MADA: Tatizo la Watoto kuchelewa kuongea. Ni kipi chanzo chake? Je, nawezaje kutatua tatizo hili?

Kama anachelewa ila mwisho wa siku anaongea, sioni tatizo kivile.
Umeisoma makala yote? Mtoto anayechelewa kuongea huwa katika hatari ya kuwa nyuma katika kila kitu. Nimesaidia watoto wa namna hiyo, kama haujawahi kusaidia wala kuwa na mtoto wa namna hiyo unaweza usione uzito wa tatizo. Usipende kurukia hitimisho rahisi kwenye matatizo sensitive kama haya kwani kuna wazazi hawalali kisa matatizo kama haya.
 
Hapo kwenye tv Ni vp mmana mtoto nahc watoto wengi hasa wa mjini huwa wanashinda kwenye tv
 
Umeisoma makala yote? Mtoto anayechelewa kuongea huwa katika hatari ya kuwa nyuma katika kila kitu. Nimesaidia watoto wa namna hiyo, kama haujawahi kusaidia wala kuwa na mtoto wa namna hiyo unaweza usione uzito wa tatizo. Usipende kurukia hitimisho rahisi kwenye matatizo sensitive kama haya kwani kuna wazazi hawalali kisa matatizo kama haya.
Mbona umepaniki kiasi hiki? Hujiamini? Sijatukana, sijatumia maneno makali. Tatizo nini mkuu? Naona dalili za ulichelewa kuongea wewe mpaka unafika ukubwani. Sasa uzi wako una maana.
 
Hapo kwenye tv Ni vp mmana mtoto nahc watoto wengi hasa wa mjini huwa wanashinda kwenye tv
TV inarudisha sana maendeleo ya ukuaji wa ubongo wa watoto. Nimefanya diagnosis kwa watoto wengi wenye tatizo hili, chanzo kwa wengi nimebaini ni TV. Nitaandika makala juu ya hili nikipata wasaa.
 
Mbona umepaniki kiasi hiki? Hujiamini? Sijatukana, sijatumia maneno makali. Tatizo nini mkuu? Naona dalili za ulichelewa kuongea wewe mpaka unafika ukubwani. Sasa uzi wako una maana.
Sijapaniki, ni ngumu kupaniki kwa jambo dogo kiasi hicho. Nimeonesha msisitizo tu. Umeonesha mzaa kwenye jambo ambalo hauna uelewa nalo. Kuna wengine huwa hadi mabubu kwa kuchelewa kuongea tu, bila ya kutafutiwa tiba mapema.
 
Nilitegemea mtoa mada utaweka na solution ya tatizo hili matokeo yake umekuwa sawa na wale wapiga ramli


Sent using IPhone X
 
Nilitegemea mtoa mada utaweka na solution ya tatizo hili matokeo yake umekuwa sawa na wale wapiga ramli


Sent using IPhone X
Naandika mara kwa mara hapa. Nitaandika juu ya suluhisho muda ujao. Ninaenda kuedit hitimisho ili watu wajue kuwa nitaandika wakati ujao. Japo napendekeza utumie lugha nzuri, hakukuwa na haja ya kejeri. Tumia lugha nzuri muda ujao kama ipo kwenye sehemu ya maadili yako.
 
Cha muhimu ni kucheza,kuimba na kuongea na mtoto. Pia ita watoto wengine wacheze nae chini ya uangalizi.
Nishaona mtoto wa miezi 10 anasema neno "baba", "mama" pia anaelewa ukimwambia lala,kula, piga makofi n.k.
Mtoto akiwa na utimamu wa afya ya mwili na akili akifika kuanzia miezi 7 cheza,imba naye.
 
Mtoto wangu wa miaka 4 na miezi 6 bado hajaongea mpaka leo ila kila kitu ukimtuma analeta na anakijua na pia hawezi kutulia kwa sehemu moja kwa mda. Je kwa mtoto kama huyu anahitaji msaada gani?

Kwa muda wote amekuwa akiudhuria mazoezi kwenye hospital Kadhaa na pia kuonana na doctor bingwa wengi.

Je, unaweza nisaidia au kunishauri hapo ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto wangu ana miaka mitatu na nusu lakin kupangilia sentens hayuko vizuri,ndio hao wanaosema nkate badala ya mkate, had vitoto vya miaka miwili vimemzidi

Ila kwny kuandika na kuhesabu anavikalisha vitoto vyote vya mtaani, yan anacatch haraka sana vitu akifundishwa

Kuna mwalimu huwa anajitolea kufundisha watoto hapa mtaan na amesema mtoto wangu ndo anaecatch vitu haraka sio wale wengine waliomzid kuongea



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto wangu yeye ana miezi 17,akitAKa kitu anakushika mkono anakuvuta mpaka kilipo kitu anachokihitAji kama anataka maji atakupelekA kwenye ndoo yA maji, na akitaka kunyonya anakuvutA mpaka kwenye kiti ili ukae anyonye .
 
Mtoto Wa mdogo wangu alichelewa kuongea, na vile ninavyompenda jamani nikawa nahisi kulia. Siku moja mama yake akanipigia "chu..." Kaongea dah nilifurahi, alianza na neno baba akiwa na umri wa miaka 3.

Ndani ya miezi mi 3 ali develop Maneno mengi zaidi, mama, Dada, bibi etc, ila Maneno mengi alikuwa anayatamka tofauti, eg, ajiwa= majiwa, sasa= Chacha, chikamo= shikamoo, bali= wali, Dage= maharage, danga=Karanga, jaji=Maji, Chule= shule chimu=simu etc
Ndani ya miezi sita alianza kuongea sana mpaka tunashangaa, akawa anaongea kila kitu as if analipiza muda ambao hakuongea.

Mtoto alikuwa mchanganfu kila mtu akawa anatamani ambebe. Ni wa kike lakini anapendwa na jinsia ya kiume mpaka basi, kila mwanaume umsalimia chikamoo baba.😁 nadhani kwakuwa neno la kwanza kutamka lilikuwa baba ndo maana anapendwa na jinsia ya me.

Kuna kipindi alikuja kukaaa na mm, wakaka wa huku wote wakitoka kazini anawapokea getini, wote anawaita baba😀 ananiomba simu awapigie 😁 hawajui majina, ila anajua vyumba vyao, anaita baba wa kule, anawapigia simu, anawambia, " nimewamichii"😀
Wanamletea jawadi😁.

Kwa sasa anaongea utadhani anachoma taarifa ya habari, ana miaka chita, anachoma daracha la kwanja.😀😀😂
 
Back
Top Bottom