Fantastic Beast
Member
- Feb 18, 2019
- 50
- 532
Kwanza naomba nianze kwa kumpa pole Dkt. Philip Mpango kwa kupambania afya yake kwa hizo wiki 2. Mungu amjalie apone kabisa mapema ili aweze kujumuika na familia yake.
Tukirudi kwenye mada, kwanza kama hujaitazama ile interview nenda youtube ukaitazame ndipo urudi hapa kuendelea kusoma. Kama haujaumwa au haujamuona anayeumwa hii nimonia kali tuliyonayo kwa sasa unaweza usielewe ukatili wa kirusi cha corona.
Tumshukuru Dr Mpango kwa kufanya ile press conference,nadhani sasa watu wataelewa na wote tutazingatia njia za kujikinga na hiki kirusi. Waziri ametoa chozi hadharani sio kwa sababu nyingine bali ni kwa sababu ameponea chupuchupu. Hii nimonia kali haifai kabisa, omba isikukute.
Machozi ya Dr Mpango yawaamshe usingizini viongozi wetu na wajue kwamba this life is precious to everyone, hakuna asiyependa kuendelea kuishi, kila uhai unatakiwa kuthaminiwa na kupewa ulinzi wa hali ya juu. Hivyo wachukue hatua sahihi zinazohakikisha kila mtu analindwa na hatari yoyote.
Dr Mpango amesema alikuwa anaishi kwa mtungi wa oksijeni nyumbani. Baadaye akahamishiwa hospitalini ambako amekaa kwa wiki 2 akipumulia oksijeni. Sasa tujiulize ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kununua mitungi ya oksijeni na kukaa nayo nyumbani pindi wanapoumwa?
Ni wachache sana hata asilimia 1 haifiki. Kwa muktadha huo njia rahisi na nyepesi ya kuepuka kufika huko ni kwa kuchukua tahadhari. Kinga siku zote huwa ni cheap kuliko tiba.
Tukirudi kwenye mada, kwanza kama hujaitazama ile interview nenda youtube ukaitazame ndipo urudi hapa kuendelea kusoma. Kama haujaumwa au haujamuona anayeumwa hii nimonia kali tuliyonayo kwa sasa unaweza usielewe ukatili wa kirusi cha corona.
Tumshukuru Dr Mpango kwa kufanya ile press conference,nadhani sasa watu wataelewa na wote tutazingatia njia za kujikinga na hiki kirusi. Waziri ametoa chozi hadharani sio kwa sababu nyingine bali ni kwa sababu ameponea chupuchupu. Hii nimonia kali haifai kabisa, omba isikukute.
Machozi ya Dr Mpango yawaamshe usingizini viongozi wetu na wajue kwamba this life is precious to everyone, hakuna asiyependa kuendelea kuishi, kila uhai unatakiwa kuthaminiwa na kupewa ulinzi wa hali ya juu. Hivyo wachukue hatua sahihi zinazohakikisha kila mtu analindwa na hatari yoyote.
Dr Mpango amesema alikuwa anaishi kwa mtungi wa oksijeni nyumbani. Baadaye akahamishiwa hospitalini ambako amekaa kwa wiki 2 akipumulia oksijeni. Sasa tujiulize ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kununua mitungi ya oksijeni na kukaa nayo nyumbani pindi wanapoumwa?
Ni wachache sana hata asilimia 1 haifiki. Kwa muktadha huo njia rahisi na nyepesi ya kuepuka kufika huko ni kwa kuchukua tahadhari. Kinga siku zote huwa ni cheap kuliko tiba.