Mabeberu, Vibaraka wa Mabeberu, Wazalendo wa Hayati Magufuli, na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo

Chige

JF-Expert Member
Dec 20, 2008
13,497
29,832
UTANGULIZI

Amini usiamini, wale wale ambao wamekuwa wakijivika uzalendo, linapokuja suala la Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, ndiyo hao hao wanaotumikia Mabeberu bila wao kujijua!

Nitajadili mada hii katika sehemu mbili:-
  • Kwanini wale wanaoitwa Mabeberu hawawezi kuwa tayari kuona miradi kama ya Bandari ya Bagamoyo inafanikiwa, na
  • Hoja zinazotolewa na Wazalendo Kupinga Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.
Kwa bahati, binafsi mwaka 2016 nilikuwa “Mbeba Mikoba” wa Researcher mmoja wa Kimarekani (Beberu?) aliyekuwa anafanya utafiti kuhusu Belt and Road Initiative (BRI).

Kazi yangu kubwa ilikuwa Literature Review!

Kwa wanaofahamu mambo ya Resech, ukifanya Literature Reviews, hususani ya wasomi kama huyu bwana, basi unapata fursa ya kufahamu mambo mengi zaidi yaliyopata kutokea hapo kabla kwenye eneo husika!

Kwa wasiofahamu, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni matokeo ya (BRI) ambayo, Rais wa China, Xi, anailezea BRI kwamba:
“China will actively promote international co-operation through the Belt and Road Initiative. In doing so, we hope to achieve policy, infrastructure, trade, financial, and people-to-people connectivity and thus build a new platform for international co-operation to create new drivers of shared development.”

Kwa lugha nyepesi, malengo ya China kupitia BRI ni kuiunganisha nchi hiyo na sehemu zingine duniani, hususani Asia, Afrika, na Ulaya! Uunganishaji huo ni kwa ujenzi wa miundombinu, hususani ya bandari, reli, na viwanja vya ndege.

Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA alipata kuchambua kwa undani kabisa suala la Belt and Road Initiative!!

Na hapo sidhani kama mtu anahitaji kuwa na Shahada ya Diplomasia ya Uchumi na Ushikirikiano wa Kimataifa kunusa “threat” ya mpango huo wa China kwa mataifa makubwa, hususani Marekani!

Kutokana na ukweli huo, ndo maana haishangazi mara tu BRI ilipotangazwa, Waandishi na Watafiti mbalimbali kutoka nchi za magharibi wakaanza kulivalia njuga suala hilo.

Makala zikaandikwa, na tafiti zikafanywa kuhusu BRI, lakini makala nyingi kama sio zote zililenga kuyatisha mataifa mengine kuwa makini na BRI!

Watu hawa wakageuka kuwa “Wajomba Zetu” Afrika, huku wakituasa tusije tukaingia kwenye mtego huo hatari wa China!

Ni kupitia hizo tafiti ndipo nami nikajikuta nipo na huyo Mtafiti Msomi kweli kweli wa Kimarekani.

Huyu Bwana case studies zake zilikuwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, Bandari ya Hambantota (Sri-Lanka), pamoja na Bandari ya Piraeus (Ugiriki).

Ukweli ni kwamba, ilinichukua chini ya dakika 3 kugundua Mtafiti huyu ni kama tayari alishakuwa na “matokeo” ya utafiti wake hata kabla kazi haijaanza! Kwa kifupi, alionesha dalili zote za kutounga mkono Mradi wa Bandari ya Bagamoyo!

Hata "beberu" niliyekuwa namtumikia, nae alikuwa pamoja na "Wazalendo" wetu!!

Binafsi, nilikuwa “in favor of” Mradi wa Bandari ya Bagamoyo, kwahiyo tukaanzisha kimdaharo kisicho rasmi!

Baada ya kuona hoja zake nyingi nazipangua, akaishia kuuliza ikiwa nadhani ni busara kwa taifa maskini kama Tanzania kuwa na bandari kubwa kama ya Bagamoyo!!

Jibu langu kwake lilikuwa rahisi sana, kwamba: Bandari ya Bagamoyo itakuwa ni kubwa mno kwa Tanzania endapo tu unaamini Tanzania na majirani zake wataendelea kuwa maskini kwa miongo kadhaa ijayo, vinginevyo, huwezi kusema ni “kubwa mno”!

Kwa ufupi, Mheshimiwa huyu, kama walivyokuwa wenzake wengine, nyimbo zao zilikuwa ni agenda ya siri ya China kuitumia BRI kama Mtego wa Madeni kwa nchi maskini!

Lilipokuja suala la Bandari ya Hambantota kule Sri-Lanka, propaganda zikasambazwa kwamba China IMEITWAA bandari ya Sri Lanka ili kufidia deni lake!

Wazalendo wetu nao wakazidaka propaganda hizo, na bila kufanya utafiti, wakaanza kutueleza kwamba “tukishindwa kulipa deni, Wachina wataichukua Bandari ya Bagamoyo kama walivyofanya kule Sri-Lanka.”

Kuweka kumbukumbu sawa, habari za Wachina KUITWAA bandari hiyo zilipotoshwa. Nitaeleza hili kinaga ubaga hapo baada kwenye makala hii.

Pamoja na suala la “Debt Trap”, watu hawa tunaowaita Mabeberu ambao kwa hili tunawaona wanajali maslahi yetu, pia wakawa wanatuambia agenda nyingine ya siri ya China ya kuanzisha “military base” kupitia BRI.

Hapa wakawa wanalenga kutuambia, hata mradi kama wa Bandari ya Bagamoyo, lengo lake ni Wachina kutaka kuweka kambi za kijeshi eneo hili la Afrika Mashariki!

Hata hivyo, hawatuambii ukweli kwamba, ni wao wenyewe ndio wanaozihofia hizo “military bases” za China endapo zitawepo!

Kila mfuatiliaji wa mambo duniani, anafahamu Marekani ina kambi za kijeshi sehemu kadhaa duniani, lakini linapokuja suala la China au mataifa mengine kufanya yale yale ambayo yeye keshayafanya kwa miongo kadhaa, hapo inageuka kuwa nongwa!

Waingereza wana msemo “If you can’t beat them, join them.”

Guys, amini usiamini, juzi yule Mtafiti niliyekuwa nae ametoa makala kwenye moja ya majarida maarufu sana duniani! Baada ya kuisoma makala ile, hapo hapo nikajisikia uchungu, na kumhurumia!

Yaani yule yule aliyekuwa anaipinga BRI, kwenye hiyo makala anaulaumu wazi wazi Utawala wa Trump kwa kutumia kete ya Debt Trap kama njia ya kuidhoofisha BRI.

Kwenye makala hiyo, kuna sehemu anahoji “Kama kweli BRI ni kitu kibaya kiasi hicho, ni kwanini basi China inaendelea kutafuta Washirika walio tayari kujiunga na BRI.”

Mwishowe, Mtafiti huyu anaisemanga serikali yake kwamba ”USA haitaweza kumzuia Rais wa China kuwekeza kupitia BRI endapo US haitakuwa na mbadala kwa mataifa yanayoshirikiana na China!

Ufaransa, imeanza kuliona hilo kama ilivyowahi kuripotiwa na France24 kwamba:
France is looking to reform its policy on aid to Africa – making it both more generous and more efficiently targeted – as part of a strategy to counter China’s rising geopolitical influence.

Desperation ya Mtafiti huyu bila shaka inatokana na vile anavyoona jinsi ambavyo nchi mbalimbali duniani jzinavyojiunga na BRI, kinyume na matarajio ya USA ambayo ilikuwa ina-lobby nchi zingine, hususani Washirika wake kutojiunga na BRI.

Kwa bahati mbaya sana, si Afrika, si Asia! Hadi baadhi ya nchi za Ulaya na Carribean zinaingia kwenye BRI. Mbaya zaidi, miradi ya BRI inaonekana kufanya vizuri sana!

Kwa mfano, mwaka 2016 Bandari ya Piraeus ilikuwa ndio ya kwanza barani Ulaya kubinafsishwa chini ya BRI. Bandari hii ndiyo bandari kubwa kuliko zote nchini Ugiriki, na ndio langu kuu la bahari linalounganisha nchi za EU na Asia!

Hapo kabla, bandari hii ilikuwa haifanyi vizuri, na ripoti za nyuma zilikuwa zinaiweka bandari hiyo kama bandari ya 17 barani Ulaya!

Baada ya Wachina kuchukua 51% ya hisa za bandari hiyo, na hatimae hisa hizo kufikia 67%; ripoti ya mwaka huu kupitia Port Economics inasema kwa sasa Bandari ya Piraeus ndiyo bandari kubwa zaidi (kwa kiwango cha makontena) kwenye ukanda wa Bahari ya Mediterranean, na ya 5 Barani Ulaya!!

Sasa haya ndo mambo ambayo watu hawakuyataka! Yaani bandari iliyo kwenye ardhi ya Mzungu, 67% imilikiwe na Mchina, na hapo hapo inaanza kutishia ushawishi wa bandari zingine zinazomilikiwa na Wazungu wenyewe!

JokaKuu
 
SEHEMU YA PILI.

Hoja zinazotolewa na Wazalendo Kupinga Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.

Wachina Watachukua Mapato YOTE ya Bandari ya Bagamoyo.

Hii ni moja ya hoja zinazotolewa na Wazalendo wetu wanaopinga Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Bandari, Deusdedit Kakoko nae alipata kusema “…Wachina wanataka kuchukua mapato yote, na wanataka wasilipe kodi kwa miaka 30.”

Ukweli ni kwamba, haya ni madai ya kushangaza!

Ni madai ya kushangaza kwa sababu ni jambo lisiloingia akilini. Na ikitokea Wachina wakachukua MAPATO YOTE basi Tanzania tutaweka historia mpya duniani kwa sababu hakuna kitu kama hicho popote pale duniani!

Labda niseme jambo moja! Aya yangu hiyo hapo juu ni namna tu ya kusema kiungwana kwamba MADAI HAYO NI UONGO!

Kakoko kasema Wachina wanataka wasamehewe kodi kwa miaka 30! Hata hivyo, hatuambii ni kodi ya aina gani wanayotaka wasamehewe!

Kubwa zaidi, maelezo ya Kakoko yalikuwa yamekaa ki-propaganda mno… propaganda zile zile za ki-MATAGA za kujifanya wao ndo Wazalendo sana na wana uchungu sana na hii nchi wakati ni WANAFIKI tu, ambao “uzalendo” wao ulikuwa kwa JPM, na sio kwa nchi!

Ni kutokana na uongo huu wa Kakoko ndo maana haikushangaza kwa mara ya kwanza kuwaona Wachina wakioka mbele na kumshutumu Kakoko kwamba ni MWONGO.

Kwa mfano, gazeti la The Citizen la October 28, 2019 lilimnukuu Mwakilishi wa Uwekezaji wa China Merchant Group, Mr. Moosa Mao akisema:-
The Investor is very disappointed to see fake information spread around, which not only damaged the ease of doing business environment of Tanzania, but also misguides the public and the top level officials of the government.

Na hata kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mr. Mao aliandika:-

Mao 1.png


China Merchant Group ndio walitarajiwa kuwekeza kwenye Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.

Hapa tuweke kumbukumbu sawa linapokuja suala la kodi kwa kuangalia muktadha wa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo.

Katika hali ya kawaida, kutakuwa na awamu mbili zinazohusiana na kodi kwenye mradi huu.

Awamu ya kwanza ni wakati wa shughuli za ujenzi wa bandari, na awamu ya pili ni pale bandari itakapoanza kufanya kazi.

Wakati wa ujenzi, tunatarajia vifaa vingi vitaagizwa kutoka nje, ingawaje tutakuwa Viumbe wa Ajabu sana endapo tutaruhusu uingizaji hadi wa vifaa ambavyo wenyewe tunavyo, kama vile saruji.

Kuhusu hilo la vifaa, hapa Mchina namtarajia atakuwa ameomba asemehewe kodi ya uingizaji wa hivyo vifaa!

Na kwa bahati, hatakuwa amefanya dhambi yoyote kwa sababu Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, yaani VAT Sura ya 148, na Sheria ya Fedha ya mwaka 2017, 2018 na 2019 zinatoa mwanya kwa Mwekezaji kuomba msamaha wa kodi “on imported capital goods”.

Hata ukiingia kwenye tovuti kuu ya serikali utakuta maneno haya:-

The applicant will submit an application for reliefs using form VAT 220/223/224, providing a description of capital goods to be imported, The application is to be accompanied by the Bill of lading, invoice, packing list and any other documents to confirm the nature and ownership of those goods.
Hivyo, hapo utaona wazi kwamba ni suala la kisheria! Na jambo kama hilo sio Tanzania tu bali sehemu mbalimbali duniani huwa wanafanya hivyo ili kuvutia uwekezaji!!

Kitaalamu, suala hilo linaitwa Tax Incentives. Na hata uki-Google “Tax Incentives in Tanzania”, moja kwa moja utakutana na link ya TRA ikiwa juu kabisa ya matokeo ya utafutaji; yaani Google Search Results!

Suala la kodi na ushuru bandari itakapoanza kufanya kazi.

Kama nilivyosema hapo awali, Mhandisi Kakoko alituambiwa “Wachina wanataka wasamehewe kodi kwa miaka 30,” huku Wazalendo wengine wakituambia TRA hawataruhusiwa hata kutia pua hapo bandarini!

Hapa ieleweke kwamba, popote pale duniani kodi ni MALI YA SERIKALI, na ndio maana, ukisoma hiyo screenshot ya Twitter kutoka kwa Moosa Mao, amekanusha suala la eti TRA hawataruhusikiwa kukusanya kodi!

Na ndio maana, wewe milikishwa ekari 1000 na baba yako, kisha tumia pesa zako mwenyewe kufanya uwekezaji bila kuomba hata senti moja kutoka popote pale!

Pamoja na yote hayo, ukimaliza tu uwezekaji wako na kuanza kufanya biashara, TRA wanakuwa wageni wako wa kudumu, ingawaje hukuchangiwa chochote na yeyote!

Lakini kwa upande mwingine, popote pale duniani, serikali huwa zinasamehe baadhi ya kodi. Bandari ya Bagamoyo ikishaanza kufanya kazi, tunatarajia kuwepo angalau kodi zifuatavyo:-

  • Kodi ya Ongezeko la Thamani… VAT on imported goods
  • Kodi ya Mapato (Income Tax)
  • Ushuru wa Uingizaji Bidhaa (Import Duty)
  • Ushuru wa Forodha, na zingine.
Sasa basi, tuseme wewe na mimi, or anyone ameagiza magari au bidhaa yoyote ambayo sio miongoni mwa bidhaa zilizo kwenye kundi la msamaha wa kodi!

Hilo likifanyika, Importer atalazimika kulipa angalau moja ya kodi nilizotaja hapo juu! Kodi hiyo ni LAZIMA IKUSANYWE NA TRA kwa sababu, kama nilivyosema awali, always, Kodi ni Mali ya Serikali.

Sasa je, kuna uwezekano Mchina akataka msamaha wa kodi baada ya bandari kufanya kazi?

Jibu ni NDIYO!

Kutokana na uzoefu niiopata kutoka kuwa Mbeba Mikoba wa Beberu, na kwa kuangalia “case studies” za bandari zingine ambako Mchina amewekeza, hapo kuna uwezekano mkubwa Mchina akaomba msamaha wa Income Tax. HOW?

Bandari ikishaanza kufanya kazi, Mchina atakuwa anatoa huduma kadhaa kama vile kuhifadhi mizigo, kupandisha na kupakuwa mizigo, kuzitoza meli ambazio zitakuwa zinafunga nanga hapo bandarini, n.k.

Kwa kutoa huduma hizo, ina maana Mchina atakuwa analipwa pesa!! Katika mazingira ya kawaida, pesa anazopata ni mapato yanayostahili kukatwa kodi!

Ni hiyo kodi itakayotokana na hizo huduma ndiyo ambayo sina shaka Mchina atataka asamehewe!! Na huu ndio ukweli ambao kwa makusudi, Mzalendo Kakoko hakutaka kusema ukweli, na badala yake akafanya majumuishi kwamba Mchina anataka kusamehewa kodi kwa miaka 30, bila kutaja ni kodi ipi!

Katika hili la kodi, nililazimika kumtumia email yule Researcher niliyekuwa nae, kwa sababu mimi binafsi sikupata fursa ya kuonana na watendaji wa serikali!

Nililazimika kumtumia email na kumuuliza ingawaje tayari nilishakuwa nafahamu majibu ya maswali yangu. Hata hivyo, nilitaka tu kujiriidhisha kutoka kwake, kwa sababu yeye ni mzoefu sana kwenye haya mambo ya uwekezaji duniani!

Jibu lake lilikuwa hili hapa chini:-

TRA.png

Swali hilo nilimuuliza miaka 2 iliyopita, na mtaona jibu lake linaenda sawa na jibu la Moosa Mao!

Aidha, miongoni mwa maswali ambayo watu wamekuwa wakijiuliza ni kwamba: Sasa kama TRA watakuwa wanachukua kodi, Mchina atarudisha vipi pesa yake!

Jibu la hilo swali unatakiwa kujiuliza: Je, Mamlaka ya Bandari huwa wanakusanya kodi? Kama hawakusanyi, je mapato yao yanatoka wapi? Jibu la swali la pili ndilo jibu la swali la Mchina atarudisha vipi mapato yake!
 
SEHEMU YA TATU

Mchina Anataka Bandari Zingine Zisiendelezwe
.

Wenyewe mmeona kwenye hiyo tweet ya Moosa Mao, kwamba huo nao ni UZUSHI. Hivi kuna haja ya kuongeza hapo?

Ngoja niongeze, isije kuonekana Mchina anajikosha tu!

Hapa tufahamishane kwamba, suala la upanuzi wa Bandari ya Dar es salaam unaoendelea hivi sasa ni ushahidi tosha kwamba HUO NI UZUSHI.

Watu wengi wanadhani maboresho yanayoendelea Bandari ya Dar es salaam yameasisiwa na JPM… HELL NO!

HELL NO hata kama Wafuasi wa JPM wanataka kuaminisha watu kwamba ile ni kazi ya JPM kwa alama zote.

Ukweli ni kwamba, Mzee wa Msoga alipoingia madarakani, serikali yake iliandaa 4 BIG MASTER PLANS zilizolenga kuifikisha nchi kwenye uchumi wa kati by 2025. Master Plans hizo ni:-

Dar es salaam Metropolitan Development Project (DMDP)

DMDP ndiyo imezaa mazagazaga yote mnayoyaona Dar es salaam hii leo. Mazagazaga hayo ni pamoja na barabara, flyovers ambazo wafuasi wa JPM wana-force atukuzwe JPM kwa hilo, Mwendo Kasi, Ubungo Interchange, na Daraja la Salender.

Hadi JK anatoka madarakani, kazi kubwa ilikuwa imeshafanyika, na Wafadhili alishawapata!

Lau kama JK angeendelea kuwapo madarakani kwa miaka mingine 5, haya yote tunayoambiwa tumuimbe JPM kama shujaa, yangekuwa yamefanywa na JK mwenyewe.

  • Power System Master Plan (Mambo ya Umeme(.
  • Tanzania Intermodal & Rail Development Project (TIRP), na
  • Dar es salaam Maritime Gateway Project (DMGP).
DMGP iliasisiwa mwaka 2009 (au 2008), na kuanzia hapo zikaanza hatua za awali kama upembuzi yakinifu na kutafuta watoaji wa fedha za kugharamia mradi wa uboreshaji wa Bandari ya Dar es salaam.

Ukiingia tovuti ya TPA wanatoa dokezo kuhusu DMGP na kutaja wafadhilwanataja wafadhili hao kwamba:-
The DMGP is a partnership between the Government of Tanzania, the Tanzania Ports Authority (TPA), other public and private stakeholders, and a coalition of development partners including the Trade Mark East Africa (TMEA), the United Kingdom Department for International Development (DFID), and the World Bank (WB) through the International Bank for Reconstruction and Development (IBRD).

Baada ya hatua mbalimbali kukamilika, Septemba 2014 ikasainiwa MoU kama inavyoelezwa kwenye Project Appraisal Report ya Benki ya Dunia kwamba:-

The DSMGP also reflects the Memorandum of Understanding and Cooperation (MoU) signed in September 2014. The MoU was signed between the Ministry of Transport, the World Bank, the United Kingdom Department for International Development (DFID), and TMEA, and reflects the commitment of the parties to support the implementation of the objectives of the GoT in the Maritime Sub-Sector.

Ripoti hiyo hapo juu ilitolewa wakati Benki ya Dunia walipoidhinisha Mkopo wa USD 345M hapo June 9, 2017 ili hatimae maboresho ya Bandari ya Dar es salaam yaanze rasmi!

Na kwa wenye uelewa wa mambo kama haya bila shaka watakuwa wamepata picha rasmi kwamba, isingewezekana JPM aliyeingia madarakani mwishoni kabisa mwa mwaka 2015, halafu miezi 18 baadae awe ameandaa mradi mkubwa kama wa uboreshaji wa bandari ya Dar es salaam, na kupewa pesa ndani ya huo muda.

Hapo hapo, Reuters October 27, 2014 inatukumbusha kwamba:-

DAR ES SALAAM (Reuters) - Construction of a Chinese-funded port and special economic zone in Tanzania worth at least $10 billion will start in July 2015, the president’s office said in a statement on Monday, for the first time setting a start date for the delayed initiative.

Sasa basi, kama serikali ilisaini MoU September 2014 ya kuboresha bandari ya Dar es salaam chini ya DSMGP, na mwezi mmoja baadae wanazungumzia suala la kuanza mradi wa Bandari ya Bagamoyo, huo ni ushahidi tosha kwamba habari za Mchina kukataza uendelezaji wa bandari zingine ni madai ya uongo na uzushi!

Na maelezo hayo moja kwa moja yanashabihiana na tweet ya Moosa Mao kwamba:-

Mao 2.png
 
SEHEMU YA NNE
Mchina Anataka Kumilikishwa Bandari kwa Miaka 99
!

Dai lingine linatolewa na Wapinzani wa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni hilo kwamba Mchina anataka kumilikishwa bandari kwa miaka 99.

Binafsi, sikuwahi kusikia madai hayo, na naweza kusema kwa kujiamini kwamba HAKUNA KITU KAMA HICHO!

Watu ni kama wanachanganya madesa!! Miaka 99 inayosemwa sio ya kumilikishwa bandari bali ya kumilikishwa ardhi!

Lakini pia tusisahau sheria zetu za umilikaji wa ardhi kwa wawekezaji zinasema unaweza kumilikishwa ama kwa miaka 33 (renewable), au miaka 66 (renewable) au miaka 99!

Kwa maana nyingine, Mchina kuomba kuomba kumilikishwa ardhi kwa miaka 99 sio jambo la kushangaza kwa sababu lipo kwenye sheria zetu!

Hata hivyo, suala la kumilikishwa ardhi kwa miaka 99 linakinzana na taarifa zisizo rasmi zinazotaja muda ambao Mchina anataka kumilikishwa Bandari! Nasema taarifa zisizo rasmi kwa sababu, wakati wa utafiti nilioutaja hapo juu, changamoto kubwa ilikuwa kupata taarifa rasmi.

Na kwa mujibu wa hizo taarifa ambazo sio rasmi, Mchina anataka kumilikishwa bandari kwa miaka 40!

Je, miaka hiyo ni mingi sana?!

Kupata picha halisi ya swali hilo mtu anatakiwa kufahamu mfumo wa ugharamiaji wa Bandari ya Bagamoyo.

Again, taarifa zisizo rasmi zinasema mradi ungegharamiwa kwa mfumo wa Build-Operate-Transfer; maarufu kama BOT Financing Scheme.

Mfumo wa aina hii ni kwamba, Mwekezaji anagharamia ujenzi (Build) kuanzia mwanzo hadi mwisho kwa pesa zako. Pamoja na mambo mengine kama misamaha ya kodi, hapa Mwekezaji anapewa miaka kadhaa ya kuendesha (Operate) mradi husika, na ile miaka ikiisha, mradi unahamishiwa (Transfer) serikalini!

Sasa basi, kwa mujibu hizo taarifa, Mchina anataka miaka 40 ya ku-operate, na baada ya hapo ndipo bandari iwe mali ya serikali!

Sasa hoja inayotakiwa kujadiliwa hapa ni kwamba, kama Mchina ataendesha bandari kwa miaka 40; sasa kwanini atake umiliki wa ardhi kwa miaka 99!

Kwa maana nyingine, labda Mchina anataka awe anatutoza ushuru kwenye ardhi yetu wenyewe kwa miaka 59 (99-40) itakayobaki!

Lakini kama sio kututoza ushuru, basi huenda Mchina anafikiria kuwekeza vitega uchumi vingine kwenye ardhi hiyo kwa mgongo huo huo wa Bandari ya Bagamoyo!

Hilo la kwanza HALIKUBALIKI lakini linazungumzika, na hilo la pili, angalau linahimilika!!

Hata hivyo, je miaka 40 ni mingi sana?!

Kama nilivyosema hapo awali, kwenye utafiti nilioutaja hapo juu, nilihusika zaidi kwenye Literature Review, na nilipitia miradi mbalimbali kwingineko duniani ambayo imejengwa chini ya BOT Scheme!

Ukweli ni kwamba, sikuona mradi hata mmoja ambao “transfer” yake ilikuwa chini ya miaka 25!

Na hapa tukumbuke kwamba, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni mkubwa mno kulinganisha na hiyo miradi ya wenzetu ambayo “transfer to the government” ni miaka 25+!
 
SEHEMU YA TANO

Wachina Wakishamaliza Kujenga Bandari, Watatunyang’anya Kama Walivyofanya Bandari ya Sri-Lanka
!

No one knows the future, kwahiyo siwezi kusimamisha mishipa na kusema “hilo haliwezekani”!

Hata hivyo, Wazalendo wamekuwa wakiizungumza sana hoja hii bila kujua hizo zilikuwa ni propaganda za nchi za Magharibi walipokuwa wanajaribu kuzitisha nchi duniani zisijiunge na Belt and Road Initiative ya China, kwa hoja nilizotaja kwenye sehemu ya utangulizi!

Ili kuweka kumbukumbu sawa, ifahamike kwamba, mosi, mfumo wa kugharamia ujenzi wa Bandari ya Hambantota, nchini Sri Lanka ni tofauti na mfumo wa ugharamiaji wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo!

Sri-Lanka wao walikopa pesa China ili kujenga bandari tajwa! Na dawa ya deni ni kulipa… simple like that!!

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, Sri Lanka walikopa kwa benki ya EXIM ya China! Na haya ndo madhara ya kukopa benki, tofauti na kukopa kwenye taasisi kama Benki ya Dunia, The Paris Club, The IMF, and the like!

Kwa mfano JPM si alikopa Credfit Suisse na Standard Chartered Bank ili kujenga SGR?! Ngoja tushindwe kulipa ndipo utaona kama ni Mchina tu ndie upora miradi kufidia pesa zake, au vipi!

Lakini tukirudi Sri Lanka, pamoja na Bandari ya Hambantota kuwa jirani kabisa na njia kuu ya meli (main shipping lane) zinazotoka Ulaya kwenda Asia, lakini bado bandari hiyo ilikuwa haifanyi vizuri! Yaani ni meli chache sana zilizokuwa zinaingia bandarini hapo.

Matokeo yake, bandari hiyo ikawa haiingizi mapato ya kutosha na kusababisha deni kuendelea kukua! Kwa kifupi, Bandari ya Hambantota iligeuka na kuwa The White Elephant Project!

Aidha, ikumbukwe kwamba, kwavile Sri-Lanka walikuwa wamekopa pesa (sio BOT kama ilivyo Bagamoyo) kujenga bandari hiyo, ina maana kwa wakati huo bandari ilikuwa ni ya kwao na walikuwa wanaindesha wenyewe!

Mwaka 2015, serikali mpya ya Sri Lanka ilipoingia madarakani, wakakuta bandari imehelemewa madeni na yalikuwa yanaelekea kwenye kutolipika!

Ili kuinusuru bandari hiyo na mzigo wa madeni uliosababishwa sana na “poor performance”, ndipo Serikali mpya ya Sri-Lanka ikaamua KUIBINAFSISHA, na kuuza 70% ya bandari.

Miongoni mwa kampuni zilizokuwa zimejitokeza kuchangamkia hiyo fursa ni China Merchants Group, ambayo ndiyo iliuziwa hizo 70% ya hisa!!

Ajabu ni kwamba, wakati huo ulikuwa ni uamuzi wa serikali kubinafsi bandari iliyokuwa inaingiza hasara, propaganda zikasambazwa kwamba China wameipoka bandari kufidia deni lao!

Na hapo Wazalendo wetu wakaidaka hiyo habari bila kuifanyia uchunguzi, na kutuambia hata Bandari ya Bagamoyo wataichukua!

Lakini hata kama waliipoka… hivi ni jambo geni hilo duniani?! Mara ngapi mabenki Tanzania yamekuwa yakiuza mali za wateja wao walioshindwa kulipa madeni?
 
SEHEMU YA SITA
Kikwete Alitaka Mradi wa Bandari ya Bagamoyo Kwavile ni Kwao
!

Hoja nyingine ambayo imekuwa ikitolewa ndo hiyo hapo juu! Katika kuhalalisha hoja hiyo, watu wamekuwa wakihoji kwanini isingeboreshwa Bandari ya Dar es salaam, au Tanga, au Mtwara!

Hapo juu tayari nimezungumzia mradi wa maboresho wa Bandari ya Dar es salaam… kwahiyo, hoja kwamba kwanini isiwe ni Dar es salaam ni hoja mfu tayari!

Aidha, watu wafahamu kwamba jiografia ya Dar es salaam inaifanya bandari hiyo iwe inaelekea kwenye ukomo wa kuiboresha endapo tunataka kuangalia miaka 100 ijayo.

Hapa ikumbukwe kwamba, ndoto za Bandari ya Bagamoyo ilikuwa ni kuifanya bandari hiyo kuwa transshipment port.

Transshipment Port ni bandari inayotumika kuhamisha mizigo kutoka kwenye meli moja kwenda kwenye meli zingine.

Hii maana yake ni kwamba, oda za mizigo mbalimbali kutoka China au Japan kwenda sehemu kadhaa Afrika; oda hizo zingekuwa zinapakiwa kwenye meli kubwa, maarufu kama megaships, ambazo zingekuwa zinatoka huko na kuja kufunga gati Bandari ya Bagamoyo!

Baada ya hizo meli kubwa kuja kufunga nanga Bagamoyo, ndipo meli zingine za kawaida kutoka bandari kadhaa barani Afrika, na kwingineko duniani zingekuwa zinafuata mizigo hapo Bagamoyo badala ya kwenda moja kwa moja China au Japan.

Lakini kwa upande mwingine, unapotaka bandari kubwa kama ya Bagamoyo vile vile unahitaji eneo kubwa la kuhifadhi mizigo, na mambo mengine kama hayo!

Hili hitaji la eneo la kuhifadhi mizigo ndilo limeimeza Kurasini.

Na ikumbukwe kwamba, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo unahusisha pia na Industrial Complex kubwa sana.

Ukitaka yote hayo yafanyike Bandari ya Dar es salaam, basi italazimika kuvunja eneo lingine… labda Mtoni kwa Aziz Ally au Keko; au zote kwa pamoja.

Itoshe tu kusema kwamba, Dar es salaam hakuna eneo la kufanya yote hayo, labda serikali iamue kuivunja tarafa nzima ya Chang’ombe!

Sasa yanini kuingia gharama zote hizo?! Yaani ili mradi tu bandari isijengwe nyumbani kwa tusiyempenda hata kama jiografia inampa faida zote?

Sasa kwanini bandari isingejengwa Tanga?

Hebu tusome kwanza gazeti la The Daily News la Julai 21, 2013. Moja ya aya za habari husika inasema:-

The project to involve construction of a deep sea and free port at Mwambani, in Tanga, and a new heavy haul standard gauge railway from there, would be operated by MWAPORC, an acronym for Mwambani Port and Railway Corridor. Already several international companies from all over the world, in particular from England, Canada, United States, Scotland, South Africa and the Middle East, have expressed commitment to inject funding for its smooth implementation.

Unaona hapo kitu kinachoitwa MWAPORC! Ngoja nifafanunue!

Hapo juu nimeeleza kuhusu Dar es salaam Maritime Gateway Project (DMGP) ambayo lengo lake lilikuwa ni kwa ajili ya Bandari ya Dar es salaam TU!

Lakini pamoja na DMGP, mwaka 2008 Mamlaka ya Bandari Tanzania iliwapa kazi Royal Haskoning ili wafanye “study” itakayoandaa Tanzania Ports Master Plan (PMP).

Tofauti na DMGP ambayo ilijikita kwa Bandari ya Dar es salaam pekee, PMP ilikuwa inaangalia Tanzania mzima… kwenye bahari, mito na maziwa!!

Hadi kufikia 2012, tayari Tanzania Ports Master Plan ikawa tayari, na hapo wakaitwa Wadau wa Uwekezaji kuangalia ikiwa wanaweza kuwekeza kwenye bandari nchini.

Mzee Rugemalila, YES, you heard me correctly, Mzee Rugemalila, yule yule wa Escrow, akiwa na Mwananchi Enginerring yake, nae akajitosa kutafuta fursa ya uwekezaji kwenye bandari!

Baada ya timu yake kufanya upembuzi yakinifu kwenye ukanda wa pwani ya Tanzania, Mzee Ruge na wenzake wakaamua kutaka kuwekeza kwenye bandari ya kina kirefu pale Tanga, chini ya walichokiita Mwambani Port and Railway Corridor Ltd (MWAPORC) iliyokuwa chini ya ukurugenzi wa Mr Beenunula Eyenunula Nunumisa.

Mradi wa MWAPORC ulitarajiwa kuwa Deep Sea Free Port ambao ungegharimu karibu Shilingi 60 Trillion!

Kwa kujua kwamba huo mradi ni mkubwa mno, Kikwete akawaahidi MWAPORC kuwasaidia kuwatafutia wawekezaji huko ughaibuni kama inavyoripotiwa na The Daily News kwamba:-

Meanwhile, President Kikwete on Saturday met a delegation of the Mwambani Port and Railway Corridor Ltd (MWAPORC) along with their Project Engineers, Mott Macdonald of the United Kingdom. The president assured the MWAPORC Company of complete support of the Government of Tanzania in their investment plans, and has directed the Ministry of Transport to guide and support the investors to implement this project as quickly as possible.
Wakati MWAPORC ilikusudia kuwekeza bandari ya kina kirefu, Mamlaka ya Bandari ilikusudia kuboresha Bandari iliyopo ya Tanga!

Aidha, kabla serikali haijaita Wadau kuangalia fursa za uwekekezaji kwenye bandari, Wachina walikuwa Kenya wakikusudia kujenga bandari kubwa sana pale Lamu! Yaani, ule Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ulikuwa ujengwe Lamu!

Baada ya China Merchant Group kupata habari za Tanzania kuita wadau kuangalia fursa za uwekezaji kwenye bandari, wao nao wakajitosa, na baada ya upembuzi wao wakachagua kuwekeza Bagamoyo, na kuachana na Lamu!

Kwahiyo madai kwamba JK alitaka kupendelea kwao ni madai yasiyo na msingi! Ni jiografia ndio imeibeba Bagamoyo, labda kama tulitaka hiyo bandari ikajengwe Chato ilikojengwa International Airport bila kufuata vigezo!

Na kwanini isingekuwa Mtwara?!

Hapo jibu ni rahisi sana!

Wakati Tanzania Ports Master Plan ikiwa tayari kutafuta wawekezaji, wakati huo huo kule kusini tayari zilishagundulika 57 trillion cubic feet za gesi!

Nisingependa kuingia kwa undani kuhusu suala la gesi manake hili nalo linahitaji mada inayojitegemea! Hata hivyo, kuweka kumbukumbu sawa, serikali iliamua uwekezaji kwenye utajiri wa gesi ufanyike kwenye mikoa yote miwili, yaani Lindi na Mtwara!

Wakati Lindi ilipangiwa Gas Processing Plant (moja ya miradi mikubwa kabisa iliyokuwa imepuuzwa na JPM), Mtwara ikapingiwa usafirishaji wa gesi kwenda ng’ambo!

Kutokana na hilo, Bandari ya Mtwara ikawa imetengwa maalumu kushughulikia biashara ya mafuta na gesi.
 
HITIMISHO

Tukubali tusikubali, fursa ya Bandari ya Bagamoyo ikituponyoka tutakuja kuijutia pale Mchina atakapoamua kurejea tena Lamu, au popote pale kwenye ukanda huu wa Bahari ya Hindi!

Inashangaza sana karne ya 21 bado kuna Watanzania wana mawazo yale yale ya Ujima kwamba, eti “madini hayaozi”, na tutakuja kuchimba wenyewe tukishapata uwezo!

Injinia Kakoko na mwenyewe aliwahi kunukuliwa akisema “…na sisi bandari ile (Bagamoyo), tulifanya feasibility study na TPA. Na TPA kupitia serikali, itawekeza na kuijenga wakati utakapokuwa umefika.

Ni wazo zuri kama serikali itakuwa na uwezo wa kujenga hiyo bandari wao wenyewe haidhuru hata kama tumeshindwa kujenga bandari yoyote ndani ya miaka 60 ya uhuru!

Hata hivyo, Kakoko na wengine wanatakiwa kufahamu kwamba, hoja sio kuwa na uwezo wa kujenga bandari bali uwezo wa ku-utilize bandari husika!

Nimetoa mfano wa Bandari ya Piraeus huko Ugiriki ambayo kabla ya uwekezaji wa China, bandari hiyo ilikuwa haifanyi vizuri. Hata hivyo, baada ya Mchina kuingia, Bandari ya Piraeus imegeuka na kuwa ndiyo bandari kubwa kuliko zote Ukanda wa Mediterranean, huku ikichukua nafasi ya 5 Barani Ulaya!

Na ndivyo hivyo kwa Bandari ya Hambantota ambayo na yenyewe ilikuwa haifanyi vizuri lakini hivi sasa hali imebadilika.

Na sababu kubwa ya China kuwa na uwezo wa kuzifanya bandari anazoendesha kufanya vizuri inatokana na ukweli kwamba China ina-handle biashara kubwa sana duniani. Kwa maana nyingine, China ina uwezo wa ku-utilize bandari zake kupitia mizigo yake tu.

Lakini kwa upande mwingine, Mradi wa Bandari ya Bagamoyo pia unahusisha Industrial Complex kubwa sana! Lengo la Mchina ilikuwa ni kujenga viwanda kwenye eneo la bandari, ili baadhi ya bidhaa zake anazosafirisha kutoka China hadi Afrika ziwe zinazalishwa Bagamoyo.

Ninachotaka kusema ni kwamba, pamoja na suala la kodi, mradi huu endapo ungekamilika, ungekuwa chanzo kikubwa cha ajira kwa wananchi!

Bandari ya Bagamoyo sio kama Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chato! Hivyo basi, hata kama tuseme Mzee wa Msoga alilenga kupendelea kwao, hivi kuna mwenye akili timamu anayeweza kuthubutu na kudai kwamba, watakaofaidika na bandari hiyo ni Wakwere na Wazaramo wa Bagamoyo?

Halafu hii nchi ilivyo na viumbe wa ajabu, hao hao wanaosema JK alikuwa anataka kupendelea kwao, kwa kiasi kikubwa ndo hao hao wanaodharau watu wa Pwani kwamba HAWAJASOMA, na kwamba wanaishia kuendekeza madrasa!

Sasa kwavile nyie ndio mliosoma, hamuoni kwamba ni nyinyi wenyewe ndio mtakaofadika na mradi huo huku Wakwere na Wazaramo wakiishia kuwauzia kahawa?

Ukubwa wa mradi ule unaweza kuzalisha Pay As You Earn (PAYE) kutoka kwa wafanyakazi ambayo ni kubwa kuzidi hata thamani ya ukodishaji wa ardhi!

Na hii PAYE ni endelevu kwa miaka na dahari!

Pamoja na yote hayo, katu simaanishi kwamba Mkataba/makubaliano/proposal ya Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo upo PERFECT, au ni bora… la hasha!! Tanzania haijawahi kusaini mkataba ulio bora!

Ambacho ningependa kukiona kwenye hili ni Watendaji na Wafanya Maamuzi kuwa “objective”, na pia waache kusambaza habari za uongo ili mradi tu kuhalalisha ajenda zao.

Wengine ajenda zao ni aibu hata kuzitaja hadharani!

Watu hawa wanatakiwa kukaa na wadau, na kuangalia ni kwa namna gani huu mradi unaweza kufanyika huku tukiacha kile kiburi chetu cha Uzalendo Fake Uliopandikizwa na Mfumo wa Ujamaa!

Aidha, wanatakiwa kukaa na wadau kuangalia ni mfumo upi utaweka mbele maslahi mapana ya taifa.

Na kama nilivyosema kwenye utangulizi wangu, Wapinzani wa Bandari ya Bagamoyo wanawatumikia wale wale wanaowaita Mabeberu bila wao kujijua! Mabeberu walianza kuipinga Belt and Road Initiative ya China tangu kuanzishwa kwake!

Kwa bahati mbaya sana, hao hao waliokuwa wanapinga BRI, hivi sasa wanaanza kuingia mmoja mmoja! Kuna dalili zote kwamba Marekani imeanza kusalitiwa na Washirika wake, hata wale wa Jumuiya ya Ulaya.

Kwa mfano, Jarida la The Diplomat la March 23, 2021 linatueleza kwamba:-

On March 23, 2019, Italy officially became part of the Belt and Road Initiative (BRI). Two years since the first G-7 country became part of the controversial Chinese project, it is time to make an initial assessment of Italy’s highly contested membership in the BRI.
Aidha, wakati Marekani ikihangaika na BRI, mwaka juzi tu hapa, huko China ulifanyika mkutano mkuuubwa wa BRI kama ilivyoripotiwa na UNDP-Asia kwamba:-

The Second Belt and Road Forum for International Cooperation (BRF) is being held in Beijing this week from April 25-27. With the theme of “Belt and Road Cooperation: Shaping a Brighter Shared Future”, the forum is a platform that aims to bring countries together under the BRI framework.

Na kwa mujibu wa Serikali ya China, kupitia Belt and Road Portal, wanasema kwamba:-
So far, 125 countries and 29 international organizations have signed BRI cooperation documents with China, according to Lu.

Among them are 16 Central and Eastern European countries and Greece. More recently, Italy and Luxembourg signed cooperation agreements with China last month to jointly build the Belt and Road. Jamaica also signed similar agreements on Thursday.
Mzee wa Msoga aliwahi kutujuza kwamba: Akili za Kuambiwa, Changanya na Zako!
 
Braza shikamoo, ila wewe jamaa una akili nyingi mnoo.
Hapa nipo na nitarudi baadaye,........

=========================================================================
Ndugu yangu Chige niliahidi ntarudi, lakini naomba nizungumzie kidogo kuhusu hili suala la The Belt-Road-Initiative (BRI). Kwanza kabisa, huu mradi ulianza kupangwa kipindi cha Raisi Hu-Juntao na aliweka wazi kabisa kwenye kikao cha halmashauri kuu ya chama cha kikomunisti cha Uchina.

Zaidi ya asilimia hamsini (50% of world merchandise) ya bidhaa za dunia hii zinapitia kwenye mfereji wa Malacca ambao ni muhimu sana kwa uchumi na usalama wa dunia. Hali hii inawafanya Uchina wajihisi kwamba lolote linaweza kutokea endepo ukanda wa Pasifiki utachafuka.

Gideon Rachman wa The Financial Times aliwahi kumnukuu moja wa Majemedari wakubwa kabisa wa Marekani akisema hivi "If the Chinese starts war in the Pasific, we will fucking sail those waters and choke them at the Malacca Strait". Mafuta yote yanayoenda Uchina, Vietnam, Japan na Korea kutoka Ghuba ya Uajemi hupitia mfereji wa Malacca.

Hivyo ukibana pale Uchina lazima atahangaika sana ukizingatia yeye ndiye nchi inayoongoza duniani kwa kuingiza mafuta na gesi kutoka nje (Greatest Importer of Oil and Gas). Pia ndiye msafirishaji mkubwa wa bidhaa duniani (The Greatest Exporter of Merchandise): Hivyo anategemea sana mfereji wa Malacca, lakini bahati mbaya sana Marekani ameshafahamu huu udhaifu ndiyo maana anaweka kambi ya jeshi eneo lile.

Uchina hili analiita The Malacca Dilemma, na Peter Navarro mmoja ya washauri wakubwa wa Raisi Donald Trump ameliandika sana kwenye kitabu chake kiitwacho Death by China: Confronting the Dragon-Global Call to Action , akikiri kwamba huu ni moja ya udhaifu ambao Marekani lazima iutumie katika kupambana na Uchina.

SASA TANZANIA INAINGIAJE KWENYE HILI:
Uchina katika kuhangaika na kukwepa hii kadhia akaamua kuja na BRI, ambapo wangefufua The GREAT SILK-ROAD ambayo itapita nchi kavu na baharini. Kama ulivyosema Bandari ya Bagamoyo ilitakiwa ijengwe Kenya na kwenye mkakati wa BRN inainyesha ni LAMU na siyo BAGAMOYO, lakini Mzee Kikwete na Benard Membe wakashawishi ije kujengwa hapa Tanzania.

Sasa lengo ni kwamba Uchina angejenga reli ndefu (Standard Gauge Railway) kutoka Uchina hadi nchini Pakistani ambapo ingekutana na bandari ya Gwadar (Gwadar Port) ambayo itakuwa na ukubwa kama ule wa bandari ya Bagamoyo. Lengo ni kwamba bandari hii itakuwa inapokea bidhaa zote kutoka Ghuba ya Uajemi na kuzipakia kwenye treni hadi Uchina, hivyo kukwepa kupita mfereji wa Malacca.

Hivyo, Bandari za Bagamoyo na Gwadar ndiyo yangekuwa malango makuu ya kuunganisha Bara la Afrika na Asia. Kwasababu Bagamoyo peke yake ingehudumia nchi nyingi sana za Afrika kwasababu ni Special Economic Zone. Pia kuna uwezekano mkubwa sana kama Bandari ya Bagamoyo ingejengwa basi ingeweza kuunganisha hadi Congo DRC, kufika Port Matada kwa njia ya reli na kufanikisha biashara baina ya Africa na Amerika Kusini.

SASA NINI TATIZO:
Watanzania wengi wanapinga sana huu mradi lakini binafsi Feasibility Study nimeiona. Pia waliohusika na kuandaa hii Study mkataba pia waliusona na nikabahatika kufahamu baadhi ya vitu. Inavyofahamika mkataba ni makubaliano ya pande mbili na huwezi kumlazimisha mtu akubali tu hata pale anapata hasara. Kuna mengi yameongelewa sana kuhusu huu mkataba, mengine yana ukweli na mengine ni propaganda zilizoambatana na ujinga wa kutofahamu mambo.

Lakini kubwa zaidi fahamu kwamba ndani ya nchi kumekuwa na kambi mbili zenye minyukano mikubwa sana. Kuna wale Pro-China na Pro-USA, bahati mbaya kuna baadhi ya watu wakubwa nchini wanahusika moja kwa moja na maslahi za hizi kambi (Hili ni jambo la hatari sana kwa usalama wa nchi). Kama tunaangalia maslahi ya kambi hizi mbili bila kuweka Tanzania mbele basi tutakuja kujuta sana huko mbele.

Kumekuwa na fitna, uzandiki na kuumizana sana, ikafika hadi kipindi tukaaminishwa kwamba Mzee Jakaya alikuwa ni mtu mpumbavu na mjinga kupindukia kiasi cha kutaka kuuza nchi yote hii kwa wakoloni wa Kichina na aliyezuia hili lisifanyike ni Mtanzania Mzalendo na Mwenye Uchungu na Nchi hii kuliko raisi mwingine yoyote kuwahi kutoke, Marehemu Raisi Magufuli. Hili kuna watu waliliamini na kuna wengine tulilitilia shaka kwasababu tulibahatika kufahamu kinachoendelea.

Nifahamuvyo mimi ni kwamba Mkataba ni makubaliono ya pande mbili na kama kuna mambo hayakaa vizuri ni vyema kurudi mezani na kufanya juu chini ili kuyazungumza upya. Alichokifanya Raisi Magufuli ni kutafuta umaarufu na kutaka kubagaza watu. Hivyo katika hili ningependa Raisi aunde tume maalumu ya wataalamu wa mikataba wa ndani ya nje ya nchi ambao watatusaidia kupitia vipengele mbalimbali, lakini pia kuajiri QUANTUM ANALYSTS ambao watafanya makadilio ya faida na hasara za kiuchumi ambazo Tanzania itazipata katika kipindi chote cha mkataba.

HILI LINANIKUMBUSHA JAMBO LILILOWAHI KUTOKEA KIPINDI CHA MZEE NYERERE:
Wakati Mzee Nyerere anataka kujenga TAZARA aliwafuata Wamarekani na wakasema ile reli ingejengwa kwa miaka 20. Kuna wataalamu wetu walipigia sana hili jambo chapuo lakini akaamua kwenda Uchina wakasema wangejenga kwa miaka 5. Mao Zedong na Zhou Enlai walimwambia Mzee Nyerere wewe ni rafiki yetu na sisi wote ni masikini, lakini mahitaji yetu na yenu ni tofauti hivyo tutawasaidia kujenga reli.

Marekani, Urusi, Uingereza na Ujerumani walipinga sana huu mradi kufanywa. Wale wahandisi walifanya uchunguzi ambapo walitembea kwa mguu kwa zaidi ya miezi tisa wakiangalia sehemu ambayo reli ingepita. Waziri Mkuu wa Uingereza bwana Harold Wilson alimwambia Nyerere kwamba mashirika ya ujasisi yamefanya uchunguzi na kufahamu kwamba mawaziri wengi wa Nyerere kama Mohamed Babu, Prof. Ibrahimu Kaduma na wengine ni majasusi wa Uchina na wanalipwa na Uchina ili kuuiza Tanzania.

Ilipingwa kampeni kubwa ambayo ilifika kipindi wakasema kwamba Tanzania inaenda kuwa koloni la Uchina. Baadhi ya wasomi wa Tanzania wa wakati huo walikubali na kuamini zile propaganda. Tofauti na Mzee Magufuli, Raisi Nyerere alikuwa ni Shrewd Statesman and an Excellent Diplomat with a clear understanding of global politics. Aliamua reli ijengwe na akasema yeye anachotaka ni pesa hajali kama ni Nyekundu kutoka kwa Wakomunisti au Bluu kutoka kwa Mabepari.

KITU AMBACHO WENGI HAWAKIFAHAMU:
Wakati reli inajengwa wamarekani walitumia vyombo vya habari na wataalamu kukashifu na kusema kwamba ile reli haitakuwa na kiwango cha ubora kama reli za Ulaya na Marekani. Wengi waliikashifu TAZARA kwa kuiita reli ya mwanzi (The Bamboo Railway): Yule Muhandisi wa kichina aliyesimamia Ujenzi wa reli na wenzake walishawahi kuvamiwa na majasusi wa Marekani hadi kupigana makonde wakati wa ujenzi wa ile reli.

SHIDA IKO WAPI SASA ???:
Nasema kwa ujasiri na uhakika mkubwa kabisa kwamba wasomi wa kitanzania walioko kwenye vyama vya siasa, jeshi na kwenye idara zetu za ujasusi na upelelezi ni watu ambao hawana uelewe mpana wa mambo. Watanzania wengi hatuna kumbukumbu ya nchi hii imetokea wapi na imefikaje hapa zaidi ya kupeana taarifa za kusimuliana tu. Hatufahamu dunia inaendaje na jinsi gani mwenendo huu wa dunia unaweza kuathiri siasa za nchi changa kama Tanzania. Pia hatufahamu wapi nchi yetu inaenda na hatuna kabisa uhakika wa taswira ya nchi yetu kwa miaka 20 ijayo.

Huwa najiuliza sana kama Mzee Nyerere angekuwa na roho nyepesi na hana uelewa mpana wa mambo sidhani kama leo hii Tanzania ingekuwa na reli ya TAZARA, sidhani. Nilimsikia Bwana Kakoko akisema kwamba Uchina ya leo siyo Uchina ile ya kipindi cha TAZARA na nikapata uhakika wa hicho nilichokisema hapo juu, cha kukosa uelewa wa siasa za dunia. AU Aidha Kakoko alikuwa anafahamu lakini akaamua kupiga Propaganda, lakini yote tisa mimi ambaye nimesoma Political Science and Diplomacy nikaamua kumsamehe kwasababu huenda hana utaalamu na haya mambo.

Ila nachokifahamu ni kwamba UCHINA alijenga TAZARA siyo kwasababu ya kusaidia wajamaa wenzake wa kiafrika peke yake, bali aliangalia maslahi ya kiuchumi ya miaka zaidi ya 40 mbele. Kama watanzania wanaamini kwamba ile reli ilikuwa ni zawadi kutoka kwa mjomba basi nawashauri waache kufikiri huo ujinga kuanzia leo. Uchina na Urusi wote walitoa misaada kwasababu ilifanikisha ajenda zao za kisiasa, kiusalama na kidiplomasia. TAZARA imemsaidia sana Uchina kidiplomasia, kiuchumi na kiusalama kama ambavyo Bagamoyo itamsaidia. Hivyo Uchina wa kipindi kile na Uchina wa leo ni walewale wale na hawajawahi badilika, kama mnadhani duniani kuna FREE-LUNCH basi mnajidanganya.

NINI KIFANYIKE SASA ???:
Katika pilika zangu za kusoma migogoro ya kimataifa, uwekezaji na kuifanyia kazi nimefahamu kitu kimoja cha msingi sana. Ili migogoro itatuliwe vizuri ni lazima kuwe na CONFIDENTIALITY, ili kusaidia Political Passion of Citizens zisivuruge kabisa majadiliano. Naamini hili suala lingekuwa wazi kuishia ngazi za Bunge tu, ambapo kamati za Bunge zingepewa mamlaka kulijadili na siyo kila raia ambaye hana hata ufahamu nalo akalizungumzia.

Sasa ili kukata mzizi wa fitina na kusaidia nchi isonge mbele Raisi angeunda tume huru ya uchunguzi (Commission of Inquiry) ya wataalamu ambayo itahusika na kupitia mkataba wa Bandari ya Bagamoyo. Tena ili kuhakikisha weledi Raisi atafute wasomi nguli hata wa nje ili kusiadia kuifanyia Consultancy hiyo Tume: Lakini pia maadamu watu walioandaa huo mkataba kipindi cha awamu ya Mzee Kikwete bado wapo basi waitwe na hiyo tume wahojiwe na watoe sababu za kwanini wao kukubaliana na ule mkataba.

Pia maadamu timu ya wataalamu wa kipindi cha utawala wa Raisi Magufuli waliomshauri akatae ule mradi kwasababu mkataba ni wa hovyo, kijinga na kifisadi bado wapo nao waitwe na tume na kutoa sababu zao. Mwisho wa siku tume ipimie nani anasema ukweli , wapi tumekwama na watoea mapendekezo ya jinsi mkataba unaweza kutekelezwa kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili (Tanzania na Uchina).

Siku zote kukiwa na utata wa namna hii njia pekee ni kuunda COMMISSION OF INQUIRY ya wataalamu ili kupima hoja zinazotolewa na pande zote mbili. Kitaalamu kama jambo limetokea na kila pande inasema kitu chake, tume za namna hii huundwa ili kutafuta ukweli ni upi, na mwisho huishia kutoa mapendekezo ya kitaalamu. Sasa nadhani suala nyeti kama hili linaweza kumalizwa na wataalamu siyo wanasiasa wasio na ufahamu wowote kuhusu hili jambo.

Mwisho kabisa Raisi na Bunge wapelekewe hiyo ripoti ya uchunguzi ili wao washauriane na kufanya maamuzi sahihi. Aidha tunaukataa huu mradi au tunaukubali: Hili la kusema eti mradi mzuri ila mkataba mbaya hatuyataki. Tukiendelea kwenda hivi gizani na kutegemea kauli za wanasiasa basi ukweli hatutaufahamu kamwe na hujuma na uzandiki vitaendelea.......

RAI YANGU KWA WASOMI WA KITANZANIA:
Mbali na maslahi ya kiuchumi ya Tanzania kuhusishwa, huu ni mtifuano mkubwa sana wa kimataifa ambao haukuanza leo wala jana. Nadhani kabla ya kukosoa, kukubali au kupinga ni vyema tukawa na taarifa sahihi kwanza. Pia tufahamu kabisa huu mradi ukijengwa au kukataliwa ni faida au hasara kwa haya mataifa mawili makubwa: Hivyo tusichague tuweke nchi yetu mbele kwanza na tupate taarifa sahihi ili kuepuka kutumika kisiasa bila kufahamu.
 
Braza shikamoo, ila wewe jamaa una akili nyingi mnoo.
Hapa nipo na nitarudi baadaye,.....
Long time no see...

Ndugu yangu Chige niliahidi ntarudi, lakini naomba nizungumzie kidogo kuhusu hili suala la The Belt-Road-Initiative (BRI). Kwanza kabisa, huu mradi ulianza kupangwa kipindi cha Raisi Hu-Juntao na aliweka wazi kabisa kwenye kikao cha halmashauri kuu ya chama cha kikomunisti cha Uchina.

Zaidi ya asilimia hamsini (50% of world merchandise) ya bidhaa za dunia hii zinapitia kwenye mfereji wa Malacca ambao ni muhimu sana kwa uchumi na usalama wa dunia. Hali hii inawafanya Uchina wajihisi kwamba lolote linaweza kutokea endepo ukanda wa Pasifiki utachafuka.

Gideon Rachman wa The Financial Times aliwahi kumnukuu moja wa Majemedari wakubwa kabisa wa Marekani akisema hivi "If the Chinese starts war in the Pasific, we will fucking sail those waters and choke them at the Malacca Strait". Mafuta yote yanayoenda Uchina, Vietnam, Japan na Korea kutoka Ghuba ya Uajemi hupitia mfereji wa Malacca.

Hivyo ukibana pale Uchina lazima atahangaika sana ukizingatia yeye ndiye nchi inayoongoza duniani kwa kuingiza mafuta na gesi kutoka nje (Greatest Importer of Oil and Gas). Pia ndiye msafirishaji mkubwa wa bidhaa duniani (The Greatest Exporter of Merchandise): Hivyo anategemea sana mfereji wa Malacca, lakini bahati mbaya sana Marekani ameshafahamu huu udhaifu ndiyo maana anaweka kambi ya jeshi eneo lile.

Uchina hili analiita The Malacca Dilemma, na Peter Navarro mmoja ya washauri wakubwa wa Raisi Donald Trump ameliandika sana kwenye kitabu chake kiitwacho Death by China: Confronting the Dragon-Global Call to Action , akikiri kwamba huu ni moja ya udhaifu ambao Marekani lazima iutumie katika kupambana na Uchina.

SASA TANZANIA INAINGIAJE KWENYE HILI:
Uchina katika kuhangaika na kukwepa hii kadhia akaamua kuja na BRI, ambapo wangefufua The GREAT SILK-ROAD ambayo itapita nchi kavu na baharini. Kama ulivyosema Bandari ya Bagamoyo ilitakiwa ijengwe Kenya na kwenye mkakati wa BRN inainyesha ni LAMU na siyo BAGAMOYO, lakini Mzee Kikwete na Benard Membe wakashawishi ije kujengwa hapa Tanzania.

Sasa lengo ni kwamba Uchina angejenga reli ndefu (Standard Gauge Railway) kutoka Uchina hadi nchini Pakistani ambapo ingekutana na bandari ya Gwadar (Gwadar Port) ambayo itakuwa na ukubwa kama ule wa bandari ya Bagamoyo. Lengo ni kwamba bandari hii itakuwa inapokea bidhaa zote kutoka Ghuba ya Uajemi na kuzipakia kwenye treni hadi Uchina, hivyo kukwepa kupita mfereji wa Malacca.

Hivyo, Bandari za Bagamoyo na Gwadar ndiyo yangekuwa malango makuu ya kuunganisha Bara la Afrika na Asia. Kwasababu Bagamoyo peke yake ingehudumia nchi nyingi sana za Afrika kwasababu ni Special Economic Zone. Pia kuna uwezekano mkubwa sana kama Bandari ya Bagamoyo ingejengwa basi ingeweza kuunganisha hadi Congo DRC, kufika Port Matada kwa njia ya reli na kufanikisha biashara baina ya Africa na Amerika Kusini.

SASA NINI TATIZO:
Watanzania wengi wanapinga sana huu mradi lakini binafsi Feasibility Study nimeiona. Pia waliohusika na kuandaa hii Study mkataba pia waliusona na nikabahatika kufahamu baadhi ya vitu. Inavyofahamika mkataba ni makubaliano ya pande mbili na huwezi kumlazimisha mtu akubali tu hata pale anapata hasara. Kuna mengi yameongelewa sana kuhusu huu mkataba, mengine yana ukweli na mengine ni propaganda zilizoambatana na ujinga wa kutofahamu mambo.

Lakini kubwa zaidi fahamu kwamba ndani ya nchi kumekuwa na kambi mbili zenye minyukano mikubwa sana. Kuna wale Pro-China na Pro-USA, bahati mbaya kuna baadhi ya watu wakubwa nchini wanahusika moja kwa moja na maslahi za hizi kambi (Hili ni jambo la hatari sana kwa usalama wa nchi). Kama tunaangalia maslahi ya kambi hizi mbili bila kuweka Tanzania mbele basi tutakuja kujuta sana huko mbele.

Kumekuwa na fitna, uzandiki na kuumizana sana, ikafika hadi kipindi tukaaminishwa kwamba Mzee Jakaya alikuwa ni mtu mpumbavu na mjinga kupindukia kiasi cha kutaka kuuza nchi yote hii kwa wakoloni wa Kichina na aliyezuia hili lisifanyike ni Mtanzania Mzalendo na Mwenye Uchungu na Nchi hii kuliko raisi mwingine yoyote kuwahi kutoke, Marehemu Raisi Magufuli. Hili kuna watu waliliamini na kuna wengine tulilitilia shaka kwasababu tulibahatika kufahamu kinachoendelea.

Nifahamuvyo mimi ni kwamba Mkataba ni makubaliono ya pande mbili na kama kuna mambo hayakaa vizuri ni vyema kurudi mezani na kufanya juu chini ili kuyazungumza upya. Alichokifanya Raisi Magufuli ni kutafuta umaarufu na kutaka kubagaza watu. Hivyo katika hili ningependa Raisi aunde tume maalumu ya wataalamu wa mikataba wa ndani ya nje ya nchi ambao watatusaidia kupitia vipengele mbalimbali, lakini pia kuajiri QUANTUM ANALYSTS ambao watafanya makadilio ya faida na hasara za kiuchumi ambazo Tanzania itazipata katika kipindi chote cha mkataba.

HILI LINANIKUMBUSHA JAMBO LILILOWAHI KUTOKEA KIPINDI CHA MZEE NYERERE:
Wakati Mzee Nyerere anataka kujenga TAZARA aliwafuata Wamarekani na wakasema ile reli ingejengwa kwa miaka 20. Kuna wataalamu wetu walipigia sana hili jambo chapuo lakini akaamua kwenda Uchina wakasema wangejenga kwa miaka 5. Mao Zedong na Zhou Enlai walimwambia Mzee Nyerere wewe ni rafiki yetu na sisi wote ni masikini, lakini mahitaji yetu na yenu ni tofauti hivyo tutawasaidia kujenga reli.

Marekani, Urusi, Uingereza na Ujerumani walipinga sana huu mradi kufanywa. Wale wahandisi walifanya uchunguzi ambapo walitembea kwa mguu kwa zaidi ya miezi tisa wakiangalia sehemu ambayo reli ingepita. Waziri Mkuu wa Uingereza bwana Harold Wilson alimwambia Nyerere kwamba mashirika ya ujasisi yamefanya uchunguzi na kufahamu kwamba mawaziri wengi wa Nyerere kama Mohamed Babu, Prof. Ibrahimu Kaduma na wengine ni majasusi wa Uchina na wanalipwa na Uchina ili kuuiza Tanzania.

Ilipingwa kampeni kubwa ambayo ilifika kipindi wakasema kwamba Tanzania inaenda kuwa koloni la Uchina. Baadhi ya wasomi wa Tanzania wa wakati huo walikubali na kuamini zile propaganda. Tofauti na Mzee Magufuli, Raisi Nyerere alikuwa ni Shrewd Statesman and an Excellent Diplomat with a clear understanding of global politics. Aliamua reli ijengwe na akasema yeye anachotaka ni pesa hajali kama ni Nyekundu kutoka kwa Wakomunisti au Bluu kutoka kwa Mabepari.

KITU AMBACHO WENGI HAWAKIFAHAMU:
Wakati reli inajengwa wamarekani walitumia vyombo vya habari na wataalamu kukashifu na kusema kwamba ile reli haitakuwa na kiwango cha ubora kama reli za Ulaya na Marekani. Wengi waliikashifu TAZARA kwa kuiita reli ya mwanzi (The Bamboo Railway): Yule Muhandisi wa kichina aliyesimamia Ujenzi wa reli na wenzake walishawahi kuvamiwa na majasusi wa Marekani hadi kupigana makonde wakati wa ujenzi wa ile reli.

SHIDA IKO WAPI SASA ???:
Nasema kwa ujasiri na uhakika mkubwa kabisa kwamba wasomi wa kitanzania walioko kwenye vyama vya siasa, jeshi na kwenye idara zetu za ujasusi na upelelezi ni watu ambao hawana uelewe mpana wa mambo. Watanzania wengi hatuna kumbukumbu ya nchi hii imetokea wapi na imefikaje hapa zaidi ya kupeana taarifa za kusimuliana tu. Hatufahamu dunia inaendaje na jinsi gani mwenendo huu wa dunia unaweza kuathiri siasa za nchi changa kama Tanzania. Pia hatufahamu wapi nchi yetu inaenda na hatuna kabisa uhakika wa taswira ya nchi yetu kwa miaka 20 ijayo.

Huwa najiuliza sana kama Mzee Nyerere angekuwa na roho nyepesi na hana uelewa mpana wa mambo sidhani kama leo hii Tanzania ingekuwa na reli ya TAZARA, sidhani. Nilimsikia Bwana Kakoko akisema kwamba Uchina ya leo siyo Uchina ile ya kipindi cha TAZARA na nikapata uhakika wa hicho nilichokisema hapo juu, cha kukosa uelewa wa siasa za dunia. AU Aidha Kakoko alikuwa anafahamu lakini akaamua kupiga Propaganda, lakini yote tisa mimi ambaye nimesoma Political Science and Diplomacy nikaamua kumsamehe kwasababu huenda hana utaalamu na haya mambo.

Ila nachokifahamu ni kwamba UCHINA alijenga TAZARA siyo kwasababu ya kusaidia wajamaa wenzake wa kiafrika peke yake, bali aliangalia maslahi ya kiuchumi ya miaka zaidi ya 40 mbele. Kama watanzania wanaamini kwamba ile reli ilikuwa ni zawadi kutoka kwa mjomba basi nawashauri waache kufikiri huo ujinga kuanzia leo. Uchina na Urusi wote walitoa misaada kwasababu ilifanikisha ajenda zao za kisiasa, kiusalama na kidiplomasia. TAZARA imemsaidia sana Uchina kidiplomasia, kiuchumi na kiusalama kama ambavyo Bagamoyo itamsaidia. Hivyo Uchina wa kipindi kile na Uchina wa leo ni walewale wale na hawajawahi badilika, kama mnadhani duniani kuna FREE-LUNCH basi mnajidanganya.

NINI KIFANYIKE SASA ???:
Katika pilika zangu za kusoma migogoro ya kimataifa, uwekezaji na kuifanyia kazi nimefahamu kitu kimoja cha msingi sana. Ili migogoro itatuliwe vizuri ni lazima kuwe na CONFIDENTIALITY, ili kusaidia Political Passion of Citizens zisivuruge kabisa majadiliano. Naamini hili suala lingekuwa wazi kuishia ngazi za Bunge tu, ambapo kamati za Bunge zingepewa mamlaka kulijadili na siyo kila raia ambaye hana hata ufahamu nalo akalizungumzia.

Sasa ili kukata mzizi wa fitina na kusaidia nchi isonge mbele Raisi angeunda tume huru ya uchunguzi (Commission of Inquiry) ya wataalamu ambayo itahusika na kupitia mkataba wa Bandari ya Bagamoyo. Tena ili kuhakikisha weledi Raisi atafute wasomi nguli hata wa nje ili kusiadia kuifanyia Consultancy hiyo Tume: Lakini pia maadamu watu walioandaa huo mkataba kipindi cha awamu ya Mzee Kikwete bado wapo basi waitwe na hiyo tume wahojiwe na watoe sababu za kwanini wao kukubaliana na ule mkataba.

Pia maadamu timu ya wataalamu wa kipindi cha utawala wa Raisi Magufuli waliomshauri akatae ule mradi kwasababu mkataba ni wa hovyo, kijinga na kifisadi bado wapo nao waitwe na tume na kutoa sababu zao. Mwisho wa siku tume ipimie nani anasema ukweli , wapi tumekwama na watoea mapendekezo ya jinsi mkataba unaweza kutekelezwa kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili (Tanzania na Uchina).

Siku zote kukiwa na utata wa namna hii njia pekee ni kuunda COMMISSION OF INQUIRY ya wataalamu ili kupima hoja zinazotolewa na pande zote mbili. Kitaalamu kama jambo limetokea na kila pande inasema kitu chake, tume za namna hii huundwa ili kutafuta ukweli ni upi, na mwisho huishia kutoa mapendekezo ya kitaalamu. Sasa nadhani suala nyeti kama hili linaweza kumalizwa na wataalamu siyo wanasiasa wasio na ufahamu wowote kuhusu hili jambo.

Mwisho kabisa Raisi na Bunge wapelekewe hiyo ripoti ya uchunguzi ili wao washauriane na kufanya maamuzi sahihi. Aidha tunaukataa huu mradi au tunaukubali: Hili la kusema eti mradi mzuri ila mkataba mbaya hatuyataki. Tukiendelea kwenda hivi gizani na kutegemea kauli za wanasiasa basi ukweli hatutaufahamu kamwe na hujuma na uzandiki vitaendelea.......

RAI YANGU KWA WASOMI WA KITANZANIA:
Mbali na maslahi ya kiuchumi ya Tanzania kuhusishwa, huu ni mtifuano mkubwa sana wa kimataifa ambao haukuanza leo wala jana. Nadhani kabla ya kukosoa, kukubali au kupinga ni vyema tukawa na taarifa sahihi kwanza. Pia tufahamu kabisa huu mradi ukijengwa au kukataliwa ni faida au hasara kwa haya mataifa mawili makubwa: Hivyo tusichague tuweke nchi yetu mbele kwanza na tupate taarifa sahihi ili kuupa kutumika kisiasa bila kufahamu.
 
Hivi nyie watu huwa hamsikii mpaka damu iwatoke masikioni eeh? Tumeshasema miradi ya wizi wizi na ujanja ujanja iliishia wakati wa Kikwete, kuanzia Magu na kuendelea tunataka kila kitu wazi wazi. Wakati wa kutuchezea akili ulienda na kikwete. Tunataka miradi ya win win situation.
Btw, ardhi yetu ya bagamoyo na uhuru wetu vina thamani zaidi kuliko maisha ya huyo mtoto aliyekamatwa na sembe.
 
Hivi nyie watu huwa hamsikii mpaka damu iwatoke masikioni eeh? Tumeshasema miradi ya wizi wizi na ujanja ujanja iliishia wakati wa Kikwete, kuanzia Magu na kuendelea tunataka kila kitu wazi wazi. Wakati wa kutuchezea akili ulienda na kikwete. Tunataka miradi ya win win situation.
Btw, ardhi yetu ya bagamoyo na uhuru wetu vina thamani zaidi kuliko maisha ya huyo mtoto aliyekamatwa na sembe.
Porojo at work!

Kila mwenye akili timamu anafahamu Jiwe nae ni miongoni mwa wezi wakubwa waliopata kutokea nchi hii.

Katumia billions of TZS kununua ndege, hata nikikuuliza wewe na ukoo wako wote ni wapi tenda ilitangazwa, hamuwezi kuwa na majibu! Ili asikaguliwe, akaamua kuhamishia Wakala wa Ndege za Serikali Ikulu, huku akiacha misukule yake ikiimba nyimbo za mapambio!!

Halafu hivi hujishtukii unavyosema "tunataka kila kitu wazi wazi" wakati utawala wa JPM ndio uliongoza kuficha yale yanayofanyika huko serikalini?!
 
Usiwaite wazalendo tuu
Waite wazalendo wajinga.

Vibaraka wa Mabeberu wa kirumi kwa Karne 21 bado wapo Afrika kuihudumia Rumi huku wao wakiwaacha waafrika wenzao wakiishi maisha magumu.Vatican wazungu wakiishi kama peponi. Waafrika wamelogwa.
 
Porojo at work!

Kila mwenye akili timamu anafahamu Jiwe nae ni miongoni mwa wezi wakubwa waliopata kutokea nchi hii.

Katumia billions of TZS kununua ndege, hata nikikuuliza wewe na ukoo wako wote ni wapi tenda ilitangazwa, hamuwezi kuwa na majibu! Ili asikaguliwe, akaamua kuhamishia Wakala wa Ndege za Serikali Ikulu, huku akiacha misukule yake ikiimba nyimbo za pongezi kwa Jiwe!!

Halafu hivi hujishtukii unavyosema "tunataka kila kitu wazi wazi" wakati utawala wa JPM ndio uliongoza kuficha yale yanayofanyika huko serikalini?!
Nenda kachukue mshiko wako umeshawasha tayari kwa kutetea miradi ya wizi.
 
Hivi nyie watu huwa hamsikii mpaka damu iwatoke masikioni eeh? Tumeshasema miradi ya wizi wizi na ujanja ujanja iliishia wakati wa Kikwete, kuanzia Magu na kuendelea tunataka kila kitu wazi wazi. Wakati wa kutuchezea akili ulienda na kikwete. Tunataka miradi ya win win situation.
Btw, ardhi yetu ya bagamoyo na uhuru wetu vina thamani zaidi kuliko maisha ya huyo mtoto aliyekamatwa na sembe.
Unajua ukubwa wa Ardhi ya kutoka Mtukula mpaka Tanga ina ukubwa gani?
Je,Hapo katikati kuna mradi wowote utakaofanyika kwenye hiyo ardhi ya bomba la mafuta la mabeberu ?

Je, huoni Bagamoyo utaibuka kuwa eneo kubwa la kubiashara na ajira ukilinganisha na maelfu ya Hekari za kutokea Mtukula mpaka Tanga yatakayo yamekufa bila shughuli yoyote ya kiuchumi?

Acheni Uzalendo wa Kikabila.
Mmeturudisha sana nyuma?
 
Unajua ukubwa wa Ardhi ya kutoka Mtukula mpaka Tanga ina ukubwa gani?
Je,Hapo katikati kuna mradi wowote utakaofanyika kwenye hiyo ardhi ya bomba la mafuta la mabeberu ?

Je, huoni Bagamoyo utaibuka kuwa eneo kubwa la kubiashara na ajira ukilinganisha na maelfu ya Hekari za kutokea Mtukula mpaka Tanga yatakayo yamekufa bila shughuli yoyote ya kiuchumi?

Acheni Uzalendo wa Kikabila.
Mmeturudisha sana nyuma?
Na pia ungemuuliza tija inayopatikana kwenye ile ardhi inayotifuliwa tifuliwa kule kwenye migodi na kutuachia mahandaki!!
 
Tutasoma yote hayo huko baadae, lakini kwa sasa nina haya machache:

1. Hakuna nchi yoyote duniani isiyopigania maslahi yake; isipokuwa labda hizi zetu za 'Banana Republic' ambazo maslahi ya viongozi wake ndiyo yanayowekwa mbele zaidi ya yale ya nchi husika.
China wana maslahi, ndiyo maana ya hiyo BRI; kwa hiyo kama nchi inao viongozi wenye akili timamu hawawezi kusubiri mpaka waambiwe na "mabeberu" ni wapi maslahi ya nchi zao yalipo.
Kama wanajua maslahi ya nchi zao yako wapi, basi watafanya uamzi sahihi kuhusu mradi ulio na manufaa kwa nchi zao.

Tuna miaka zaidi ya sitini sasa tukijiamlia mambo yetu. Tunao watu waliosoma vizuri na kuelewa mambo vizuri karibu katika kila fani. Hatuna visingizio tena vya kusema hatuna raslimali watu. Iliyopo sasa ni kutojua tu jinsi ya kuitumia vyema raslimali hiyo.

Acha mchina aje na BRI yake atuonyeshe anataka kufanya nini, na sisi tumueleze mategemeo yetu ni nini, bila ya aibu au woga wowote.
Tujadiliane, tukikubaliana, ajenge kwa makubaliano tuliyofikia pamoja na yeye; kama hatukubaliani juu ya matakwa yake, aende zake, na wala isiwe tena hizi kelele za mabeberu hivi au mabeberu vile. Huu utakuwa ni uamzi wetu.

Na hii haituzuii kuingia kwenye mapatano mengine juu ya mradi huo, eti kwa kuogopa tu "mabeberu".
Tayari Biden na BoJo wanajadili uwezekano wa kuweka $65 Billion mezani kwa kazi hiyo ya kupambana na BRI. Hatuwezi kuwaogopa hawa wala mwingine yeyote, kama tunajua maslahi yetu ni yapi.Hizo enzi za kuyumbishwa na kugawanywa zimepitwa na wakati - ni maslahi yetu pekee ndiyo yaliyo muhimu.

Na si hawa pekee, yaani China na Mabeberu tunaoweza kushirikiana nao kujenga mradi huo, na sio lazima iwe mmoja, wawili au kundi lwa wawekezaji. Huu ni mradi mkubwa, kwa hiyo kila mtu anaweza kushiriki ankoona kunamfaa, na tutakaribisha aje tujadili, tukiafikiana anajiunga.

Tunaweza pia kuanza kujenga sisi wenyewe taratibu, kama Lamu inavyojengwa hivi sasa, baada ya kukosa mwekezaji wa kuuchukua kama huyo BRI na wengine.

2. Ukweli ni kwamba, Tanzania na pwani yake ipo pazuri mno. Wenzetu hapo juu wanahangaika kwelikweli kujiuza bila ya mafanikio yoyote.

Ni viongozi wetu tu watumie akili zao na uzalendo wao ili nchi yetu ifaidike na mahali ilipowekwa kijiografia.

Hakuna lazima ya kujisalimisha kwa mchina kama masharti yake hayana maslahi kwetu.
 
Back
Top Bottom