Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,890
wabongo sita, wakiwemo mabondia wanne, inasemekana wametiwa mbaroni huko mauritius leo asubuhi kwa kile kilichoelezwa kukutwa na madawa ya kulevya.
kwa mujibu wa tovuti ya http://www.defimedia.info/ watuhumiwa hao walikamatwa na kikosi cha kuzuia mihadarati na kwamba watafikishwa mahakama ya Mahébourg mchana huu na kustakiwa kwa kukutwa na mihadarati.
huo unaweza kuwa ndio mwisho wa safari ya timu ya taifa ya ndondi ambayo iko huko kwa ajili ya kushiriki kwenye ubingwa wa afrika, kwani timu yote pamoja na kocha wao imehusishwa katika kashfa hiyo.
pichani juu shoto ni bondia emilia patrick ambaye ndiye bondia pekee wa bongo ambaye anatakiwa atuwakilishe kwenye michuano ya olympic huko beijing. wa chini yake ni kocha nassoro michael na kulia chini ni petro mtagwa. majina ya wengine hayakupatikana mara moja.
Kwa mujibu wa waandaji wa michuano hiyo wamesema tukio hilo halitoathiri mashindano hayo, ila tanzania ndio imeshajitoa yenyewe..
kwa mujibu wa tovuti ya http://www.defimedia.info/ watuhumiwa hao walikamatwa na kikosi cha kuzuia mihadarati na kwamba watafikishwa mahakama ya Mahébourg mchana huu na kustakiwa kwa kukutwa na mihadarati.
huo unaweza kuwa ndio mwisho wa safari ya timu ya taifa ya ndondi ambayo iko huko kwa ajili ya kushiriki kwenye ubingwa wa afrika, kwani timu yote pamoja na kocha wao imehusishwa katika kashfa hiyo.
pichani juu shoto ni bondia emilia patrick ambaye ndiye bondia pekee wa bongo ambaye anatakiwa atuwakilishe kwenye michuano ya olympic huko beijing. wa chini yake ni kocha nassoro michael na kulia chini ni petro mtagwa. majina ya wengine hayakupatikana mara moja.
Kwa mujibu wa waandaji wa michuano hiyo wamesema tukio hilo halitoathiri mashindano hayo, ila tanzania ndio imeshajitoa yenyewe..