Machache yanayonifanya niamini uwepo wa Mungu: Hatari ya kuamini hakuna Mungu

Ahmet

JF-Expert Member
Oct 15, 2019
1,537
3,404
Dunia imebadilikia, utandawazi unatukutanisha na watu mbalimbali duniani. Fikra mpya, filosofia na elimu inatujuza mitazamo ya watu mbalimbali katika Historia na hata ulimwengu tulio nao.

Moja kwa moja niende kuelezea kwanini naamini uwepo wa Mungu kwa kutumia hoja za kisayansi zenye kufikirika na hoja za kiroho (kihisia)

HOJA ZA KIULIMWENGU
kwa kuuangalia ulimwengu jinsi ulivyoumbwa basi ni alama tosha ya kuthibisha uwepo wa Mungu.

Sayari, nyota, nebula, Galaksi, mashimo meusi (black holes), miezi, magimba na vyengine vingi.
Nikijaribu kusoma ulimwengu, basi nafsi yangu inaniambia kabisa kuwa Kuna muumba wa vitu vyote hivi. Hivi ni kweli nyota kubwa kubwa Kama Stephenson 2-18, Betelgause, Rigel, Sirius A na nyengine, Nebula kama Carina nebula, Orion nebula, Helix nebula na nyengine nyingi, havina mtengenezaji? Hivi ni kweli vitu vyote hivi vimetokea kwa bahati nasibu?
Screenshot_20220723-205020~2.png

Screenshot_20220723-205105~2.png

Ulimwengu ni mkubwa na umeumbwa kwa namna ya kushangaza sana. Mnapo tarehe 11 julai 2022, shirika la utafiti wa anga la Marekani NASA kwa kutumia darubini ya James Webb limeweza kupiga picha za mbali kabisa, wanasayansi wanahuita ukingo wa ulimwengu (edge of the observable universe). Kwakweli picha hizo ni zenye kupendeza sana. Kilichonistaajabisha sana ni kuwa kuna picha imechukuliwa kutoka umbali wa miaka ya mwanga bilioni 4.5 (4.5 billion light years). Umbali huu ni mrefu sana ambao mwanadamu hawezi akapata picha halisi. Lakini kwa tafsiri yenye kueleweka ni kuwa mwanga umesafiri kutoka huko katika ukingo wa ulimwengu hadi hapa duniani kwa miaka bilioni 4.5 iliyopita na hizo galaksi tunazoziona kwenye picha basi tunaziona jinsi nilivyokuwa miaka bilioni 4.5 iliyopita.
FB_IMG_1657906007839.jpg

Screenshot_20220723-205038~2.png

Wanasayansi wanathibitisha ya kuwa ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu ndogo tu ya ulimwengu mzima, ni nukta tu ya ulimwengu mzima. Wapo wanaothibitisha ya kuwa Kuna ulimwengu zaidi ya mmoja (multiverse). Hivi kwa uumbaji huu ni kweli hakuna mwenye nguvu zisizo za kawaida ambae ndio katengeneza vyote hivyo?

Uwingi wa nyota, galaksi, nebula na vyengine vingi. Uwingi tu wa vitu hivyo unastaajabisha sana. Hizi vyota tumaziona ni nyota chache tu kati ya nyota nyingi katika galaksi yetu yaani milky way. Inakadiliwa kuwa Kuna nyota bilioni 100 hadi 400 katika galaksi yetu yaani milky way. Ni nyota nyingi ambazo kama ungeweza kuziangalia kutoka katika umbali fulani basi ungepata picha halisi. Sasa hii ni galaksi moja na wanasayansi wanakadiria pia kuwa kuna takribani galaksi bilioni 100 hadi 200 katika ulimwengu unaoonekana. Na huu ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu tu ya ulimwengu mzima, je Kuna vitu vingapi katika ulimwengu usiooneka?
Screenshot_20220713-215324.png

Screenshot_20220723-164059.png

Mifumo ya kiulimwengu yenye kutulinda wanadamu. Nikiangalia jinsi tabaka la ozoni (ozone layer) inavyotulinda kutokana na mionzi ya UV, mzunguko wa jua na dunia, mwezi na sayari nyengine ambapo Kama vitaenda tofauti basi maisha ya mwanadamu yatakuwa hatarini. Ukitafakari mfumo wa uzungukaji wa maji (water cycle) unaweza ukapata taswira ya kivipi maisha yetu yanategemea huruma ya Mungu. Dunia ingeweza hata kuhama kutoka katika obiti yake. Lakini kuna mlizi wetu ambae halali, anaetupenda.
Kuna magimba makubwa yanayodondoka kila siku, kila saa na dakika, Lakini Mungu kaweka utaratibu wake, magimba hayo huyayuka kabla ya kutufikia binadamu katika uso wa dunia. Ni njia ya Mungu kutulinda binadamu kwani kuna sayari ngapi huangukiwa na magimba hayo.
Screenshot_20220723-205030.png


SABABU ZA KIROHO (KIHISIA)
Kutambua uwepo wa Mungu ni suala la asili ya mwanadamu na viumbe wengine. Tangu tunazaliwa, tunakuwa na utambuzi wa asili juu ya uwepo wa Mungu. Hakuna mtoto ambae haamini uwepo wa Mungu. Ingawa Mungu haonekani lakini mara zote watoto hutaja neno Mungu. Kiasili kila mtu ana schema ya kutambua uwepo wa Mungu lakini mazingira yanaweza yakambadilisha na kuamini kuwa hakuna Mungu.

Mapenzi ya mzazi kwa mtoto, upendo wa mzazi hasa wa mama ni alama ya uwepo wa Mungu. Ukitafakari kwa kina utagundua kuna alieweka mapenzi haya ambae ni Mungu. Na hii si kwa binadamu tu bali hata kwa wanyama pia. Mzazi yuko tayari kuhatarisha uhai wake ili awalinde watoto wake, ona kuku anavyowalinda vifaranga vyake dhidi ya mwewe, nyoka na wanyama wengine. .

Utofauti wa binadamu na wanyama wengine. Hapa najiuliza kwanini binadamu tunavaa nguo, tunasoma elimu mbalimbali, tuna majumba mazuri, teknolojia, usafiri wa anga na kila kitu kizuri, Kila leo binadamu hubadilika na kugundua vitu vipya, mitindo mipya ya mavazi, nyumba na magari hubadilika pia. Maisha ya viumbe wengine yapo hivyo hivyo miaka nenda, miaka rudi. Si ajabu kabisa kuku kumpanda mama yake, kujamiiana kwao huwa ni sehemu yoyote. Binadamu tunahifadhi hadi kinyesi chetu, lakini wanyama hawana utaratibu huo. Ni jambo gumu kwa binadamu kumla binadamu mwenzake lakini leo ukichinja kuku nyumbani kwako basi mabaki ya nyama hiyo unawatupia kuku wengine. Hivi binadamu kuwa na utambuzi, fikra, akili, uwezo kwa kupanga na kuamua umekuja kwa bahati nasibu au ni Mungu ndio kapanga iwe hivyo?

Mifumo ya mwili na jinsi inavyofanya kazi. Hakika binadamu na wanyama wengine wameumbwa katika namna tata sana. Ona Kuna mfumo wa chakula, mfumo wa hewa, mfumo wa utoaji taka mwili, mfumo wa Neva, mfumo wa mzunguko wa damu na mifumo mingine mingi. Mungu amempa Mwanaamu changamoto ya kuumba hata sisimizi na kamwe hataweza.

NI IPI HASARA YA KUTOAMINI MUNGU?
Mbali na hasara kuu ambayo mtu ataipata siku ya malipo kwa kutoamini kwakwe, pia kuna hasara nyingi ambazo zinaitesa dunia ya leo kutokana na upingaji huu.
Kutoamini Mungu kunaondoa utu, mtu ambae haamini Mungu anaweza akaingia katika matendo ambayo hayatamtofautisha yeye na mnyama. Kama tulivyoona awali kuwa mnyama na binadamu ni tofauti basi mtu ambae haamini uwepo wa Mungu anaweza akakaribiana kimatendo na mnyama.
Mambo yafuatayo yamesababishwa kwa kiasi kikubwa na kuto kuwa na imani ya Mungu

i. Filamu za ngono, matamasha ya kutembea utupu na mfano wa hayo.
Dunia leo inashuhudia kilele cha maovu ya mwanadamu. Kuna maelfu kwa malaki ya waigizaji wa filamu za ngono tena kwa namna tofauti.

ii. Kukua kwa matendo ya ushoga, usagaji na kuwekewa kampeni maalumu ili kukuza vitendo hivyo.

iii. Ujambazi, ukatili, mauwaji na maovu mengine. Jamii ambayo watu wake hawaamini Mungu basi ni rahisi sana kuangukia katika dunia yenye migogoro kuuwana na ukatili wa aina zote.

Ili tuijenge jamii yenye ustawi mzuri, maadili mema, ukuaji uchumi na hatimae maendeleo endelevu basi tusimsahau Mungu wetu.
ELIMU, KAZI NA SALA
 
Hoja yako ya kwanza imeanza kwa assumption

Umejuaje ulimwengu umeumbwa?

Kuna record yeyote iliyowahi kuhakikiwa kwa uthibitisho kuonesha ulimwengu fulani umewahi kuumbwa ili ikupe urahisi kwa wewe kusema ulimwengu huu uliumbwa?

Kama ni ngumu kufikiria nyota, mwezi na vitu vingine vyenye complex kuwa vimejiumba kwanini kanuni hiyo usiipeleke mbali kwa huyo muumbaji kwa kujiuliza swali hilo hilo?

Kama itakuwa rahisi kusema muumbaji hana chanzo, maana yake ili kilichopo kiwepo hakipaswi kuwa na chanzo, sasa nini mantiki yako ya kufikiria source ya vitu?

Unatofauti gani na mtu mwingine anayekuambia ulimwengu upo na hauna chanzo?
 
Dunia imebadilikia, utandawazi unatukutanisha na watu mbalimbali duniani. Fikra mpya, filosofia na elimu inatujuza mitazamo ya watu mbalimbali katika Historia na hata ulimwengu tulio nao.

Moja kwa moja niende kuelezea kwanini naamini uwepo wa Mungu kwa kutumia hoja za kisayansi zenye kufikirika na hoja za kiroho (kihisia)

HOJA ZA KIULIMWENGU
kwa kuuangalia ulimwengu jinsi ulivyoumbwa basi ni alama tosha ya kuthibisha uwepo wa Mungu.

Sayari, nyota, nebula, Galaksi, mashimo meusi (black holes), miezi, magimba na vyengine vingi.
Nikijaribu kusoma ulimwengu, basi nafsi yangu inaniambia kabisa kuwa Kuna muumba wa vitu vyote hivi. Hivi ni kweli nyota kubwa kubwa Kama Stephenson 2-18, Betelgause, Rigel, Sirius A na nyengine, Nebula kama Carina nebula, Orion nebula, Helix nebula na nyengine nyingi, havina mtengenezaji? Hivi ni kweli vitu vyote hivi vimetokea kwa bahati nasibu?
View attachment 2301621
View attachment 2301612
Ulimwengu ni mkubwa na umeumbwa kwa namna ya kushangaza sana. Mnapo tarehe 11 julai 2022, shirika la utafiti wa anga la Marekani NASA kwa kutumia darubini ya James Webb limeweza kupiga picha za mbali kabisa, wanasayansi wanahuita ukingo wa ulimwengu (edge of the observable universe). Kwakweli picha hizo ni zenye kupendeza sana. Kilichonistaajabisha sana ni kuwa kuna picha imechukuliwa kutoka umbali wa miaka ya mwanga bilioni 4.5 (4.5 billion light years). Umbali huu ni mrefu sana ambao mwanadamu hawezi akapata picha halisi. Lakini kwa tafsiri yenye kueleweka ni kuwa mwanga umesafiri kutoka huko katika ukingo wa ulimwengu hadi hapa duniani kwa miaka bilioni 4.5 iliyopita na hizo galaksi tunazoziona kwenye picha basi tunaziona jinsi nilivyokuwa miaka bilioni 4.5 iliyopita.
View attachment 2301572
View attachment 2301618
Wanasayansi wanathibitisha ya kuwa ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu ndogo tu ya ulimwengu mzima, ni nukta tu ya ulimwengu mzima. Wapo wanaothibitisha ya kuwa Kuna ulimwengu zaidi ya mmoja (multiverse). Hivi kwa uumbaji huu ni kweli hakuna mwenye nguvu zisizo za kawaida ambae ndio katengeneza vyote hivyo?

Uwingi wa nyota, galaksi, nebula na vyengine vingi. Uwingi tu wa vitu hivyo unastaajabisha sana. Hizi vyota tumaziona ni nyota chache tu kati ya nyota nyingi katika galaksi yetu yaani milky way. Inakadiliwa kuwa Kuna nyota bilioni 100 hadi 400 katika galaksi yetu yaani milky way. Ni nyota nyingi ambazo kama ungeweza kuziangalia kutoka katika umbali fulani basi ungepata picha halisi. Sasa hii ni galaksi moja na wanasayansi wanakadiria pia kuwa kuna takribani galaksi bilioni 100 hadi 200 katika ulimwengu unaoonekana. Na huu ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu tu ya ulimwengu mzima, je Kuna vitu vingapi katika ulimwengu usiooneka?
View attachment 2301578
View attachment 2301583
Mifumo ya kiulimwengu yenye kutulinda wanadamu. Nikiangalia jinsi tabaka la ozoni (ozone layer) inavyotulinda kutokana na mionzi ya UV, mzunguko wa jua na dunia, mwezi na sayari nyengine ambapo Kama vitaenda tofauti basi maisha ya mwanadamu yatakuwa hatarini. Ukitafakari mfumo wa uzungukaji wa maji (water cycle) unaweza ukapata taswira ya kivipi maisha yetu yanategemea huruma ya Mungu. Dunia ingeweza hata kuhama kutoka katika obiti yake. Lakini kuna mlizi wetu ambae halali, anaetupenda.
Kuna magimba makubwa yanayodondoka kila siku, kila saa na dakika, Lakini Mungu kaweka utaratibu wake, magimba hayo huyayuka kabla ya kutufikia binadamu katika uso wa dunia. Ni njia ya Mungu kutulinda binadamu kwani kuna sayari ngapi huangukiwa na magimba hayo.
View attachment 2301584

SABABU ZA KIROHO (KIHISIA)
Kutambua uwepo wa Mungu ni suala la asili ya mwanadamu na viumbe wengine. Tangu tunazaliwa, tunakuwa na utambuzi wa asili juu ya uwepo wa Mungu. Hakuna mtoto ambae haamini uwepo wa Mungu. Ingawa Mungu haonekani lakini mara zote watoto hutaja neno Mungu. Kiasili kila mtu ana schema ya kutambua uwepo wa Mungu lakini mazingira yanaweza yakambadilisha na kuamini kuwa hakuna Mungu.

Mapenzi ya mzazi kwa mtoto, upendo wa mzazi hasa wa mama ni alama ya uwepo wa Mungu. Ukitafakari kwa kina utagundua kuna alieweka mapenzi haya ambae ni Mungu. Na hii si kwa binadamu tu bali hata kwa wanyama pia. Mzazi yuko tayari kuhatarisha uhai wake ili awalinde watoto wake, ona kuku anavyowalinda vifaranga vyake dhidi ya mwewe, nyoka na wanyama wengine. .

Utofauti wa binadamu na wanyama wengine. Hapa najiuliza kwanini binadamu tunavaa nguo, tunasoma elimu mbalimbali, tuna majumba mazuri, teknolojia, usafiri wa anga na kila kitu kizuri, Kila leo binadamu hubadilika na kugundua vitu vipya, mitindo mipya ya mavazi, nyumba na magari hubadilika pia. Maisha ya viumbe wengine yapo hivyo hivyo miaka nenda, miaka rudi. Si ajabu kabisa kuku kumpanda mama yake, kujamiiana kwao huwa ni sehemu yoyote. Binadamu tunahifadhi hadi kinyesi chetu, lakini wanyama hawana utaratibu huo. Ni jambo gumu kwa binadamu kumla binadamu mwenzake lakini leo ukichinja kuku nyumbani kwako basi mabaki ya nyama hiyo unawatupia kuku wengine. Hivi binadamu kuwa na utambuzi, fikra, akili, uwezo kwa kupanga na kuamua umekuja kwa bahati nasibu au ni Mungu ndio kapanga iwe hivyo?

Mifumo ya mwili na jinsi inavyofanya kazi. Hakika binadamu na wanyama wengine wameumbwa katika namna tata sana. Ona Kuna mfumo wa chakula, mfumo wa hewa, mfumo wa utoaji taka mwili, mfumo wa Neva, mfumo wa mzunguko wa damu na mifumo mingine mingi. Mungu amempa Mwanaamu changamoto ya kuumba hata sisimizi na kamwe hataweza.

NI IPI HASARA YA KUTOAMINI MUNGU?
Mbali na hasara kuu ambayo mtu ataipata siku ya malipo kwa kutoamini kwakwe, pia kuna hasara nyingi ambazo zinaitesa dunia ya leo kutokana na upingaji huu.
Kutoamini Mungu kunaondoa utu, mtu ambae haamini Mungu anaweza akaingia katika matendo ambayo hayatamtofautisha yeye na mnyama. Kama tulivyoona awali kuwa mnyama na binadamu ni tofauti basi mtu ambae haamini uwepo wa Mungu anaweza akakaribiana kimatendo na mnyama.
Mambo yafuatayo yamesababishwa kwa kiasi kikubwa na kuto kuwa na imani ya Mungu

i. Filamu za ngono, matamasha ya kutembea utupu na mfano wa hayo.
Dunia leo inashuhudia kilele cha maovu ya mwanadamu. Kuna maelfu kwa malaki ya waigizaji wa filamu za ngono tena kwa namna tofauti.

ii. Kukua kwa matendo ya ushoga, usagaji na kuwekewa kampeni maalumu ili kukuza vitendo hivyo.

iii. Ujambazi, ukatili, mauwaji na maovu mengine. Jamii ambayo watu wake hawaamini Mungu basi ni rahisi sana kuangukia katika dunia yenye migogoro kuuwana na ukatili wa aina zote.

Ili tuijenge jamii yenye ustawi mzuri, maadili mema, ukuaji uchumi na hatimae maendeleo endelevu basi tusimsahau Mungu wetu.
ELIMU, KAZI NA SALA
Hasante bwana
 
Dunia imebadilikia, utandawazi unatukutanisha na watu mbalimbali duniani. Fikra mpya, filosofia na elimu inatujuza mitazamo ya watu mbalimbali katika Historia na hata ulimwengu tulio nao.

Moja kwa moja niende kuelezea kwanini naamini uwepo wa Mungu kwa kutumia hoja za kisayansi zenye kufikirika na hoja za kiroho (kihisia)

HOJA ZA KIULIMWENGU
kwa kuuangalia ulimwengu jinsi ulivyoumbwa basi ni alama tosha ya kuthibisha uwepo wa Mungu.

Sayari, nyota, nebula, Galaksi, mashimo meusi (black holes), miezi, magimba na vyengine vingi.
Nikijaribu kusoma ulimwengu, basi nafsi yangu inaniambia kabisa kuwa Kuna muumba wa vitu vyote hivi. Hivi ni kweli nyota kubwa kubwa Kama Stephenson 2-18, Betelgause, Rigel, Sirius A na nyengine, Nebula kama Carina nebula, Orion nebula, Helix nebula na nyengine nyingi, havina mtengenezaji? Hivi ni kweli vitu vyote hivi vimetokea kwa bahati nasibu?
View attachment 2301621
View attachment 2301612
Ulimwengu ni mkubwa na umeumbwa kwa namna ya kushangaza sana. Mnapo tarehe 11 julai 2022, shirika la utafiti wa anga la Marekani NASA kwa kutumia darubini ya James Webb limeweza kupiga picha za mbali kabisa, wanasayansi wanahuita ukingo wa ulimwengu (edge of the observable universe). Kwakweli picha hizo ni zenye kupendeza sana. Kilichonistaajabisha sana ni kuwa kuna picha imechukuliwa kutoka umbali wa miaka ya mwanga bilioni 4.5 (4.5 billion light years). Umbali huu ni mrefu sana ambao mwanadamu hawezi akapata picha halisi. Lakini kwa tafsiri yenye kueleweka ni kuwa mwanga umesafiri kutoka huko katika ukingo wa ulimwengu hadi hapa duniani kwa miaka bilioni 4.5 iliyopita na hizo galaksi tunazoziona kwenye picha basi tunaziona jinsi nilivyokuwa miaka bilioni 4.5 iliyopita.
View attachment 2301572
View attachment 2301618
Wanasayansi wanathibitisha ya kuwa ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu ndogo tu ya ulimwengu mzima, ni nukta tu ya ulimwengu mzima. Wapo wanaothibitisha ya kuwa Kuna ulimwengu zaidi ya mmoja (multiverse). Hivi kwa uumbaji huu ni kweli hakuna mwenye nguvu zisizo za kawaida ambae ndio katengeneza vyote hivyo?

Uwingi wa nyota, galaksi, nebula na vyengine vingi. Uwingi tu wa vitu hivyo unastaajabisha sana. Hizi vyota tumaziona ni nyota chache tu kati ya nyota nyingi katika galaksi yetu yaani milky way. Inakadiliwa kuwa Kuna nyota bilioni 100 hadi 400 katika galaksi yetu yaani milky way. Ni nyota nyingi ambazo kama ungeweza kuziangalia kutoka katika umbali fulani basi ungepata picha halisi. Sasa hii ni galaksi moja na wanasayansi wanakadiria pia kuwa kuna takribani galaksi bilioni 100 hadi 200 katika ulimwengu unaoonekana. Na huu ulimwengu wenyekuonekana ni sehemu tu ya ulimwengu mzima, je Kuna vitu vingapi katika ulimwengu usiooneka?
View attachment 2301578
View attachment 2301583
Mifumo ya kiulimwengu yenye kutulinda wanadamu. Nikiangalia jinsi tabaka la ozoni (ozone layer) inavyotulinda kutokana na mionzi ya UV, mzunguko wa jua na dunia, mwezi na sayari nyengine ambapo Kama vitaenda tofauti basi maisha ya mwanadamu yatakuwa hatarini. Ukitafakari mfumo wa uzungukaji wa maji (water cycle) unaweza ukapata taswira ya kivipi maisha yetu yanategemea huruma ya Mungu. Dunia ingeweza hata kuhama kutoka katika obiti yake. Lakini kuna mlizi wetu ambae halali, anaetupenda.
Kuna magimba makubwa yanayodondoka kila siku, kila saa na dakika, Lakini Mungu kaweka utaratibu wake, magimba hayo huyayuka kabla ya kutufikia binadamu katika uso wa dunia. Ni njia ya Mungu kutulinda binadamu kwani kuna sayari ngapi huangukiwa na magimba hayo.
View attachment 2301584

SABABU ZA KIROHO (KIHISIA)
Kutambua uwepo wa Mungu ni suala la asili ya mwanadamu na viumbe wengine. Tangu tunazaliwa, tunakuwa na utambuzi wa asili juu ya uwepo wa Mungu. Hakuna mtoto ambae haamini uwepo wa Mungu. Ingawa Mungu haonekani lakini mara zote watoto hutaja neno Mungu. Kiasili kila mtu ana schema ya kutambua uwepo wa Mungu lakini mazingira yanaweza yakambadilisha na kuamini kuwa hakuna Mungu.

Mapenzi ya mzazi kwa mtoto, upendo wa mzazi hasa wa mama ni alama ya uwepo wa Mungu. Ukitafakari kwa kina utagundua kuna alieweka mapenzi haya ambae ni Mungu. Na hii si kwa binadamu tu bali hata kwa wanyama pia. Mzazi yuko tayari kuhatarisha uhai wake ili awalinde watoto wake, ona kuku anavyowalinda vifaranga vyake dhidi ya mwewe, nyoka na wanyama wengine. .

Utofauti wa binadamu na wanyama wengine. Hapa najiuliza kwanini binadamu tunavaa nguo, tunasoma elimu mbalimbali, tuna majumba mazuri, teknolojia, usafiri wa anga na kila kitu kizuri, Kila leo binadamu hubadilika na kugundua vitu vipya, mitindo mipya ya mavazi, nyumba na magari hubadilika pia. Maisha ya viumbe wengine yapo hivyo hivyo miaka nenda, miaka rudi. Si ajabu kabisa kuku kumpanda mama yake, kujamiiana kwao huwa ni sehemu yoyote. Binadamu tunahifadhi hadi kinyesi chetu, lakini wanyama hawana utaratibu huo. Ni jambo gumu kwa binadamu kumla binadamu mwenzake lakini leo ukichinja kuku nyumbani kwako basi mabaki ya nyama hiyo unawatupia kuku wengine. Hivi binadamu kuwa na utambuzi, fikra, akili, uwezo kwa kupanga na kuamua umekuja kwa bahati nasibu au ni Mungu ndio kapanga iwe hivyo?

Mifumo ya mwili na jinsi inavyofanya kazi. Hakika binadamu na wanyama wengine wameumbwa katika namna tata sana. Ona Kuna mfumo wa chakula, mfumo wa hewa, mfumo wa utoaji taka mwili, mfumo wa Neva, mfumo wa mzunguko wa damu na mifumo mingine mingi. Mungu amempa Mwanaamu changamoto ya kuumba hata sisimizi na kamwe hataweza.

NI IPI HASARA YA KUTOAMINI MUNGU?
Mbali na hasara kuu ambayo mtu ataipata siku ya malipo kwa kutoamini kwakwe, pia kuna hasara nyingi ambazo zinaitesa dunia ya leo kutokana na upingaji huu.
Kutoamini Mungu kunaondoa utu, mtu ambae haamini Mungu anaweza akaingia katika matendo ambayo hayatamtofautisha yeye na mnyama. Kama tulivyoona awali kuwa mnyama na binadamu ni tofauti basi mtu ambae haamini uwepo wa Mungu anaweza akakaribiana kimatendo na mnyama.
Mambo yafuatayo yamesababishwa kwa kiasi kikubwa na kuto kuwa na imani ya Mungu

i. Filamu za ngono, matamasha ya kutembea utupu na mfano wa hayo.
Dunia leo inashuhudia kilele cha maovu ya mwanadamu. Kuna maelfu kwa malaki ya waigizaji wa filamu za ngono tena kwa namna tofauti.

ii. Kukua kwa matendo ya ushoga, usagaji na kuwekewa kampeni maalumu ili kukuza vitendo hivyo.

iii. Ujambazi, ukatili, mauwaji na maovu mengine. Jamii ambayo watu wake hawaamini Mungu basi ni rahisi sana kuangukia katika dunia yenye migogoro kuuwana na ukatili wa aina zote.

Ili tuijenge jamii yenye ustawi mzuri, maadili mema, ukuaji uchumi na hatimae maendeleo endelevu basi tusimsahau Mungu wetu.
ELIMU, KAZI NA SALA
Nilipongeze shirika la Anga la Russia kwa kufungua njia hao wengineo ni kama harusi hawakosekaniki wasindikizaji.
Katika tafiti zao wanafika mahala wanaamini yupo mwenye vyake.
China juzi kati kaotesha mimea huko angani kaja ipanda duniani tujiulize kwa nini aioteshee huko?

Kuna mahala nilisoma mti uloteremshwa na malaika wengi 99 ni mwarobaini.
 
Sio Russia ni USA
Nilipongeze shirika la Anga la Russia kwa kufungua njia hao wengineo ni kama harusi hawakosekaniki wasindikizaji.
Katika tafiti zao wanafika mahala wanaamini yupo mwenye vyake.
China juzi kati kaotesha mimea huko angani kaja ipanda duniani tujiulize kwa nini aioteshee huko?

Kuna mahala nilisoma mti uloteremshwa na malaika wengi 99 ni mwarobaini.
 
Hoja yako ya kwanza imeanza kwa assumption

Umejuaje ulimwengu umeumbwa?

Kuna record yeyote iliyowahi kuhakikiwa kwa uthibitisho kuonesha ulimwengu fulani umewahi kuumbwa ili ikupe urahisi kwa wewe kusema ulimwengu huu uliumbwa?

Kama ni ngumu kufikiria nyota, mwezi na vitu vingine vyenye complex kuwa vimejiumba kwanini kanuni hiyo usiipeleke mbali kwa huyo muumbaji kwa kujiuliza swali hilo hilo?

Kama itakuwa rahisi kusema muumbaji hana chanzo, maana yake ili kilichopo kiwepo hakipaswi kuwa na chanzo, sasa nini mantiki yako ya kufikiria source ya vitu?

Unatofauti gani na mtu mwingine anayekuambia ulimwengu upo na hauna chanzo?
Kumbe upo braza, hatujaonana mudaaa✌

Mnaopinga uwepo wa Mungu mna bahati hadi kidogo nawaonea 'kawivu'.

Maana mnaopingana nao wanakuwaga na kaustaarabu fulani kakimungumungu, hawatukani na wanawaheshimu na kuwapenda hadi hao 'maadui' wanaobishana nao - hasa wakristu.

Sawa wengine wanaweza kukutishia kukudhuru physically lakini sio sana maana kuna haki fulani ya kimungu imetawala waamini wooote.

Bwana wee! ushawahi kubishana na watetea uchawi/ushirikina hata kidogo? Duuh ni noma, kwanza hakuna heshima, na hawataki hata kutumia mantiki/logic yaani utaoga matusi tu na matisho. Ubishi wake hauna raha kama huu.

Kwa kweli Scars na wenzio mumushukuru Mungu [mtakoma kama hamtaki kutambua yupo, sisi tunaendelea tu kuweka hiyo a-priori, bampa to bampa😏😂] kwa hilo, mna raha sana: Ona mfano hapa jamaa anazo hadi pointi zenye sayansi ndani yake, mantiki kama zote. Raha sana hata unapotoa hoja yako unajua zinatua katika akili yenye akili na zitajibiwa kiakili.
 
Hoja yako ya kwanza imeanza kwa assumption

Umejuaje ulimwengu umeumbwa?

Kuna record yeyote iliyowahi kuhakikiwa kwa uthibitisho kuonesha ulimwengu fulani umewahi kuumbwa ili ikupe urahisi kwa wewe kusema ulimwengu huu uliumbwa?

Kama ni ngumu kufikiria nyota, mwezi na vitu vingine vyenye complex kuwa vimejiumba kwanini kanuni hiyo usiipeleke mbali kwa huyo muumbaji kwa kujiuliza swali hilo hilo?

Kama itakuwa rahisi kusema muumbaji hana chanzo, maana yake ili kilichopo kiwepo hakipaswi kuwa na chanzo, sasa nini mantiki yako ya kufikiria source ya vitu?

Unatofauti gani na mtu mwingine anayekuambia ulimwengu upo na hauna chanzo?
Sio kila kitu kinapaswa kuwa na chanzo, Mungu hana chanzo, ulimwengu una chanzo. Akili yetu iko limited kuweza kuaccomodate concept ya kuwa Kuna vitu havina chanzo. Akili zetu ni dhaifu mno. Kuna mambo hatuwezi hata kuyafikiria. Kumuamini Mungu inahitaji zaidi ya akili unayoitumia kuvuka barabara. Inahitaji mtu kuwa honest na mtu ambae haitaji kujua sababu ya kila kitu.

Ushawahi kujiuliza ulimwengu utaishi milele? How is this possible? Kama ulimwengu utakuwa na mwisho then nini kitakuja baada yake? Kama ulimwengu utakuwa na mwisho, then hizi nyota, sayari, nebula na vitaenda wapi? Hivi Kuna uwezekano wa kutokuwepo kitu chochote? Yaani no universe, no stars, no galaxies, no planets, no anything? Hiyo hali inaitwaje na inawezekana vipi?

Ukiweza kujibu maswali haya basi unaweza kujiuliza chanzo cha Mungu pia.
 
Sio kila kitu kinapaswa KUWA na chanzo, Mungu hana chanzo, ulimwengu una chanzo. Akili yetu iko limited kuweka kuaccomodate concept ya kuwa Kuna vitu having chanzo. Akili zetu ni dhaifu mno. Kuna mambo hatuwezi hata kuyafikiria. Kumuamini Mungu inahitaji zaidi ya akili unayoitumia kuvuka barabara barabara. Inahitaji mtu kuwa honest na mtu ambae haitaji kujua sababu ya kila kitu.

Ushawahi kujiuliza ulimwengu utaishi milele? How is this possible? Kama ulimwengu utakuwa na mwisho then Nini kitakuja baada yake? Kama ulimwengu utakuwa na mwisho, then hizi nyota, sayari, nebula na vitaenda wapi? HIVI Kuna uwezekano wa kutokuwepo kitu chochote? Yaani no universe, no stars, no galaxies, no planets, no anything? Hiyo hali inaitwaje na inawezekana vipi?

Ukiweza kujibu maswali haya basi unaweza kujiuliza chanzo cha Mungu pia.
Kama kila kitu sio lazima kiwe na chanzo basi hata ulimwengu hauna chanzo

Kama unakubali akili zetu haziwezi kufikiria kwa usahihi kwasababu ziko limited, utajuaje kuwa hata hilo wazo la kusema muumbaji wa ulimwengu ni Mungu sio muendelezo ule ule wa kufikiria majibu yasio sahihi?

Kabla ya kusema kumuamini Mungu hapo unakuwa umeruka vipengele baadhi ambavyo havijaonesha namna gani umefika hapo

Umejuaje kuna Mungu ambaye anapaswa kuaminiwa?

Ni akili ipi uliyoitumia kujua hilo?

Katika maswali yako uliyojiuliza kuhusu hatma ya ulimwengu nakujibu kwa kukupa maswali zaidi

Hapa nachukua upande wa dini ambao najua wengi ndio mnasimamia

Dini zimesema hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na ardhi

Kumbuka huo ni mwanzo, unaweza kujiuliza kabla ya mwanzo kulikuwaje?

Kama mwanzo umeanza na Mungu kuumba mbingu na ardhi, je huo sio mwanzo wa uwepo wa Mungu pia?

Kama Mungu alikuwepo kabla basi huo sio mwanzo

Lakini utajiuliza tena alikuwa akiishi wapi maana mbingu na ardhi kaviumba leo ambayo ndio mwanzo, na yeye wansema ni wamilele. Alikuwa akiishi wapi?

Haya huko pia alipokuwa akiishi kuliumbwa na nani?

Na kama kulikuwa kuna sehemu anaishi bado tu hii ya ulimwengu na ardhi itaendelea kuhesabika kama mwanzo?

Au tuseme ni mwanzo wa uumbaji na tukubaliane kwamba hakukuwa na uimbaji mwingine uliotangulia kabla ya huo?

Hapo kuna maswali mengi magumu naomba tupaache tuelekee section ya pili na huwezi kukuta pastor ana hubiri hoja tata kama hizo

Haya tujiulize mazingira ya uumbaji yalivyofanyika

Mfano leo hii ukitaka kuchimba shimo lazima utaanzia juu ya ardhi, nikiwa na maana kwamba utasimama ukiwa hapo na likikamilika utaweza kuingia ndani

Leo hii ukimkuta mtu yupo shimoni baada ya kuchimba shimo itakuwa ni rahisi kufikiria kuwa kabla ya kuingia shimoni kulikuwa na ardhi ambayo iko level ambapo hapo ndio alisimama akachimba mpaka kutengeneza shimo

Sasa Mungu aliumba ulimwengu akiwa wapi?

Huwezi kufikiria aliumba ulimwengu akiwa ndani ya ulimwengu kwasababu itaonekana hapo anaufanyia repair kwa maana ya kwamba ulikwisha jengwa
 
Kumbe upo braza, hatujaonana mudaaa✌

Mnaopinga uwepo wa Mungu mna bahati hadi kidogo nawaonea 'kawivu'.

Maana mnaopingana nao wanakuwaga na kaustaarabu fulani kakimungumungu, hawatukani na wanawaheshimu na kuwapenda hadi hao 'maadui' wanaobishana nao - hasa wakristu.

Sawa wengine wanaweza kukutishia kukudhuru physically lakini sio sana maana kuna haki fulani ya kimungu imetawala waamini wooote.

Bwana wee! ushawahi kubishana na watetea uchawi/ushirikina hata kidogo? Duuh ni noma, kwanza hakuna heshima, na hawataki hata kutumia mantiki/logic yaani utaoga matusi tu na matisho. Ubishi wake hauna raha kama huu.

Kwa kweli Scars na wenzio mumushukuru Mungu [mtakoma kama hamtaki kutambua yupo, sisi tunaendelea tu kuweka hiyo a-priori, bampa to bampa😏😂] kwa hilo, mna raha sana: Ona mfano hapa jamaa anazo hadi pointi zenye sayansi ndani yake, mantiki kama zote. Raha sana hata unapotoa hoja yako unajua zinatua katika akili yenye akili na zitajibiwa kiakili.
Vitisho ni silaha ya mwisho ya mjinga

Dini nayo inatumia dhana hiyo, hata wewe hapo una amini Mungu kwasababu umetishiwa moto

Huna tofauti na mtoto anayeenda shule kwa hofu ya viboko.
 
Vitisho ni silaha ya mwisho ya mjinga

Dini nayo inatumia dhana hiyo, hata wewe hapo una amini Mungu kwasababu umetishiwa moto

Huna tofauti na mtoto anayeenda shule kwa hofu ya viboko.
Sio wote wanaoamini Mungu ni kutokana na vitisho.

Mfano mimi nimeamini kwa upendo, imani na kuamini [trust].

Kwa wajinga vitisho ni muhimu kwao maana uoga ndio unaowatawala ila sio wote.

Hata shule wengine huenda kwa hofu ya viboko, wengine kuwaiga rafiki zao, wengine kupanda mabasi, wengine kuwapenda walimu, wengine kukua, wengine etcetc
 
Kama kila kitu sio lazima kiwe na chanzo basi hata ulimwengu hauna chanzo

Kama unakubali akili zetu haziwezi kufikiria kwa usahihi kwasababu ziko limited, utajuaje kuwa hata hilo wazo la kusema muumbaji wa ulimwengu ni Mungu sio muendelezo ule ule wa kufikiria majibu yasio sahihi?

Kabla ya kusema kumuamini Mungu hapo unakuwa umeruka vipengele baadhi ambavyo havijaonesha namna gani umefika hapo

Umejuaje kuna Mungu ambaye anapaswa kuaminiwa?

Ni akili ipi uliyoitumia kujua hilo?

Katika maswali yako uliyojiuliza kuhusu hatma ya ulimwengu nakujibu kwa kukupa maswali zaidi

Hapa nachukua upande wa dini ambao najua wengi ndio mnasimamia

Dini zimesema hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na ardhi

Kumbuka huo ni mwanzo, unaweza kujiuliza kabla ya mwanzo kulikuwaje?

Kama mwanzo umeanza na Mungu kuumba mbingu na ardhi, je huo sio mwanzo wa uwepo wa Mungu pia?

Kama Mungu alikuwepo kabla basi huo sio mwanzo

Lakini utajiuliza tena alikuwa akiishi wapi maana mbingu na ardhi kaviumba leo ambayo ndio mwanzo, na yeye wansema ni wamilele. Alikuwa akiishi wapi?

Haya huko pia alipokuwa akiishi kuliumbwa na nani?

Na kama kulikuwa kuna sehemu anaishi bado tu hii ya ulimwengu na ardhi itaendelea kuhesabika kama mwanzo?

Au tuseme ni mwanzo wa uumbaji na tukubaliane kwamba hakukuwa na uimbaji mwingine uliotangulia kabla ya huo?

Hapo kuna maswali mengi magumu naomba tupaache tuelekee section ya pili na huwezi kukuta pastor ana hubiri hoja tata kama hizo

Haya tujiulize mazingira ya uumbaji yalivyofanyika

Mfano leo hii ukitaka kuchimba shimo lazima utaanzia juu ya ardhi, nikiwa na maana kwamba utasimama ukiwa hapo na likikamilika utaweza kuingia ndani

Leo hii ukimkuta mtu yupo shimoni baada ya kuchimba shimo itakuwa ni rahisi kufikiria kuwa kabla ya kuingia shimoni kulikuwa na ardhi ambayo iko level ambapo hapo ndio alisimama akachimba mpaka kutengeneza shimo

Sasa Mungu aliumba ulimwengu akiwa wapi?

Huwezi kufikiria aliumba ulimwengu akiwa ndani ya ulimwengu kwasababu itaonekana hapo anaufanyia repair kwa maana ya kwamba ulikwisha jengwa
Kila kitu sio lazima kiwe na chanzo, yes but ulimwengu una chanzo. Hata wanasayansi wanathibitisha kuwa ulimwengu wetu huu ulianza miaka bilioni 13 iliyopita (big bang theory).

Mungu ndio hana chanzo, ambapo nimekuambia kuwa kwa akili yako dhaifu haiwezi comprehend Hilo.

Pia kumbuka sio lazima kuwa ulimwengu kuwa ndio sehemu pekee ambayo existence inaweza kuwepo. Ushawahi kujiuliza kuwa ulimwengu una mipaka? Kama ipo, iyo mipaka itakuwa inatenganisha ulimwengu na Nini? Kama ulimwengu hauna mipaka, then utakuwa unaextend Hadi wapi?

Tunatambua uwepo wa Mungu kwa sababu Mungu mwenyewe katupa ishara juu ya uwepo wake. Katika Qur'an Mungu anatumbia tuangalie jinsi alivyoumba mbingu (universe), na jinsi alivyoipendezesha mbingu ya chini na nyota (observable universe). Hizi ishara nimezielezea kwa undani katika post yangu and infact ishara ziko nyingi, kuna wanyama, bahari, milima, miti na vyengine (every designing implies designer).

Shida ni akili yako ambayo haiwezi comprehend kuwa Kuna vitu havina mwanzo na Kuna kuna space outside universe kwasababu hata wanasayansi wanakadiria kuwa Kuna uwezekano Kuna zaidi ya ulimwengu mmoja (multiverse).

Kwenye mfano wako wa shimo, sio lazma mchimbaji aingie shimoni, Mungu anatuambia kuwa yeye ni mkubwa sana zaidi ya universe. Kwaiyo kwenye mfano wako wa shimo na mchimbaji haviwezi kuendana. Chukulia mfano wa mtu anavyotengeneza mpira, si lazima aingie katika huo mpira, afterall nani kakuambia Mungu katengeneza ulimwengu kwa mikono yake.

Mungu, anasema elimu aliyotupa ni ndogo Sana, sehemu ambayo tumeigundua katika ulimwengu ni ndogo sana. Tuna LIMIT kujua baadhi ya vitu na vitu vingi hatuvijui, science inathibisha Hilo.
 
Ni
Sio wote wanaoamini Mungu ni kutokana na vitisho.

Mfano mimi nimeamini kwa upendo, imani na kuamini [trust].

Kwa wajinga vitisho ni muhimu kwao maana uoga ndio unaowatawala ila sio wote.

Hata shule wengine huenda kwa hofu ya viboko, wengine kuwaiga rafiki zao, wengine kupanda mabasi, wengine kuwapenda walimu, wengine kukua, wengine etcetc
Enzi za secondary niliipenda shule kwa sababu ya SoMo la Geography 😂😂
 
Mkuu

Mungu yupo

LAKINI

Taasisi za kiroho ni nyingi zinaamini zenyewe Ndio sahihi mbele za Mungu na kuwagawa watu Ndipo MAUMIVU yanapo anza!!
Natamani labda dini yangu ndio iwe inawafuasi wengi but for the emergency at least binadamu wanatakiwa angalau tu watambue uwepo wa Mungu.
 
Kila kitu sio lazima kiwe na chanzo, yes but ulimwengu una chanzo. Hata wanasayansi wanathibitisha kuwa ulimwengu wetu huu ulianza miaka bilioni 13 iliyopita (big bang theory).

Mungu ndio hana chanzo, ambapo nimekuambia kuwa kwa akili yako dhaifu haiwezi comprehend Hilo.

Pia kumbuka sio lazima kuwa ulimwengu kuwa ndio sehemu pekee ambayo existence inaweza kuwepo. Ushawahi kujiuliza kuwa ulimwengu una mipaka? Kama ipo, iyo mipaka itakuwa inatenganisha ulimwengu na Nini? Kama ulimwengu hauna mipaka, then utakuwa unaextend Hadi wapi?

Tunatambua uwepo wa Mungu kwa sababu Mungu mwenyewe katupa ishara juu ya uwepo wake. Katika Qur'an Mungu anatumbia tuangalie jinsi alivyoumba mbingu (universe), na jinsi alivyoipendezesha mbingu ya chini na nyota (observable universe). Hizi ishara nimezielezea kwa undani katika post yangu and infact ishara ziko nyingi, kuna wanyama, bahari, milima, miti na vyengine (every designing implies designer).

Shida ni akili yako ambayo haiwezi comprehend kuwa Kuna vitu havina mwanzo na Kuna kuna space outside universe kwasababu hata wanasayansi wanakadiria kuwa Kuna uwezekano Kuna zaidi ya ulimwengu mmoja (multiverse).

Kwenye mfano wako wa shimo, sio lazma mchimbaji aingie shimoni, Mungu anatuambia kuwa yeye ni mkubwa sana zaidi ya universe. Kwaiyo kwenye mfano wako wa shimo na mchimbaji haviwezi kuendana. Chukulia mfano wa mtu anavyotengeneza mpira, si lazima aingie katika huo mpira, afterall nani kakuambia Mungu katengeneza ulimwengu kwa mikono yake.

Mungu, anasema elimu aliyotupa ni ndogo Sana, sehemu ambayo tumeigundua katika ulimwengu ni ndogo sana. Tuna LIMIT kujua baadhi ya vitu na vitu vingi hatuvijui, science inathibisha Hilo.
Kumbuka swala la wanasayansi kusema ulimwengu una mwanzo limetokana na uthibitisho wa kiutafiti

Sasa wewe madai yako ya kusema Mungu hana chanzo yana uthibitisho?

Umesema akili ya kawaida haiwezi kutambua, vipi kama hata swala lako la kusema Mungu yupo sio majibu potofu ya akili yako?
 
Kati ya Nyota na Bacteria, Nyota ni kitu rahisi zaidi kiasi kwamba nafasi ya Nyota kuundwa Kwa mnyororo wa matukio ya bahati nasibu ni kubwa kuliko ya Bacteria.

Hivyo uwepo wa nyota sio sababu kubwa ya kufanya uamini lazima kuwe na muundaji mwenye utashi (intelligent designer) nyuma yake.

Hata hivyo hoja ya "muundaji mwenye utashi" haina mashiko kama ukiichunguza Kwa makini bila upendelea wowote.

Na kitu cha ajabu, ndio hoja pendwa zaidi ya waamini wengi humu.

Tuseme hivi, tuna kubaliana kuwa, kitu chochote "tata",

Nikiwa na maana kuwa, kitu chochote kile kilichoundwa na sehemu ndogo ndogo zinazofanya kazi kwa kutegemeana kutimiza lengo moja, mfano Jicho, ubongo au mfumo mzima wa fahamu hauwezi tokea tu kwa bahati nasibu, ni lazima uwe na muumbaji/muundaji nyuma yake.

Inabidi tujiulize swali moja la msingi kabla hatuja endelea na hoja yetu.

Kati ya kitu "tata" na muumbaji wa hiki kitu, yupi ni "mtata" zaidi?

Kwa lugha ya kingereza, "Which/Who is more complex between the created and creator"?

Kwa maneno mengine, yupi mwenye nafasi kubwa ya kutokea kwa bahati nasibu kati ya kiumbe na muumbaji?

Akili ya kawaida inatwambia Muumbaji ni tata zaidi kuliko kiumbe, au kiumbe kina nafasi kubwa ya kutokea kwa bahati nasibu kuliko muumbaji, kwa sababu muumbaji ni mtata/complex zaidi kuliko kiumbe

Kwa maana hio basi, kwa mujibu wa msingi wa hoja yetu, kama kitu chochote tata kinahitaji muumbaji, basi muumbaji pia atahitaji muumbaji , na huyu muumbaji wa pili atahitaji muumbaji wa tatu na orodha inaendelea milele (infinite regression)

Hivyo hoja haiwezi kuwa sahihi, na tukisema muumbaji yeye hahitaji kuumbwa, yeye yupo tu siku zote kwanini tusikubali kuwa kiumbe pia hakihitaji muumbaji?, kwa sababu kiumbe ni rahisi zaidi kuliko muumbaji.

Hivyo ukilazimisha kuwa huu ulimwengu unahitaji muumbaji lazima pia utupatie jibu kuwa huyu muumbaji kaja vipi bila kutumia majibu (ambayo tumeona hapo juu ni ya kijinga) kama muumbaji huyu yupo tu siku zote au hahitaji kuumbwa.

Pia, utaona hapo kuwa, kuna kibarua kingine cha kuthibitisha

Tu assume, umetupa jibu kuwa huyu muumbaji katoka wapi Kwa kukwepa infinite regression fallacy tuliyoiona

Itakulazimu uthibitishe huyu muumbaji ndio huyu Mungu unayemuamini

Mfano kama wewe ni mkristo, inabidi uthibitishe kuwa huyu muumbaji hapo juu

1.Ni mmoja na sio wengi
2.Ana mtoto anaitwa Yesu
3.Aliwahi kuzungumza na binadamu wa zamani mlimani na kuwapa orodha ya vitu 10 ambayo hataki uvifanye
4.Anataka tozo ya 10% ya mshahara wako

Niamini Mimi, huwezi thibitisha aina hii ya hoja.

Lakini kuna namna nyingine LA kutatua hili tatizo la uumbaji.

Kwa sababu swali kumbwa tunalokutana nalo, tunapo chunguza viumbe au utendaji kazi wa Miili yetu kwa mfano.

Ni kipi Kilicho tengeneza huu ubunifu?
Ni nani aliyegundua ili jicho lifanye kazi lazima liwe kwenye muundo huu?

Hatuwezi tumia hoja yetu ya mwanzo kwa sababu tunajua haiwezi fanya kazi.

Ila vipi kama, tuki apply Evolution by natural selection?

Siwezi endelea zaidi kuhusu Evolution na jinsi gani ni jawabu sahihi zaidi la hili swali la uumbaji, ila amini inafanya kazi.

Hata hao NASA, wanaitumia kuunda vifaa vyao vya anga za juu.

In case you don't know, tunaweza Ku simulate evolution by natural selection kwenye computer na tukapata program inayoweza Ku design sophisticated things kama Camera bila utashi wowote...

That is how Real Evolution works.
 
Binafsi naamini Mungu yupo lakini siamini katika dini yoyote na siamini katika #(Mungu wa israel)
 
Kati ya Nyota na Bacteria, Nyota ni kitu rahisi zaidi kiasi kwamba nafasi ya Nyota kuundwa Kwa mnyororo wa matukio ya bahati nasibu ni kubwa kuliko ya Bacteria.

Hivyo uwepo wa nyota sio sababu kubwa ya kufanya uamini lazima kuwe na muundaji mwenye utashi (intelligent designer) nyuma yake.

Hata hivyo hoja ya "muundaji mwenye utashi" haina mashiko kama ukiichunguza Kwa makini bila upendelea wowote.

Na kitu cha ajabu, ndio hoja pendwa zaidi ya waamini wengi humu.

Tuseme hivi, tuna kubaliana kuwa, kitu chochote "tata",

Nikiwa na maana kuwa, kitu chochote kile kilichoundwa na sehemu ndogo ndogo zinazofanya kazi kwa kutegemeana kutimiza lengo moja, mfano Jicho, ubongo au mfumo mzima wa fahamu hauwezi tokea tu kwa bahati nasibu, ni lazima uwe na muumbaji/muundaji nyuma yake.

Inabidi tujiulize swali moja la msingi kabla hatuja endelea na hoja yetu.

Kati ya kitu "tata" na muumbaji wa hiki kitu, yupi ni "mtata" zaidi?

Kwa lugha ya kingereza, "Which/Who is more complex between the created and creator"?

Kwa maneno mengine, yupi mwenye nafasi kubwa ya kutokea kwa bahati nasibu kati ya kiumbe na muumbaji?

Akili ya kawaida inatwambia Muumbaji ni tata zaidi kuliko kiumbe, au kiumbe kina nafasi kubwa ya kutokea kwa bahati nasibu kuliko muumbaji, kwa sababu muumbaji ni mtata/complex zaidi kuliko kiumbe

Kwa maana hio basi, kwa mujibu wa msingi wa hoja yetu, kama kitu chochote tata kinahitaji muumbaji, basi muumbaji pia atahitaji muumbaji , na huyu muumbaji wa pili atahitaji muumbaji wa tatu na orodha inaendelea milele (infinite regression)

Hivyo hoja haiwezi kuwa sahihi, na tukisema muumbaji yeye hahitaji kuumbwa, yeye yupo tu siku zote kwanini tusikubali kuwa kiumbe pia hakihitaji muumbaji?, kwa sababu kiumbe ni rahisi zaidi kuliko muumbaji.

Hivyo ukilazimisha kuwa huu ulimwengu unahitaji muumbaji lazima pia utupatie jibu kuwa huyu muumbaji kaja vipi bila kutumia majibu (ambayo tumeona hapo juu ni ya kijinga) kama muumbaji huyu yupo tu siku zote au hahitaji kuumbwa.

Pia, utaona hapo kuwa, kuna kibarua kingine cha kuthibitisha

Tu assume, umetupa jibu kuwa huyu muumbaji katoka wapi Kwa kukwepa infinite regression fallacy tuliyoiona

Itakulazimu uthibitishe huyu muumbaji ndio huyu Mungu unayemuamini

Mfano kama wewe ni mkristo, inabidi uthibitishe kuwa huyu muumbaji hapo juu

1.Ni mmoja na sio wengi
2.Ana mtoto anaitwa Yesu
3.Aliwahi kuzungumza na binadamu wa zamani mlimani na kuwapa orodha ya vitu 10 ambayo hataki uvifanye
4.Anataka tozo ya 10% ya mshahara wako

Niamini Mimi, huwezi thibitisha aina hii ya hoja.

Lakini kuna namna nyingine LA kutatua hili tatizo la uumbaji.

Kwa sababu swali kumbwa tunalokutana nalo, tunapo chunguza viumbe au utendaji kazi wa Miili yetu kwa mfano.

Ni kipi Kilicho tengeneza huu ubunifu?
Ni nani aliyegundua ili jicho lifanye kazi lazima liwe kwenye muundo huu?

Hatuwezi tumia hoja yetu ya mwanzo kwa sababu tunajua haiwezi fanya kazi.

Ila vipi kama, tuki apply Evolution by natural selection?

Siwezi endelea zaidi kuhusu Evolution na jinsi gani ni jawabu sahihi zaidi la hili swali la uumbaji, ila amini inafanya kazi.

Hata hao NASA, wanaitumia kuunda vifaa vyao vya anga za juu.

In case you don't know, tunaweza Ku simulate evolution by natural selection kwenye computer na tukapata program inayoweza Ku design sophisticated things kama Camera bila utashi wowote...

That is how Real Evolution works.
Ukubwa na udogo wa kitu huonyesha ukuu wa Mungu, ingawa kwenye post sikuzungumzia kuhusu vitu vidogo.

Kwanza Kuna vitu unabidi uvielewe kuhusu dini na imani;

•Nimesema kuwa (according to religious teachings), hatujapewa elimu juu vitu vyote. Akili ya binadamu ni limited.
Hata science bado haiwezi kuelezea mambo mengi ambayo tunayaona kila siku.
Hiyo science unayoiamini bado haina majibu juu ya mambo mengi tu;
Mfano
a. Kwanini tunalala?
b. Kwanini tunaota?
c. Kwanini tunapiga miayo?
d. Kwanini nyanya ina gini nyingi zaidi ya binadamu?
e. Mysteries of black holes
f. How magic works?
g. Source of disappearances in Bermuda triangle

Jiulize ni asilimia ngapi ya ulimwengu ishakuwa explored na binadamu?

Huko mbali, wanasayansi wenyewe wanasema ni asilimia tano tu ya bahari ndio imegunduliwa.
Vip kuhusu hii solar system yetu?
Vipi kuhusu our milky way galaxy?
Then what about billion of galaxies out there?

Kuamini Mungu kwanza you have to submit to the will of God. You have to admit that your mind, level of thinking, intellect and observation are very weak kitu ambacho atheist wengi hawataki kukubali.

Kama akili yako haiwezi kusolve vitu vidogo tu vipi inaweza kudiscuss vitu vikubwa kama creation. Binadamu alieshindwa kujua what is going on in Bermuda triangle!!🤣

Kama akili yako imeshindwa kuaccomodate kuwa Mungu ndio mkubwa zaidi, yeye ndio tata zaidi, hana chanzo, hatakuwa na mwisho na yeye ndio kaumba least complex beings.

Vipi wewe unaamini universe ilianza as tiny particle? Hiyo particle ilitokea wapi? iliundwa na vitu gani, hivyo vitu vilitokea wapi? How can something emerge from nothing? Mwisho wa siku utakuja kuconclude kwamba akili yako haiwezi KAMWE kutolea maelezo vitu vyote. Science is true lakini ina LIMIT yake, uelewa wetu una limit pia.

Msingi mkubwa wa dini/imani ni belief. Hata science imejengwa katika kuamini na kwa ufupi kila taarifa ili ikubalike unapaswa kuiamini.

Kwa layman, kivipi unakubali kuwa binadamu alitua mwezini?

Kivipi unakubali picha za NASA ni real? Sio editing?

Kivipi unakubali uwepo wa black holes na haujawahi kushika hata binoculars/telescope?

Huko mbali, umeshahi kuziona sayari katika mfumo wetu wa jua kwa kutumia devices?

Unaamini matukio ya kihistoria? Je una empirical evidences at you hand?

Kama unakubali kuwepo kwa vitu hivyo basi wewe pia unaamini tu (not witness), na hii haimaanishi kuwa vitu hivyo havipo.

Kwanza ili uamini, unatakiwa kupewa evidence, na evidence ya uwepo wa Mungu ni vitabu vya Mungu, Maisha ya Manabii na Mambo waliyoyafanya.

Pili ili kuithibitisha taarifa fulani you only need to trust the informer (sio lazima information iwe perceived katika sense organ zako)

Kama mnavyowaamini NASA, Historians, researchers, theorists and philosophers ndivyo hivyo nasisi tunawaamini Manabii, their miracles, revelations, books of God n.k.

Haya yote tunayaongea ni kugusia tu kati ya vingi vilivyozungumziwa, bali ushahidi wa uwepo wa Mungu upo katika vitabu vyake. Ni uvivu wa kusoma lakini Kama utasoma vitabu hivyo basi hiyo doubt uliyokuwa nayo itaondoka.

Kuna kila aina ya ushahidi kwenye vitabu hivyo lakini MMEGOMA kuchukua maarifa huko.

Kwa ufupi tu, kama hivi vitabu vya dini vilitungwa na watu, viliwezaje kuzungumzia mambo ya kisayansi ambayo leo yanathibitishwa kuwa ni kweli.

Mfano katika Quran vimezungumziwa vitu vingi ambavyo vinaendana na modern science

-Embryology
-The sky's protection
-Beginning of universe
-Iron within meteorites
-The meeting of the seas
-Sun moving in orbit (galactic revolution of solar system)
-Mountains as stakes
-Expansion of the universe
-Pain receptors and many more.

Katika kutofautiana, unaweza ukachagua cha kuamini na ukakitafutia sababu za kuamini lakini kuna upande mmoja tu ambao uko sahihi.
 
Back
Top Bottom