Mabele Marando aliondokaje Usalama wa Taifa?

Status
Not open for further replies.

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,342
6,467
Marando amesema mwenyewe kuwa alikuwa mwajiliwa wa usalama wa taifa, sasa ni vipi aliacha kazi hiyo? Alifukuzwa? Kwa nini alifukuzwa? Alistaafu? Na alikuwa na wadhifa gani wakati anatoka huko? Je, si bado mmoja wao?
 
Marando amesema mwenyewe kuwa alikuwa mwajiliwa wa usalama wa taifa, sasa ni vipi aliacha kazi hiyo? Alifukuzwa? Kwa nini alifukuzwa? Alistaafu? Na alikuwa na wadhifa gani wakati anatoka huko? Je, si bado mmoja wao?
Du..Maswali mazito kwelikweli haya!..pia nina wasiwasi baadhi yake yanamhitaji yeye mwenyewe ayajibu kwa usahihi, vinginevyo utalishwa sumu hapa!
 
ah sikuwahi kujiuliza hii ishu. ila labda kuna muda wa kustaafu au kustaafishwa kwa manufaa fulani.....
 
UWT watu wanastafuu na kuruhusiwa kufanya shughuri nyingine. Mwiko kwake ni kutoa taarifa za ndani kwa wakati ule alipokuwa anafanya kazi. Kuna wabunge wengi ndani ya CCM walikuwa UWT, mfano Dr Kitine tena aliwahi kuwa bosi pale, na alikuwa mbunge wakati wa Mkapa, sasa kuna kosa ngani marando kuwa Chadema?
 
Marando amesema mwenyewe kuwa alikuwa mwajiliwa wa usalama wa taifa, sasa ni vipi aliacha kazi hiyo? Alifukuzwa? Kwa nini alifukuzwa? Alistaafu? Na alikuwa na wadhifa gani wakati anatoka huko? Je, si bado mmoja wao?

Hiyo statement aliitamka lini???
tufaamishe kwanza..
ila kwa mawazo yangu ya haraka atakua aliacha nafasi ile wakati anijiingiza kwenye mchakato wa kuanzisha vyama vingi..
mana yeye ni kati ya wale waasisi wachache
 
UWT watu wanastafuu na kuruhusiwa kufanya shughuri nyingine. Mwiko kwake ni kutoa taarifa za ndani kwa wakati ule alipokuwa anafanya kazi. Kuna wabunge wengi ndani ya CCM walikuwa UWT, mfano Dr Kitine tena aliwahi kuwa bosi pale, na alikuwa mbunge wakati wa Mkapa, sasa kuna kosa ngani marando kuwa Chadema?

una akika unachoKINENA???
 
PAS- ndio ilivyo. Marando kwa ufahamu kidogo nilionao, alitoka UWT siku nyingi(Baada ya Nyerere Kusataafu). wakaanzia vuguvugu la vyama vingi, 1992 wakiwa na agenda yao ya NCCR(Sikumbuki kilefu chake, ila kipo). Hivyo ndio iliyo za chama cha NCCR-Mageuzi baada ya mfuno wa vyama vingi kupitishwa. Kwenye nchi yenye utawala wa kisheria sio tatizo kwa afisa wa UWT kustaafu na kushirika katika siasa. Najua wako wengi ndani ya CCM kwa sasa ambao ni wabunge na wanatoka UWT, mfano ni PM-Mizengo Pinda. Tatizo ni kwamba kazi ya UWT ni kulinda National Interst, na sio ya chama kama wanavyofanya sasa. UWT kama wangukuwa wanafanya kazi yao sawa sawa, Richmond isngetokea, kwani wanatakiwa kujua mapema nini kinaendelea. Lakini kwa kuwa wao ni sehemu ya CCM, hawakuona. ila nadhani wapo wacheche ambao wanajua kazi zao, watafanya nini sasa?
 
Nimewahi kusikia hawa watu huwa wanatumika hata baada ya kustaafu,na ukumbuke ni amri.Je haitupi wasiwasi na UWT uliogeuka kuwa UWC(Usalama Wa CCM) ukawa na mikono kwenye vyama vya upinzani kupitia watu kama Marando?NCCR palitokea mgogoro kikadhoofu sana,naomba mwenye taarifa za utendaji wake,kama alihusika na migogoro au la,na kivipi kwa wakati akiwa NCCR pia kilichomtoa huko ni nini.Nina wasiwasi naye saana.
 
Wapo wengi tuu mtaani ambao wamestaafu so sioni shida kwa marando
Tena wapo ambao wametoka baada ya kuona usalama wa taifa umekuwa usalama wa chama
 
Nadhani gogolo la pale NCCR lilitokana na Mrema-Mwanausalama mwingine, kuwa agenda yake pale. ndipo mambo hayakuwa sasa.
 
Mabere Nyaucho Marando alikuwa mwajiriwa wa UWT tangu enzi za Mwl Nyerere.Mabere Marando alikuwa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kudai mfumo wa vyama vingi kabla ya mfumo huo kuruhusiwa rasmi.

Marando alikuwa mwenyekiti wa mwanzo wa NCCR Mageuzi kabla hajampisha A L Mrema mwaka 1994.Marando alibakia na nafasi ya katibu mkuu wa NCCR Mageuzi na mbunge wa Rorya na baadae mbunge wa Afrika mashariki.Marando alishiki kwa kiasi kikubwa kuisambaratisha NCCR Mageuzi kwa kuhakikisha mkutano mkuu wa NCCR Mageuzi unashindwa kufanyika,alishikiri kuandaa vijana kuanzisha vurugu ndani ya mkutano hali iliyosababisha Mwenyekiti wake Mzee wa Kiraracha kujificha chini ya meza.Marando alizawadiwa ubunge wa EAC na CCM kama malipo ya kuisambaratisha NCCR Mageuzi.

Mabere Nyaucho Marando mwanasheria na kachero wa juu alishiriki vita vya kumwangusha idd Amin wa Uganda.Alitumia taaluma yake ya ukachero kuingia ndani ya nchi ya Uganda kabla majeshi yetu yaliyokuwa yakiongozwa na kamanda David Musuguri hayajatia mguu Kampala.

Taaluma ya ukachero si mbaya kama baadhi ya watu wanavyodhani inategemea inavyotumiwa na watawala.Tanzania ukachero enzi za Mwl Nyerere ulijikita zaidi kwenye mambo ya ulinzi na usalama wa nchi,wakati huo Tanzania ilitumia rasilimali zake nyingi kuzukomboa nchi zilizokuwa zinatawaliwa na wakoloni [Waingerezera,Wareno na nk].Bahati mbaya baada ya vita vya ukombozi kumalizika kwa mafanikio makubwa usalama wa taifa [UWT] wamejikita kulinda viongozi walioko madarakani kwa kutumia mbinu haramu.

Nchi zilizoendelea na zinazoinukia kiuchumi kitengo cha ukachero pamoja na mambo ya usalama kinatumiwa kuangalia maslahi ya kiuchumi zaidi.Dunia ya leo uchumi mzuri na wenye nguvu ni usalama tosha kwa taifa lolote makini.UWT haina habari ya uchumi wa nchi ndiyo maana baadhi ya maofisa wake walishiriki bila hofu yoyote kwenye ufisadi uliofanyika BOT.UWT haioni ubaya madini yetu ya Tanzanite yakiuzwa kama malighafi India.UWT haina hofu raia wa nchi za kigeni wakiajiriwa kwenye makampuni mabali mbali nafasi ambazo zingekuwa za raia wa Tanzania.UWT imeshindwa kuishauri serekali kwamba ingetakiwa kuwa mbia wa migodi yote ya madini ya dhahabu.UWT imeshikilia kazi moja kubwa ya kulinda serekali ya CCM isiondoshwe madarakani.
 
Mabere Nyaucho Marando alikuwa mwajiriwa wa UWT tangu enzi za Mwl Nyerere.Mabere Marando alikuwa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kudai mfumo wa vyama vingi kabla ya mfumo huo kuruhusiwa rasmi.

Marando alikuwa mwenyekiti wa mwanzo wa NCCR Mageuzi kabla hajampisha A L Mrema mwaka 1994.Marando alibakia na nafasi ya katibu mkuu wa NCCR Mageuzi na mbunge wa Rorya na baadae mbunge wa Afrika mashariki.Marando alishiki kwa kiasi kikubwa kuisambaratisha NCCR Mageuzi kwa kuhakikisha mkutano mkuu wa NCCR Mageuzi unashindwa kufanyika,alishikiri kuandaa vijana kuanzisha vurugu ndani ya mkutano hali iliyosababisha Mwenyekiti wake Mzee wa Kiraracha kujificha chini ya meza.Marando alizawadiwa ubunge wa EAC na CCM kama malipo ya kuisambaratisha NCCR Mageuzi.

Mabere Nyaucho Marando mwanasheria na kachero wa juu alishiriki vita vya kumwangusha idd Amin wa Uganda.Alitumia taaluma yake ya ukachero kuingia ndani ya nchi ya Uganda kabla majeshi yetu yaliyokuwa yakiongozwa na kamanda David Musuguri hayajatia mguu Kampala.

Taaluma ya ukachero si mbaya kama baadhi ya watu wanavyodhani inategemea inavyotumiwa na

Nchi zilizoendelea na zinazoinukia kiuchumi kitengo cha ukachero pamoja na mambo ya usalama kinatumiwa kuangalia maslahi ya kiuchumi zaidi.Dunia ya leo uchumi mzuri na wenye nguvu ni usalama tosha kwa taifa lolote makini.UWT haina habari ya uchumi wa nchi ndiyo maana baadhi ya maofisa wake walishiriki bila hofu yoyote kwenye ufisadi uliofanyika BOT.UWT haioni ubaya madini yetu ya Tanzanite yakiuzwa kama malighafi India.UWT haina hofu raia wa nchi za kigeni wakiajiriwa kwenye makampuni mabali mbali nafasi ambazo zingekuwa za raia wa Tanzania.UWT imeshindwa kuishauri serekali kwamba ingetakiwa kuwa mbia wa migodi yote ya madini ya dhahabu.UWT imeshikilia kazi moja kubwa ya kulinda serekali ya CCM isiondoshwe madarakani.

Mkuu nimeikubali hiyo post yako marando bado haeleweki... ila DOKTA SLAA ni mtu makini pamoja na chama chake hivyo kama marando ni mamluki atatimuliwa kama ilivo kua kwa KAFULILA
 
yeye kama raia mwingine wowote ana uhuru wa kushiriki shuguli mbalimbali za kijamii kwa maslahi ya tanzania , kushiriki shuguli za kisiasa ni kwa interests za taifa pia hata huko kwenye vyama kuna watu wa usalama wa kutoa taarifa na kuwashauri viongozi maswala mbalimbali kwahiyo msiogope sana - usalama wa taifa wako kwa maslahi yetu ni wananchi wa kawaida kama nyie sema utafauti uko kwenye utendaji wa kazi ni sawa na dereva wa basi na konda wake wote wana majukumu kutokana na mkataba wao wa kazi
 
Mkuu nimeikubali hiyo post yako marando bado haeleweki... ila DOKTA SLAA ni mtu makini pamoja na chama chake hivyo kama marando ni mamluki atatimuliwa kama ilivo kua kwa KAFULILA

Unasema Kafulia alikuwa alikuwa mamluki ? UNAWEZA UKAELEZEA ZAIDI.
 
Mkuu nimeikubali hiyo post yako marando bado haeleweki... ila DOKTA SLAA ni mtu makini pamoja na chama chake hivyo kama marando ni mamluki atatimuliwa kama ilivo kua kwa KAFULILA

Heshima kwako PAS,

Mkuu sina hakika sana kama Marando kapewa assigment ya kuisambatratisha CHADEMA,mara nyingi watu wa system wanatumia hali ya mambo ya wakati husika kufanikisha mipango yao.Mfano CHADEMA wakati huu wana vita ya chini chini ya kugombea nafasi ya kiongozi wa upinzani bungeni Zitto Kabwe naibu katibu mkuu na Mwenyekiti Freeman Mbowe wanaweza kusababisha yaliyotokea NCCR Mageuzi yajirudie tena.Rejea tena bandiko langu kazi kubwa ya UWT kipindi hiki ni kusambaratisha upinzani Marando yuko tena kwenye chama kinachoitia hofu CCM akifanikiwa tena anaweza kufananishwa na yule kachero mashuhuri sana nchini Israel Bwana Eli Cohen.
 
yeye kama raia mwingine wowote ana uhuru wa kushiriki shuguli mbalimbali za kijamii kwa maslahi ya tanzania , kushiriki shuguli za kisiasa ni kwa interests za taifa pia hata huko kwenye vyama kuna watu wa usalama wa kutoa taarifa na kuwashauri viongozi maswala mbalimbali kwahiyo msiogope sana - usalama wa taifa wako kwa maslahi yetu ni wananchi wa kawaida kama nyie sema utafauti uko kwenye utendaji wa kazi ni sawa na dereva wa basi na konda wake wote wana majukumu kutokana na mkataba wao wa kazi

Theories!

Haufahamu ulichoandika hapo juu (red/bold)... Inawezekena umesoma Ukurasa wa kwanza wa "Mission Statement ya TISS"!
 
sasa hapo utasema juu ya zitto tena kungombe uongozi na bosi wake. kama hajui hilo liko wazi. kwakuwa myenyekiti wake yupo bungeni ndie anaongoza bunge -upinzani
 
sasa hapo utasema juu ya zitto tena kungombe uongozi na bosi wake. kama hajui hilo liko wazi. kwakuwa myenyekiti wake yupo bungeni ndie anaongoza bunge -upinzani

Mkuu Andrewk,

Ni kweli ukitazama mfumo wa tawala nyingi dunia eg Uk na Austria kiongozi wa upinzani bungeni pia ndiye kiongozi wa chama.Jiulize unadhani yanayoendelea ni bahati mbaya !.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom