Maboresho katika karatasi ya kupigia kura ili kuleta usawa kati ya wagombea

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Nimejaribu kuichunguza karatasi ya kupigia kura ya Urais wa JMT katika uchaguzi huu uliopita, na nina machache ya kuchangia.

Nianze kwanza kwa kusema karatasi ya kupigia kura inabidi kuichukulia kama ni nyaraka muhimu sana. Uzito wa kipekee unahitajika katika kuibuni, kuichapisha, kuisambaza na kuihifadhi. Kwa nilichokiona katika uchaguzi huu wa 2020, sidhani kama lolote kati ya hayo yalizingatiwa. Najua nayasema haya katika nyakati na mazingira ambayo inaonyesha kama wenye mamlaka wameamua waitupe mkono mfumo wa demokrasia na siasa safi, lakini matumaini bado yapo kuwa siku yaja ambayo tutarudi nyuma na kujirekebisha.

Ngoja sasa niorodheshe baadhi ya vitu nilivyoona katika karatasi hii:

KURA URAIS.jpg


  • Picha ya mgombea wa Urais inatakiwa ndiyo ianze kushoto na ya mgombea mwenza ifuate, kinyume na walivyofanya.
  • Pia nitazungumzia 'inconsistencies' katika karatasi hii. Hapa namaanaisha jambo moja kufanyika kwa mgombea mmoja lakini halikufanyika kwa mgombea mwingine. Nitatoa mifano michache:
    • Mgombea mwenza wa CCM, Samia Suluhu Hassan ametajwa kwanza kwa jina la kwanza. Ukiangalia Mgombea mwenza wa CHADEMA, ametajwa kwanza kwa jina lake la Mwisho. Sijajua kwa wagombea wengine kwa sababu siwafahamu vizuri.
    • Mgombea wa CCM, John Magufuli ametajwa kwanza kama Dkt. wakati mgombea wa CUF, title yake ya Prof. haikuwekwa.
    • Kwenye majina ya vyama, font size hazifanani na zingine kama ziko bold wakati zingine haziko bold, mfano za ACT, CHADEMA, CHAUMMA, etc. ni ndogo zaidi ya nyingine.
  • Hakuna haja wala umuhimu wa kurudia title ya 'CHAMA', 'MGOMBEA UMAKAMU WA RAIS', 'MGOMBEA URAIS' wala 'ALAMA' kwa kila mgombea. Hizi titles zingewekwa tu juu pale zikiwa bold na maandishi makubwa zinatosha.
  • Kuna hili suala lingine ambalo limeongelewa sawa la utaratibu gani ulitumika katika kuamua orodha hii ya wagombea iwekwe vipi. Ninavyokumbuka, NEC walisema ilitokana na jinsi wagombea walivyorudisha fomu zao. Hili sitaliongelea kwa sababu wote tunajua hizo zilikuwa ni geresha tu. Itoshe kusema huo siyo utaratibu wala majibu ya kisomi kwa watu walioelimika. Nadhani utaratibu sahihi ni kufuata alphabetical order ya majina ya chama au majina ya mwisho ya wagombea. Na hili liwekwe wazi katika kanuni za uchaguzi ili kuepuka 'surprises'.
  • Mfano wa karatasi hii utolewe mapema zaidi, ili mapungufu yaweze kurekebishwa na maboresho kufanywa. Kama nilivyosema hapo awali, muundo wa karatasi hii utajwe wazi katika sheria kuu za uchaguzi na kusiwe na room ya kirahisi rahisi ya kuzibadilisha kama inavyofanyika sasa.
  • Jukumu la kuelimisha njia sahihi za kuitumia karatasi hii libebwe na NEC wenyewe. Kuna wagombea walitoa matamko ambayo kisheria walitakiwa waadhibiwe. Kuna mmoja alinukuliwa akisema 'wewe angalia mtu wa kwanza tu hapo juu, weka tiki, wengine huko chini siyo wagombea halali'
  • Karatasi ya kupigia kura iorodheshwe kama ni nyaraka muhimu sana katika nchi, Sheria itungwe ambayo itasema kuwa atakayekutwa na karatasi hii zaidi ya copy moja nje ya kituo cha kupigia kura, adhabu kali ichukuliwe dhidi yake.

Nimalizie tu kwa kusema, ukiacha mapungufu haya niliyotaja hapo juu ambayo nadhani mengine yalifanywa kama maamuzi ya makusudi, sidhani kama hii ikaratasi imekuwa designed na professional designing na printing company inayojitambua. Inaonyesha ni kama karatasi ambayo imetengenezwa katika kaduka ka stationery na dada mmoja ambaye pia anauza vocha za tigo. Maandishi ya majina hayana uwiano, baadhi yako juu zaidi, mengine katikati, mengine kushoto zaidi. Halafu unaniambia kuna mabilioni yametumika hapa kwa kazi hii?

Tanzania ni urithi wetu sote, hakuna atakayeweza kulibadilisha hilo.
 
Kwa taarifa yako hizo karatasi zilichapwa na TISS kwa lengo la kumbeba Magufuli na chama chake. Kwa maneno marahisi hakukuwa na uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Bila mawakala kuruhusiwa hiyo karatasi hata iboreshwe vipi haitasaidia wananchi kumchagua wamtakae.
Wanasema 'there is more than one way to skin a cat'. Unaweza kuruhusiwa kuingiza mawakala wako woote na bado ukafanyiwa figisu kwingine.

Mimi nimeona niliangalie hili suala moja kwa leo ambalo nalo lina umuhimu wa kipekee.
 
Kwa taarifa yako hizo karatasi zilichapwa na TISS kwa lengo la kumbeba Magufuli na chama chake. Kwa maneno marahisi hakukuwa na uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Mkuu sikupingi.

Tunapoangalia mbele, tuchunguze na tujadili kila uchochoro uliotumika na unaoweza kutumika kufanya hayo uliyoita 'maonyesho ya ujinga'.
 
NYAZIFA ZA JUU SELIKALINI ZINATOLEWA KINDUGU AMA KIKABILA.

Umeandika mambo ya muhimu sana Mkuu nimekuelewa sana.

Hoja zako ni nzito na zenye mashiko sana.

SHIJA NAWAOPEWA NAFASI ZA UTEUZI UWEZO WAO NI MDOGO SANA WANAPEWA KINDUGU NA MAMLAKA ILI WATAWALIWE WANVYOTAKA.

TANZANIA NI NCHI MASIKINI SANA.
NA TUNA LAANA YA UMASIKINI WA FIKRA.

jiwe anazidi kutuangusha.
 
Kwa taarifa yako hizo karatasi zilichapwa na TISS kwa lengo la kumbeba Magufuli na chama chake. Kwa maneno marahisi hakukuwa na uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Najiuliza kama hadi TISS waakikuwa hawamuungi mkono Lisu alitegemea atashinda vipi sasa?

Yani huungwi mkono na chombo cha usalama hata kimoja utashindaje sasa?

Lisu akikuwa debe tupu. Hajui siasa
 
Mkuu sikupingi.

Tunapoangalia mbele, tuchunguze na tujadili kila uchochoro uliotumika na unaoweza kutumika kufanya hayo uliyoita 'maonyesho ya ujinga'.

Siku ccm ikiwa na uhakika wa kushinda kwa njia ya Kura, haya mapendekezo yako ndio yatafanyiwa kazi.
 
Kwa taarifa yako hizo karatasi zilichapwa na TISS kwa lengo la kumbeba Magufuli na chama chake. Kwa maneno marahisi hakukuwa na uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Wala siyo ujinga wa mtu mweusi, bali uroho wa wenye mamlaka Afrika. Museveni nae kaliamsha huko Uganda. Mungu aturehemu!
 
Najiuliza kama hadi TISS waakikuwa hawamuungi mkono Lisu alitegemea atashinda vipi sasa?

Yani huungwi mkono na chombo cha usalama hata kimoja utashindaje sasa?


Lisu akikuwa debe tupu. Hajui siasa

Kwa hiyo unatwambia kuwa/kupata Cheo cha nafasi ya Uraisi ni mpaka ukubalike na Tiss sio !?Kwa hiyo hatufuati Sheria ,tunafanya mambo yetu kwa matakwa ya watendaji wa Tiss.

Basi sawa tume kuelewa Mkuu.
 
Najiuliza kama hadi TISS waakikuwa hawamuungi mkono Lisu alitegemea atashinda vipi sasa?

Yani huungwi mkono na chombo cha usalama hata kimoja utashindaje sasa?

Lisu akikuwa debe tupu. Hajui siasa

Kwani Tiss wanapenda kufanya waliyofanya, au muundo wa katiba ndio hauwaruhusu kusimamia wanachopaswa?
 
Kwa hiyo unatwambia kuwa/kupata Cheo cha nafasi ya Uraisi ni mpaka ukubalike na Tiss sio !?Kwa hiyo hatufuati Sheria ,tunafanya mambo yetu kwa matakwa ya watendaji wa Tiss.

Basi sawa tume kuelewa Mkuu.
Huwezi kutumwa na Amsterdam uje ugombee urais TISS wakakuangalia tu. Uwepo wao utakuwa hauna maana.
 
Kwani Tiss wanapenda kufanya waliyofanya, au muundo wa katiba ndio hauwaruhusu kusimamia wanachopaswa?
Unafikri Lisu angekuwa anakubarika hao TISS hawana uwezo wa kuumuunga mkono awe rais?

Sasa mtu kaja hapa kaenda Zanzibar anasema Yeye na chadema hawana maslahi na Zanzibar. Mara Amsterdam kila siku anatoa vitisho kwa taasisi za selikali kwa sababu anampigania Lisu awe rais.

Wakamzoom wakaona hapa hatuna mtu tuna kopo tu.
 
Huwezi kutumwa na Amsterdam uje ugombee urais TISS wakakuangalia tu. Uwepo wao utakuwa hauna maana.

Uwe na hakika ya unacho kisema Mkuu ,hata angetumwa na Nyani bado angetakiwa kutawala Nchi kwa kufuata Katiba na sio kwa matakwa ya Nyani.
 
Uwe na hakika ya unacho kisema Mkuu ,hata angetumwa na Nyani bado angetakiwa kutawala Nchi kwa kufuata Katiba na sio kwa matakwa ya Nyani.
Yule mtu hafai hata juwa mjumbe wa nyumba 10
 
Unafikri Lisu angekuwa anakubarika hao TISS hawana uwezo wa kuumuunga mkono awe rais?

Sasa mtu kaja hapa kaenda Zanzibar anasema Yeye na chadema hawana maslahi na Zanzibar. Mara Amsterdam kila siku anatoa vitisho kwa taasisi za selikali kwa sababu anampigania Lisu awe rais.

Wakamzoom wakaona hapa hatuna mtu tuna kopo tu.

Hili la maslahi ya Zanzibar alilizungumzia katika uungwaji mkono kwenye masuala ya kupiga kura tu na sio katika mambo ya Muungano kama Nchi na uendeshwaji wake.

Swala la Amsterdam Lissu alishasema yule ni Wakili wake na hakuna Kosa kisheria yeye kuwa na Wakili katika kumsimamia.
 
Unafikri Lisu angekuwa anakubarika hao TISS hawana uwezo wa kuumuunga mkono awe rais?

Sasa mtu kaja hapa kaenda Zanzibar anasema Yeye na chadema hawana maslahi na Zanzibar. Mara Amsterdam kila siku anatoa vitisho kwa taasisi za selikali kwa sababu anampigania Lisu awe rais.

Wakamzoom wakaona hapa hatuna mtu tuna kopo tu.

Hao Tiss wana kura ngapi? Kama hao Tiss waliona Lisu hafai kwa sababu zako za kuokoteza, mbona hawakumpa Slaa urais?
 
Unafikri Lisu angekuwa anakubarika hao TISS hawana uwezo wa kuumuunga mkono awe rais?

Sasa mtu kaja hapa kaenda Zanzibar anasema Yeye na chadema hawana maslahi na Zanzibar. Mara Amsterdam kila siku anatoa vitisho kwa taasisi za selikali kwa sababu anampigania Lisu awe rais.

Wakamzoom wakaona hapa hatuna mtu tuna kopo tu.
TZ hatuna TISS,tuna kundi la wahuni na wauaji tu!
 
TZ hatuna TISS,tuna kundi la wahuni na wauaji tu!
Kwa vile wamemzuia AMSTERDAM asitawale nchi yetu kwa mgongo wa Lisu ndio wanakuwa wahuni?

Tulipokuwa tunawaambia Amsterdam anamharibia Lisu mlikuwa mmeziba masikio?
 
Back
Top Bottom