Machafuko: Raia Burkina Faso kupatiwa silaha kupambana na wanamgambo wenye uhusiano na makundi ya kigaidi

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,545
1580804604933.png

Wabunge nchini Burkina Faso wamepitisha kwa kauli moja muswada utakaowezesha raia wa kupewa silaha ili kupambana na makundi yenye ya waasi.

Muswada huo ambao sasa unasubiri kutiwa saini na Rais unalengo la kupunguza mashambulizi yanayofanywa na wanamgambo wenye uhusiano na makundi ya al-Qaeda na Islamic State.

Kwa mujibu wa wabunge hao, uwezo wa jeshi wa kupambana na wanamgambo hautoshi kutokana na idadi yao kuwa ndogo lakini pia hawana mafunzo ya kutosha.

“Kwasababu ya tishio linaloendelea, watu wameelezea utashi wao wa kushiriki kikamilifu katika kuilinda nchi yao, lakini huu sio ushahidi wa udhaifu wa jeshi,” ilisisitiza taarifa ya Bunge hilo kwa vyombo vya habari.

Awali Wizara ya Mawasiliano ilisema kuwa wengine watakapewa silaha hizo ni pamoja na kikosi cha kujilinda cha Ufaransa kilichokuwapo wakati wa uvamizi wa Ujerumani wakati wa vita kuu ya pili ya dunia.

Wakosoaji wa wamehoji ikiwa hatu mpya itawafanya watu waumie, lakini serikali inasisitiza kuwa watu watakaojitolea kuwa na silaha ni muhimu kwani watasaidia kumaliza kusambaa kwa ghasia.

Hata hivyo, hatua hiyo imepingwa na baadhi ya wadau wa haki za binadamu kwa madai kuwa ni hatari kwa usalama wa raia.

Kwa muda mrefu Burkina Faso imekubwa na machafuko yanayofanywa na wanamgambo wa kundi la Islamic State.

Chanzo: Mwananchi
 
Acha wawape ...ili wakishawapa... wazitumie kwa kuwaondoa wao madarakani..huku wakiona vitendo vya kihalifu vikizidi kuongeza...wenye ukwasi hawato kuwa salama na mali zao...amani ya nchi ndio itazidi kuwa anasa
Kweli sisi ni shithole
Unawapa silaha wakati wana njaa
Sasa si biashara hiyo ya kuwauzia hao?
Yaani Bunge zima limekaa likaongea hayo
Kweli tuna safari ndefu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Haya mataifa ya "Francophone" yana tatizo la kuwa na majeshi dhaifu sana. Yanaitegemea Paris kwa karibu kila kitu.

Nashangaa wanasumbuliwa na hayo magaidi uchwara yanayoamini ktk mungu feki na wa kusadikika.
MUNGU yupi?
 
Haya mataifa ya "Francophone" yana tatizo la kuwa na majeshi dhaifu sana. Yanaitegemea Paris kwa karibu kila kitu.

Nashangaa wanasumbuliwa na hayo magaidi uchwara yanayoamini ktk mungu feki na wa kusadikika.
Wafaransa ni wasengerema tu.

dodge
Hayo mataifa yamefanywa kuwa dhaifu kiulinzi kwa makusudi kabisa na aliyekuwa mtawala wao "Ufaransa" ili aendelee kubaki hapo alinde maslahi yake.
 
Badala ya kutatua tatizo unaongeza tatizo! Mwanachi asiye na weledi wowote unampa silaha? Hiyo ni serikali iliyofeli! Badala ya kunnuua hizo silaha wangewaajiri vijana zaidi kwenye jeshi na kuongeza nguvu zaidi huko ambako kuna hivyo vikundi vya waasi
 
Back
Top Bottom