Mabadiliko makubwa yaja mahakamani..........Tekinolojia mpya....

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Mahakama nchini yaingia enzi mpya
Monday, 06 December 2010 21:52



12_10_ubuj2w.jpg


Makamu wa Rais,Dk,Mohammed Gharib Bilal,(wa pili kushoto walioinama) na Jaji Mkuu,Augustino Ramadhani,(kushoto) wakiangalia Kompyuta wakati wa Uzinduzi wa Mfumo wa kurekodi mashauri Mahakamani kwa Kompyuta na Tovuti ya Mahakama Kuu Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani. (Picha na Yusuf Badi)

12_10_hj8m4g.jpg


THE Vice-President, Dr Mohammed Gharib Bilal (second right), gestures during the inauguration of the High Court website which will contain information on various court proceedings in Dar es Salaam on Monday. He is flanked by the Chief Justice, Mr Augustino Ramadhani (left), and the Secretary of ICT, Mr John Kahyoza (right). (Photo by Yusuf Badi)


James Magai
HATIMAYE Mhakama ya Tanzania imeanza rasmi safari ya matumizi ya teknolojia kuendesha shughuli zake, hususan uendeshaji kesi, baada ya kuzindua mfumo mpya wa kuweka kumbukumbu za mashauri mbalimbali mahakamani kwa kutumia kompyuta.

Mfumo huo ambao kwa kitaalamu huitwa mfumo wa ‘digitali’ ulizunduliwa jana na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal, katika ukumbi wa Mahakama Kuu Dar es Salaam, huku wadau wakielezea manufaa na changamoto mbalimbali zinazoambatana na mfumo huo mpya.
Pia, Mahakama imezindua tovuti yake ambamo taarifa kama vile sheria mbalimbali zinazotumika nchini, hukumu za kesi mbalimbali tangu mwaka 1979 na nyingine kuhusiana na kesi zinazoendelea mahakamani zitakuwa zinapatikana humo.
Kutokana na kuzinduliwa kwa mfumo huo, sasa Majaji wa Mahakama Kuu na wa Mahakama ya Rufani, hawatalazimika kuchukua kumbukumbu za mwenendo wa kesi mbalimbali kwa kuandika kwa mikono, badala yake, kazi hiyo itafanyika kwa kutumia kompyuta maalum.

Katika mfumo huo mwenendo wa kesi utakuwa unaingia kwenye kifaa maalumu cha kuhifadhia sauti kwenye kompyuta, kisha baada ya dakika tatu sauti hizo huanza kuchapwa na wataalumu na kuwekwa katika maandishi.
Kwa kuanzia mfumo huo utaanza kutumiwa na Majaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu Dar es Salaam, kabla ya kuziunganisha kanda nyingine 14 ikiwamo mahakama za chini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo huo, Dk Bilal alisema matumizi ya teknolojia hiyo kuweka kumbukumbu za mashauri mahakamani, sio tu kutasaidia kuharakisha usikilizaji wa kesi, lakini kutajenga mazingira mazuri kwa wawekezaji nchini.

Dk Bilal alisema ingawa ni matakwa ya haki na Katiba ya nchi kuwa kesi zinazofikishwa mahakamani zimalizike muda muafaka, lakini Mahakama zimekuwa zikilalamimiwa kwa kuchelewesha kumaliza kesi mbalimbali.
Alitaka mahakama kutumia sheria kwa ufanisi na kwamba, kasi katika kuhitimisha kesi humaanisha upatikanaji wa haki badala ya kuzua mashaka.

Badala ya kuahirisha kesi mara kwa mara, Dk Bilal alitaka mahakama kuhakikisha zinaendeshwa kwa kasi, kwa wakati ikiwamo kuhitimishwa kwa haki na usawa.
Alisema matarajio ni kwamba kampuni ambazo zina matatizo ya kisheria katika shughuli zake za biashara, lazima ziweze kutatuliwa haraka ili kuwezesha uzalishaji wa bidhaa na utoaji huduma.
Dk. Bilal alisisitiza kwamba haki za binadamu na Katiba yetu zimejenga mazingira ya haki na usawa katika usikilizaji mashauri na kwamba, Mahakama ndio yenye jukumu hilo.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi, Jaji Mkuu Augustino Ramadhani, alisema Mahakama imekuwa ikilalamikiwa kwa kuchelewa kumaliza mashauri kutokana na kutumia zaidi mfumo wa uchukuaji kumbukumbu unaotegemea kuandika kwa mkono.
Jaji Ramadhani alisema kuzinduliwa kwa mfumo huo mpya, kutawawezesha majaji kuepukana na mfumo huo wa kizamani jambo ambalo litawezesha kuharakisha usikilizaji mashauri.
Alisema faida kubwa ya mfumo huo ni kumwezesha Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi, kujua kila kinachofanywa na kila Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu.
 
It is a good move. Mungu saidia wachakachuaji wasitie mikono yao kwenye mfumo huu.
 
"Teknolojia" italeta mabadiliko pale tutakapoamua kutofautisha siasa na teknolojia - Idara nyingi za Serikali zina "state of art" teknolojia lakini watendaji wa juu ni "wanasiasa" kwa hiyo wataalam wa teknolojia wanakaa kusoma magazeti au kusafiri kwenda kwenye semina!
 
Ni habari inayoashiria kukaribia kuwa njema lakini haitoshi MPAKA KWANZA Wa-Tanzania tukapate kuwafahamu 'MAFISADI' waliojificha nyuma ya DOWANS kulikamua taifa kupitia TANESCO na kuacha taifa gizani na ajira kutokomea kabisa.

Hata hivyo, swali langu ni kwamba, je sasa kesi ndio zitaweza kuendeshwa mahakamani kwa MAJENERETA ya kichina wanazokaribia kuruhusiwa wahindi wachache kuziagiza kuingia nchini kama asante ya CCM kwao kukichangia fedha kwenye kwenda kununulia uchaguzi???


Hiyo mifumo ya Kompyuta hakika ni mzuri lakini wananchi tutaifadi tu mara BAADA YA KUANDIKA UPYA KATIBA na kuwabana vilivyo MAFISADI wafilisi nchi wanaofanya taifa letu umeme kuwa ni dili yao binafsi ya kutuibia hazina na kuuzima kila wanapotaka kusababisha UKOSEFU WA UMEME KWA MTINDO WA KUCHONGA TU (Artificial Electric Supply SCARCITY).
 
bila umeme wa uhakika,ofisi za kisasa ni bure tuu teknolojia itakua ya mahakama kuu tuu
 
Jamaa, ogopeni sana VIWAVI JESHI vinavyoitwa MAFISADI!!!

Taifa linalowalea watu kama hawa siku zote hubakia kudumaa kimaendelea kuliko hata yale mataifa ambayo siku zote wanakumbwa na misukosuko ya kivita. Sawa sawa na kiwavijeshi kinavyotafuna majani yote ambayo mti huhitaji kujitengenezea chakula chake, hivyo vivyo ndivyo wanavyofanya 'Viwavijeshi Mafisadi' kutafuna kila idara tegemezi la taifa na kurudisha maendeleo yetu nyuma licha ya kuwa na amani miaka yote.

Ama kweli wakati mwingine huwa najikuta nakubaliana kabisa na kauli ya Mhe Ndesamburo bungeni Dodoma kwamba 'MAFISADI' ambao sisi hapa Tanzania tunawalea wenyewe kwa kuwafichia madhambi yao, kwingineko huko ma-Ughaibuni huko watu hawa hupigwa risasi hadharani.

Technolojia hiyo ya kompyuta ni mzuri sana si kwa mahakama zetu tu bali na idara nyinginezo nyingi tu lakini KWANZA NI SHARTI VIWAVIJESHI UFISADI viondolewe kwa KATIBA MPYA, SHERIA MPYA, na TUME HURU YA UCHAGUZI MPYA nchini.
 
Back
Top Bottom