Machinga waanza kunyanyaswa rasmi hawatakiwi huu si wakati wa wanyonge

Mwendazake aliwatumia Machinga kwa faida ya kujijenga kisiasa. Kwanza aliwaita wanyonge. Mnyonge naliona kama tusi kwa Watanzania. Tafsiri yake hii hapa:

1.mtu dhaifu; mtu asiyekuwa na nguvu Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni (ms) Synonyms: mnyela
2. mtu mwenye tabia ya upole na ya kunyenyekea
3. mtu wa hali ya chini Mnyonge kupata haki ni mwenye nguvu kupenda (methali)

Binafsi silipendi hili neno, tupaze sauti sauti wana siasa wasituite sisi wanyonge, watumie neno wananchi au Watanzania, waache kutusanifu.

Hao machinga, kuambiwa wafuate utaratibu wa mipango miji na Halmashauri siyo manyanyaso
 
Machinga kufanya biashara popote haikuwa solution ya muda mrefu bali ilikuwa opinion ya mtu mmoja na hakuna mtu anaishi milele ila systems zinaishi milele.

Nadhani department husika zitatafuta solution ya muda mrefu ili kutatua hiyo changamoto once and for all.

Suggestion yangu ni serikali itenge budget ya kujenga miondombinu bora kwenye maeneo maalum na hawa machinga wakafanye biashara zao huko.

Hiyo ndio best solution.
Machinga kukaa kwenye jengo ni ngumu sana! Kuna style moja niliona Moshi nafikiri ile ndio sahihi! Kunajengwa jengo kama mall kisha hao machinga wapange biashara zao humo kwa siku maalum ndani ya week!

Inajulikana kabisa ni sale!
 
Ndo maana sheria zikawepo,kama waliruhusiwa kufanya biashara popote mbona hawafanyii biashara zao ikulu au kwenye kambi za jeshi? Magufuli amekua Magufuli
 
Hili ni Eneo la Shule ya Sekondari Mabati Mjini Njombe ambako Meza za Wafanyabiashara wadogo (#Machinga) zimetupwa na Mgambo wa Halmashauri ya Mji huku wafanyabiashara hao wakitakiwa kuondoka pembezoni mwa Barabara na wahamie katika Soko la Dodoma.
Maskini baba aliwambia kufanya biashara popote pale jamani.

Haya mengine ni ya kutazama vyema jamani Mgambo tena wanarudi? jamani Rafiki wawamachinga Dah!!!! Leo Jpm angekuwepo Huki sijui mkuu wa MKOA mkuu wa wilaya MKURUGENZI wa halmashauri ANGEKUWA na hali gani aisee.

Kama uliona watu wanalia wanatandika nguo zao ili tu gari iliyobeba mwili wa Magufuli ipite juu ya nguo zao. Kitendo kile kilikuwa na maana ya pekee. Hiki ndicho hasa kilichokuwa #kikiwaliza msibani watanzania walijua siku za mateso #zinakaribia na sasa mateso ndiyo hayo.

#PUMZIKA kwa amani Magufuli wetu dah. Nimeandika hii msg nimehisi kutokwa na MACHOZI. Unavunjiwa banda lako ambalo ulikuwa umeweka nguvu zako huko kwa ajili ya watoto na maisha yaendelee.

KWELI ULE USEMI PAKA AKITOKA PANYA HUTAWALA NIMEAMINI SASA..View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457View attachment 1759457
Hao machinga wenyewe wachafuzi wa mazingira.Usijifanye unampenda hayati Magufuli.Mnatandaza bidhaa zenu sehemu za wapita kwa miguu,inawabidi wapite ndani ya barabara kuu ,watoto wa shule,na wengineo wanagongwa na magari,daladala,bodaboda n.k mmetandaa kote hadi mbele ya maduka na mahoteli ya walipa kodi.Waongo nyie.Hongera manispaa zinazofuata utaratibu wa kuwaondoa hao machinga mabarabarani.watengeeni maeneo maalum.Nchi lazima iwe safi na kwa mpangilio.sio kila mtu akiambiwa ukweli anajifanya mnyonge anaonewa.Nashauri Zoezi la kuwaondoa machinga mabarabarani na maeneo mengine yaendelee.Mfano nenda kituo cha mabasi cha Magufuli Mbezi,Yaani utasema nchi yetu haina serikali.Vurugu mtindo mmoja.wamachinga,mama lishe kibao.uchafu unaletwa na hao machinga.muda wowote magonjwa ya milipuko itatokea.Wamachinga,mama lishe watengewe sehemu maalum kama wenzetu wa nchi nyingine.
 
aiseh!

unajua, siku zote, wanaopiga kura kwa wingi nchini ni watu wasio kuwa na twitter, instagram ama account kwenye forums kama hapa jamii forums.

labda wengi wao wangekua kwenye hii mitandao ya jamii, tengepata mawili matatu!

pole yao!
 
Mbona umeweka picha hiyo hiyo moja mara nyingi hivyo? Naungana na serikali maana Jiwe aliwadanganya sana hawa Machinga, tunataka miji iwe safi bwana! Watu wanaangalia bidhaa mpaka mwenye maduka ya wenzao bwana, hapana hatuwezi kwenda hivyo!
Ningependa thge same ifanyike kwa miji yote nchini ikiwa ni pamoja na K/koo, Stand mpya ya mabus ya Mbezi Dar. Wamachinga waendeshe biashara zao kwa kufuata sheria zilizowekwa na mamlaka husika kwa usalama wao na muendelezo wa biashara zao.
 
Nilipita mitaa ya Posta ndani ya Dar Es Salaam, baadhi ya mitaa imeharibiwa kabisa na vibanda vya wamachinga. Yaani hakuna mpangilio wala sehemu ya wapita miguu. Ni kero kubwa sana, waondolewe na wapelekwe sehemu maalum ya kufanya biashara zao.
 
Wangeomba kwa baba hati miliki
Ila kwa kuwa zilikuwa kauli zake basi vumilieni tu wasafishe mji kwa sheria na kanuni badala ya neno la mtu mmoja
 
Wamachinga wangeweza kujipanga nchi nzima wawe na umoja wao,uongozi wao
Wangetisha sana

Ova
 
Hawa machinga nikiangalia kwa jiji la dar hawa ndio wanaosababisha foleni barabarani wanapanga bidhaa zao sehemu ambayo ni za watembea kwa miguu mwisho wa siku wananchi wamekuwa wanapita barabara za magari
 
Machinga hawa wanatakiwa wawe sehemu sahihi kulingana na level yao , unakuta mtu analipa frem laki Saba , mbele yake kuna machinga analipa 50000 , af anachekelea na kujiita mpambanaji... ..Fukuza kabisa hao watu waende sehemu sahihi ya umachinga
Mkuu umekosea siyo 50,000 wanalipa 20,000 wanapewa Kitambulisho cha kuvinjaro popote watakapo kufanyia Biashara
 
Back
Top Bottom