Macron yuko China kuishinikiza kusaidia amani nchini Ukraine

HERY HERNHO

Member
Mar 4, 2022
70
313
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu nchini China ambako pamoja na mengineyo analenga kulishawishi taifa hilo mshirika wa Urusi, kusaidia juhudi za kuleta amani katika mzozo wa Ukraine.


65223510_803.jpg

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aidha anataraji kuirai China kuacha kuisaidia Urusi kwa silaha. Macron yuko China wakati rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akiwa nchini Poland kwa ziara rasmi ya kikazi kwa mshirika wake huyo ambaye amesaidia pakubwa kuyahamasisha mataifa ya magharibi kumsaidia jirani yake kijeshi na hata kisiasa.

Rais Emmanuel Macron amesema mapema leo akiwa Beijing kwamba taifa hilo lina nafasi kubwa ya kufungua njia ya kupatikana kwa amani nchini Ukraine kutokana na uhusiano wa karibu uliopo kati yake na Urusi, ingawa ameonya kwamba Urusi haipaswi kupewa fursa ya kuwa na majadiliano ya kina na taifa hilo. Amesema hayo katika hotuba yake ya kwanza tangu alipowasili China kwa ajili ya ziara hiyo, alipokutana na raia wa Ufaransa, katika mji mkuu Beijing. Amesema Ufaransa inaweza pia kuwa sehemu ya jukumu hilo la kupatikana kwa amani na utulivu.

"Vita hivi ambavyo nimekuwa nikivieleza mara kwa mara kuwa ni vya kibeberu na kikoloni, vimekiuka misingi mingi ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Hivyo China, haswa kwa sababu ya uhusiano wake wa karibu na Urusi, ambao umethibitishwa tena katika siku za hivi karibuni, inaweza kuwa na jukumu

Na taarifa kutoka Berlin zinasema kaimu kansela wa Ujerumani Robert Habeck kwa mara nyingine amelikumbusha taifa hilo kujua ukomo wake katika kuisaidia Ukraine, akionya halipaswi kuwa sehemu ya mzozo. Amesema hayo kabla ya kurejea nyumbani akitokea Kyiv alikokuwa kwa ziara ya siku mbili.
 
Hapo unaposema eti Macron ameenda "kuishinikiza" China kuhusu amani ya Ukraine unakuwa unakosea.

China wameshaweka mezani "12 Point Peace Proposal" ambayo hao EU wameishia kuitolea macho tu na kukaa kimya na US kusema hataki amani.

Huyo Macron anatakiwa aende kule USA kumshinikiza Biden kuhusu Peace na sio kwenda China.
 
Sidhani kama Ziara yake itafanikiwa kwa hili! Kwa sasa katika mabadiliko ya dunia yanavyoshika kasi kutoka Unipolar kwenda Multipolar,adui wa Russia ni adui wa China,na adui wa China ni adui wa Russia! Leo vita ikitokea kati ya China na Taiwan,Ufaransa atakuwa upande wa Taiwan.
Anyway hatujui huenda ziara yake ikawa na mafanikio!
 
China siyo tz,chumi za west na china zinavyotegemeana ni ngumu kuweka hivyo vikwazo vya kuumiza bila kujiumiza wenyewe
Waambie hao

UN regular budget 2023:

USA 🇺🇸 (22% of the UN budget),
China 🇨🇳 (15.25%),
Japan 🇯🇵 (8.03%) and
Germany 🇩🇪 (6.11%)

– together finance some 51% of the entire UN budget.

Source: UN
 
Sidhani kama Ziara yake itafanikiwa kwa hili! Kwa sasa katika mabadiliko ya dunia yanavyoshika kasi kutoka Unipolar kwenda Multipolar,adui wa Russia ni adui wa China,na adui wa China ni adui wa Russia! Leo vita ikitokea kati ya China na Taiwan,Ufaransa atakuwa upande wa Taiwan.
Anyway hatujui huenda ziara yake ikawa na mafanikio!
upo sahihi kabisa na rais wa Taiwan ameitembelea Marekani wakati China hataki kusikia kitu kama hicho

Kwa hali hiyo tusitegemee onyo ama karipio lolote kutoka China kwenda Russia kwa sababu ya ukaribu wa Marekani na Taiwan

Zaidi tutegemee vifaa vya kivita kutoka China kwenda Russia
 
Sidhani kama Ziara yake itafanikiwa kwa hili! Kwa sasa katika mabadiliko ya dunia yanavyoshika kasi kutoka Unipolar kwenda Multipolar,adui wa Russia ni adui wa China,na adui wa China ni adui wa Russia! Leo vita ikitokea kati ya China na Taiwan,Ufaransa atakuwa upande wa Taiwan.
Anyway hatujui huenda ziara yake ikawa na mafanikio!
Paris: Mwambie rafiki yako akae mezani tumwachie maeneo yake ya historia.

Beijing: Jamaa amekereka na hatua zenu za kusaidia silaha Kiev na sasa nina uhakika anaenda kuchukua eneo lote la Ukraine.
 
Back
Top Bottom