Mabilioni ya Uswisi yaguswa na Rasimu!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,800
Rasimu ya Katiba mpya iliyozinduliwa juzi na Makamu wa Rais wa Tanzania,Dr.Mohamed Gharib Bilal imeyazungumzia mabilioni ya vigogo,hasa viongozi wa umma. Ibara ya15, Ibara ndogo ya 2 inakataza kiongozi wa umma kufungua na kendesha akaunti ya benki nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isipokuwa tu kwa utaratibuutakaoruhusiwa na sheria.

Ibara 15(2) ya Rasimu inasomeka:
(2)Mtumishi wa Umma -
(a)hatafungua au kuendesha akaunti ya benki nje ya Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna ambayo sheria za nchi zinaruhusu.(Msisitizo ni wangu)

Tume ya Jaji Joseph Sinde Warioba imeyakumbuka mabilioni yaUswisi, ambayo kwa siku za hivi karibuni yalikuwa maarufu na kujaribu kuyazungumzia kikatiba. Taarifa za ndani na nje ya nchi zinaonesha kuwa viongozi mbalimbali wa sasa na wa zamani wa umma wa Tanzania wanamiliki akauntiz enye mabilioni ya pesa katika nchi za Uswisi na kwingineko.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Zitto Zuberi Kabwe alishawasilisha Hoja Maalum Bungeni kutaka Serikali isaidie ili mabilioni ya Uswisi yarudi nchini kujenga uchumi wetu.Hatahivyo,hadi sasa Serikali iko kimya na Hoja ya Zitto iko ‘pending'.

Ni juzi juzi tu,Zitto amemuandikia barua Waziri Mkuu wa Uingereza,David Cameron kumuomba msaada wa kufanikisha kurejeshwa kwa mabilioni hayo toka Uswisi.

Waungwana,utekelezaji wa Ibara hii,kama ikipita kama ilivyo,utakuwaje? Jambo hili litawezekana kuwakataza ‘wenye nchi' kuficha ‘visenti'vyao nje ya Tanzania?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Rasimu ya Katiba mpya iliyozinduliwa juzi na Makamu wa Rais wa Tanzania,Dr.Mohamed Gharib Bilal imeyazungumzia mabilioni ya vigogo,hasa viongozi wa umma. Ibara ya15, Ibara ndogo ya 2 inakataza kiongozi wa umma kufungua na kendesha akaunti ya benki nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isipokuwa tu kwa utaratibuutakaoruhusiwa na sheria.

Ibara 15(2) ya Rasimu inasomeka:
(2)Mtumishi wa Umma -
(a)hatafungua au kuendesha akaunti ya benki nje ya Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna ambayo sheria za nchi zinaruhusu.(Msisitizo ni wangu)

Tume ya Jaji Joseph Sinde Warioba imeyakumbuka mabilioni yaUswisi, ambayo kwa siku za hivi karibuni yalikuwa maarufu na kujaribu kuyazungumzia kikatiba. Taarifa za ndani na nje ya nchi zinaonesha kuwa viongozi mbalimbali wa sasa na wa zamani wa umma wa Tanzania wanamiliki akauntiz enye mabilioni ya pesa katika nchi za Uswisi na kwingineko.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Zitto Zuberi Kabwe alishawasilisha Hoja Maalum Bungeni kutaka Serikali isaidie ili mabilioni ya Uswisi yarudi nchini kujenga uchumi wetu.Hatahivyo,hadi sasa Serikali iko kimya na Hoja ya Zitto iko ‘pending'.

Ni juzi juzi tu,Zitto amemuandikia barua Waziri Mkuu wa Uingereza,David Cameron kumuomba msaada wa kufanikisha kurejeshwa kwa mabilioni hayo toka Uswisi.

Waungwana,utekelezaji wa Ibara hii,kama ikipita kamai livyo,utakuwaje? Jambo hili litawezekana kuwakataza ‘wenye nchi' kuficha ‘visenti'vyao nje ya Tanzania?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Si kila mtu ni binadamu mkuu.
 
Tatizo ni hayo maneno "mtumishi wa umma!" Inaonesha kwamba mtu asiye mtumishi wa umma anaweza kufungua akaunti nje ya nchi. Huu ni mwanya mzuri sana wa watumishi wa umma kuwatumia wasio watumishi wa umma kufungua akaunti nje ya nchi!
 
Mkuu Buchanan umenena vyema.Lakini,Ibara husika iko Sura ya Tatu juu ya Maadili na Miiko ya Uongozi na Utumishi wa Umma
 
Last edited by a moderator:
vp kuhusu wafanya biashara? naweza kuiba fedha serikalini nikiwa kama mtumishi wa umma alafu nikajiuzulu na kuzipeleka uswisi, by the time nazipeleka uswisi mimi sio mtumishi wa umma tena.
wanasheria mnasemaje kuhusu hilo,
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom