Mabucha kupigwa marufuku Tanzania

Shakazulu

JF-Expert Member
Feb 23, 2007
957
280
Tanzania yatangaza mpango mpya wa kuuza nyama

*Mabucha ya nyama kupigwa marufuku nchini kote

* Nyama kuuzwa Supermarket na maeneo maalum



Na Muhibu Said


SERIKALI inapanga kupiga marufuku uuzaji nyama kwenye mabucha na badala yake biashara hiyo itakuwa ikifanywa na maduka makubwa (supermarkets) na maeneo maalum yatakayotengwa nchini.


Mpango huo mpya ambao serikali imedhamiria kuutekeleza kwa dhati wakati wowote katika siku za usoni, ulitangazwa na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Anthony Diallo, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, jijini Dar es Salaam jana.


Waziri Diallo alisema mpango huo umelenga kukidhi mahitaji ya afya za walaji wa nyama na soko la nje la bidhaa hiyo na kwa kuzingatia hilo, wizara yake inafanya mazungumzo na halmashauri ili waweze kuanza kuutekeleza.


Alisema utayarishaji wa nyama katika mabucha unaofanywa kwa ajili ya kuwauzia walaji hivi sasa, umekuwa ukitishia afya zao kutokana na wauzaji kutumia nyenzo zilizotumika kwa muda mrefu, kama vile magogo ya kucharangia nyama, ambayo ubora wake haukidhi mahitaji ya afya.


?Yapo magogo mengine kwenye mabucha yana umri mrefu kuliko hata umri wenu mliopo hapa, yanaendelea kutumika kukatiakatia nyama,? alisema Waziri Diallo huku akiwanyooshea kidole waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wake wa jana.


Alisema mpango huo mpya, utawezesha nyama inayotayarishwa nchini kukubalika kuuzwa katika soko la nje ya nchi kwa kuwa bidhaa hiyo itakuwa imetayarishwa na kuhifadhiwa katika mazingira mazuri.


?Tunazungumza na halmashauri tuweze kubadilisha uuzaji wa nyama ili ziweze kuuzwa kwenye supermarket au kwenye maeneo maalum. Haiwezekani iwe inauzwa kwenye mabucha,? alisema Waziri Diallo.


Mbali na hilo, Waziri Diallo alisema wizara kwa kushirikiana na wadau wengine, imepanga kuongeza uzalishaji wa maziwa na kupanua soko lake nchini, ikiwa ni pamoja na kuhamaisha unywaji wa maziwa na kutekeleza Mpango wa Unywaji Maziwa Shuleni (SMP), ambao unatarajiwa kutekelezwa katika mikoa yote.


Kwa sasa SMP inatekelezwa katika wilaya za Arusha, Hai, Moshi Vijijini, Tanga na Njombe katika shule 39 na inafadhiliwa na wazazi na wasindikaji wadogo.


Alisema wizara imeshauriana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) ambalo limeahidi kuitafutia serikali wafadhili zaidi kwa ajili ya kusaidia kupanua mpango huo katika wilaya nyingine nchini kwa lengo la kuwanufaisha wanafunzi 840,000 kutoka 12,985 wanaonufaika kwa sasa.


Waziri Diallo alisema wizara pia imewasiliana na kampuni mojawapo kubwa ya maziwa duniani ya TETRAPAC kuhusu SMP ambao nao wameahidi kushiriki iwapo serikali itaanzisha mpango huo.


Alisema kutokana na mpango huo, kiasi cha lita milioni 43.7 za maziwa zitanyweka shuleni ikilinganishwa na lita 337,610 zinazonyweka kwa sasa.


?Mpango wa unywaji maziwa shuleni unalenga kuboresha afya za watoto, kuongeza mahudhurio shuleni, kujenga utamaduni wa kunywa maziwa, kupanua wigo wa soko la maziwa na kuongeza ajira,? alisema Waziri Diallo.


Alisema baada ya Sheria ya Maziwa kupitishwa na Bunge mwaka 2004, Bodi ya Maziwa ilianzishwa na tayari imeshaanza kazi na kwamba utaratibu unaandaliwa wa kuanzisha Bodi ya Nyama baada ya sheria husika kupitishwa na Bunge mwaka juzi.


?Sheria hizi zitasimamia ubora wa bidhaa husika kuanzia kwa mfugaji mpaka usindikaji na uuzaji wake ili ufikie viwango vya kimataifa na kuiwezesha nchi kuuza bidhaa bora ndani na nje ya nchi,? alisema Waziri Diallo.


Alisema serikali pia imeanzisha mfumo wa utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo nchini ambapo kupitia mfumo huo, mifugo yote, hususan ng?ombe itatambuliwa, kuandikishwa na kufuatiliwa ili kuhakiki ubora wa mifugo kuanzia katika maeneo inakofugwa.


Diallo alisema katika kutekeleza mfumo huo, mifugo yote, hususan ng?ombe kwa kuanzia, itatakiwa kuvikwa hereni maalum na kwamba mifugo yote itakayouzwa minadani ni ile ambayoimeandikishwa kwenye Rejista ya Taifa ya Takwimu za Mifugo nchini.


Alisema kwa kutumia mfumo huo, katika mwaka 2006/2007, wizara itasajili mashamba ya mifugo 100 na wafugaji 5,000, wakiwamo wa asili, kutambua ng?ombe 20,000 na kuanzisha Rejista ya Taifa ya Takwimu za Mifugo.


Diallo alisema serikali pia inaandaa mpango wa kitaifa wa unenepashaji ng?ombe nchini ambao utekelezaji wake utasimamiwa na serikali za mitaa.


Alisema mpango huo utahusisha unenepeshaji wa mifugo, hususan ng?ombe wa nyama katika umri wa kati ya miaka miwili na mitatu kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa nyama ili kukidhi mahitaji ya soko na kwamba katika mwaka 2006/2007 takriban ng?ombe 26,400 walinenepeshwa kupitia mfumo huo.


Hata hivyo, Diallo alisema wizara inaendelea kuhamasisha uzalishaji wa nyama kupitia mfumo huo kwa wafugaji wadogo kwa kutumia mbinu shirikishi ya shamba darasa (FFS).


Alisema katika mwaka 2006/2007, mauzo ya mifugo na mazao yake yaliyouzwa nje ya nchi, yaliliingizia taifa jumla ya Sh17.3 bilioni ambapo katika mauzo hayo, jumla ya ng?ombe 2,542 na mbuzi 1,852 wenye thamani ya Sh1.3 bilioni waliuzwa nchini Comoro, Kuwait, Falme za Kiarabu (Dubai), Oman na Burundi na tani 92 za nyama ya mbuzi, kondoo na ng?ombe zenye thamani ya Sh352 milioni ziliuzwa nje ya nchi.


Kwa mujibu wa Diallo, Tanzania inakadiriwa kuwa na ng?ombe milioni 18.8, mbuzi wakiwa milioni 13.5, kondoo milioni 3.6, nguruwe milioni 1.37, kuku wa asili milioni 33 na wa kisasa milioni 20 .


Alisema zao la ngozi limeendelea kuwa zao kuu la mifugo linaloliingizia taifa fedha za kigeni ambapo jumla ya vipande vya ngozi za ng?ombe milioni 1.7, mbuzi milioni 1.5 na kondoo 925,530 vyenye thamani ya Sh16.2 bilioni viliuzwa nje ya nchi katika kipindi hicho.


Waziri Diallo alisema mkakati wa kudhibiti ugonjwa wa sotoka, umetekelezwa kwa mafanikio makubwa ambapo Tanzania imetambuliwa na kupewa cheti na Shirika la Afya ya Wanyama Duniani kutokana na virusi vya ugonjwa huo.


Alisema pia mkakati wa kudhibiti ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (RVF) uliotokea nchini kuanzia Februari, mwaka jana, unatekelezwa na kwamba serikali ilitoa Sh4.798 kudhibiti ugonjwa huo na pia mkakati wa kudhibiti ugonjwa wa mafua makali ya ndege, unatekelezwa kwa kujenga uwezo wa kutambua na kufuatilia ugonjwa huo.


Hata hivyo, alisema hadi sasa ugonjwa huo haujathibitika kuwapo nchini ingawa umetokea katika nchi 55, zikiwamo kumi na moja za Afrika ambazo ni Burkina Faso, Cameroon, Ivory Coast, Djibout, Ghana, Misri, Niger, Nigeria, Sudan, Benin na Togo.


Alizitaja changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo kuwa ni pamoja na maeneo ya ufugaji na uhaba wa miundombinu ambayo yamesababisha wafugaji kuhamahama na kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira, kuenea kwa magonjwa ya mifugo na migogoro baina ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.


Nyingine ni uwekezaji mdogo katika sekta ya mifugo ambao umesababisha ukuaji mdogo wa sekta kuliko ilivyotarajiwa, kuwapo kwa magonjwa mbalimbali ya mifugo, tishio la ugonjwa wa mafua makali ya ndege, uhaba wa viwanda na uzalishaji duni wa vilivyopo kwa ajili ya kusindika mazao ya mifugo, ukosefu wa masoko ya uhakika, kutokuwapo kwa taasisi za mikopo yenye masharti nafuu kwa wafugaji, tija ndogo katika uzalishaji wa mifugo hasa ya asili na gharama kubwa za pembejeo za mifugo, zikiwamo dawa za kuogeshea mifugo.
 
basi kazi hipo,hivi hawa viongozi huwa wakiamka tu basi ile ndoto waliyoiota usiku ndio ajenda ya asubuhi.ni sawa na kujenga madarasa bila walimu.
Hapa kinachotakiwa ni kuweka viwango vinavyokidhi ubora na usalama wa mlaji ili kuboresha huduma.ni sawa na kukagua gari kabla ya kuliingiza nchini lakini baada ya hapo hakuna usimamizi wa kuhakikisha ubora wa magari yanayotumika ktk barabara zetu.
 
Huyu anakurupukatu!

Supermarket???? labda mie sijui maana ya supermarket, ama yeye ni waziri wa Dar tu?? hata hivo ni dar ya city center, anaongea supermarket boko, tandahimba, nanyamba , mbamba bay na kibondo kasulu-kigoma ambako hata treni inatumia siku tatu kufika? tena mara moja kwa wiki siku hizi nasikia??

Hizi ni ndoto za mchana! umeme wenyewe wa kuendesha hizo standard za supermarket uko wapi? ama kwa vile yeye shoping yake ni shorprite basi anajua Tanzania nzima iko hivo!!! mwe!
 
Rwabu,

Kumbuka kuwa Diallo ni mfanyabiashara..........(mwenye supermarkets pia).........kapiga chabo kaona upenyo wa uwekezaji.........jinsi gani ya kujiwekea mazingira mazuri ya ulaji.......ndio mawazo (vague) kama hayo yanakuja........wee angalia na fuatilia utasikia........wee unafikiri ulaji uko migodini tu!!!??? no way!.........mbuzi anakula kutokana na urefu wa kamba yake ati!!!......

In short kutokana na hii criticism ya hapa atakuja (Diallo) na version mpya

Agreed Diallo........mazingira ya uuzaji nyama nyumbani kwa kweli sehemu zingine yanatisha na yanitishia afya zetu......hata utayarishaji wa nyama wakati mwingine una mashaka.........sasa je solution ni kufunga??

NO.......Diallo
1. Jaribu kuwawekea watu standards za mabucha na wasipozi-meet wafungiwe.......mfano mzuri tuliona from Mama Ntilie to Mama Lishe (that was credible move).........ingawaje enforcement bado imekuwa very poor ku-aprehend biashara ya mama lishe na suala zima la usafi
 
Mlalahoi anazidi kunyang'anywa tonge mdomoni na siri kali. Hizi bucha zimekuwepo Tanzania miaka nenda miaka rudi na siku zote zimetoa huduma nzuri kabisa. Na nyama wanayouza ni fresh na nyama ya nguruwe, ng'ombe, mbuzi, kondoo inayouzwa katika mabucha hayo ni mifugo ya Tanzania ukilinganisha na ile ya supermarket ambayo ama itakuwa inatoka SA au ulaya ambayo imeshatiwa madawa chungu nzima na si ajabu imekaa siku chungu nzima!

Maisha bora kwa kila Mtanzania hayo! Halafu watu wakiamua kuwa majambazi kwa kukosa shughuli halali za kuwawezesha kuwa na kipato tunalalamika! Kumbe sera za hii sirikali iliyojaa wendawazimu ndio chanzo cha kuongezeka ujambazi kwa sera za kipumbavu kama hii.
 
another pumba by our serikali...ningependa wenye uwezo wa kumfikishia ujumbe huu huyo mtalii aliyeanza safari za ndani ya tz akisaka wachawi wenye nguvu zaidi wamfikishie...

je wazo hili ni la serikali ama ni la diallo peke yake??as ka ni la dialo i will elewa as jamaa ana ma supermarket dat whyanataka aenjoy...

if ni la serikali basi nadiriki kusema wakubwa woote walisupport hili ni ma faaaaa laaaaaaa wanisamehe kwa kuwatusi tena ningekua nina uwezo ningewatusi zaidi na ningependa wafikishiwe huo mzigo wa matusi ila it wont help a thing....

hivi wanawaaambia nini hao wenye ma butcher kwa sasa...wakizi ban wakafanye kazi gani???ndio ajira milioni ngapi hizo she nziii zao kabsaaa

na wanawaambia nini wa tz katika kupata huduma hiyoo??sehemu ambayo hamna supermarket karibu watu wafunge safari kufuata nyama??mbagala kule ndani ndani ukonga sijui na mikoani huko vijijini kusiko na supermarkets?????

i wish ningekua nina personal address za wakuu hao niwatukane vyema....mvi za babazao kabsaaaa!!!

yaani walichokalia wao ni how to benefit matumbo yao na ndugu zao ma bwe geeee sanaaa hawa watu halaf na 2010 watathubutu kurudi tena sema walisaidia maisha ya watanzania!!

kunguru maji kabisa hawa watuuu

leo ndio wanajali afya za watu siku zooote mbona hakijawahi kutokea hayo wanyosema hata wakati kulipokua na rift valley???

kikwete na wasaidizi wako wote ~~*@#~#@##*|~!@ zenu na za wanaowazunguka zina........

natanguliza msamaha kwa ndugu zangu wa JF kwa lugha hii nimejitahid sana ku hold my hasiraz
naomba kwenye personal address ya mkubwa mmojawapo animuvuzishie hata kwa PM yangu then i will take it from there....
 
Hii wazimu tupu viongozi kukosa kazi za kufanya... Kwanza Bongo hakuna mtu anayenunua nyama ilolala siku moja tu...
Tupo huku majuu lakini hata siku moja hatuwezi linganisha nyama za huku na Bongo maanake ukizungumzia magonjwa huku nje nyama yao ndio Uozo kabisa.. nusu saa nje ya friji nyama huvunda pale pale..sii wali wala mayai ni lazima yawe ktk friji hata kama hali ya hewa ni baridi. Kwa hiyo tukiacha mbali umasikini wetu ambao unawafanya wauza nyama wengi wasiwe na uwezo wa kumudu vifaa vya kutendea kazi acha mbali jengo lenyewe..maradhi hayaanzi buchani bali hata majumbani mwa watu ambako nyama huhifadhiwa.
Kwa mtazamo finyu, hii sheria ni sawa kabisa na kusema kuwa serikali ina mpango wa kupiga marufuku vyoo vya shimo Tanzania nzima!...
 
Alisema utayarishaji wa nyama katika mabucha unaofanywa kwa ajili ya kuwauzia walaji hivi sasa, umekuwa ukitishia afya zao kutokana na wauzaji kutumia nyenzo zilizotumika kwa muda mrefu, kama vile magogo ya kucharangia nyama, ambayo ubora wake haukidhi mahitaji ya afya.

Kama hii ndio sababu waliyogundua kwa nini wasiitafutie suluhisho kwanza.
 
exactly kasana!!!......that is what im talking about..........
 
OGAH,,MKANDARA,,/MTAALAM

huyu bwana ana matatizo makubwa,,HUYU NDIE OWNER WA COMMUNITY AIRLINE,,,AMEKUJA NA KASI
NA BEI YAKE NZURI DAR MWZ ,DAR JRO SASA AMEANZA KUFEEL LOSS ANATAKA KUFIDIA KWENYE,,MIFGO KWA KUZIFUNGA BUCHA,,,MHESHIMIWA HAPO UMECHEMSHA NA NDIO UTAKAPOWAJUA WATANZANIA HATUTAKI KUCHEZEWA,,,ONGEZA NAULI KUFIDIA NA WALA SI KUUMIZA WANANCHI,,,EMBU ANGALIENI HUYU MTU KAMA SI WAZIMU,,NDEGE MOJA KAAJIRI WAFANYAKAZI WA NDANI WA NDEGE 31,,
NDEGE INARUKA NA WATU 3 PER DAY,,KAMA SI WAZIMU NINI NINI??HIVI SASA KWA WASIORUKA ATI WANAENDA PALE AIRPORT KUFANYA KAZI KAMA SECURITY HUU NI UUNGWANA????KWA HIYO HUYU MTU MUWE NAE MAKINI SANA,,HAWA VIJANA WANAJULIKANA KWAO WANAFANYA KAZI KWENYE NDEGE HALAFU WANAPITA NDUGU ZAO WANAKUTA WAKI SUPERVISE MIZIIGO WEWE DIALLO UKIWA KAMA MZAZI MWANAO AMEFANYIWA HIVI UNGEJISSIKIAJE ACHENI KUWANYANYASA WATU KAMA MNAJUA HAMNA UWEZO JARIBUNI KUAJIRI WACHACHE MUWEZE KUWALIPA VYEMA,,,ONA ATI KWA KUWAKIMBIZA WAMEANDIKA MIKATABA YAO MICHAFU AMBAYO NI TOFAUTI NA SHERIA ZA TCCA,,UNAMWANDIKIA MTU MKATABA ,,,ANALIPWA FLYING ALLOWANCE ILA UKIULIZA MBONA HAIPO KIPENGELE CHA FLYING ALLOWANCE UNAAMBIWA TUNAKUAKIKISHIA UTATAPATA,,,,,WEWE KAMA COMMUNITY IMEKUSHINDA USIJARIBU KUFIDIA KWINGINE JARIBU KUWA KAMA WAZIRI NA NINACHOFURAHI NAJUA UMESOMA ILA MAMBO ANAYOFANYA HUWEZI KUJUA KAMA NI MSOMI,,,,
HONGERA KWA CA KEEP IT UP ILA UKIJA KWENYE MABUCHA HATUKUACHI
 
Ogah,
Unajua hata huku nje hakuna bucha inayoruhusiwa kukata nyama juu ya meza ya bati ama Plastic isipokuwa mbao tena basi hiyo meza inatakiwa kuwa na upana wa at least 2" na sio chini ya hapo. Kwa hiyo wenye mabucha wengi hujenga meza kwa kutumia kuunganisha mbao za 2x2. Sasa sielewi ni kitu gani kilichopo ktk mbao hizi tofauti sana na magogo yanayotumika nyumbani, zaidi ya hapo ikiwa swala ni kuwepo meza kama hizi kwa nini asingesema hivyo?
 
Correct Bob!!

we need to standardise some of our stuffs.....and to do this a big committment is required na sio hizi hadithi za Charlie Champlin!!!!!..............huyu bwana ni very funny na anahitaji ushauri "nasaha" wala sitanii........

kama ktk ilani ya CCM ni kuongeza ajira, ingefaa aeleze pia kwa kuchukua hatua hiyo anaongeza au kupunguza ajira kwa kiasi gani, majosho na machinjio anayaimarisha kivipi, ni maeneo gani ya miji/mikoa hiyo sheria ita-apply (thats the funny part of Diallo's tamko),.............wow i can go on and on and on..............sasa jamaa naona anakurupuka tu.

anyway pengine waandishi wetu wamem-quote vibaya....ngoja tusikie majibu yake kutokana na reaction za watu

....si unasikia media ya US wanavyo laumiana wao kwa wao kuhusu exaggeration na watu kuwa out of context kutokana na media........isije ikatukuta na hapa JF sometimes
 
Nina wazo nalo ni la kuona mbali.....

Kwanza ni kukusanya mtaji, BOT etc

Pili ni kuwekeza ktk biashara kubwa kubwa.

Tatu ni kuanza kuwazidishia maskini umaskini, Funga maduka mitaani maana bidhaa zina expire wao wanaendelea kuuza, funga bucha za nyama, standard za usafi sio mzuri.

Nne ni kuhamishia biashara hizo kwenye ma super market au ministores zetu tulizokwisha kufungua.

Tano ni usafiri na nyumba. Dala dala zote piga marufuku. Akina Ogah wenye vi daladala kimoja OUT! sie tuliokwisha kusanya tunaleta mabasi makubwa (yes tunazo hela!!!)

Sita hairuhusiwi kujenga, lazima ukitaka kujenga ujengewe na Property developers, Yes! ndio standard nyumba hizo! sure inabidi Johson Lukaza na associates ndio wakujengee!

Baada ya hapo uchumi na mali vipo mikononi mwetu, tunamchagua rais tumtakaye na tunafanya tutakavyo!

Well, baada ya vision hiyo, mi naenda kujiunga nao! naenda kuwa FISADI..nyie endeleeni kulalamika!

Just thinking aloud!
 
"
Alisema mpango huo mpya, utawezesha nyama inayotayarishwa nchini kukubalika kuuzwa katika soko la nje ya nchi kwa kuwa bidhaa hiyo itakuwa imetayarishwa na kuhifadhiwa katika mazingira mazuri."

This is really another pumba. Hivi nyama iliyoko buchani Tandale kwa Tumbo for local consumption tutawezaje ku impress exports? Hawezi kuwa mjinga kiasi hiki, huyu inawezekana anafanya makusudi.
 
Haswaa FD,

nami nakuja mniuzie share mzee...........nshachoka na haka kadaladala kangu hahahahahah!!

Na huo ndio ukweli wenyewe FD
 
Msameheni jamaa huyu kwa vile hajui atendalo. Ningemaspoti sana kama angesema kuwa wanaweka standard za usafi kwenye mabucha ya nyama, lakini siyo kukurupuka na kudai kuwa watafunga mabucha. Wanataka wale mashemeji wangu wa kigogo wanaomiliki mabucha hapo Dar wakale wapi ati, wakawe ombaomba?
 
basi kazi hipo,hivi hawa viongozi huwa wakiamka tu basi ile ndoto waliyoiota usiku ndio ajenda ya asubuhi.ni sawa na kujenga madarasa bila walimu.
Hapa kinachotakiwa ni kuweka viwango vinavyokidhi ubora na usalama wa mlaji ili kuboresha huduma.ni sawa na kukagua gari kabla ya kuliingiza nchini lakini baada ya hapo hakuna usimamizi wa kuhakikisha ubora wa magari yanayotumika ktk barabara zetu.

Kwa nchi nzima ndoto kama hii haitatekelezeka kamweeeee. Ni kweli hii ni sawa na ujenzi wa shule fasta wakati walimu huna au sawa na kutangaza vita wakati hata gobole huna. Bila shaka Waziri hadi anaketi kitini alikuwa hajajua atazungumza nini. Likamtoka
 
"
Alisema mpango huo mpya, utawezesha nyama inayotayarishwa nchini kukubalika kuuzwa katika soko la nje ya nchi kwa kuwa bidhaa hiyo itakuwa imetayarishwa na kuhifadhiwa katika mazingira mazuri."

This is really another pumba. Hivi nyama iliyoko buchani Tandale kwa Tumbo for local consumption tutawezaje ku impress exports? Hawezi kuwa mjinga kiasi hiki, huyu inawezekana anafanya makusudi.


The stuff in red is great
 
Hii nchi haiwezi kupiga hatua za kimaendeleo kwa fikra duni kama hizi. Kwa kufunga hayo mabucha mnaondoa ajira ngapi za waTZ? Je huko vijijini mtapeleka hayo ma supermarketi? This Is nonsense Mr Diallo, muwe mnafikiria mara 1000 ndio mtamke maana mara 2 naona haitoshi
 
FD,

Wewe umekuwa msataarabu sana. Ukweli ni kuwa jamaa wavutia kwenye penu zao halafu wanaweka matundu kwenye penu za wengine wote ili wahakikishe zinavuja.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom