Mabadiliko Jeshi la Polisi: IGP Sirro ampeleka Kamanda Mambosasa Dodoma, Wambura amrithi kanda maalum Dar

Sisi tulitaka tu aondolewe kama DPP maana wote hawana staha, operation zake zitatusaidia nini?
Mkuu, operations ni pamoja na mazuio ya mikutano, maandamano na aina yoyote ya usimamiaji wa amani. Hizo order mara nyingi hushuka kutoka kwa mkuu wa operations (Chief of operations), japo kuna IGP ambaye ndiye ana maamuzi ya mwisho kwa jambo kufanyika au la.

Kumbuka yeye ndiye mkuu wa operations makao makuu ya polisi nchini, siyo mkoani. Kikubwa tu lazima atasoma muelekea wa uongozi uliopo na kwenda nao.
 
Baada ya mwendazake bavicha mmechukua jukumu lakusifu, mataga hatuna chetu tena
Police au JWTZ .na BAVICHA au MATAGA vina uhusiano gani? Hayo ni majeshi ya nchi. Kila mtanzania yuko entitled kwayo, yaani watanzania wote 60mil. Baadhi ya polisi wachache wanaojinasibu na CCM ni kuwa na elimu ndogo tu hivyo kutojua namna ya utendaji. Ukienda kwa upande wa JWTZ wanajitambua sana, hawana huo ujinga.
 
Mkuu, operations ni pamoja na mazuio ya mikutano, maandamano na aina yoyote ya usimamiaji wa amani. Hizo order mara nyingi hushuka kutoka kwa mkuu wa operations (Chief of operations), japo kuna IGP ambaye ndiye ana maamuzi ya mwisho kwa jambo kufanyika au la. Kumbuka yeye ndiye mkuu wa operations makao makuu ya polisi nchini, siyo mkoani. Kikubwa tu lazima atasoma muelekea wa uongozi uliopo na kwenda nao.
Akiendelea na upumbafu wake muda siyo mrefu atamfuata mwendazake
 
Mwenye ile picha ya Mambosasa akielezea jinsi alivyopatikana Mo Dewji naiomba tafadhali
 
Kapanda daraja. Maana katoka Mji maarufu kwenda makao makuu ya Tanzania nzima. Viongozi wote wa chama, wabunge na serikali ngazi ya juu wapo pale. Kuwalinda hao si kazi mchezo.

Du, Mambosasa ana Nyota kali. Akitoka hapo ni ukuu wa polisi TZ.
Kwani kaenda kuwa kamanda wa mkoa?
 
Nadhani unashindwa kuelewa. Dodoma RPC ni Muroto siyo huyo unayemuita Muliro. Huyu Mambosasa anakwenda Dodoma makao makuu ya polisi kuwa kamanda wa operation (Chief of Operation) siyo RPC.
Nimesema nimefananisha tu Majina yao tatizo liko wapi? Wewe huwa hukosei?
 
Safi sana Poti wangu mkubwa kutoka Mkoani Mara ( Musoma ) kwa Shavu hilo Kubwa. Hii nafasi ilikuwa inakusubiria Kitambo tu na najua huyu aliyetolewa alikuwa akikufitinisha sana na Wakubwa zako ili Yeye asitolewe hapo kwa Kulindwa Kwake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

Kiukweli sikuwahi kuona Jipya la Kiutendaji kwa Mambosasa zaidi tu ya Ubabe, Ukatili, Vitisho na Roho Mbaya yake aliyoambukizwa vyema na Rafiki yake Paul Makonda aliyekuwa Mkuu wa Mkoa mbovu kuwahi kutokea katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Nyololo = Mafinga = Daud Mwangosi
 
Tangu Dar ianze kuwa Kanda maalum hajatokea afande aliyeheshimika na kumudu kazi take Kama Kaka Tibaigana.

Kova alipenda zaidi kuuza sura.

Sirro ndiyo kiasi lakini

Mambosasa alikuwa ni kituko na atasahaulika mapema sana au akumbukwe kwa ubaya Kama Sabaya na Ile stori yake na MO.
 
SACP Lazaro Mambosasa ametakiwa kuhama kutoka kuwa Mkuu wa Polisi kanda Maalum Dar, na kwenda kuwa Mkuu wa Oparesheni UPEL Dodoma.
Polisi wengine waliohamishwa ni SACP Camilius Mongoso Wambura ambaye anatoka Dodoma na kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam.


ACP Daniel Shillah amehamishiwa Dar na atakuwa Mkuu wa Upelelezi. ACP Longinus Tibishibwamu atakuwa Kamanda Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mara.

SSP Optatus Maganga amehamisha kutoka kuwa OCD Makete kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Njombe. SP Vitus Marekani atakuwa OCD wilaya ya Makete.
Ulikuwa wapi mkuu! Hii taarifa ina siku kadhaa humu jukwaani.
 
Back
Top Bottom