Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,000
- 9,861
Tanzania imeboresha hatua za kuchukuliwa ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya #CoronaVirus kwa Wasafiri na kujuisha hatua za usafirishaji wa bidhaa na huduma
Watanzania na wageni wanaoishi nchini wametakiwa kutosafiri kwenda nchi zilizoathiriwa kama hakuna ulazima. Wasafiri wote watakaoingia nchini watawekwa karantini kwa gharama zao
Baada ya siku 14 muhusika aliyewekwa Karantini ataruhusiwa kutoka na atatakiwa kuacha taarifa binafsi zitakazosaidia katika ufuatiliaji
Wasafiri wote watakaoingia nchini watafanyiwa ukaguzi wa kina pamoja na kuchukuliwa vipimo vya #Covid19 pale itakapotakiwa kufanywa hivyo
Mashirika ya ndege yanashauriwa kuwa na seti mbili za Wahudumu (crew) ili wabadilishwane watakapofika nchini na kuondoa ulazima wa kukaa Katantini
Endapo msafiri atapata dharura yoyote ya afya atatakiwa kupiga simu ya bure ya afya 199. Ushauri huu unaweza kuendelea kuboreshwa kulingana na mabadiliko na hali ya #CoronaVirus nchini
#JFCOVID19_Updates
Watanzania na wageni wanaoishi nchini wametakiwa kutosafiri kwenda nchi zilizoathiriwa kama hakuna ulazima. Wasafiri wote watakaoingia nchini watawekwa karantini kwa gharama zao
Baada ya siku 14 muhusika aliyewekwa Karantini ataruhusiwa kutoka na atatakiwa kuacha taarifa binafsi zitakazosaidia katika ufuatiliaji
Wasafiri wote watakaoingia nchini watafanyiwa ukaguzi wa kina pamoja na kuchukuliwa vipimo vya #Covid19 pale itakapotakiwa kufanywa hivyo
Mashirika ya ndege yanashauriwa kuwa na seti mbili za Wahudumu (crew) ili wabadilishwane watakapofika nchini na kuondoa ulazima wa kukaa Katantini
Endapo msafiri atapata dharura yoyote ya afya atatakiwa kupiga simu ya bure ya afya 199. Ushauri huu unaweza kuendelea kuboreshwa kulingana na mabadiliko na hali ya #CoronaVirus nchini
#JFCOVID19_Updates