Madafu yaendelea kuporomoka, leo yaanza kunusa 1,500 kwa US$1

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,182
307
Je hii maana yake nini?

Kwa wiki kadhaa sasa shiling ya Tanzania imeendelea kupoteza thamani ikilinganishwa na dollar ya Marekani kwa speed ambayo si ya kawaida. Mpaka mwishoni mwa mwaka jana US$1 ilikuwa inacheza kwenye Tshs 1,300 lakini leo hii US$1 inacheza kwenye Tshs 1,460 -1,500. Hii si habari njema sana kwa uchumi wetu kwa sababu kila kitu kitapanda ukizingatia kuwa vitu vingi vinaagizwa nje ya nchi kwa kutumia (mafuta, bidhaa nyingi za maisha ya kila siku).

Je hii ni dalili nyingine ya kushindwa kwa serikali ya Kikwete?
 
Dalili mbaya sana hii ndo maana fuel ni very expensive sasa.Tanzania zaidi ya uijuavyo, uchumi poromoka mbaya.Sielewi mkulu atasemaje kuhusu hili au bado maisha bora kwa kila mtanzania?
 
Ni hatari sana hii,
Na cha ajabu,ndani ya mwezi huu tu...ipanda zaidi ya30-50 shillings..hii ina maana gani jamani wanauchumi?
 
Kama umekuwa ukifuatilia miaka ya nyuma, hii ni hali ya kawaida kabisa kwani waagizaji/wawekezaji husita kuagiza kwa kuhofia pengine yanaweza kutokea machafuko nao wakapata hasara. Baada ya election hali inarudi kama kawaida
 
http://www.exchange-rates.org/history/TZS/USD/G/M
Chart.aspx

Chart.aspx


Hii sio dalili nzuri
 
Pamoja na kuelekea kwenye uchaguzi lkn hali imekuwa mbaya mno. Nadhani umefika wakati sasa ikafanyika intervention but with cautious. Kwanini?
Kwasababu kpimo chetu siku zoote kimekuwa ni US dollar lakini ukweli ni kwamba dollar imeregain chap chap hivi karibuni against almost all major currencies kwahiyo TSh haiwezi kufurukuta.
Lakini zipo hatua tunaweza kutumia km kuongeza dollar kwenye mzunguko (interventaion-forex quantitative easing) na kuzuia matumizi ya sarafu za kigeni nchini na huku tukijitahidi kuzalisha kwa wingi ili kupunguza kuagiza vitu nje.
 
Je hii maana yake nini?

Kwa wiki kadhaa sasa shiling ya Tanzania imeendelea kupoteza thamani ikilinganishwa na dollar ya Marekani kwa speed ambayo si ya kawaida. Mpaka mwishoni mwa mwaka jana US$1 ilikuwa inacheza kwenye Tshs 1,300 lakini leo hii US$1 inacheza kwenye Tshs 1,460 -1,500. Hii si habari njema sana kwa uchumi wetu kwa sababu kila kitu kitapanda ukizingatia kuwa vitu vingi vinaagizwa nje ya nchi kwa kutumia (mafuta, bidhaa nyingi za maisha ya kila siku).

Je hii ni dalili nyingine ya kushindwa kwa serikali ya Kikwete?

Ni kweli kama export of goods imeshuka ambayo ni chanzo cha foreign currency specifically USD, while imports of goods which is the source for spending USD abroad, ni wazi kutakuwa na Increase in demand for USD locally ultimately will lead into high price of dollar (high exchange rate).

Another source huenda kuna movement of our forex into foreign banks kwa njia za kifisadi na kuacha ombwe, ila pia inawezekana BOT wamezuia ku-release USD in the locala market kwa sababu wanazozijua wao. Huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo tutarajie low foreign investments flowing in Tanzania and sometime even movement of capital outside due to the fear of election chaos. Unajua ni hatari sana kuuweka uchumi mikononi mwa wageni ambao wakati wa amani wanachuma na kutunyonya, inapokaribia wakati wa uchaguzi wanahofia vurugu na kukimbiza mitaji yao nje.

Ila hii yote inasababishwa na sera za CCM za kutopunguza politcal risks kwa Investors kwa kuonesha kuwa watatenda haki katika uchaguzi na hivyo possibility of political chaos will be low. Matendo kama kukatalia baadhi ya vyama usajili wa kudumu, kupiga danadana kesi ya mgombea binafsi, kutokuwepo tume huru ya uchaguzi; hivi vyote ni viashiria vya kutokuwepo free and fair election which might lead into political violence afterwards.
 
Ni kweli kama export of goods imeshuka ambayo ni chanzo cha foreign currency specifically USD, while imports of goods which is the source for spending USD abroad, ni wazi kutakuwa na Increase in demand for USD locally ultimately will lead into high price of dollar (high exchange rate).

Another source huenda kuna movement of our forex into foreign banks kwa njia za kifisadi na kuacha ombwe, ila pia inawezekana BOT wamezuia ku-release USD in the locala market kwa sababu wanazozijua wao. Huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo tutarajie low foreign investments flowing in Tanzania and sometime even movement of capital outside due to the fear of election chaos. Unajua ni hatari sana kuuweka uchumi mikononi mwa wageni ambao wakati wa amani wanachuma na kutunyonya, inapokaribia wakati wa uchaguzi wanahofia vurugu na kukimbiza mitaji yao nje.

Ila hii yote inasababishwa na sera za CCM za kutopunguza politcal risks kwa Investors kwa kuonesha kuwa watatenda haki katika uchaguzi na hivyo possibility of political chaos will be low. Matendo kama kukatalia baadhi ya vyama usajili wa kudumu, kupiga danadana kesi ya mgombea binafsi, kutokuwepo tume huru ya uchaguzi; hivi vyote ni viashiria vya kutokuwepo free and fair election which might lead into political violence afterwards.

Mkuu tuko pamoja, lakini kuna ukweli mwingine ambao inawezekana umefichika na haujauzungumzia hapo kwenye maelezo yako. Ukiangalia uchumi wa dunia kwa ujumla dola ya marekani kwa mwezi huu imepata nguvu za ajabu. Ukweli huu unaweza kuuona kwenye exchange rate ya dola dhidi ya Euro. Euro imepoteza nguvu kwa dola na leo BBC nimesikia wanasema bei za bidhaa kule marekani na hasa mafuta vimeshuka bei wakati bei ilibaki bila kubadilika for the past 13 months. Hivyo kuporomoka kwa shilingi dhidi ya dola kumechangiwa na mambo mengi zaidi ya tunavyofikiria.

Tiba
 
Wazuie matumizi ya dollar ndani ya nchi! Period

TRA wanacharge in terms of dollars, Hotels almost zote zinataka dollar, wafanyabiashara kariakoo wanatrade kwa dollar. Unategemea nn kwenye situations kama hizi! Na tusitegemee kwamba dollar itashuka, tukumbuke wafadhili wataacha kutusaidia kwenye budget ya mwaka ujao kwa kiwango tulicho tarajia, so tutakuwa na scarcity ya poreign currencies.

Government izuie matumizi ya dollar ndani ya nchi, pamoja na ubadilishaji holela wa shilling kwenda dollar! Tujifunze kutoka South Africa.
 
Wazuie matumizi ya dollar ndani ya nchi! Period

TRA wanacharge in terms of dollars, Hotels almost zote zinataka dollar, wafanyabiashara kariakoo wanatrade kwa dollar. Unategemea nn kwenye situations kama hizi! Na tusitegemee kwamba dollar itashuka, tukumbuke wafadhili wataacha kutusaidia kwenye budget ya mwaka ujao kwa kiwango tulicho tarajia, so tutakuwa na scarcity ya poreign currencies.

Government izuie matumizi ya dollar ndani ya nchi, pamoja na ubadilishaji holela wa shilling kwenda dollar! Tujifunze kutoka South Africa.

Mkuu, Notice in red, kwa kweli inashangaza TZ ilivyoachia mambo kiholela hasa kwenye exchage of currency, nchi zilizoendelea huwezi kukuta vioski vya kubadili fedha kama ilivyo TZ.

huu umbayuwayu sijui utaisha lini
 
Back
Top Bottom