Mabadiliko gani yanatakiwa ndani ya CHADEMA?

Kuna sababu kubwa cahadema waache ushabiki wauze sera,,
Kwa tathmini tu ya harakaharaka siku ikatokea richmond,, epa, escrow, melemet, stanibank, na vinginevyo vikakomeshwa na huo ndio utakua mwisho wa CDM

Bado naliona pengo la slaa na zito.

Tatizo lingine ni kwenye uwasilishaji wa maada husika,, wawakilishi hasa wabunge wamekua wakitumia njia mbaya ya uwasilishaji wa maada,, mfano lugha chafu,, na kujipandikizia jazba zisizo za msingi. Kwa hili kiukweli wanapaswa angalau waelimike wajifunze kwa mbowe, mnyika, enzi za slaa na zitto kabwe,.

2. Mbinu inayotumika hivi sasa,, yaani nadhani hapa wamefeli kwa kiwango cha juu. Yaani viongozi wanataka kumshambulia mtu kwa slaha nzito mno ambayo wanajua kabisa hua inapiga nyuma na mbele,, sasa wataalamu walokua wanajua kuitumia wameasi na kibaya zaidi wamewaachi wakijua atakaekuja kuitumia la zima atasimama nyuma atakapo piga mbele itamsambua na nyuma
Hapa na manisha nini?? Namanisha hii mbinu ya kuimba ufisadi watu washajua ni kweli na kibaya zaidi walokuwa wanawatuhumu leo tunawasafisha,, hapo wanawaaminisha watu kulekule kua kelele za mwenye njaa dawa yake ni supu,, huo ufisadi, wizi, uhujumu, uliofanywa na ccm, kuna watu tumekuja kuwakumbatia na bila sababu za msingi.
Hapo slaa sijui ilikuaje na zito kabwe.
Ushauri.
Mbinu mpyaa ya kukiendeleza chama itafutwe haraka iwezekanavyo

3. Tatizo lingine ni kwa viongozi kujihesabu wao ni bora kuliko wanachama.
Hapa inajidhihirisha hata katika mikutano ya ndani ya chama.
Wajue kabisa chama cha siasa ni bidhaa na mteja ni mwanainchi, unatakiwa kuwa mbunifu na hata kujishusha ili kufanikiwa katika uenezi wako, lakini sasa wao kwao ni tofauti, inaonekana walisharidhika na wafuasi walionao,, embu waige mfano wa slaa na zito basi ili kiende

4. Hawataki kwenda na wakati hua wanafuata matukio.
Hili kiukweli linajidhihirisha,, ikumbukwe kua pamoja na yoote watanzania wanademokrasia iliyokomaa ila tatizo lomebaki kwa viongozi, na ndio maana hua wanamsikiliza kila mgombea, ukizubaa unaweza sema wote ni wanachama wako kumbe wanakuja kukusikiliza jee unawafaa au lah.
Wakikuta huwafai kikweli hata wanachama walo wanakukimbia.
Sasa basi hapa wasiendeshe chama kwa kupata poonti za kiongozi wa sisiemu anapoteleza au kukosea wanapaswa wawe na hoja zenye mashiko na sio kukalia matukio.
Kwa mfano kwa kipindi hiki raisi aliyemo kaja kufuta yoote tuloyokua tunasubiri tunayafanyie kazi, mfano kupambana na ufisadi rushwa na aina yoote ya uchafu kazi ambayo wakina slaa, mbowe, mnyika na zitto pamoja na lisu ndiyo iliyowafanya wakomae na watanzania tukawaelewa,
Kwa sasa hivi tunafanya kinyume kabisaa kwani ikumbukwe kwa mtanzania mwenye uelewa mdogo ukitumia mbinu ngumu utamchanganya. Mfano rahisi ni pale ambapo Rais dr. JPM ameamua kuweka sheria kando sasa nikutumbua tuuu na kutoa matamko, kwa wanaoelewa ambao ni wachache mno ni kweli anakosea,, lakini kwa yule mwenzangu na mimi aliyezoea mwizi akishikwa anapigwa kwanza ndio anaenda polisi, hapo mnakua mmemchanganya inaonekana mnatetea wizi. Sasa muwe wabunifu mzichambue mbinu vizuri.

5. CDM wajue nini maana ya upinzani kwa zama hizi
Hapo sitaki kuongea sana kwani wamesha jidhihirisha kwa hilo,, kuna haja yakutumia mbinu za kuikosoa serikali na zingine za kuinga mkono angalau pale ushauri wao unapotekelezwa na kuzaa matunda,, hapo wanainchi watajua hili cfm iliishauri serikali na wametekeleza na manufaa yamepatikana.
Cha zaidi sasa hivi naona wanaingia bungeni kunukuu vifungu vya sheria tuu hata pasipohitajika. Eoote wanataka kua wanasheria na si watetezi wa wanainchi wao


Najua mkija mtasema nimechanganyikiwa lah hasha, mi nimemba wa cdm toka enzi za akina slaaa na leo nimeyaongea haya nikiwa kwenye kahawa na wazee wanaoipenda chadema
Msipuuzie huku vijijini hayo ndoo yaliyopo msiiangaloe chadema kanda ya kaskazini hata huku tupo tuliojitolea kuifuta chadema
 
Back
Top Bottom