Junior Lecturer
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 904
- 526
FUATILIA KISA HIKI CHA PATRICK.
Patrick Oita Nyapara police jamii nchini Kenya alimuua mpenzi wake kwa kumtandika Risasi 47 baada ya binti huyo kujifanya mjanja.
Kwa maelezo ya Patrick ni kwamba alimchukua mdada Christine Maonga kutoka ktk family duni iliyokuwa ikiishi kijijini na kumpeleka mjini Nairobi kama mke wake ambapo aliamua kumsomesha mpaka chuo kikuu.
Wakati akimlipia karo na mahitaji mengine Patrick alikuwa akituma pesa pia kwa mama mzazi wa binti huyo kama msaada kutokana na family hiyo kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha.
Baada ya kuhitimu masomo yake Christine alimwambia mpenzi wake kuwa amechoka kuwa naye kwani ni MTU asiyekuwa na hadhi yoyote na hafai kuwa mpenzi wake hivyo ni vyema kila MTU afanye mambo yake.
"Nimepata mpenzi mwingine ambaye ananifaa sana pia ni mkurugenzi wa kampuni moja kubwa sana jijini Nairobi hivyo siwezi kuwa na wewe Patrick MTU usiyekuwa na future na ni daraja D ambalo ni dhaifu kwangu" aliongeza Christine.
Patrick alichanganyikiwa sana akaamua kwenda kijijini kwa mama yake na Christine kuomba msaada wa suluhu ili aweze kumuoa binti yao kwani alikuwa ametumia gharama kubwa mno kumsomesha.
Mama yake binti alijibu kuwa hawezi kumpangia Mme wa kumuoa binti yake hivyo anapaswa aachwe ajiamlie yeye mwenyewe.
Patrick hakukubali akamtafuta Dada yake Christine na kumwelezea hali halisi lakini alijibiwa kuwa hana hadhi ya kumiliki mwanamke aliyehitimu chuo kikuu hivyo atafute wa level ya mgambo kama yeye.
Aliondoka na kurudi nyumbani kufanya uamzi mgumu wa kumuita Christine sehemu ya hotel au nyumbani, walikubaliana kukutana wayamalize na waachane kabisa na binti alienda nyumbani kwa Patrick mapema zaidi.
Alifika na kumkuta Patrick amejihami kama boko haram, hawakuzungumza chochote zaidi ya kumkandamiza risasi 47 na zote zikapita mwilini mwa Christine hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
Inauma lakini ndiyo hivyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Patrick Oita Nyapara police jamii nchini Kenya alimuua mpenzi wake kwa kumtandika Risasi 47 baada ya binti huyo kujifanya mjanja.
Kwa maelezo ya Patrick ni kwamba alimchukua mdada Christine Maonga kutoka ktk family duni iliyokuwa ikiishi kijijini na kumpeleka mjini Nairobi kama mke wake ambapo aliamua kumsomesha mpaka chuo kikuu.
Wakati akimlipia karo na mahitaji mengine Patrick alikuwa akituma pesa pia kwa mama mzazi wa binti huyo kama msaada kutokana na family hiyo kutokuwa na uwezo wa kumudu gharama za maisha.
Baada ya kuhitimu masomo yake Christine alimwambia mpenzi wake kuwa amechoka kuwa naye kwani ni MTU asiyekuwa na hadhi yoyote na hafai kuwa mpenzi wake hivyo ni vyema kila MTU afanye mambo yake.
"Nimepata mpenzi mwingine ambaye ananifaa sana pia ni mkurugenzi wa kampuni moja kubwa sana jijini Nairobi hivyo siwezi kuwa na wewe Patrick MTU usiyekuwa na future na ni daraja D ambalo ni dhaifu kwangu" aliongeza Christine.
Patrick alichanganyikiwa sana akaamua kwenda kijijini kwa mama yake na Christine kuomba msaada wa suluhu ili aweze kumuoa binti yao kwani alikuwa ametumia gharama kubwa mno kumsomesha.
Mama yake binti alijibu kuwa hawezi kumpangia Mme wa kumuoa binti yake hivyo anapaswa aachwe ajiamlie yeye mwenyewe.
Patrick hakukubali akamtafuta Dada yake Christine na kumwelezea hali halisi lakini alijibiwa kuwa hana hadhi ya kumiliki mwanamke aliyehitimu chuo kikuu hivyo atafute wa level ya mgambo kama yeye.
Aliondoka na kurudi nyumbani kufanya uamzi mgumu wa kumuita Christine sehemu ya hotel au nyumbani, walikubaliana kukutana wayamalize na waachane kabisa na binti alienda nyumbani kwa Patrick mapema zaidi.
Alifika na kumkuta Patrick amejihami kama boko haram, hawakuzungumza chochote zaidi ya kumkandamiza risasi 47 na zote zikapita mwilini mwa Christine hali iliyopelekea kifo chake papo hapo.
Inauma lakini ndiyo hivyo.
Sent using Jamii Forums mobile app