Mabadiliko ya Katiba ya nchi si takwa la watawala, hulazimishwa na wananchi

Fundi Madirisha

Senior Member
Jun 30, 2020
184
987
Kuna mtu anaweza kuja na nadharia zake dhaifu kupinga lakini huu ndio ukweli. Hakuna mtawala aliyewahi kukubali kukaa chini na kupendekeza mabaliko ya katiba bila msukumo kutoka kwa wananchi kupitia matukio magumu yatakayomlazimu kukaa kupatanishwa na mahasimu wake.

Alipata kuyasoma haya Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Prof Kitila Mkumbo akiwa mwenyekiti wa UDASA enzi hizo. Naomba ujumbe huu uwafikie wanaharakati,wanasiasa, wafia nchi yao na wananchi wazalendo. Ni ukweli ulio wazi kua katiba iliyopo ni mbovu na haikidhi kabisa mahitaji ya dunia na mazingira ya sasa.

Tusidai katiba mpya tukifikiria kua serikali itatoa kama zawadi, alitaka kujaribu Zawadi hiyo JK lakini yakamshinda kwa kupelekeshwa na chama chake. Hakuangalia maslahi ya taifa bali ni maslahi ya chama chake, alitanguliza ubinafsi ambao ndio matokeo yake vilio hivi sasa.
Tukubali kama kweli tunawaza Tanzania mpya ijayo kwa faida ya vizazi vyetu, basi tusiogope maumivu yatakayotokana na madai haya.


Msikilize Prof Kitila Mkumbo hapa;👇👇
 

Attachments

  • VID-20210922-WA0094.mp4
    1.6 MB
Lakini huyo huyo Kitila leo hii anakula matapishi yake ndoo kabisaa anasema Katiba ni nzuri na inakidhi mahitaji ya watu na dunia ya sasa.
 
Unafiki ndio chanzo kikubwa Cha matatizo katika nchi hii,watu wanaona matumbo yao ni bora kuliko ustawi wa taifa,

angalia kwa mfano mienendo ya aliyekuwa naibu mwenyekiti kwenye bunge maalumu la katiba alivyo sn*tch kuhusu suala ambalo alisimamia mwenyewe anavyo ruka Kama kima ametoka katika agenda muhimu za taifa Kama katiba mpya na kuwa rais mwanaharakati wa mambo ya jinsia kutaka sympathy ya kuchaguliwa(2025) kisa ni Mwanamke.

Nchi inapita kwenye kipindi kigumu Cha mfumuko wa bei wa vitu, ukosefu wa ajira,mfumo mbovu wa elimu,tozo za hovyo,uchumi mbovu nk yeye akili na fikra zake anawaza uchaguzi wa 2025.
JamiiForums-17373280~2.jpg
 
Back
Top Bottom