Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,876
- 2,744
Mabadiliko ya kweli yananukia, na kweli yapo. Mabadiliko ambayo yataubadilisha mfumo wa uongozi wa sasa na kuweka mfumo mpya kabisa. Ndipo ninapoona dhahiri kabisa kuwa kuna nguvu mbili muhimu zenye kuweza kufanya hayo. Moja ni M4C na la pili ni uislam.
M4C imekuwa na nguvu ambayo kwa sasa haielezeki. Pale watawala wanapodhani kuwa hii nguvu itayumba ndipo nguvu zake zinapoongezeka. Tangu uchaguzi mkuu uliopita hii nguvu imekuwa kazini hadi wakati huu tukiwa tunaelekea uchaguzi mwingine. Ni harakati ambazo zinawafungua watanzania wengi akili na ufahamu wa hali halisi; kwamba chama kilichopo madarakani kwa sasa kina porojo tu, na kweli kina porojo, tena na vitisho juu. Watanzania awali walikuwa hawana mbadala wa mfumo lakini sasa ni wazi kuwa mbadala huo umepatikana na ni suala la muda na maamuzi tu ili kuung'oa mfumo uliopo na kuweka mwingine, chini ya chama kingine. Hilo liko wazi.
Jambo la pili ni uislam. Waislam popote duniani wamekuwa ni chachu ya mabadiliko na vuguvugu la mifumo mipya ya kiutawala. Hili lipo wazi hasa tukitazama harakati za Arab Spring. Wameweza kung'oa mifumo mingi kandamizi katika mataifa yao na hatimaye wakawa na punje za ahueni.
Tunapowatazama waislam wa nchi hii, binafsi sioni tofauti na ninayoyaona huko kwingine. Tofauti kubwa ni kuwa hapa kwetu tuna imani mchanganyiko zaidi kuliko wenzetu.
Jana wakati napata hizi taarifa za waislam kuungana na kuandamana, tena bila umma wa watanzania kujua kabla kuwa haya yatatokea, nilijiwa na wazo kuwa hawa NDUGU zetu wanaweza kuwa ni chachu ya mabadiliko.
Sasa basi, ili kuona kuwa hili linawezekana, waislam wana madai yao ya msingi kabisa. Moja kuu ni Mahakama ya Qadhi. Hili halina athari yoyote katika secular state kama Tanzania. M4C ichukue hii ajenda na itoe ahadi kwa waislam kuwa mahakama ya kadhi ni halali yao pale cdm itakaposhika Dola. Kwa mwendo huu hizi nguvu mbili zikiungana mabadiliko yapo. Pia muungano huu utaondoa dhana ya udini iliyopandikizwa na mahasimu wa kisiasa wa M4C. Hakika hii itakuwa ni jambo jema sana kwani pia itapunguza msuguano wa kiimani katika Taifa hili Teule. Na wote tuseme 'Na iwe hivyo'.
M4C imekuwa na nguvu ambayo kwa sasa haielezeki. Pale watawala wanapodhani kuwa hii nguvu itayumba ndipo nguvu zake zinapoongezeka. Tangu uchaguzi mkuu uliopita hii nguvu imekuwa kazini hadi wakati huu tukiwa tunaelekea uchaguzi mwingine. Ni harakati ambazo zinawafungua watanzania wengi akili na ufahamu wa hali halisi; kwamba chama kilichopo madarakani kwa sasa kina porojo tu, na kweli kina porojo, tena na vitisho juu. Watanzania awali walikuwa hawana mbadala wa mfumo lakini sasa ni wazi kuwa mbadala huo umepatikana na ni suala la muda na maamuzi tu ili kuung'oa mfumo uliopo na kuweka mwingine, chini ya chama kingine. Hilo liko wazi.
Jambo la pili ni uislam. Waislam popote duniani wamekuwa ni chachu ya mabadiliko na vuguvugu la mifumo mipya ya kiutawala. Hili lipo wazi hasa tukitazama harakati za Arab Spring. Wameweza kung'oa mifumo mingi kandamizi katika mataifa yao na hatimaye wakawa na punje za ahueni.
Tunapowatazama waislam wa nchi hii, binafsi sioni tofauti na ninayoyaona huko kwingine. Tofauti kubwa ni kuwa hapa kwetu tuna imani mchanganyiko zaidi kuliko wenzetu.
Jana wakati napata hizi taarifa za waislam kuungana na kuandamana, tena bila umma wa watanzania kujua kabla kuwa haya yatatokea, nilijiwa na wazo kuwa hawa NDUGU zetu wanaweza kuwa ni chachu ya mabadiliko.
Sasa basi, ili kuona kuwa hili linawezekana, waislam wana madai yao ya msingi kabisa. Moja kuu ni Mahakama ya Qadhi. Hili halina athari yoyote katika secular state kama Tanzania. M4C ichukue hii ajenda na itoe ahadi kwa waislam kuwa mahakama ya kadhi ni halali yao pale cdm itakaposhika Dola. Kwa mwendo huu hizi nguvu mbili zikiungana mabadiliko yapo. Pia muungano huu utaondoa dhana ya udini iliyopandikizwa na mahasimu wa kisiasa wa M4C. Hakika hii itakuwa ni jambo jema sana kwani pia itapunguza msuguano wa kiimani katika Taifa hili Teule. Na wote tuseme 'Na iwe hivyo'.