FrankMakeps
Member
- Apr 1, 2013
- 93
- 70
Yapo mwaka wa pili huu km co wa tatuNi machimbo mapya haya nadhani
Yapo mwaka wa pili huu km co wa tatuNi machimbo mapya haya nadhani
Mkuu Mshana Jr kuna hii connection ya madereva ambao wanaweza kufika hapo Soga Kibaha leo au kesho waende fasta. (See the attachment)Habarini wana jumuiya kubwa ya JamiiForums,
Ni wakati sasa wa kuwa na mada yetu maalum kwa kaliba hii kubwa na pana yenye dhamana adhimu ya kuhakikisha tunasafiri na kufika tuendako salama iwe:
Ni kaliba hii adhimu pia yenye dhamana kubwa ya kufikisha salama mizigo na vifurushi vyetu vyote vya kibiashara, kikazi nknk
- Makazini
- Kwenye starehe
- Kwenye dharura
- Kutembeleana nknk
Mada hii maalum ni jumuishi ya:
Mada hii ni maalum pia ya kusimuliana changamoto mbalimbali za barabarani kuanzia vibali, uendeshaji mbovu, ushirikina, maafisa usalama, mamlaka zenye dhima na usafiri nk.
- Madereva wa magari makubwa na madogo ya mizigo
- Madereva wa boda to boda
- Madereva wa magari yote ya abiria
- Madereva wa viongozi, matajiri na watu maarufu
- Madereva wa mitambo
- Madereva bajaj bodaboda wote kwa ujumla wao
- Na mwisho kabisa madereva wa magari binafsi
Kuna ishu ya uzoefu pia ambayo tunaweza kushirikishana hapa ili kupata uzoefu incase likitokea la kutokea ujue jinsi ya kukabiliana nalo
Hakuna mahali hapakosi vituko na vibweka. Kwenye hii kaliba pana ya usafiri vipo vya kutosha. Je, una kituko chochote? Huu ni uwanja wako sasa.
La mwisho lakini ambalo si la mwisho kabisa ni swala zima la kupeana connection. Madereva wazoefu na wazuri ni wengi mno lakini shida inakuja kwenye ajira. Kupitia mada hii nina HAKIKA TUNAWEZA KUPEANA SHAVU LA AJIRA
Ni mada pana na yenye ulingo mpana sana. Kuna mengi ambayo sijaandika hapa. Naomba ushiriki wenu kwa yale niliyosahau.
Dondoo baadhi za uzoefu wangu kwenye udereva
Tutazidi kushirikina mengi kadiri mada itakavyokuwa inaendeleea, na hata kama kuna links za kazi za udereva tutapeana hapa
- Nidhamu barabarani huepusha ajali nyingi
- Barabarani derava hapaswi kuwa na maamuzi mawili kwa wakati mmoja
- Muda wote ni dereva anapokuwa kwenye usukani ni lazima macho yake yaone sekunde 15 mbele toka alipo
- Inapotokea dharura ya pancha si vema kufunga breki ghafla
- Muhimu muda wote kusoma taa za tahadhari kwenye dashboard
Nitangulie kuwatakia maandalizi mema ya sikukuu za mwisho wa mwaka.
Kwa madereva wenzangu tuna DHIMA kubwa ya kuzivusha salama mwaka huu roho za mamilioni ambazo ni ndugu jamaa marafiki na wanadamu wenzetu.
Sent from my Infinix X627 using JamiiForums mobile app
PoapoaNaamini halishindikani jambo wadau.View attachment 1715690
Hivi sisi waendesha baiskeli sio madereva? Kiukweli tunanyanyasika sana barabarani!
Bila shaka hapa crt chalinze ndio mkosaji.Mwidu moya iyoView attachment 1743171