2015ready
JF-Expert Member
- Feb 15, 2011
- 372
- 130
MABOMU YALIPUKA!!!!
:A S 20:
Kwanza kabisa nawapa pole wale wote walio poteza ndugu na mali zao katika janga hili.
Pili nawapa pole wale wote ambao wamejeruhiwa kwa namna moja au nyingine kutokana na mkasa huu wa mabomu kulipuka.
Tatu. Raisi Kikwete hakikisha unapokea taarifa kamili kuhusu mkasa mzima na uitangazie umma ni nini kilicho sababisha mabomu hayo kulipuka. Hakikisha wahusika wote kuanzia juu mpaka chini unawa-wajibisha kikamilifu. Wafukuze kazi mara moja kwa kuwa wazembe katika kazi zao. Hakikisha wale wote walioathirika na janga hili wanafidiwa kisawasawa. Kwa walio poteza maisha yao, hakikisha wanazikwa kwa heshima zote na wewe ukihuzulia mazishi yao.
Nne. Hakikisha ghala la kuhifadhia silaha za serikali zinahamishwa na kuwekwa mbali na makazi ya watu kwaajili ya usalama wa watanzania pamoja na usalama wa silaha zenyewe. Hakikisha idadi ya mabomu yote inapatikana (yaliyo lipuka pamoja na yaliyosalia).
Kama utashindwa kufanya hivyo, basi nakuomba wewe mwenyewe ujiwajibishe kwa kuachia ngazi.
Tano. Hili ni janga la Taifa zima na usizani kuwa ni la CCM pekee.
:A S 20:
Kwanza kabisa nawapa pole wale wote walio poteza ndugu na mali zao katika janga hili.
Pili nawapa pole wale wote ambao wamejeruhiwa kwa namna moja au nyingine kutokana na mkasa huu wa mabomu kulipuka.
Tatu. Raisi Kikwete hakikisha unapokea taarifa kamili kuhusu mkasa mzima na uitangazie umma ni nini kilicho sababisha mabomu hayo kulipuka. Hakikisha wahusika wote kuanzia juu mpaka chini unawa-wajibisha kikamilifu. Wafukuze kazi mara moja kwa kuwa wazembe katika kazi zao. Hakikisha wale wote walioathirika na janga hili wanafidiwa kisawasawa. Kwa walio poteza maisha yao, hakikisha wanazikwa kwa heshima zote na wewe ukihuzulia mazishi yao.
Nne. Hakikisha ghala la kuhifadhia silaha za serikali zinahamishwa na kuwekwa mbali na makazi ya watu kwaajili ya usalama wa watanzania pamoja na usalama wa silaha zenyewe. Hakikisha idadi ya mabomu yote inapatikana (yaliyo lipuka pamoja na yaliyosalia).
Kama utashindwa kufanya hivyo, basi nakuomba wewe mwenyewe ujiwajibishe kwa kuachia ngazi.
Tano. Hili ni janga la Taifa zima na usizani kuwa ni la CCM pekee.