~ * ~ Mabusu Yangu Dazeni ~* ~

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
HAYA NI MABUSU YANGU DAZENI


Mabusu yangu dazeni, nayatuma kwako moyo!
Ulipo hapo mjini, natuma bila uchoyo,
Pokea wangu wa ndani, ni dazeni nikupayo,
Kwa hili Busu la kwanza, beti nazifungulia!
Mwah!!
Hilo la kwanza kwenye paji!

Mabusu yangu dazeni, moja moja narushia,
Nimeketi barazani, ujumbe nakutumia,
Wenye wivu jinyongeni, wa kwangu namwagia,
Kwa hili busu la pili, asante kwa yote pia!
Mwah!!
Hilo la pili, shavu la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, tumetoka sisi mbali,
Nakumbuka vya zamani, tulipoanza wawili,
Mioyo ikashikani, mahaba yakashamili,
Kwa hili busu la tatu, mbali nakukumbushia!
Mwah!
Hilo la tatu, shavu la kulia!

Mabusu yangu dazeni, ninamshukuru Mola,
Mtukufu wa Mbinguni, mwenye kuzipinga hila,
Kakuleta ubavuni, ni bure siyo kwa hela,
Kwa hili busu la nne, ujue nakuhitaji!
Mwah!
Hilo la nne, shingoni kushoto!

Mabusu yangu dazeni, nisamehe nipokosa,
Yamenijaa pomoni, hata uliponiasa,
Kurudia sitamani, kufanya hivyo ni kosa,
Kwa hili busu la tano, nakuomba samahani
Mwah!
Hilo la tano, shingoni kulia!

Mabusu yangu dazeni, Mungu amekujalia,
Uzuri wako wa shani, binti wa Kitanzania,
Wengineo siwaoni, wewe najichagulia,
Kwa hili busu la sita, nashukuru wewe wangu!
Mwah!
Hilo la sita, mgongoni!!

Mabusu yangu dazeni, penzi lako limefana,
Twapendana kama nini, mitimani twashibana,
Kama tuliopeponi, mahaba yametunona,
Kwa hili Busu la saba, mpenzi nakutamani!
Mwah!
Hilo la saba, kwenye titi la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, wanipa penzi si haba,
Wanipa kiulaini, tena siyo kwa kibaba,
Ya wengine siyaoni, la kwako limeniziba!
Kwa hili busu la nane, naapa mimi ni wako!
Mwah!
Hilo la nane, kwenye titi la kulia!

Mabusu yangu dazeni, wewe nakuaminia,
Mashaka kwako sioni, penzilo limetulia,
Habiba waniamini, moyo umenishikia,
Kwa hili busu la tisa, asante kuniamini!
Mwah!
Hilo la tisa, kitovuni!

Mabusu yangu dazeni, tusiwajali wakora,
Kulivunja watamani, penzi letu lawakera,
Visa wanavyovibuni, tuachane kwa papara,
Kwa hili busu la kumi, tugange mbele kwa mbele!
Mwah!
Hilo la kumi, nyongani kushoto!

Mabusu yangu dazeni, naapa mimi ni wako,
Moyo wangu mkononi, ushike unipe wako,
Kama kufuri langoni, funguo iwe ni yako,
Kwa hili kumi na moja, milele tutapendana!
Mwah
Kumi na moja, nyongani kulia!

Mabusu yangu dazeni, la mwisho nimefikia,
Wabarakatau Ma'nani, kwake nimejiachia,
Akupe afya mwilini, baraka kukumwagia,
Kwa hili busu dazeni, UJUE NINAKUPENDA
Mwah!
Busu hili la dazeni!!......

Haya basi mabusu yote,
Mwah! kwenye paji
Mwah! shavu la kushoto
Mwah! shavu la kulia
Mwah! shingoni kushoto
Mwah! shingoni kulia
Mwah! mgongoni
Mwah! Titi la kushoto
Mwah! Titi la kulia
Mwah! Kitovuni
Mwah! Nyongani kushoto
Mwah! Nyongani kulia
Mwah! ........


na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
mwanakijijiatjamiiforums.com
 
MKuu kumbe huvumi lakini umo ehhhhhhhh!Nilijua wewe ni wa siasa tuuu!
Congrats kwa hizo cheche nimeanza craming nikamwimbie sabuni yangu ya roho!
Umezipangilia kwelikweli!
 
HAYA NI MABUSU YANGU DAZENI


Mabusu yangu dazeni, nayatuma kwako moyo!
Ulipo hapo mjini, natuma bila uchoyo,
Pokea wangu wa ndani, ni dazeni nikupayo,
Kwa hili Busu la kwanza, beti nazifungulia!
Mwah!!
Hilo la kwanza kwenye paji!

Mabusu yangu dazeni, moja moja narushia,
Nimeketi barazani, ujumbe nakutumia,
Wenye wivu jinyongeni, wa kwangu namwagia,
Kwa hili busu la pili, asante kwa yote pia!
Mwah!!
Hilo la pili, shavu la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, tumetoka sisi mbali,
Nakumbuka vya zamani, tulipoanza wawili,
Mioyo ikashikani, mahaba yakashamili,
Kwa hili busu la tatu, mbali nakukumbushia!
Mwah!
Hilo la tatu, shavu la kulia!

Mabusu yangu dazeni, ninamshukuru Mola,
Mtukufu wa Mbinguni, mwenye kuzipinga hila,
Kakuleta ubavuni, ni bure siyo kwa hela,
Kwa hili busu la nne, ujue nakuhitaji!
Mwah!
Hilo la nne, shingoni kushoto!

Mabusu yangu dazeni, nisamehe nipokosa,
Yamenijaa pomoni, hata uliponiasa,
Kurudia sitamani, kufanya hivyo ni kosa,
Kwa hili busu la tano, nakuomba samahani
Mwah!
Hilo la tano, shingoni kulia!

Mabusu yangu dazeni, Mungu amekujalia,
Uzuri wako wa shani, binti wa Kitanzania,
Wengineo siwaoni, wewe najichagulia,
Kwa hili busu la sita, nashukuru wewe wangu!
Mwah!
Hilo la sita, mgongoni!!

Mabusu yangu dazeni, penzi lako limefana,
Twapendana kama nini, mitimani twashibana,
Kama tuliopeponi, mahaba yametunona,
Kwa hili Busu la saba, mpenzi nakutamani!
Mwah!
Hilo la saba, kwenye titi la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, wanipa penzi si haba,
Wanipa kiulaini, tena siyo kwa kibaba,
Ya wengine siyaoni, la kwako limeniziba!
Kwa hili busu la nane, naapa mimi ni wako!
Mwah!
Hilo la nane, kwenye titi la kulia!

Mabusu yangu dazeni, wewe nakuaminia,
Mashaka kwako sioni, penzilo limetulia,
Habiba waniamini, moyo umenishikia,
Kwa hili busu la tisa, asante kuniamini!
Mwah!
Hilo la tisa, kitovuni!

Mabusu yangu dazeni, tusiwajali wakora,
Kulivunja watamani, penzi letu lawakera,
Visa wanavyovibuni, tuachane kwa papara,
Kwa hili busu la kumi, tugange mbele kwa mbele!
Mwah!
Hilo la kumi, nyongani kushoto!

Mabusu yangu dazeni, naapa mimi ni wako,
Moyo wangu mkononi, ushike unipe wako,
Kama kufuri langoni, funguo iwe ni yako,
Kwa hili kumi na moja, milele tutapendana!
Mwah
Kumi na moja, nyongani kulia!

Mabusu yangu dazeni, la mwisho nimefikia,
Wabarakatau Ma’nani, kwake nimejiachia,
Akupe afya mwilini, baraka kukumwagia,
Kwa hili busu dazeni, UJUE NINAKUPENDA
Mwah!
Busu hili la dazeni!!......


na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
mwanakijijiatjamiiforums.com

Ha ha ha kofia nakuvulia mzee...
 
kweli nimeikosa hii burudani muda mrefu,wewe kweli Gwiji.sijui kwanii walitoa ile column ya lugha sikujua mambo kama yanaendelea humu kwa wapenzi.
Hongera.
 
kweli nimeikosa hii burudani muda mrefu,wewe kweli Gwiji.sijui kwanii walitoa ile column ya lugha sikujua mambo kama yanaendelea humu kwa wapenzi.
Hongera.

Tena kuhusu hiyo column ya Lugha mtaniwia radhi kwenda out of topic!Kuna mtu anaweza kunipa hili neno kwa Kiswahili?
Global Positioning System ( GPS )?
 
Tena kuhusu hiyo column ya Lugha mtaniwia radhi kwenda out of topic!Kuna mtu anaweza kunipa hili neno kwa Kiswahili?
Global Positioning System ( GPS )?



pardon me for asking but who you gonna tell abt GPS in kiswahili wakati hajui ni nini hiyo?
au just for the seek ya kujua...?
Ninashangaa bado.

just google KAMASI SANIFU on line alafu utaona
 
Sanda... umenichekesha..

Nadhani Global Positioning System naweza kuiita kuwa ni Chombo/Mfumo wa/cha Kuonesha Mahali
 
Du! Hii sasa ni kali haswa.. Mzee MNKJJ sikujua kama unagonga pande zote kwa level hizi...

Burudani tosha asubuhi yangu ya leo...
 
Nashukuru natumaini nimewapa watu burudani tosha na kwa sekunde chache kuyatoa mawazo yenu kwenye mambo ya kuumiza vichwa..
 
HAYA NI MABUSU YANGU DAZENI


Mabusu yangu dazeni, nayatuma kwako moyo!
Ulipo hapo mjini, natuma bila uchoyo,
Pokea wangu wa ndani, ni dazeni nikupayo,
Kwa hili Busu la kwanza, beti nazifungulia!
Mwah!!
Hilo la kwanza kwenye paji!

Mabusu yangu dazeni, moja moja narushia,
Nimeketi barazani, ujumbe nakutumia,
Wenye wivu jinyongeni, wa kwangu namwagia,
Kwa hili busu la pili, asante kwa yote pia!
Mwah!!
Hilo la pili, shavu la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, tumetoka sisi mbali,
Nakumbuka vya zamani, tulipoanza wawili,
Mioyo ikashikani, mahaba yakashamili,
Kwa hili busu la tatu, mbali nakukumbushia!
Mwah!
Hilo la tatu, shavu la kulia!

Mabusu yangu dazeni, ninamshukuru Mola,
Mtukufu wa Mbinguni, mwenye kuzipinga hila,
Kakuleta ubavuni, ni bure siyo kwa hela,
Kwa hili busu la nne, ujue nakuhitaji!
Mwah!
Hilo la nne, shingoni kushoto!

Mabusu yangu dazeni, nisamehe nipokosa,
Yamenijaa pomoni, hata uliponiasa,
Kurudia sitamani, kufanya hivyo ni kosa,
Kwa hili busu la tano, nakuomba samahani
Mwah!
Hilo la tano, shingoni kulia!

Mabusu yangu dazeni, Mungu amekujalia,
Uzuri wako wa shani, binti wa Kitanzania,
Wengineo siwaoni, wewe najichagulia,
Kwa hili busu la sita, nashukuru wewe wangu!
Mwah!
Hilo la sita, mgongoni!!

Mabusu yangu dazeni, penzi lako limefana,
Twapendana kama nini, mitimani twashibana,
Kama tuliopeponi, mahaba yametunona,
Kwa hili Busu la saba, mpenzi nakutamani!
Mwah!
Hilo la saba, kwenye titi la kushoto!

Mabusu yangu dazeni, wanipa penzi si haba,
Wanipa kiulaini, tena siyo kwa kibaba,
Ya wengine siyaoni, la kwako limeniziba!
Kwa hili busu la nane, naapa mimi ni wako!
Mwah!
Hilo la nane, kwenye titi la kulia!

Mabusu yangu dazeni, wewe nakuaminia,
Mashaka kwako sioni, penzilo limetulia,
Habiba waniamini, moyo umenishikia,
Kwa hili busu la tisa, asante kuniamini!
Mwah!
Hilo la tisa, kitovuni!

Mabusu yangu dazeni, tusiwajali wakora,
Kulivunja watamani, penzi letu lawakera,
Visa wanavyovibuni, tuachane kwa papara,
Kwa hili busu la kumi, tugange mbele kwa mbele!
Mwah!
Hilo la kumi, nyongani kushoto!

Mabusu yangu dazeni, naapa mimi ni wako,
Moyo wangu mkononi, ushike unipe wako,
Kama kufuri langoni, funguo iwe ni yako,
Kwa hili kumi na moja, milele tutapendana!
Mwah
Kumi na moja, nyongani kulia!

Mabusu yangu dazeni, la mwisho nimefikia,
Wabarakatau Ma'nani, kwake nimejiachia,
Akupe afya mwilini, baraka kukumwagia,
Kwa hili busu dazeni, UJUE NINAKUPENDA
Mwah!
Busu hili la dazeni!!......

Haya basi mabusu yote,
Mwah! kwenye paji
Mwah! shavu la kushoto
Mwah! shavu la kulia
Mwah! shingoni kushoto
Mwah! shingoni kulia
Mwah! mgongoni
Mwah! Titi la kushoto
Mwah! Titi la kulia
Mwah! Kitovuni
Mwah! Nyongani kushoto
Mwah! Nyongani kulia
Mwah! ........


na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
mwanakijijiatjamiiforums.com
Hadith yko inatufndsha nn mkuu
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom