Mabadiliko yatachukua muda kutokana na unafiki wa wanasias.

Mzee Uchwara

Senior Member
Oct 28, 2013
119
35
Ndugu wana Jf, kutokana na hali ya kiuchumi ya nchi yetu kuwa katika hali isiyoridhisha tunahitaji mabadiliko ya haraka ya kiuongozi. Lakini inashindikana kutokana na unafiki wa wanasiasa. Ndani ya chadema kuna sinto fahamu inayoendelea kuhusu kuvuliwa madaraka bwana zito na wenzake, tumeshuhudia matamko mengi sana kila kukicha, Embu tujikumbushe toka nyuma kuhushu shutuma ambazo zito zilimrenga hazikuanza leo zilianza toka zamani na zilitokana na yeye kutaka kugombea U/kiti. Pia hali hii ilimtokea marehe chacha wangwe. Mwaka 2010 baada ya uchaguzi mkuu chadema kilichukua uongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni. Nakumbuka hakukuwa na shutuma za zito kuuza majimbo ya uchaguzi. Embu tujiulize je kama zito aliuza majimbo na hakushiriki kikamilifu ktk kumpigie dr slaa kampeni kwa nini alichaguliwa kuwa naibu kiongozi wa upinzani? Na kuhusu suala la posho chadema hao hao walimshambulia sana shibuda kipindi kile alipo kataa msimamo wa kutochukua posho je mmesahau? Na pia chadema waliitaka serikali ipunguze matumizi ikiwa pamoja na kutotumia magari yenye gharama kubwa na mh mbowe alirudisha gari la KUB lakini kutokana na unafiki wa wanasiasa wa kuto simamia yale wanayoongea alilifata kimiya kimiya na kuanza kulitumia. Pia tumeshuhudia mh lema akisahau na kuanza kutetea posho na kuanza kumshambulia zito. Embu tujiulize hivi hawa akina yericko, ben, nasari hizi nguvu za kumzushia na kumkashfu zito wanatoa wapi? Na kwa nini hawachukuriwi hatua? Mbona wale wanaomsema mbowe huchukuliwa hatua na kuitwa wasaliti! Ukitazama kwa makini utagundua unafiki wa wanasiasa kwa kuchochea migogoro kwa maslai yao binafsi na kuwazuia na kuwakwamisha wale wanaotaka madiliko ya kweli katika nchi yetu.
 
Embu tujiulize je kama zito aliuza majimbo na hakushiriki kikamilifu ktk kumpigie dr slaa kampeni kwa nini alichaguliwa kuwa naibu kiongozi wa upinzani?.
pengine MM alijihakikishia anajipigia pande kama ilivyo ada kwakuwa yeye ni mwenye tamaa na madaraka, na mara zote ameonyesha hilo. hata kutokutaka kutoka chadema ni kiashiria kuwa anajua atapoteza mashiko machoni mwa watu na ndio maana anang'ang'ana akidai sababu za yeye kutolewa sio zile walizomtuhumu.


Na kuhusu suala la posho chadema hao hao walimshambulia sana shibuda kipindi kile alipo kataa msimamo wa kutochukua posho je mmesahau? Na pia chadema waliitaka serikali ipunguze matumizi ikiwa pamoja na kutotumia magari yenye gharama kubwa na mh mbowe alirudisha gari la KUB lakini kutokana na unafiki wa wanasiasa wa kuto simamia yale wanayoongea alilifata kimiya kimiya na kuanza kulitumia.

haina uhusiano na swala la sasa la MM, MM anataka kupata pa kutokea. kitendo cha yeye kukataa kumpa sapoti m/kiti wake katika vikao ni dalili kuwa alitaka amzunguke ili mwishowe aonekane yeye ndiye bora kuliko aliyepo. lengo lake sio mafanikio ya chama bali yake binafsi. MM alitakiwa ajue chochote alichokifanya hakukifanya kwaajili yake bali kwa maslahi ya Taasisi, kwani kashfa yeyote ingemkuta MM katika yale aliyoyafichua nchi hii yangekuwa si yake bali ya Taasisi(kitu cha msingi sana alitakiwa kukijua.

Pia tumeshuhudia mh lema akisahau na kuanza kutetea posho na kuanza kumshambulia zito. Embu tujiulize hivi hawa akina yericko, ben, nasari hizi nguvu za kumzushia na kumkashfu zito wanatoa wapi? Na kwa nini hawachukuriwi hatua? Mbona wale wanaomsema mbowe huchukuliwa hatua na kuitwa wasaliti! Ukitazama kwa makini utagundua unafiki wa wanasiasa kwa kuchochea migogoro kwa maslai yao binafsi na kuwazuia na kuwakwamisha wale wanaotaka madiliko ya kweli katika nchi yetu.

hawa wakina lema walishaonywa kuacha ushabiki,
pia umegusia neno maslahi binafsi, je umewahi kuthubutu kujiuliza M2 ni nani na kwanini waliomba radhi lakini wamekataa kumtaja?. Na kwanini hakuna anayehoji huku nje, jechama hakimjui na kwanini hakimtaji kama kinamjua,na pengine hapa ndipo mzizi wa matatizo ya kutokuaminiana kunapoanzia katika kuendesha chama. mengi tunayojadili ni yale bila kumjua M2, na hapa tunaishia kuwa washabiki tu.
kiukweli ni kuwa MM anataka kugombea urais 2015 kama alivyowahahidi wafuasi wake na ametumia utaalam =mkubwa kumsoma mpinzani wake na ndipo hali tete inapoanzia.
 
MM ana tamaa ya madaraka...
Ndio maana yeye anajiona ni maarufu kuliko chama...
MM anayosupport kutoka TISS na miCCM flan...kwa lengo maalum...

Hayo matamko yanayotolewa na watu chumbani yanaratibiwa kwa ukaribu na CCM

Hii issue ya MM kugombana na CHADEMA ndio kete ya mwisho kwa CCM/TISS kudeal na Chadema before 2015...

Kuna uchaguzi Chadema...umetangazwa..kitakachofanyika CCM wanataka kumweka mtu wao..kwa lengo maalum

Tambua uchaguzi mkuu 2010 MM alikuwa na mawasiliano na TISS...ili kuvujisha siri za Chadema...tafuta mahojiano ya Zitto hapa JF..alikiri mwenyewe ila hakutoa sababu za msingi za mawasiliano..

Utagundua uongozi wa juu wa Chadema ni matatizo makubwa kwa CCM...hawahongeki..
Ila imeletwa dhana ya UKABILA makusudi kutoka CCM...ili kuwalaghai watanzania/wadanganyika ili mimi na wewe tuamini kirahisi ili wao waendeleze mikataba feki..elimu duni afya mbovu nk

Tambua watanzania hawajui kuchambua mambo kiundani..ni rahisi mno kuamini propaganda za ccm..
 
Slaa kapigwa marufu kwenda Kigoma. Akifanya mchezo kina Afande Sele watampiga marufuku kwenda Morogoro.

Slaa kwa sasa bora awe mpole tu na kumuomba radhi Zitto kwa fitina alizomfanyia...
 
Slaa kapigwa marufu kwenda Kigoma. Akifanya mchezo kina Afande Sele watampiga marufuku kwenda Morogoro.

Slaa kwa sasa bora awe mpole tu na kumuomba radhi Zitto kwa fitina alizomfanyia...
Slaa lazima amuombe msamaha zitto vinginevyo dunia ataiona mbaya sana make kwa mungu tayari alishaharibu sasa ataharibu na duniani.
 
Ndugu wana Jf, kutokana na hali ya kiuchumi ya nchi yetu kuwa katika hali isiyoridhisha tunahitaji mabadiliko ya haraka ya kiuongozi. Lakini inashindikana kutokana na unafiki wa wanasiasa. Ndani ya chadema kuna sinto fahamu inayoendelea kuhusu kuvuliwa madaraka bwana zito na wenzake, tumeshuhudia matamko mengi sana kila kukicha, Embu tujikumbushe toka nyuma kuhushu shutuma ambazo zito zilimrenga hazikuanza leo zilianza toka zamani na zilitokana na yeye kutaka kugombea U/kiti. Pia hali hii ilimtokea marehe chacha wangwe. Mwaka 2010 baada ya uchaguzi mkuu chadema kilichukua uongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni. Nakumbuka hakukuwa na shutuma za zito kuuza majimbo ya uchaguzi. Embu tujiulize je kama zito aliuza majimbo na hakushiriki kikamilifu ktk kumpigie dr slaa kampeni kwa nini alichaguliwa kuwa naibu kiongozi wa upinzani? Na kuhusu suala la posho chadema hao hao walimshambulia sana shibuda kipindi kile alipo kataa msimamo wa kutochukua posho je mmesahau? Na pia chadema waliitaka serikali ipunguze matumizi ikiwa pamoja na kutotumia magari yenye gharama kubwa na mh mbowe alirudisha gari la KUB lakini kutokana na unafiki wa wanasiasa wa kuto simamia yale wanayoongea alilifata kimiya kimiya na kuanza kulitumia. Pia tumeshuhudia mh lema akisahau na kuanza kutetea posho na kuanza kumshambulia zito. Embu tujiulize hivi hawa akina yericko, ben, nasari hizi nguvu za kumzushia na kumkashfu zito wanatoa wapi? Na kwa nini hawachukuriwi hatua? Mbona wale wanaomsema mbowe huchukuliwa hatua na kuitwa wasaliti! Ukitazama kwa makini utagundua unafiki wa wanasiasa kwa kuchochea migogoro kwa maslai yao binafsi na kuwazuia na kuwakwamisha wale wanaotaka madiliko ya kweli katika nchi yetu.
Jiungeni na CHAMA CHA KIGOMA CHAUMMA mnalia lia nini? ZITTO na Kafulila walishaanzisha CHAMA na kumpa Mkigoma Mwenzao si mjiunge?!! Ili muone kuwa kwa unafiki wenu kinaishia KIGOMA?
 
Slaa kapigwa marufu kwenda Kigoma. Akifanya mchezo kina Afande Sele watampiga marufuku kwenda Morogoro.

Slaa kwa sasa bora awe mpole tu na kumuomba radhi Zitto kwa fitina alizomfanyia...
Jiungeni na CHAMA CHA KIGOMA CHAUMMA mnalia lia nini? ZITTO na Kafulila walishaanzisha CHAMA na kumpa Mkigoma Mwenzao si mjiunge?!! Ili muone kuwa kwa unafiki wenu kinaishia KIGOMA?
 
Back
Top Bottom