sangu mnene
Member
- Sep 5, 2012
- 92
- 35
Akichangia katika mjadala wa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi, Mheshimiwa Mkosamali (Mbunge), amewalaumu viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge wa CCM kuwa, baada ya kusomeshwa bure na serikali ya Mwalimu Nyerere, wao
wamegeuka, wameanzisha matabaka, wanapeleka watoto wao shule binafsi maarufu kama 'English Medium', wanawaanzishia watoto wa walalahoi shule za kata zisizo na vitabu, walimu, maabara na madawati.
Kwa uzembe wao wamesababisha watoto wafeli na baadhi yao wanakuwa vibaka na machangudoa. Amedai shule binafsi zinamchukia sana Dr Ndalichako maana amezuia mitihani isivuje,"walizoea kuiba mitihani hawa,sasa Ndalichako kawabana,wanafeli vibaya, wanamtaka aje mwingine atakayekuwa tayari kuuza mitihani kwao". Amewaonya viongozi wa CCM kuwa siku zao zinahesabika."Ole wenu maana vijana mliowanyima elimu wanafahamu mnapoishi, si mnaishi Masaki, watawafuata hukohuko, hapo ndipo kutakapokuwepo kilio cha kusaga meno". Baadhi ya wabunge wamelaumu kauli hiyo ya Mkosamali na kuiita ya kichochezi.
Hivi wana JF;
1.Ninini hasa anachomaanisha Mkosamali? Je, ni kuwa yatawapata kama yaliyowapata mawaziri wa CCM wa Mtwara?
2.Je, viongozi wengi walionufaika na Elimu ya bure ya mwalimu, wanaishi Masaki na maeneo mengine mazuri?
3.Je, matokeo mabovu ya mitihani ya NECTA, yanastahili kubebeshwa viongozi wa Elimu na CCM?
4.Je, chuki ya vijana waliofeli ni kubwa kwa serikali kiasi cha kuwapa onyo viongozi wa CCM wanaoishi maeneo mazuri kama Masaki?
wamegeuka, wameanzisha matabaka, wanapeleka watoto wao shule binafsi maarufu kama 'English Medium', wanawaanzishia watoto wa walalahoi shule za kata zisizo na vitabu, walimu, maabara na madawati.
Kwa uzembe wao wamesababisha watoto wafeli na baadhi yao wanakuwa vibaka na machangudoa. Amedai shule binafsi zinamchukia sana Dr Ndalichako maana amezuia mitihani isivuje,"walizoea kuiba mitihani hawa,sasa Ndalichako kawabana,wanafeli vibaya, wanamtaka aje mwingine atakayekuwa tayari kuuza mitihani kwao". Amewaonya viongozi wa CCM kuwa siku zao zinahesabika."Ole wenu maana vijana mliowanyima elimu wanafahamu mnapoishi, si mnaishi Masaki, watawafuata hukohuko, hapo ndipo kutakapokuwepo kilio cha kusaga meno". Baadhi ya wabunge wamelaumu kauli hiyo ya Mkosamali na kuiita ya kichochezi.
Hivi wana JF;
1.Ninini hasa anachomaanisha Mkosamali? Je, ni kuwa yatawapata kama yaliyowapata mawaziri wa CCM wa Mtwara?
2.Je, viongozi wengi walionufaika na Elimu ya bure ya mwalimu, wanaishi Masaki na maeneo mengine mazuri?
3.Je, matokeo mabovu ya mitihani ya NECTA, yanastahili kubebeshwa viongozi wa Elimu na CCM?
4.Je, chuki ya vijana waliofeli ni kubwa kwa serikali kiasi cha kuwapa onyo viongozi wa CCM wanaoishi maeneo mazuri kama Masaki?