Mabilionea 100 anaotengeza Kikwete ni kina nani?

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Kwa muda sasa nimekuwa nafuatilia kwa makini sana juhudi za Kikwete za kutengeza mabilionea mia moja tu (100) wa kitanzania katika kipindi chake cha uongozi.

Kwa muda haikuniingia akilini kuwa ni sera gani ya kiuchumi au ni mshauri gani wa kiuchumi ambaye Kikwete anamfuata ili kufanya hili liwe kweli. Swali la nyongeza ni kuwa je ni pesa au vyanzo gani vya pesa vitatumiwa na Kikwete kutengeneza hawa mabilionea watanzania mia moja?

Taarifa ya mkaguzi wa mahesabu ya serikali kwa mwaka 2006 ilionyesha kuwa kuna matumizi zaidi ya bilioni moja ya ikulu ya Kikwete ambayo hayakuwa na ufafanuzi wowote (soma kuwa walitumia kila aina ya wizi na uongo lakini bado wakashindwa kuficha pesa bilioni moja, je ni kiasi gani walifanikiwa?), mwaka 2007 ulijaa report ya matumizi mabaya ya pesa katika miradi mibovu kama ya richmonduli, wizara ya ujenzi, wizara ya ulinzi, nk.

Baada ya report ya wizi wa BOT, nimeanza sasa kutambua maana ya maneno ya Kikwete ya kutengeneza mabilionea mia moja. Taratibu majina ya vijana mafisadi wanaokuja juu kina Lukaza na wengine yameanza kutengeneza list hii. Wakili fisadi na mtetezi wa mafisadi mengi Tanzania ndugu Mkono ameingia moja kwa moja kwenye hii list. Mzee wetu wa Richmonduli - Lowasa naye bado hajachoka na ulaji wa pesa ya bure ya serikali.

Hii ya wizi wa BOT na ushiriki wa kina Rostam Azizi na kampuni yake ya Kagoda imezidi kufunua maana ya maneno ya Kikwete. Kitendo cha mtoto wa Kikwete kuingia kwenye kampuni la kifisadi la wanasheria wa IMMA kinaelezea vizuri mwelekeo wa Kikwete na juhudi zake za kutengeneza mabilionea mia moja.

Swali linalounguza sasa hivi (burning question) ni kuhusu hao wengine ambao watakuwemo kwenye hii list ya aibu. Kwa vile Kikwete anapata 10% ya kila tukio la kifisadi linalotokea nchini (kama huamini muulize karamagi swali kuwa ni kwanini bado yeye ni waziri), basi kuna uwezekano kabisa kuwa Kikwete atakuwa ni number moja kwenye hii list. Katika siku zinazofuatia nitajaribu kutafuta mabilionea wengine ambao Kikwete anatengeneza kwa njia za wizi na kifisadi na ubadhilifu wa mali za watanzania.

Swali binafsi kwako Kikwete, wewe na hao mabilionea 99 wenzako mnategemea kuishi wapi siku ya siku ikifika?
 
Sitajali nikiwemo mimi wenu mtiifu Nyani Amulunde Libimpopo Bangoi Wa Bangoi Kukunvinza Kasamba Nyani Wa Ngabu
 
MwK:
Je, hiyo orodha ya mabilionea ni kuanzia 2005, wakati utawala wa Kikwete ulipoanza? (yaani waliotengenezwa na Kikwete mwenyewe); au tuanzie huko alikotokea Mkapa?

Basi, mimi naanzia orodha tokea enzi ya Mkapa:
1. Mkapa mwenyewe
2. Mama Mkapa
3. Rostam
4. Mkono
5. Kikwete
6. Lowasa
7. Mramba
8. Manji
9. Mengi
10.Dewji
11. Backresa

Kwa hiyo tunaweza kusema hadi hapo 2010, atakuwa ametimiza kabisa hilo lengo lake la hao mabilionea 100!

What a joke for the poor wananchi!!! This is what they wanted?
 
Jeetu Patel: fedha za Epa si ndo zilizonunulia Mahindra 200 kwa ajili ya CCM.
Tanil Somaiya, Vithlathi: Radar,Ndege ya Rais, na Iveco za Jeshi
Balali. hapa sina cha kusema sana.

Rostam Aziz:si ndo Pagoda?

EL: si ndo Richmond

Kina Makanza, Malegesi na Company

Nazir Karamagi: Buzwagi
 
MwK:
Je, hiyo orodha ya mabilionea ni kuanzia 2005, wakati utawala wa Kikwete ulipoanza? (yaani waliotengenezwa na Kikwete mwenyewe); au tuanzie huko alikotokea Mkapa?

Basi, mimi naanzia orodha tokea enzi ya Mkapa:
1. Mkapa mwenyewe
2. Mama Mkapa
3. Rostam
4. Mkono
5. Kikwete
6. Lowasa
7. Mramba
8. Manji
9. Mengi
10.Dewji
11. Backresa

Kwa hiyo tunaweza kusema hadi hapo 2010, atakuwa ametimiza kabisa hilo lengo lake la hao mabilionea 100!

What a joke for the poor wananchi!!! This is what they wanted?

Pamoja na mabilionea wa Mkapa ambao wana their separate own day in court, ninahangaishwa sana na hawa mabilionea wa Kikwete ambao yeye anawatengeneza in less than two years!
 
Kalamu,
Mbona unamsahau mheshimiwa mwenyewe? Atatengenezaje mabilionea na yeye abaki nje? Pili, Lowassa anastahili kuchukua namba 2 siyo sita kama ilivyoorodhesha hapo. Nadhani yeye mali aliyojilimbikizia ni maradufu ya Mkapa. Hata hivyo Mkapa hayuko mbali sana katika catching up.
 
Hivi kuna raha gani kuishi maisha ya ufahari katikati ya mafukara? Huku ukijua kwamba ni resources za hao mafukara ndio umezitumia kujineemesha wewe na familia na ndugu zako wa karibu.
Kwani mafisadi kama vile Ferdinand Marcos, Mobutu Sese Seko, Chiluba na wengine wengi wameishia wapi?
 
Capitol Hill fahari ya maisha ya mtu tajiri kati ya mafukura ni uwezo wa kuwaonesha kuwa yeye "kaukata"!
 
Mbona unamsahau mheshimiwa mwenyewe? Atatengenezaje mabilionea na yeye abaki nje?

Mkuu Jasusi,

Heshima mbele, huyu bado ni msafi unless kuna something unajua kiweke hapa tumkome nyani maana wewe ninakuaminia!
 
Capitol Hill fahari ya maisha ya mtu tajiri kati ya mafukura ni uwezo wa kuwaonesha kuwa yeye "kaukata"!

Nimekupata mkuu..this way watu kama akina Edward Lowassa wanapoenda kwenye majimbo yao kama vile EL anavyoenda Monduli na kufanya kufuru kwa ku throw New Years party na kualika anybody who can come which means almost wilaya mzima. Yes, I am speaking from a real experience kwani I have been to one of those New Years parties two years ago ni ni balaa. Watu ni wengi mno, nafikiri wanaweza kujaa Target Center Naona ni huo ufahari na sifa za kusimamishwa makanisani kusalimia waumini ndizo zinazo wa drive watu kutaka more and more. On the other side, ukiangalia on average a Monduli resident ni masikini na wenye unrealibale sources of income.
 
Field Marshall Es,
Inasemekana hilo bomba la mafuta kwenda bara litakuwa chini yake kupitia nyumba ndogo!...Oooops!
 
Hao mabilionea wa bongo....mmh..wengi wao ukidadisi tu maisha hata ya wapwa zao ni shida ngumu...ndio wawawase walalahoi!
I am not for this utajiri wa kujiwekea grill hadi uvunguni....some kind of prison!
 
Kwa muda sasa nimekuwa nafuatilia kwa makini sana juhudi za Kikwete za kutengeza mabilionea mia moja tu (100) wa kitanzania katika kipindi chake cha uongozi.

Kwa muda haikuniingia akilini kuwa ni sera gani ya kiuchumi au ni mshauri gani wa kiuchumi ambaye Kikwete anamfuata ili kufanya hili liwe kweli. Swali la nyongeza ni kuwa je ni pesa au vyanzo gani vya pesa vitatumiwa na Kikwete kutengeneza hawa mabilionea watanzania mia moja?

Taarifa ya mkaguzi wa mahesabu ya serikali kwa mwaka 2006 ilionyesha kuwa kuna matumizi zaidi ya bilioni moja ya ikulu ya Kikwete ambayo hayakuwa na ufafanuzi wowote (soma kuwa walitumia kila aina ya wizi na uongo lakini bado wakashindwa kuficha pesa bilioni moja, je ni kiasi gani walifanikiwa?), mwaka 2007 ulijaa report ya matumizi mabaya ya pesa katika miradi mibovu kama ya richmonduli, wizara ya ujenzi, wizara ya ulinzi, nk.

Baada ya report ya wizi wa BOT, nimeanza sasa kutambua maana ya maneno ya Kikwete ya kutengeneza mabilionea mia moja. Taratibu majina ya vijana mafisadi wanaokuja juu kina Lukaza na wengine yameanza kutengeneza list hii. Wakili fisadi na mtetezi wa mafisadi mengi Tanzania ndugu Mkono ameingia moja kwa moja kwenye hii list. Mzee wetu wa Richmonduli - Lowasa naye bado hajachoka na ulaji wa pesa ya bure ya serikali.

Hii ya wizi wa BOT na ushiriki wa kina Rostam Azizi na kampuni yake ya Kagoda imezidi kufunua maana ya maneno ya Kikwete. Kitendo cha mtoto wa Kikwete kuingia kwenye kampuni la kifisadi la wanasheria wa IMMA kinaelezea vizuri mwelekeo wa Kikwete na juhudi zake za kutengeneza mabilionea mia moja.

Swali linalounguza sasa hivi (burning question) ni kuhusu hao wengine ambao watakuwemo kwenye hii list ya aibu. Kwa vile Kikwete anapata 10% ya kila tukio la kifisadi linalotokea nchini (kama huamini muulize karamagi swali kuwa ni kwanini bado yeye ni waziri), basi kuna uwezekano kabisa kuwa Kikwete atakuwa ni number moja kwenye hii list. Katika siku zinazofuatia nitajaribu kutafuta mabilionea wengine ambao Kikwete anatengeneza kwa njia za wizi na kifisadi na ubadhilifu wa mali za watanzania.

Swali binafsi kwako Kikwete, wewe na hao mabilionea 99 wenzako mnategemea kuishi wapi siku ya siku ikifika?
Sikushangaa niliposoma haya angekua ameandika MWANAKIJIJI ningelisoma twice angalau kutafuta ukweli but hoja kama hii kuandikwa na wewe si ajabu huna FACTS but its full of HISIA na Mawazo Mgando.Kitu ambacho ni kawaida yako.

Labda unijibu swali moja unauthibitisho upi wa kudai 10% anapewa kikwete na karamagi.Richmunduli what is it?Rostam Aziz ametengenezwa vipi na kikwete kua mmoja wa mabilionea? Kuna uhusiano upi btn Rostam na Kagoda husomi vyombo vya habari?hujaenda brella kujua Directors wa Kagoda?LOWASA umedai anakula hela za wananchi bure ni zipi hizo?

Nacho shangaa inakuaje mtu unaongozwa na hisia bila facts ifike mahali tu conclude hapa ni FORUM YA MAJUNGU.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Sikushangaa niliposoma haya angekua ameandika MWANAKIJIJI ningelisoma twice angalau kutafuta ukweli but hoja kama hii kuandikwa na wewe si ajabu huna FACTS but its full of HISIA na Mawazo Mgando.Kitu ambacho ni kawaida yako.

Labda unijibu swali moja unauthibitisho upi wa kudai 10% anapewa kikwete na karamagi.Richmunduli what is it?Rostam Aziz ametengenezwa vipi na kikwete kua mmoja wa mabilionea? Kuna uhusiano upi btn Rostam na Kagoda husomi vyombo vya habari?hujaenda brella kujua Directors wa Kagoda?LOWASA umedai anakula hela za wananchi bure ni zipi hizo?

Nacho shangaa inakuaje mtu unaongozwa na hisia bila facts ifike mahali tu conclude hapa ni FORUM YA MAJUNGU.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Sikushangaa niliposoma haya angekua ameandika MWANAKIJIJI ningelisoma twice angalau kutafuta ukweli but hoja kama hii kuandikwa na wewe si ajabu huna FACTS but its full of HISIA na Mawazo Mgando.Kitu ambacho ni kawaida yako.

Labda unijibu swali moja unauthibitisho upi wa kudai 10% anapewa kikwete na karamagi.Richmunduli what is it?Rostam Aziz ametengenezwa vipi na kikwete kua mmoja wa mabilionea? Kuna uhusiano upi btn Rostam na Kagoda husomi vyombo vya habari?hujaenda brella kujua Directors wa Kagoda?LOWASA umedai anakula hela za wananchi bure ni zipi hizo?

Nacho shangaa inakuaje mtu unaongozwa na hisia bila facts ifike mahali tu conclude hapa ni FORUM YA MAJUNGU.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI


Haya yako ndio MAWAZO MGANDO hiviunataka facts gani au zipi????
Hivi hujui ni hapa hapa ndio Hilo SAGA la BOT ndio limeaanzia?? na RIchmond,Buzwagi na mengineyo na sasa anza kua mwangalifu wewe na wenzio tutawataja mmoja mmoja huu ni mwanzo tu...

Wana JF mbona mnawasahau kuwaweka mambwana zao (mabilionea ) DUGU ZETU TANZANIA ENYE ASILI YA KIHINDI........!!!???
hao ndio wanao wafichia ,mapesa yao na siri zao.
 
watu wengine wanataka kuharibu threads za watu. kama huna cha kuchangia si ukatafune bigijii!

yaani wewe kwako ni Mwanakijiji tu.........mmmmm
 
Mtoto wa Mkulima,

Mkuu JK alisema kwa mdomo wake mwenyewe kuwa anajenga Mabillionea 100 sasa nadhani itakuwa vema kama utatupa mwanga wa picha ya utekelezaji wa mkakati huo maanake sisi wengine tupo kizani.
Kisha tunaweza pima uzito wa maelezo ya Bibie hapo juu na facts ambazo unazo. Kunradhi lakini!
 
Sikushangaa niliposoma haya angekua ameandika MWANAKIJIJI ningelisoma twice angalau kutafuta ukweli but hoja kama hii kuandikwa na wewe si ajabu huna FACTS but its full of HISIA na Mawazo Mgando.Kitu ambacho ni kawaida yako.

Labda unijibu swali moja unauthibitisho upi wa kudai 10% anapewa kikwete na karamagi.Richmunduli what is it?Rostam Aziz ametengenezwa vipi na kikwete kua mmoja wa mabilionea? Kuna uhusiano upi btn Rostam na Kagoda husomi vyombo vya habari?hujaenda brella kujua Directors wa Kagoda?LOWASA umedai anakula hela za wananchi bure ni zipi hizo?

Nacho shangaa inakuaje mtu unaongozwa na hisia bila facts ifike mahali tu conclude hapa ni FORUM YA MAJUNGU.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Wewe nawe kwa kujikombakomba kwa Mwanakijiji? Huna taarifa kuwa Mkjj hapendi watetezi wa mafisadi kama wewe kujikombakomba kwake?
 
Sikushangaa niliposoma haya angekua ameandika MWANAKIJIJI ningelisoma twice angalau kutafuta ukweli but hoja kama hii kuandikwa na wewe si ajabu huna FACTS but its full of HISIA na Mawazo Mgando.Kitu ambacho ni kawaida yako.

Labda unijibu swali moja unauthibitisho upi wa kudai 10% anapewa kikwete na karamagi.Richmunduli what is it?Rostam Aziz ametengenezwa vipi na kikwete kua mmoja wa mabilionea? Kuna uhusiano upi btn Rostam na Kagoda husomi vyombo vya habari?hujaenda brella kujua Directors wa Kagoda?LOWASA umedai anakula hela za wananchi bure ni zipi hizo?

Nacho shangaa inakuaje mtu unaongozwa na hisia bila facts ifike mahali tu conclude hapa ni FORUM YA MAJUNGU.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Ama kweli Mtot wa Mkulima (sic). Hivi unajua ofisi za BRELLA ziko wapi, na umeshaingia mule ndani ukaona the way they keep their records. Unapiga simu na shillingi elfu sitini mkononi kesho yake kampuni unayo, tuulize tunaoijua BRELA!

Je unajua Tanzania inapoteza US$ 500 million kila mwaka kwa kile ambacho kinaiitwa kutokuwa na FACTS! Na unajua kuwa kila siku unaziona hizo FACTS na huzitambuai.

Wake up my brother nchi, inaisha FACTS zingine ukionyeshwa hutaishi, watakuua au utajinyonga brother. Ngoja nikupe moja tu - Je unajua kuwa mafuta yanayosamehemwa kodi tanzania ni zaidi ya yale yanayolipiwa kodi. Na kodi inayokusanywa kutokana na mafuta ni zidi ya US$ 120 kila mwezi sasa piga hesabu mwenyewe! Je unajua kuwa wenye uwezo wa kulipa kodi ndo wanasamehewa kodi Tanzania? Au unataka FACTS zaidi!

Angalia brother you might get what you asked for, read the fine print and between the lines! Pia achana na mambo ya CCM wengine tumekuwepo tumeyaona na hata T-Shirt tukavaa na sasa tumezivua!
 
Lakini Rais Kikwete hakuishia hapo. Amewaagiza Mwanasheria Mkuu, IGP na Takukuru, kuchunguza na kuwachukulia hatua za kisheria wezi wote wa pesa za BoT; ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zao.
 
Back
Top Bottom