fabinyo
JF-Expert Member
- Aug 5, 2011
- 2,991
- 2,108
Monday, 20 February 2012 11:09 |
LUSAKA, Zambia FURAHA ya ubingwa wa Chipolopolo imepitiliza kwani mara baada ya timu ya Taifa ya Zambia kutwaa ubingwa, wanawake wanaofanya biashara ya kuumiza miili yao walitangaza ofa kwa mashabiki wa timu hiyo. Gazeti la The Independent Post la Zambia lilitonywa kuwa katika klabu za usiku zilizoko maeneo ya Kanyama za Kanchembele na Chine Chikayeba zilikutwa watu wakiwa foleni kusubiri kupata ofa hiyo. Malaya mmoja alikuwa akifanya mapenzi na wastani wa wanaume 11 na kulikuwa na wanaume zaidi ya 200 wakisubiri ofa hiyo ikiwa ni sehemu ya kushangilia ushindi wa kwanza wa Zambia tangu mwaka 1994 walipoingia fainali. Hali ilikuwa hivyo pia katika klabu ya usiku iliyoko John Laing ya Corogo. Habari zaidi zinasema kuwa, katika klabu hiyo ya Corogo, mtu mmoja alichukua mkong'oto na waliokuwa foleni baada ya kukaa muda mrefu na malaya mmoja huku wengine wakisubiri ofa hiyo. Ndiyo, tulimtwanga mangumi kwa kuwa alichukua muda mrefu 'kumaliza'. Tuko watu kibao hapa, lakini jamaa kachukua muda mrefu ikabidi tumtoe kinguvu kwa mangumi, alisema shuhuda mmoja aliyejitambulisha kwa jina la James. Katika klabu za usiku maeneo ya Chawama na Kalingalinga, malaya walitoa ofa kwa mashabiki wengi wa Chipolopolo ikiwa ni sehemu ya kushangilia ubingwa huo. Shabiki mwingine ambaye hakutaka kukimbilia ofa hiyo alisema kuwa inaweza kuwaletea matatizo baadaye. Mike Tembo alisema kuwa kutokana na hali hiyo, vijana wengi wanaweza kuambukizwa virusi vya HIV ama magonjwa ya zinaa kutokana na ngono ya ubingwa. Nafikiri wakati Zambia wanacheza fainali, kulikuwa na kila sababu ya kugawa kondom bure kwa ajili ya kulinda vijana wetu. Wengi walifanya mapenzi na malaya hawa bila kuvaa kondom, alisema Tembo kwa masikitiko. Wakati huo huo, baa moja nchini Zimbabwe nayo ilikuwa ikigawa bia za ofa kushangilia ushindi wa Chipolopolo. Mwakilishi wa mashabiki wa Chipolopolo nchini Zimbabwe, George Chivhunga ambao ni wanachama katika baa hiyo alisema wametoa ofa hiyo kwa sababu wanaiunga mkono Chipolopolo na kwa kuwa Wazimbabwe na Wazambia ni kitu kimoja hivyo hakuna gharama za kununua bia katika baa hiyo. --------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Sijui sisi tukichuaga ubingwa itakuwaje,kazi kweli kweli. |