Madai haya ya Zitto kama ni ya kweli, basi hii ni moja ya sababu kwanini sisi ni masikini na tutaendelea kuwa hivyo

Moja kasoro kubwa inayotumaliza Watanzania ni hii tabia ya wanasiasa kutudumuza kuwa kila kitu kifanywe ni (mwingine) na sio sisi wenyewe. Zitto is simply full of hot air. Yeye amefanya nini, amelima hata nusu eka ya mchikichiki? Anataka watu wa Kigoma WALETEWE WACHINA, WAARABAB, WAMERAKANI ETC kulima michikichiki? Kwanini asihamasiche watu wa Kigoma wakalima?
Zitto ana uwezo wa kuufanya research?
Mbegu zilizopo ni za asili na zina viwango duni. Research Institution za Tanzania ndio zilitakiwa ziandae Mbegu. Wizara ya kilimo iwajibike. Alafu ndio tumzodoe Zitto kwa kutolima hiyo robo eka. Mwalimu wangu wa uchumi A level aliwahi kutuambia Wafaransa wanakopa sera zilizofanyiwa tafiti chuo kikuu na wanazimodifai wanasongesha uchumi wao. 2014 Nilienda Uganda wamewaleta wataalamu kutoka Indonesia wamewawezesha wakulima wa michikichi meneja wa mradi akaniambia wanazalisha zaidi ya 75% inayotumika Uganda. Kampuni ya Bidco imeingia mikataba maalumu na serikali ya Uganda. Visiwa vilivyopo ziwa Victoria vyote vimegeuzwa mashamba. Kisiwa kimojawapo nilichotembelea kinaitwa Kalangala. Huyo meneja mradi aliniambia Mbona Tanzania hamlimi na amewahi kufanya kazi Tabora na anaijua kigoma? Tusipokuwa na taratibu wa kuwahoji Viongozi wetu na uwezo wa kuwawajibisha wanapofanya madudu tukakalia siasa na kuhoji mbona yeye hajalima. Je akilima ekari Mia zitatatua tatizo? Hii issu ni ya kitaifa sio ya Zitto na bila idara za serikali kuingiza fedha Zitto huwezi chochote hata angelima ekari 1000. Hivi hata bajeti ya kilimo ya mwaka huu umeisikia ilivyo ya aibu? Tujaribu walau kuiga Uganda, serikali imeingiza fedha na kushirikiana na wawekezaji sio kuwatisha.
 
Zitto Mjinga tu kigoma mawese ndio wakulima wakubwa Tanzania lakini huyaoni madukani wala supermarket Tanzania singida na alizeti zao wamefght mafuta ya alizeti nchi nzima yapo huyu nusu kaputi kichwani anaongelea mafuta ya kupikia ya malyasia badala ya mawese ya kigoma anakotoka
Naona na wewe umeamua kuchangia tu uonekane. Issue iko hivi. Mawese yote yako kigoma yakikamuliwa mafuta na alizeti yote ikikamuliwa mafuta ni 30% tu ya mafuta yanayoitajika Tanzania. 70% inayobaki inatoka nje.
 
Zitto amedai kuwa watu kutoka Malaysia walikuja nchini kwetu wakachukua mbegu za michikichi na kwenda kulima kwao na leo hii wanatuuzia sisi mafuta ya kula!l. Ajabu kabisa!

Niseme wazi tu tangu niliposikia kauli hii ya Zitto hakika inanipa shida sana pale ninapojaribu kuitafakari inatupa ujumbe gani sisi watanzania.

Tafsiri rahisi ya maneno haya ni kuwa, sisi kwa miaka mingi tumeshindwa kuwekeza katika kilimo ambacho kingezalisha malighafi kwa bidhaa za viwandani (processing industries) kisha tukazalisha bidhaa za viwandani ambazo zingetosheleza mahitaji yetu ya ndani na ziada tungeuza nje ya nchi na hivyo tungeingiza fedha nyingi za kigeni na hata shilingi yetu ingekuwa na thamani dhidi ya dollar na fedha nyingine za kigeni.

Najiuliza hivi sisi na Malaysia ni nani wenye ardhi kubwa inayofaa kwa kilimo na yene mabonde na mito mingi inayofaa hata kwa kilimo cha umwagiliaji?

Hakika umaskini wetu ni wa kujitakia
umeona eeeh . . . hivi unapozalisha mafuta ya kula ya kujitosheleza kwa asilimia 30 tu huku una zaidi ya miaka 50 ya kujitawala mwenyewe tafsiri yake ni nini?
Pamoja na kuwa na haya maono ya processing industries katika mpango wetu wa sasa wa miaka mitano wa maendeleo ya taifa sijaona hatua madhubuti na za makusudi za kuwaita wawekezaji katika sekta hii ili kuweza kuzalisha mafuta ya kutosha kwa ajili ya mahitaji yetu na kuuza nje.

Hawa Malaysia na Vietnam tuliwafundisha kilimo cha michikichi na kuwapa samaki sasa hivi wanatuzidi,
upuuzi tu
 
Jamani zito ni mbunge miaka mingapi? Jitihada zake za kuleta wawekezaji hana kwa ajili ya watu wajimboni kwake? Mimi ninavyoona Zito Kabwe anauwezo yeye binafsi angalau kuleta hata muwekezaji moja, ndiyo kazi ya kiongozi aliyewepewa dhamana Na wananchi wa jimboni kwake,, kila siku data za kukosoa ,kama mbunge moja ya jukumu lake nikuwasaidia wakulima wake, kama Mama Kilango machela alivyopambana nakufanikisha kiwanda cha Tangawizi,Tunataka jitihada zako Binafsi Zito Kabwe angalau utakumbukwa na wana Kigoma ukiwezesha walau kujenga kiwanda cha mawese, acha maneno fanya mambo
kama Zitto akileta mwekezaji ipi hasa ni kazi ya waziri wa viwanda, biashara na masoko? tunamlipa ili afanye nini hasa?
kazi ya mkurugenzi wa TIC itakuwa ni ipi? tunamlipa ili akae tu ofisini? kazi ya katibu mkuu biashara na uwekezaji ni nini?
hao ndiyo wa kuwabana ili wawe na mikakati thabiti ya kuvutia uwekezaji

kazi ya mpinzani ni kukosoa ili serikali ifanye kazi na sio kusifia
 
Moja kasoro kubwa inayotumaliza Watanzania ni hii tabia ya wanasiasa kutudumuza kuwa kila kitu kifanywe ni (mwingine) na sio sisi wenyewe. Zitto is simply full of hot air. Yeye amefanya nini, amelima hata nusu eka ya mchikichiki? Anataka watu wa Kigoma WALETEWE WACHINA, WAARABAB, WAMERAKANI ETC kulima michikichiki? Kwanini asihamasiche watu wa Kigoma wakalima?
Ahamasishe watu walime halafu serikali iagize nje
 
Malaysia walikuja Bongo wakachukua Idea ya Ukawa wakaenda nayo kwao wakaunganisha vyama vyote bya Upinzani Na kukitoa Chama Tawala kilichodumu Kwa 60 years , inakuaje Ukawa walishindwa ku practise lakin wa Malysia waliweza?
Mkuu, kwani mwaka 2015 nani alishinda!? Angalia vizuri, sijasema nani alitangazwa, nimeuliza hivi; "NANI alishinda!?"
 
Mkuu, kwani mwaka 2015 nani alishinda!? Angalia vizuri, sijasema nani alitangazwa, nimeuliza hivi; "NANI alishinda!?"

Kushinda nini?

Prof J alishinda, Mayor Jacob alishinda, Job Ndugai alishinda, Dkt John Magufuli alishinda Urais , Livinhstone Lusinde alishinda ,

Una maanisha kushinda kitu gani Kwa level gani?
 
Zitto amedai kuwa watu kutoka Malaysia walikuja nchini kwetu wakachukua mbegu za michikichi na kwenda kulima kwao na leo hii wanatuuzia sisi mafuta ya kula!l. Ajabu kabisa!

Niseme wazi tu tangu niliposikia kauli hii ya Zitto hakika inanipa shida sana pale ninapojaribu kuitafakari inatupa ujumbe gani sisi watanzania.

Tafsiri rahisi ya maneno haya ni kuwa, sisi kwa miaka mingi tumeshindwa kuwekeza katika kilimo ambacho kingezalisha malighafi kwa bidhaa za viwandani (processing industries) kisha tukazalisha bidhaa za viwandani ambazo zingetosheleza mahitaji yetu ya ndani na ziada tungeuza nje ya nchi na hivyo tungeingiza fedha nyingi za kigeni na hata shilingi yetu ingekuwa na thamani dhidi ya dollar na fedha nyingine za kigeni.

Najiuliza hivi sisi na Malaysia ni nani wenye ardhi kubwa inayofaa kwa kilimo na yene mabonde na mito mingi inayofaa hata kwa kilimo cha umwagiliaji?

Hakika umaskini wetu ni wa kujitakia

Ndugu

Leo umezungumzia jambo la kitaifa, Malesia NA Vietnam walikuja enzi za Hayati Nyerere NA wakachukua miche ya Mawese (MALESIA) na Mikorosho (Vietnam), NA leo wote hao wamekuwa wanaongoza ulimwenguni kwenye uzalishaji wa hayo mazao.

Kwa hili watanzania wote NA haswa viongozi wetu tunazo lawama za ujinga na ku kosa uweledi.

Hayo yalipokuwa yakitokea wakati Baba wa Taifa alikuwa akituongoza na wasaidizi wake walioko hai leo ni akina Mzee Mwinyi, Msuya, Malecela, Lowasa, Mtei, NA kati ya hawa ukiangali mshauri wake mkubwa aliyekuwa Kwenye mambo ya uchumi alikuwa Mtei.

Japokuwa Mwalimu aliweza kuwekeza kwenye viwanda ambavyo vilishindwa kufanya kazi kwa weledi, hadi uamuzi a kuviuza kwa bei ya kutupa NA hadi kufanywa magofu.

Mfano mwengine ni mashamba ya mikonge, hili Linasikitisha sana, mashamba yamekufa Ardhi imekaa bure, wangepewa wanavijiji at least tungeweza pats chakula cha kutosha, lakini msimamo ni kuwa zao hilo Lina bei NA hakuna MAKORONA ya kusaga katani, Machine zimekufa tokea miaka ya 80.

Watanzania tumezoea kupigia kelele mambo yasioya NA tija kwa taifa, haya ndio mambo ya kuyasimamia , tuungane kuyapigania mpaka tuone mambo yanabadilika. Serekali ikiwekeza kwenye mazao haya mawili tuu, ninajakika ajira ya maelfu na maelfu zitazaliwa, NA tutaweza kujitosheleza.
 
Ndugu

Leo umezungumzia jambo la kitaifa, Malesia NA Vietnam walikuja enzi za Hayati Nyerere NA wakachukua miche ya Mawese (MALESIA) na Mikorosho (Vietnam), NA leo wote hao wamekuwa wanaongoza ulimwenguni kwenye uzalishaji wa hayo mazao.

Kwa hili watanzania wote NA haswa viongozi wetu tunazo lawama za ujinga na ku kosa uweledi.

Hayo yalipokuwa yakitokea wakati Baba wa Taifa alikuwa akituongoza na wasaidizi wake walioko hai leo ni akina Mzee Mwinyi, Msuya, Malecela, Lowasa, Mtei, NA kati ya hawa ukiangali mshauri wake mkubwa aliyekuwa Kwenye mambo ya uchumi alikuwa Mtei.

Japokuwa Mwalimu aliweza kuwekeza kwenye viwanda ambavyo vilishindwa kufanya kazi kwa weledi, hadi uamuzi a kuviuza kwa bei ya kutupa NA hadi kufanywa magofu.

Mfano mwengine ni mashamba ya mikonge, hili Linasikitisha sana, mashamba yamekufa Ardhi imekaa bure, wangepewa wanavijiji at least tungeweza pats chakula cha kutosha, lakini msimamo ni kuwa zao hilo Lina bei NA hakuna MAKORONA ya kusaga katani, Machine zimekufa tokea miaka ya 80.

Watanzania tumezoea kupigia kelele mambo yasioya NA tija kwa taifa, haya ndio mambo ya kuyasimamia , tuungane kuyapigania mpaka tuone mambo yanabadilika. Serekali ikiwekeza kwenye mazao haya mawili tuu, ninajakika ajira ya maelfu na maelfu zitazaliwa, NA tutaweza kujitosheleza.
Inasikitisha sana kwa aina ya viongozi tulioanao.Tuna-invest karibu nusu trilioni kwenye ndege (biashara isiyo na uhakika) alafu tuna-invest bilioni 11 kwenye kilimo wakati ndio kingeweza kutuvusha kama Taifa.

Hawa viongozi wa leo na hao waliopita wote hawana msaada kwa hili Taifa licha ya kulipwa vizuri na kutunzwa na serikali mpaka leo hii.

Ngozi nyeusi sijui tumelaniwa?!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Moja kasoro kubwa inayotumaliza Watanzania ni hii tabia ya wanasiasa kutudumuza kuwa kila kitu kifanywe ni (mwingine) na sio sisi wenyewe. Zitto is simply full of hot air. Yeye amefanya nini, amelima hata nusu eka ya mchikichiki? Anataka watu wa Kigoma WALETEWE WACHINA, WAARABAB, WAMERAKANI ETC kulima michikichiki? Kwanini asihamasiche watu wa Kigoma wakalima?
Kasoro kubwa zaidi ni pale watu wqnapojaribu kuonyesha mapungufu ya serikali, wanaibuka wachumia tumbo kushambulia wanaoonyesha kasoro husika. Kumbe kwanini tunaingia gharama kulipa mishahara na posho mawaziri, manaibu waziri, makatibu , wakurugenzi na watendaji wengine wizara ya Kilimo kama tunaweza kuulizana wewe umefanya nini kisa tu umeonyesha udhaifu wq serikali? Kuruhusu njaa itafune ubongo ni dhambi kubwa sana!
 
Rais anasema HAPA KAZI TU na kiujumla 80℅ ya kazi tz ni kilimo.
Kwa hiyo watu wanatakiwa kujiingiza katika kilimo. Viongozi lazima waweke fursa ili watu waweze huwezi kusema kalime na kuishia hapo.
10℅ ya watz wanaishi mijini hawajawahi hata kushika jembe ni mipango ipi inawaongoza waweze kuenda kuanzisha kilimo.
Elimu yetu inawaandaaje vijana ili washiriki kilimo ili viongozi wapate nguvu ya kusema NENDENI KULIMA
 
Yeye kama mbunge. Msomi, Kwa nini asilime shamba la michikichi na hamasisha watu kigoma kulima serekali ailimi
Ndio hapo inaposhangaza?!?!?! Ningemuelewa angesema watu wa Kigoma wana lima michikichi amuombe waziri husika ajenge kiwanda cha kusindika mafuta ya mawese Kigoma!
 
Jamani kama kuna waTanzania hawajaona fursa basi watabaki hivyo hivyo wakati wenzao wakitumia fursa. Kwa sasa kuna fursa nyingi zinatangazwa. Kwa sasa kuna vijana wengi wasomi wamejikita kwenye kilimo na wanatajirika sana. Sasa sijui hawa wanaolalamika ni wahenga wenzangu au vipi?!?!? Kwa wasioona fursa katika Awamu hii ya 5 basi hawatakaa wazione hata wakiwekewa milangoni mwa nyumba zao! Cha muhimu sikiliza redio. sikiliza na kuanga lia TV. Jifunzeni kuangalia TV yen a Taifa sio mnakalia bongo flavor huko East Africa TV halafu mnakuja mitandaoni kulalamika! Nchi zote zilizoendelea ziliendelea kwa kufanya kazi na si kwa kulalamika!
 
Shughuli zenyewe za kisiasa mmezipiga marufuku.Mkiwaona wanazunguka majimboni mara muwakamate au muwazuie sasa hata kama mtu ana nia hiyo kwa sasa ataweza kuifanikisha?

Hivi karibuni kafanya ziara katika kata zinazoongozwa na madiwani wa chama chake akawa mara wamkamate mara wamzuie mradi tu kumwakamisha.Sasa mnadhani tutaendelea kwa style hii?
Sasa Siasa za kugombanisha wananchi na Serekali ndio siasa gani. Hawa wazungu kutuletea vyama vingi kwa Africa bado hatujaelewa. Nilitembelea Sweden na kwenda kwenye Serekali za Mitaa- jamani Rais Magufuli najua unapata taarifa mbalimbali kutoka mitandaoni. Tafadhali tenga kiasi cha pesa uwapeleke Chama Tawala na apinzani Nchini Sweden wakajifunze maana ya Vyama vya upinzani. Wao wanakueleaza mara tu baada ya Uchaguzi focus ni kumletea Mwananchi maendeleo na siyo kutamba kwenda kupeleka sumu kwa wananchi no way! Nami nikiri kuna Halmashauri nitaitaja moja , Bunda yenyewe ilikuwa inaendasha Halmashauri yao kwa misingi kuwa baada ya uchaguzi ni maendelea ya wananchi bila kujali itikadi za Chama. Pamoja na kuwa qwajumbe wa CCm walikuwa wengi kulik wa Upinzani. Kulikuwa hakuna eti mpinzani anatoka kwenda kuwaeleza eti CCM haihamasisha wananchi kulima Mawese. Shame on you ZITTO, ni lini ulitetea kiwanda cah kusindika mawese??? je unahamasishaje wananchi wa Kigoma ( mwenye datata za uchangiaji wa pato la taifa la kigoma naomba data) kufanya kazi ili kujiletea maendeleo? aanzie na maeneo ya Ujiji.
 
Back
Top Bottom