MADA YA WEEKEND: Wazee wa Dar na Benz la Mwinyi

Mama alishasema yeye na JPM ni kitu kimoja, tuendelee kuwa wavumilivu hadi tutakapo pata kitu kingine cha tofauti!.
Huyu ni mwana siasa sasa ulitegemea aseme mimi sio kama JPM? huyu alikuwa makamu wa Rais na alipigia kampeni sera za chama kwa kumsaidia JPM vipi aje amkane hadharani? Kweli unataka kuniambia unaamini kauli za mwanasiasa? Hadharani wanasema kingine faragha wanafanya vingine ndio hulka ya wanasiasa.
 
Utetezi wako umekuwa mdogo sana mkuu Heijah nadhani tuishie hapo although hakuna la maana katika kusadikisha ununuzi wa Benz, katiba na ustaafu.
 
Utetezi wako umekuwa mdogo sana mkuu Heijah nadhani tuishie hapo although hakuna la maana katika kusadikisha ununuzi wa Benz, katiba na ustaafu.
Mimi sina sababu yoyote ya kumtetea lakini pia nashangaa na chuki za watu kwa mzee utasema kana kwamba sababu ya kupewa benzi basi ndio chanjo za umaskini wetu kukosa hosptial za kutosha maji safi na mengine sababu ya benzi hii aliyopewa mzee wakati tuna miaka 60 ya uhuru. Kuna budget ya Billion 9 kila mwaka inapitishwa kuwatunza wastaafu hau haipiti huko bungeni tunakuja kugombana baada ya matokeo. 9 billion kila mwaka inatengwa sasa kama wametoa Million 200 shida nini.
 
Wamempa gari mtu asiyehitaji gari, yaani hata mwanae Rais wa Znz angeweza mmnunulia gari , ila wale wazee walikuwa wanahitaji wamepewe hata elfu 30 tu kwa mwezi wametoswa
Ndiyo hapo ujue kuna wenye nchi na wananchi
 
kichoniuma zaidi ni kuahirishwa mechi ya simba na yanga, nilikaa na mwanangu nikamsimulia mambo mengi sana hasa enzi za kina edo, masatu, mogela, mkapa, athuman, runyamila, nakadhalika. enzi hizo za UNO & Taifa Kubwa... ALAFU GHAFLA OLA kisa babu anatoa kitabu kinachouzwa 75,000. Mshahara wa mlinzi wa mwezi mzima.
 
Tofauti ni moja wale ni wananchi wa kawaida walioenda kumsikiliza rais... Na yule ni rais mstaafu mwenye mtoto rais, aliyeenda kuzindua kitabu cha maisha yake
Kila mmoja hapo anakula kwa urefu wa kamba yake..
Hivi kwa nchi za ulimwengu wa tatu,Kuna ufahari gani kuwapa viongozi wastaafu mali na ukwasi kiasi hicho wakati nchi ni maskini?
Kwanini kila Mbwa anayeingia Ikulu anataka kutuaminsha kwamba "it's on our own intellect,and it is good for us,we normal citizen"kwamba kugawa majumba na magari ya kifahari kwa hawa wastaafu
 
Hivi kwa nchi za ulimwengu wa tatu,Kuna ufahari gani kuwapa viongozi wastaafu mali na ukwasi kiasi hicho wakati nchi ni maskini?
Kwanini kila Mbwa anayeingia Ikulu anataka kutuaminsha kwamba "it's on our own intellect,and it is good for us,we normal citizen"kwamba kugawa majumba na magari ya kifahari kwa hawa wastaafu
Nakuunga mkono kwa kila neno ulilosema katika bandiko lako, ila neno moja tu 'mbwa'. Ni utovu mkubwa wa nidhamu hasa hasa kwetu sisi Waafrika. Ungetumia tusi jingine la kiiungwana.
 
Nakuunga mkono kwa neno ulilosema katika bandiko lako, ila neno moja tu 'mbwa'. Ni utovu mkubwa wa nidhamu hasa hasa kwetu sisi Waafrika. Ungetumia tusi jingine la kiiungwana.
Niwie radhi mkuu,ulimi umetereza,
Machungu ya ndugu,mie nakula buku kwa siku,mwanangu anasoma kayumba,siijuhi kesho yake itakuwaje,harafu watu wanapeana mabenz tu,inauma mazee,tusameane tu
 
Hivi kwa nchi za ulimwengu wa tatu,Kuna ufahari gani kuwapa viongozi wastaafu mali na ukwasi kiasi hicho wakati nchi ni maskini?
Kwanini kila Mbwa anayeingia Ikulu anataka kutuaminsha kwamba "it's on our own intellect,and it is good for us,we normal citizen"kwamba kugawa majumba na magari ya kifahari kwa hawa wastaafu
Kama kuna mambo yanayotufanya waafrika kutakiwa kutawaliwa ni tabia na aina ya mfumo wa maisha tuliyonayo kupitia wanasiasa.

Kwanza hatuna sheria zenye nguvu kusimamia wanasiasa ndiyo maana mtu akishika shoka tu anafanya anachojua kazi ya shoka ni nini!.
 
Mzeee kapewa gari kwa shuguli za kiserkari Asa watu wanafula nn
Pia n blessing kuwa na kiongoz mkuu wa nchi kwa umri huu
Mwacheni mzee ale utulivu kwenye s class
 
Mzeee kapewa gari kwa shuguli za kiserkari Asa watu wanafula nn
Pia n blessing kuwa na kiongoz mkuu wa nchi kwa umri huu
Mwacheni mzee ale utulivu kwenye s class
Hizi akili hizi,kipindi fulani Wakenya walikuja juu pale wabunge wapya baada ya kuapishwa wakadai nyongeza ya mshahara..mbunge mmoja katika kutetea hayo madai yao akasema"Kenyans should be proud that they can pay that amount of salaries and others to their members of parliament"yaani wananchi wanatakiwa wajisikie furaha na ufahari kwamba kupitia Kodi zao wanaweza kuwalipa wabunge mishahara minono na marupurupu mengine,.
Kwa nchi ilipo sasa,mama mwenyewe kasema uchumi umeshuka,sasa inakuaje ni kipaumbele kumnunulia Raisi mstaafu gari la kifahari?
Alichotakiwa kufanya ni kupunguza ukubwa na matumizi ya Serikali,
Mwinyi analipwa mshahara,anapewa ulinzi,ana majumba kibao mengine inawezekana yalipstikana kwa wizi,huyu mtu ana ukwasi mkubwa tu,
Kweli mama akaona zawadi ya kuwapa wazee wa Dar ni kumzawadia gari ya millioni 450!
Pale Rwanda Nkurunzinza kabla hajafa,alitaka serikali imjengee hekalu kama Ikulu,likajengwa,akatunga sheria asishitakiwe,
Mungu mkubwa akafa.
Sasa huyu mama anatuchekea chekea huku akionyesha mahaba kwa hawa wastaafu,harafu anataka sie tupige makofi
 
Shida ni Kuwa ,serikali ya CCM wanakula nchi peke yao , saa mzee Mwinyi alikuwa na shida ya gari kweli?!
Kama shida ni kupanda gari wangemnunulia Lexus au Toyota Crown. Hilo benz halifai kwa barabara za kwenda Mkuranga Itabidi atumie ile ile V8!!
 
Hizi akili hizi,kipindi fulani Wakenya walikuja juu pale wabunge wapya baada ya kuapishwa wakadai nyongeza ya mshahara..mbunge mmoja katika kutetea hayo madai yao akasema"Kenyans should be proud that they can pay that amount of salaries and others to their members of parliament"yaani wananchi wanatakiwa wajisikie furaha na ufahari kwamba kupitia Kodi zao wanaweza kuwalipa wabunge mishahara minono na marupurupu mengine,.
Kwa nchi ilipo sasa,mama mwenyewe kasema uchumi umeshuka,sasa inakuaje ni kipaumbele kumnunulia Raisi mstaafu gari la kifahari?
Alichotakiwa kufanya ni kupunguza ukubwa na matumizi ya Serikali,
Mwinyi analipwa mshahara,anapewa ulinzi,ana majumba kibao mengine inawezekana yalipstikana kwa wizi,huyu mtu ana ukwasi mkubwa tu,
Kweli mama akaona zawadi ya kuwapa wazee wa Dar ni kumzawadia gari ya millioni 450!
Pale Rwanda Nkurunzinza kabla hajafa,alitaka serikali imjengee hekalu kama Ikulu,likajengwa,akatunga sheria asishitakiwe,
Mungu mkubwa akafa.
Sasa huyu mama anatuchekea chekea huku akionyesha mahaba kwa hawa wastaafu,harafu anataka sie tupige makofi
Nmekuelewa ila kumbuka mzee mwinyi anapewa huduma kama ex president so bado n sawa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom