Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu na haswa mashabiki na wapenzi wa chama cha magamba, hili ni onyo kwenu na mkipuuzia ole wenu siku yaja tena inabisha hodi. Katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni imejitokeza tabia ya askari kuua raia wasio na hatia. Tukio la hivi karibuni ni la Nyamongo ambapo raia zaidi ya watano tena wasio na hatia waliuawa. Jambo hili limeanza kuzoeleka miongoni mwetu na kuonekana kuwa ni la kawaida. Lakini ukweli ni kuwa huo ni unyama mkubwa usiovumilika. Inawezekana mimi na wewe msomaji bado hujawa mhanga wa hiyo tabia ya askari lakini piga picha ya watu waliondokewa na wapendwa wao kutokana na risasi za askari wanajisikiaje. Lazima wana hasira sana.
Chama cha magamba kisipokemea serikali yake kuacha mauaji ya raia wake, kitambue kuwa kinajichimbia kaburi. Damu ya watanzania haiwezi kupotea bure. Chama cha magamba kitambue kuwa suluhisho la mtatizo ya watanzania haliwezi kupatikana kwa kupiga risasi na kuua raia. Suluhisho ni kutenda haki na kuwapatia maendeleo wananchi. Trend hii ya kuua raia ikiachwa iendelee, mwisho wake siyo mzuri.
Chama cha magamba kisipokemea serikali yake kuacha mauaji ya raia wake, kitambue kuwa kinajichimbia kaburi. Damu ya watanzania haiwezi kupotea bure. Chama cha magamba kitambue kuwa suluhisho la mtatizo ya watanzania haliwezi kupatikana kwa kupiga risasi na kuua raia. Suluhisho ni kutenda haki na kuwapatia maendeleo wananchi. Trend hii ya kuua raia ikiachwa iendelee, mwisho wake siyo mzuri.