Mabalozi wetu nje ya nchi wanatuma intelijensia gani huku nyumbani?

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Songombinde ya sakata la sarawili imeniacha nikijiuliza kama kuna mambo yoyote yale ya "kiintelinjensia" yanayotumwa na mabalozi au watumishi wa balozi zetu kutoka ng'ambo kuja huku nyumbani. Maana kuna mengi ambayo yamekuwa kero hapa nyumbani yaliyotokea nje ya nchi ambako tuna mabalozi wetu. Kuanzia mikataba mibovu ya madini, bidhaa feki, kupunjwa kwenye mauzo, n.k. n.k. Ni nini basi wanachokifanya huko ukiachilia mbali kusaidia mara moja moja Watanzania wanaopoteza maisha ughaibuni na kupokea wageni wa serikali kwenye ziara zao huko??! Or are we too intelligent to gather some intelligence overseas???

Mbona nchi kama Marekani mabalozi, watumishi na majasusi wao wanaonekana kutuma kila kitu ambavyo vingine hata hapahapa Bongo si wenyewe hatuvijui?? Somehow I just wish hizi cables za wikileaks zingelihusu ubalozi wa serikali ya Uingereza, maana connection yao na mambo wafanyayo na viongozi wa nchi yetu ni ya kutuacha midomo wazi!!!
 
Kwenye mabalozi wanapelekana kiushikaji sana.Mfano nilishakutana na mtu mmjoa anatoka nje.Alipewa viza kuja Tz alipofika hapa maofisa wa Uhamiaji wakamwambia visa yaho imekosewa.Nikawauliza sasa nani anakosa mpewa visa au mtoa viza wakasema sisi hatujui huyo mgeni lazima alipe tena.Nikabisana nao sana baadae wakasema huko kwenye Ubalozi waliopo siyo maafisa wa Uhamiaji bali wamepelkwa tu hata hawana sifa za uhamiaji.Nikamwambia mgeni alipe tena.Kwa hiyo huko wanapelekana tu bila kuangalia vigezo vya nafsi husika.
 
Kwenye mabalozi wanapelekana kiushikaji sana.Mfano nilishakutana na mtu mmjoa anatoka nje.Alipewa viza kuja Tz alipofika hapa maofisa wa Uhamiaji wakamwambia visa yaho imekosewa.Nikawauliza sasa nani anakosa mpewa visa au mtoa viza wakasema sisi hatujui huyo mgeni lazima alipe tena.Nikabisana nao sana baadae wakasema huko kwenye Ubalozi waliopo siyo maafisa wa Uhamiaji bali wamepelkwa tu hata hawana sifa za uhamiaji.Nikamwambia mgeni alipe tena.Kwa hiyo huko wanapelekana tu bila kuangalia vigezo vya nafsi husika.

This is true, ubalozini huko wamejazana kina Malecela, Sokoine, Mongella etc na wanajeshi.
 
Mkuu Kiranga, jambo jingine ni lile la kuwa na mabalozi eti "wa kudumu"?? What the heck is this... ufalme ubalozini au ndiyo hukumu kwa familia nyingine kwamba hazitakuja ziwe na vijana wenye sifa za kuwa mabalozi??!!
 
Songombinde ya sakata la sarawili imeniacha nikijiuliza kama kuna mambo yoyote yale ya "kiintelinjensia" yanayotumwa na mabalozi au watumishi wa balozi zetu kutoka ng'ambo kuja huku nyumbani. Maana kuna mengi ambayo yamekuwa kero hapa nyumbani yaliyotokea nje ya nchi ambako tuna mabalozi wetu. Kuanzia mikataba mibovu ya madini, bidhaa feki, kupunjwa kwenye mauzo, n.k. n.k. Ni nini basi wanachokifanya huko ukiachilia mbali kusaidia mara moja moja Watanzania wanaopoteza maisha ughaibuni na kupokea wageni wa serikali kwenye ziara zao huko??! Or are we too intelligent to gather some intelligence overseas???

Mbona nchi kama Marekani mabalozi, watumishi na majasusi wao wanaonekana kutuma kila kitu ambavyo vingine hata hapahapa Bongo si wenyewe hatuvijui?? Somehow I just wish hizi cables za wikileaks zingelihusu ubalozi wa serikali ya Uingereza, maana connection yao na mambo wafanyayo na viongozi wa nchi yetu ni ya kutuacha midomo wazi!!!

Nimewai kuazisha thread na katika hiyo thread nikatoa comment hii

Mtazamaji said:
Nadahni tatizo la masingi sio utashi wa kisiasa tatizo la msingi ni Muundo wenyewe wa hizi tasisi zetu. Mfano mdogo jiulize maswali haya au nisahihishe kama nimekosea.

Kwenye baadhi ya balozi zetu utasikia kuna mwambata wa kijeshi. sijui wana kazi gani? je kwa nini msisitizo usiwe kuweka wambata wa kiuchumi/kiteknolojia kwenye balozi hizo kama South africa.? katka karne ya sasa kuna faida ya kuwa na mwambata wa kijeshi south africa???? nadhani ni kukariri na kukosa kwenda na wakati au kukosa ubunifu?

Pili maono au hisia zangu ofisi zetu za balozi ziko underutilised. Nasema hivi sijui kama mablozi wetu wanawajibika kutuma report za kiuchumi au kitekonolojiia zinatozotekea kwenye nchi walizopo zinazoweza kuwafaidisha watanzania.?

Vile vile nina hakika kuna opportunities nyingi kwa watanzania zinapatikana china zaidi ya zile zinajulikana . nani anatakiwa kuwa mstari wa mbele kuziwakilisha. Upande wao wachina makampuni yao na watu wao wana taarifa ni km ngapi za bara bara na miradi ya ujenzi itajengwa mwaka ujao wa fedha Tanzania. Je ubalozi wa Tannzani tunajua wachina wanatumia chai ya dola ngapi kwa mwaka? Je tunajua % kubwa ya chai ya wanayotumia wachina wanaagiza kutoka wapi na kwa nini?

Sio Lazima afanye kazi kijasusi nadhani mchumi wa kawaida akipewa kazi ubalozini ya na kuelekezwa na takwimu gani tunataka kutoka china au nchi yeyote atazipata na hii itatusukuma mbele.

Mfano mwingine ofisi ya uBalozi wa japan nchini tanzania itakuwa na takwimu ni toyota ngapi used na new wataanzania wanaagiza kwa mwaka. Lakini unaweza kuuuliza na usipate jibu ubalozi wa tanzania nchini japan kuhusu Tanzanite/dhahabu ya shilingi ngapi wajapan wananunua kotoka tanzania. source https://www.jamiiforums.com/jamii-intelligence/62245-tanzania-yetu-ina-majasusi-wa-aina-gani-2.html

Kwa kweli Inashangaza eti karne hii tunaona umuhimu wa kuwa na mwambata wa kijeshi Afrika kusini lakini tunshidnwa kupata akili ya kuwa na cheo kama hicho cha mwambata wa kitaalii, mwambata wa kiuchumi au biashara au mwambata kitenolojia....... L

Labda bado tuko kwenye vita ya ukombozi
 
Songombinde ya sakata la sarawili imeniacha nikijiuliza kama kuna mambo yoyote yale ya "kiintelinjensia" yanayotumwa na mabalozi au watumishi wa balozi zetu kutoka ng'ambo kuja huku nyumbani. Maana kuna mengi ambayo yamekuwa kero hapa nyumbani yaliyotokea nje ya nchi ambako tuna mabalozi wetu. Kuanzia mikataba mibovu ya madini, bidhaa feki, kupunjwa kwenye mauzo, n.k. n.k. Ni nini basi wanachokifanya huko ukiachilia mbali kusaidia mara moja moja Watanzania wanaopoteza maisha ughaibuni na kupokea wageni wa serikali kwenye ziara zao huko??! Or are we too intelligent to gather some intelligence overseas???

Mbona nchi kama Marekani mabalozi, watumishi na majasusi wao wanaonekana kutuma kila kitu ambavyo vingine hata hapahapa Bongo si wenyewe hatuvijui?? Somehow I just wish hizi cables za wikileaks zingelihusu ubalozi wa serikali ya Uingereza, maana connection yao na mambo wafanyayo na viongozi wa nchi yetu ni ya kutuacha midomo wazi!!!

Wanachunguza kama kuna maandamano ya kuipinga serikali ya mtukufu Dr Alcohol
 
Back
Top Bottom