhangaikia riziki.
Tatizo la walimu shule za kata lingeweza tatuliwa kwa wanachuo kuwa part time instructors.
Vyuoni ratiba za wanachuo ugawanywe katika vipindi viwili, ili kuwepo na wahudhuriaji wa kipindi cha asubuhi na wahudhuriaji wa kipindi cha alasiri. Muda ambao wanafunzi wako huru ndio wanatakuwa wanafanya kazi kujikimu kama kufundisha mashuleni nk.

Hatima wanachuo waweke kando starehe ili kupunguza gharama za maisha zisozolazima ili kupanga vizuri bajeti ya chuoni

Kumbe unayetuletea hii mada ni wewe uliyesoma enzi za mwalimu. Ndo maana unahamisha mazingira ya siku hizo unataka yawepo sasa. Tena bila aibu unasema posho ya elfu 5 inatosha wakati ulikuwa unalipiwa kila kitu enzi hizo.
Mzee mambo yamebadilika sana. Kama ulikuwa unafanya kazi wakati wa likizo sasa hivi hizo kazi hazipo. Hakuna hivo viwanda ulikuwa unafanyia kazi enzi hizo. Vwanda vilvokuwepo kwa uchu wa mali mmeviharibu na sasa watoto na wajukuu wenu hatuna pa kushika.
Unasema kufundisha kungepunguza makali ni kweli lakini ni sehemu gani ya wanafunzi watakaoingia kufundisha kabla hizo shule hazijafurika na pia sio wote ni waalimu.
Nimekuwa chuo kimoja miaka ya karibuni sio chuo cha serikali hivo wengi wanajilipia. Ukweli ni kuwa wale wanaotegemea mikopo ya serikali ambao wengi wao ni watoto wa wakulima wana hali mbaya mno. Hizo anasa wanazopayuka nazo watu hapa zipo lakini si kwa watu hawa wanaopata elf5 kwa siku. Kwa kifupi hawa watu kawaida wanakula mlo mmoja kwa siku wanaita lon pass. Yaani ukipiga chai asubuhi unapata tena dinner jioni. Balaa linakuja pale hizo pesa kidogo zinapochelewa.
Mnawasingizia vijana wenu kuwa wanatumia pesa vibaya bila kuweka mchangunuo utakavotumia hiyo elf 5 ikutoshe. Inaposemwa elf 5 akili zenu zinahamia kwenye chakula tu hadi mmoja anaropoka kuwa kama wanataka kuishi kwenye hoteli za kifahari. Elf 5 hata guest house bubu pengine isitoshe sembuse hoteli.
Mimi ckutumia mkopo wa serikali lakni nnavojua beneficiaries ambao kwao hawakuwa na psa za kuongezea walikuwa na shida sana hata wakati mwingine hawakufanya mitihani kwa kutokamilisha ADA.
Tuache ushabiki na kuangalia vtu kwa jujuu pasipo kufanya utafiti huku tukilinganishe enzi hizo kongwe na Tanzania ya sasa. Elf 5 haitoshi na haitatosha.
 
Usemayo yanawezekana ikiwa kuna mfumo usiobadilika sana wa bei ktk nchi yetu,

Kwa kumbukumbu yangu kiwango cha Tsh. 5000 kwa siku ilipanda kwa Mara ya Mwisho mwaka 2006, hapo unaweza kutathmini ni miaka mingapi imepita na kuna mabadiliko yapi.

Wanayo haki ya kudai hiyo pesa, na labda na ujue kuwa hiyo pesa si kwamba wote hutumia ovyo wapo ambao huagizia kwa familia zao vijijini.

Huko kijijini unakosema eti wahitimu wakimbilie kuna nini? Iwapo hata hao wanakijiji wanalalamika? Na kwa mitaji ipi wanayotoka nayo vyuo?

Vijana hawa bado wanayo haki na kwa hakika wanaumia na hasa nkijaribu kuangalia gharama za chakula kwa siku, usafiri kwa wale wakaao off campus, matumizi ya utoaji vivuli makaratasi ya kiada na ziada, kulipia pango na nk.

Wanayo haki na kweli wanaumizwa na ni lazima serikali iwafikirie maombi yao, kuliko huku kupambana na polisi kuumiza vijana wetu na hata kuleta hofu miongoni.

Bado na nasema bado wanafunzi wa chuo wanadharauliwa na hii ni kutokana na kipato chao kidogo, wanaishi ktk umasikini mkubwa mchana kutwa wanavuja jasho kwa kutembea toka Mabibo hadi Campus na chupa za maji mikononi kujipooza, wanajipa matumaini kwa kuvaa suruali za vitambaa na tai shingoni, siri ya mifuko yao mungu ndio anajua;

Nasema na nina uchungu katika hilo kwani nimeyajua mateso kwa miaka mitano sasa.

Hakika wanayo shida na tusiwadharau au kuwabeza kwani si kweli wote ni wajinga na wana akili moja, yapo magumu yalowasibu na sasa wamechoka.

Ombi lao wananchi tuwasaidie.

tukiludi kwa mtz wakawaida sh 1000 kwasikukuipata nimiujiza 5000kwamwanachuo kwasiku kwakujinyima ingekuwa tz nimasikini mafisadikirasiku wanajichoteyamamilioni natumewasomeshakwakodi zetu inakuwejehawa wanyanyasike ingawa wasomindowaliochangiakuihalibu tz wanashelia wanasiasa wataalam nyanjazote mumesomakwakodi zetu niayibutulipofikia utafikiliwotenimambumbumbu ushaulikwawanachuo somenisanaatakamakwamazingilamagum ndomutakuwanauchungu zaidi nahaomafisadi sikuzaozinaesabika
 
Ni kweli nimesoma miaka ya 80 na 90 nchini mwangu Tanzania na matatizo ya maisha shuleni siku hizo yalikuwa magumu zaidi kuliko siku hizi. Tulitembea kwa miguu na usafiri tutokapo likizoni kwenda chuoni tulitembea kwenye malori yaliyojaza magunia. Shuleni tulisoma kwa vibatari. Hakuna mama ntilie ilibidi tuchukua chakula tuwapo safarini kujikimu kabla hatujafika shuleni. Cha msingi tulijua tunataabika kwa muda na tukishahitimu tunaanza tengeneza maisha yetu.
Mazingira ya leo huwezi linganisha na ile ya miakia ya 80 na 90. Leo unapata sukari lakini wakati ule ni kwa mgao, na kwa mwanafunzi sahau neema ikunyeshee. Bulger ya mmarekani ndo iliyotupa nguvu ya kuzungusha matufe ya kutuelimisha jiografia, lakini wanachuo wa leo wanataka wakale McDonalds restaurant.

Vijana wengi siku hizi ni mafundi wa kulaumu zaidi kuliko kufikiria namna gani kutafuta mbinu ya kujitegemea kuongeza kipato. Siku hizi mwanafunzi anafikiria kupata pesa za kustarehe weekend badala ya kufikiria kununua vitabu vya kiada. Wanachuo siku hizi wanafikira computer kwa ajili ya kuchati mambo yao ya urafiki wanayofahamiana badala ya kufikiria kutumia online kwa ajili ya kupanua elimu yao. Wanachuo siku hizi ndio wanaojaa kwenye madisco na nyumba nyingi za starehe siku za weekend badala ya kutulia na kufanya homework au kufanya vibarua kujijpatia pesa za matumizi.
Tukubali tuko wavivu wa kufikiria njia bora ya kujiongezea kipato na tunapenda tu dezo.

Ni miaka mitatu tu iliyopita nimetoka kuhitimu chuo nchi mojawapo iliyoendelea, hakuna dezo ni kuchakalika usiku na mchana hadi nahitimu. Nasoma na huku nafanyakazi ili kulipia karo, kununua vitabu, chakula na rent ya nyumba ninayoishi. Raia wenyewe wa nchi niliyosoma walinafanya vivyo hivyo, sikuona anayelalamika au kuandamana eti serikali inawapunja.

Kama ni mkopo nilifanikiwa kupata lakini ni nusu ya ada ya chuo, ikabidi nusu nilipie mwenyewe kwa awamu kidogo kidogo kila mwenzi hadi namaliza chuo tokana na kazi.
Tusidanganyane, Watanzania tunapenda njia ya mkato, na kwa maandamano ya chuo cha mlimani hapana.
 
Sitachangia sana ila niungane na mleta hoja...kwamba kiasi cha sh 5000 kwa siku yumkini hakitoshi ila madai ya sh 10000 ni kikubwa mno kulingana na idadi ya wahitaji...kwa maana chuo kikiuu cha Dar es salaam hakina tofauti (sizungumzii ukongwe) kimahitaji na vyuo vingine...
 
WACHINA..jpg


Kazi kama hizi nchi nyingine unaona wanachuo wanachangamkia kupata mahitaji ya kujikimu, lakini wanachuo wa Tanzania anafikiria tu kazi nzuri za ofisini. Kuna kazi nyingi ambazo vyuoni ungekuwepo utaratibu mzuri zingefanywa na wanafunzi badala ya kila kazi kuajiri watu. Kwa maana hiyo ratiba za vyuoni zingeratibiwa vizuri wanafunzi wangeweza punguza gharama za mishahara wanazolipwa wafanyakazi na hivyo baadhi ya kazi zikafanywa na wanafunzi na malipo nafuu ili kuokoa bajeti ya chuo. Vyuo vingi mataifa makubwa hufanya hivyo.

Mwanachuo ukianzisha genge fulani la kuuza nyanya baada ya chuo na siku za weekend kuna shida gani? Wa kitivo cha sayansi ya computer kwa nini wasiwe na kazi za kusaidia kuondoa minyoo kwenye komputer nyingi za watu na hivyo kupa pesa kidogo za kununulia mihogo ya breakfast? Wanachuo msipende tu breakfast ya mikate na omlet, kuleni mihogo inadumu zaidi uwapo darasani.

Wakati naenda chuo moja ya taifa kubwa ilibidi nitafute international supermarket kupata mihogo na unga wa ugali, nilipobahatika nikaukata, maana nikishakula mlo mmoja wa ugali napiga kitabu na huo huo unatosha kupiga box siku imepita, na ujue hapo hela nimesave.
Wabongo tujifunze kubanga bajeti na raha tukishamaliza vyuo, vinginevyo tunalalamikia vitu ambavyo ni nje ya uwezo wa serikali, kwani serikali ina mengi wajamani.
 
Back
Top Bottom