Mabenki yaanza kukusanya Tozo za Serikali kwenye miamala wanayofanya wateja

je parle

JF-Expert Member
Nov 28, 2018
1,847
3,561
LEO NIMEPATA SMS KUTOKA NMB BANK IKISEMA IFUATAVYO:

Ndugu Mteja, tunakusanya tozo ya serikali kwenye akaunti yako kwa miamala ya tarehe 8 Sep 2021 mpaka 6 Oct 2021. Unaweza hakiki kupitia taarifa ya akaunti.

Ujumbe huo. Watanzania inafika point huna pakupumua kila sehemu tozo bank tozo kwenye simu tozo. Mnataka tuende wapi? Juzi nimetuma crdb to crdb nimeliwa 7500 huku nmb napo wanachukua tozo.

Kwenye simu miamala moto unawaka. Tunaumizana sana nchi hii

NMB.JPG
 
KWENU, National microfinance bank(nmb), hua mnajinasibu na kujifaragua kwamba ukiwa na akaunti ya nmb kutuma pesa kwenda nmb ni bure (Kama nimekosea msomaji mwingine anaweza kunikosoa au kunirekebisha) Sasa Jana usiku mmeniletea ujumbe yakwamba tunakusanya tozo za serikali kutokana na miamala uliofanya.

Miamala niliofanya ni ya kwenda nmb pia,Sasa je Kuna tozo nmb kwenda NMB? Kama lipo mbona wateja hatufahamu?

Kama ndio hivyo ondoeni Ile tangazo kwamba kutuma pesa nmb kwenda nmb ni bureeeeee,
 
KWENU, National microfinance bank(nmb),hua mnajinasibu na kujifaragua kwamba ukiwa na akaunti ya nmb kutuma pesa kwenda nmb ni bure...
Ndugu Mteja, tunakusanya tozo ya serikali kwenye akaunti yako kwa miamala ya tarehe 8 Sep 2021 mpaka 6 Oct 2021. Unaweza hakiki kupitia taarifa ya akaunti.
 
Nimepata ujumbe mfupi kutoka NMB ya unaosema" Ndugu Mteja, tunakusanya tozo ya serikali kwenye account yako kwa miamala ya tarehe 8 Sep 2021 mpaka 6 Oct 2021. Unaweza hakikisha kupitia taarifa ya akaunti".

Nimejisikia vibaya sana. Sasa naelewa kwa nini CCM hawapendi constructive idea za akina Mbowe, Msigwa, Chacha, Sugu, Lema nk. Badala yake wanatekeleza idea za watu wanaosema tuhamie Rwanda au tupasuke.

Mungu wa haki hatawaacha salama.
 
Nimeshangaa niliweka hela flani nikakuta hela imepungua after one week na sio account yenye makato ya kila mwezi. sijui ni nini hizi mambo aisee
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom