Toosweet
JF-Expert Member
- May 27, 2012
- 2,141
- 1,982
Kwenu,
Hii ni mada iliyochochewa na kauli ya Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kwamba kuwe na mjadala kuhusu Elimu ili kuinusuru.
Kati ya walioko mezani ni waalimu Dr. Kalaghe na Prof. Rwaitama.
Prof Rwaitama;
Wakati wa Mwalimu kulikuwa na falsafa iliyoongoza elimu ambayo ni Elimu ya Kujitegemea. Elimu ya msingi ilikuwa lazima na ilitolewa bure, ukiikosa unapata Elimu ya Watu wazima.
Matatizo ya elimu yetu yako katika maeneo matatu,
Mitaala
Ushindani
Usimamizi na kugharimia Elimu.
Kwa sasa hakuna mtaala rasmi. Kila mwalimu anatumia kitabu chake. Mitaala inabadilishwa bila kushirikisha wadau na ikibadilika vitabu havipatikani au havipatikani kwa wakati. Walimu hawapati semina za kuwanoa.
Kila Waziri wa Elimu anafanya mabadiliko ya kimfumo kwa kutoa hiki na kuingiza kile bila sababu za msingi.
Imethibitika kuwa wanafunzi wetu wanaomaliza vyuoni hawana uwezo wa kushindana na wenzao wa nchi jirani au wa nje. Wahitimu hawawezi kujiajiri kwa kuwa wamefundishwa kuajiriwa. Waajiri wanabainisha kuwa vyuo havizalishi wahitimu kulingana na mahitaji ya soko.
Wahitimu wa vyuo hawawezi kujieleza.
Mwalimu ana msururu wa mabosi, kuanzia Mratibu Elimu Kata hadi Mkuu wa Mkoa.Walimu hawakaguliwi, hawapewi stahiki kwa wakati.
Walimu wetu si mahiri. Wanatokana na waliofeli kidato cha nne.
Muda wa ku-train walimu umepunguzwa toka miaka minne hadi miaka mitatu. Hii imepunguza au kuondoa muda wa mazoezi kwa vitendo kwa walimu na hata wakipata muda wa mazoezi hakuna wasimamizi wenye taaluma inayoendana na masomo yanayofanyiwa mazoezi.
Dr.Kahyarara,
Ripoti ya World Bank ilionesha kuwa 20% ya walimu waliopimwa hawakupata 80% ya alama ambayo ndiyo ilikuwa minimum. Vilevile walimu wanatumia nusu tu ya muda unaotakiwa kutumika.
Ili kupambana na changamoto za elimu tunatakiwa kutenga 20% ya bajeti kwenye elimu. Bajeti ya elimu imeshuka hadi 15% mwaka 2017,toka 16% mwaka 2016,toka 17% mwaka 2015.
Toka Serikali itangaze kufuta michango primary na secondary, wazazi wameacha kuchangia chakula. Kufuta michango kumeongeza idadi ya wanaojiunga na shule.
Somo la TEHAMA halifundishiki kwenye mazingira ya shule zetu. Linahitaji vitendo, hakuna umeme wala walimu wenye ujuzi.
Hizi ni baadhi ya dondoo.
Karibuni.
Hii ni mada iliyochochewa na kauli ya Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kwamba kuwe na mjadala kuhusu Elimu ili kuinusuru.
Kati ya walioko mezani ni waalimu Dr. Kalaghe na Prof. Rwaitama.
Prof Rwaitama;
Wakati wa Mwalimu kulikuwa na falsafa iliyoongoza elimu ambayo ni Elimu ya Kujitegemea. Elimu ya msingi ilikuwa lazima na ilitolewa bure, ukiikosa unapata Elimu ya Watu wazima.
Matatizo ya elimu yetu yako katika maeneo matatu,
Mitaala
Ushindani
Usimamizi na kugharimia Elimu.
Kwa sasa hakuna mtaala rasmi. Kila mwalimu anatumia kitabu chake. Mitaala inabadilishwa bila kushirikisha wadau na ikibadilika vitabu havipatikani au havipatikani kwa wakati. Walimu hawapati semina za kuwanoa.
Kila Waziri wa Elimu anafanya mabadiliko ya kimfumo kwa kutoa hiki na kuingiza kile bila sababu za msingi.
Imethibitika kuwa wanafunzi wetu wanaomaliza vyuoni hawana uwezo wa kushindana na wenzao wa nchi jirani au wa nje. Wahitimu hawawezi kujiajiri kwa kuwa wamefundishwa kuajiriwa. Waajiri wanabainisha kuwa vyuo havizalishi wahitimu kulingana na mahitaji ya soko.
Wahitimu wa vyuo hawawezi kujieleza.
Mwalimu ana msururu wa mabosi, kuanzia Mratibu Elimu Kata hadi Mkuu wa Mkoa.Walimu hawakaguliwi, hawapewi stahiki kwa wakati.
Walimu wetu si mahiri. Wanatokana na waliofeli kidato cha nne.
Muda wa ku-train walimu umepunguzwa toka miaka minne hadi miaka mitatu. Hii imepunguza au kuondoa muda wa mazoezi kwa vitendo kwa walimu na hata wakipata muda wa mazoezi hakuna wasimamizi wenye taaluma inayoendana na masomo yanayofanyiwa mazoezi.
Dr.Kahyarara,
Ripoti ya World Bank ilionesha kuwa 20% ya walimu waliopimwa hawakupata 80% ya alama ambayo ndiyo ilikuwa minimum. Vilevile walimu wanatumia nusu tu ya muda unaotakiwa kutumika.
Ili kupambana na changamoto za elimu tunatakiwa kutenga 20% ya bajeti kwenye elimu. Bajeti ya elimu imeshuka hadi 15% mwaka 2017,toka 16% mwaka 2016,toka 17% mwaka 2015.
Toka Serikali itangaze kufuta michango primary na secondary, wazazi wameacha kuchangia chakula. Kufuta michango kumeongeza idadi ya wanaojiunga na shule.
Somo la TEHAMA halifundishiki kwenye mazingira ya shule zetu. Linahitaji vitendo, hakuna umeme wala walimu wenye ujuzi.
Hizi ni baadhi ya dondoo.
Karibuni.