Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Viwango vya ukandamizaji wa kisiasa na kijamii vimekua vikubwa zaidi katika awamu hii kuliko awamu yeyote ile katika uongozi wa Tanzania.
Niseme tu, yametosha machozi yaliyomwagika kwaajili ya maziwa yaliyomwagika!
Tunahitaji kufanya jambo!
Tufanye nini?
Wanaosota rumande ni ndugu zetu.
Wanaozunguka mahakamani kila leo ni jamaa zetu.
Walioko jela na waliopotea ni washkaji zetu.
Na waliopigwa risasi pia, wote ni ndugu, ndugu katika mapambano lakini zaidi ndugu katika maendeleo na hatuwezi kuwatupa.
Ukimya wetu ni usaliti kwao na kulalamika kwetu sio heshima stahiki kwa hao waliojitoa sadaka kupigana mstari wa mbele!
Nimesikitika kusoma eti Ndugu yetu Lema hajui tufanye nini?
Lema usifanye chochote, wewe Ongoza!
Tumia karama yako ya kuongoza utuongoze kupaza sauti na kujibu vitendo vyote vya kihuni vinavyofanywa kuinajisi demokrasia yetu.
Lazima maandamano ya kisiasa yawepo, Lazima maandamano ya kijamii yawepo!
Lazima vyama vya wafanyakazi vishiriki kupaza sauti juu ya uhujumu wanaofanyiwa.
Kwanza kabisa lazima watu wapewe ujasiri wa kufungua midomo kabla ya mikono ili baadae wawe na ujasiri wa kutumia mikono.
Haitakuwa kwa maandamano ya siku moja.
Na haitakuja bila sadaka.
Hakuna lelemama kwenye kutafuta haki!
Niseme tu, yametosha machozi yaliyomwagika kwaajili ya maziwa yaliyomwagika!
Tunahitaji kufanya jambo!
Tufanye nini?
Wanaosota rumande ni ndugu zetu.
Wanaozunguka mahakamani kila leo ni jamaa zetu.
Walioko jela na waliopotea ni washkaji zetu.
Na waliopigwa risasi pia, wote ni ndugu, ndugu katika mapambano lakini zaidi ndugu katika maendeleo na hatuwezi kuwatupa.
Ukimya wetu ni usaliti kwao na kulalamika kwetu sio heshima stahiki kwa hao waliojitoa sadaka kupigana mstari wa mbele!
Nimesikitika kusoma eti Ndugu yetu Lema hajui tufanye nini?
Lema usifanye chochote, wewe Ongoza!
Tumia karama yako ya kuongoza utuongoze kupaza sauti na kujibu vitendo vyote vya kihuni vinavyofanywa kuinajisi demokrasia yetu.
Lazima maandamano ya kisiasa yawepo, Lazima maandamano ya kijamii yawepo!
Lazima vyama vya wafanyakazi vishiriki kupaza sauti juu ya uhujumu wanaofanyiwa.
Kwanza kabisa lazima watu wapewe ujasiri wa kufungua midomo kabla ya mikono ili baadae wawe na ujasiri wa kutumia mikono.
Haitakuwa kwa maandamano ya siku moja.
Na haitakuja bila sadaka.
Hakuna lelemama kwenye kutafuta haki!