hendeboy
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 218
- 21
TANGAZO
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawatangazia wateja wake wanaotumia mita za LUKU, Shirika litafanya maboresho kwenye mfumo wa kuuza LUKU tarehe 01/09/2012.MTEJA WA TANESCO UNAYETUMIA MITA ZA LUKU ZINGATIA YAFUATAYO:
MABORESHO YA UINGIZAJI UMEME KWENYE MITA ZA LUKU NCHINI
- Nunua umeme wa kwanza kuanzia tarehe 01/09/2012 kutoka ofisi za TANESCO au wakala wa LUKU. Baada ya hapo utaendelea kununua umeme kwa njia yoyote upendayo kama kawaida.
- Utakaponunua umeme kwenye ofisi za TANESCO au wakala wa LUKU utapatiwa namba mbili za maboresho pamoja na Vocha ya umeme .
- Mara upatapo namba hizo, tafadhali ziingize kwenye mita yako ukianzia na namba ya mabadilisho ya kwanza (Key Change Token 1), halafu bonyeza au #, kisha ingiza namba ya pili (Key Change Token 2) halafu bonyeza au #. Mwisho ingiza namba zilizoko kwenye Vocha ya LUKU.
- Tembelea ofisi za TANESCO ili kujua wakala wa LUKU unapopaswa kununua umeme na maelekezo zaidi. Pia orodha ya Mawakala immebandikwa kwenye ofisi zao.