Elections 2015 Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio!

Wanasiasa wa kitanzania hawana malengo maalumu ya kushinda uchanguzi.Wakenya walifanikiwa baada ya kungundua "KANU ILIANZA KUWA DHAIFU KWA KUONDOKEWA NA WANACHAMA WAKE MUHIMU".Hapa Tanzania ni ajabu sana....mnamtenga silaha kama Lowassa?. Kwanza mshukuru sana ccm kumkata huyu bwana...Lowassa kama angepitishwa na ccm hakika Upinzani/ukawa msinge muweza hata kidogo.Unganisheni nguvu muondoe ccm.Lengo kuu iwe ni kuondoa ccm bila kuangalia unadhifu wa askari.

Faida ya LOWASSA KUJA UKAWA NI KUBWA SANA.AU mnagombea vyeo?kwanza unganisheni nguvu mshinde.

Wito wangu kwa DR.SLAA TOKA ULIPO NA SEMA LOWASSA TOSHA....TWENDE MBELE.

mimi sijui dr slaa kapatwa na ugonjwa gani! Yaani tunamshangaa sana tena sana.

Mkuu ni ukweli usiopingika kwamba hakika lowassa angepitishwa na chama cha mapinduzi, upinzani ungefutika kabisa kwenye ramani ya siasa za Tanzania,

mimi na mfahamu sana Ndugu lowassa na jinsi anavyokubalika na wananchi, nitofauti na uzushi uliokua unasambazwa kwamba alikua akiwa honga watu waje kwenye mikutano yake ya kutafuta wadhamini alipokua ccm,

ukweli ni kwamba watu walikua wanakuja kwa ajili ya mapenzi yao kwake,

na kosa kubwa walilolifanya chama cha mapinduzi ni umbea na majungu ndio yaliopelekea kuondolewa kwa lowassa kwenye uteuzi wa chama.

Huyu Bwana kuja chadema ni turufu nzuri sana kuelekea kushinda uchaguzi uhu, maana sisi tunao kaa na jamii kubwa ya watu hawafichi upendo wao kwa ndugu lowassa na wanahapa kumpa kurazao,

sasa ndio maana tunaanza kupata mashaka pengine dkt slaa ameamua kutumiwa na chama cha mapinduzi. Ili kutuvunja moyo viongozi na wapenda mabadiliko.

Ushauri wangu kwa viongozi wa chadema na (UKAWA)
msife Moyo kama dkt slaa hataki amezira. Mwacheni ninyi songambele tena kwa kasi kubwa na hari kubwa kabisa kwani dalili za ushindi zipo wazi kwa lowassa,

nawatakia kila na kheri viongozi wangu,
 
Uloi nga mâché68;13480334 said:
UHAROOO! Unafikiri kwa ma.... Tangu lini machinga wakapiga kura! Jidanganyeni tu. CCM haiwezi kung'olewa na mtu mmoja mwenye kupania kwenda IKULU kwa gharama yoyote

CCM itatolewa tu na sababu ni kwamba huyo mtu mmoja anayetaka kuingia IKULU 1.aliweza kumuingiza Rais aliyepo madarakani ikulu
2.ana wafuasi wengi nje na ndani ya chama alichotoka
3.kajiunga na umoja ambao ndiyo haswa tumaini la sisi wanyonge amabao ndiyo haswa tupo wengi katoka nchi hii
4..CHAKACHUENI MUONE..
 
Mimi napata shida sana sasa hiv kila mtu anaongea juu ya mabadiliko hasa kn isse za kisiasa. naomba nisaidieni tunaposema mabadiliko ni kubadisha chama tawala au kubadilisha nini? au neno MABADILIKO linatumika vibaya?
 
Kwa muktadha wa wakati wa sasa watanzania wanavozungumzia mabadiliko wanamaanisha kuondoa chama tawala kilichoshindwa kuwaondolea changamoto zao kwa miaka 50 nakueka chama kingine madarakani ili kutengeneza mfumo wa siasa za ushindani zitakazoondoa ulevi wa madaraka kwa vyama vya siasa ambavyo vinajiamninisha kwamba vitaonhoza milele
 
11822347_1473512346297011_906599183081388649_n.jpg

Wanabodi,
Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imekuwa ikipokea, na kulinganisha ruzuku hiyo imefanyia nini, utakubaliana na mimi, kuwa fedha hiyo, ingetosha kabisa kujenga jengo jingine kwenye eneo la kutosha. Hali hii imetokana na upangaji mbovu wa vipaumbele vyake, hali iliyopelekea matumizi mabovu ya ruzuku, kama yalivyofafanuliwa kwenye ripoti ya CAG.

Pasco

Source ya Taarifa hii ni observation yangu binafsi.

NB. Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, hajawahi kujiunga na chama chochote cha siasa, sio mfuasi, mshabiki wala mkereketwa wa chama chochote au mwanasiasa yoyote, ila kuna baadhi ya wanasiasa ambao ninawakubali sana akiwemo Edward Lowassa. Ila sijawahi kuwa team Lowassa wala kuhudhuria tukio lolote lililomhusu Lowassa, wala sina mpango wowote, wa kumfuata yoyote, popote, kazi yangu ni to tell nothing but the truth, with objectivity, impartiality and balance from all sides!.
Nafanya mapitio tuu.
P.
 
Pasco,
Kama huelewi kitu ni bora kuuliza, we ni mwandishi mkongwe, FYI makao makuu ya CHADEMA si nyumba za kupaga, hizo ni mali za CHAMA toka 2012.

Na pia hakuna mpango wa kuhama, lengo ni kuitoa CCM madaraka si kuwa na HQ ya kifahari
Makuu Ntobi kuna hii hoja
View attachment 463874

Mmiliki wa nyumba inayotumika kama ofisi ya CHADEMA Makao Makuu iliyoko mtaa wa Ufipa Kinondoni Manyanya ametoa notisi ya siku 14, kwa chama hicho kuhama katika nyumba yake kutokana na kukiukwa kwa mkataba wa malipo na upangishwaji.

Hatua hiyo inakuja baada ya mmiliki huyo kujaribu mara kadhaa kutuma barua kwenda kwa uongozi wa juu wa chama hicho bila ya mafanikio kwa kujibiwa kua chama hakina hela.

Chama hiko kimepewa hadi tarehe 9 kiwe kimeachia ofisi hiyo ili apewe mpangishaji mwingine.
Naomba urejee utueleze ukweli.

Au mwenye nyumba aliuza sasa kasahau, au Chedema iliingizwa mjini kuuziwa na asiye mmiliki, au tulidanganywa tuu humu JF! .

Paskali
 
Baada ya Lowassa kusifiwa na rais Magufuli kuwa ni super man, nimemkumbuka naomba nimdurusu kidogo, niliwaji kusema nini humu kumhusu mtu huyu.

P.
 
Nafanya tuu a quick compare and contrast ujio wa Lowassa kujiunga Chadema na yale mafuriko ya watu wake, na kupima alileta nini na sasa ameondoka ameacha nini, na kulinganisha huu ujio wa Maalim Seif ACT, amekuja na nini, ili kuwaanda kisaikolojia Wana ACT original, wasishangilie sana na kujisahau, mgeni apokelewe kwa mikono miwili, na zawadi zake zipokelewe, ukiwemo ule mswala mzuri wenye nakshi nakshi, wa kuswalia, ila nawashauri ile mbachao yao wanayoiswalia siku zote wasiitupe jumla kwa kanuni ya "usiache mbachao kwa mswala upitao" siku mgeni akiondoka, atabeba na mswala wake, hivyo kulazimika, kuirudia mbachao yao.
Na hata kwa kulinganisha utamu wa embe dodo na dafu, kiukweli embe ni tamu zaidi, lakini ni muhimu "usidharau dafu, embe tunda la msimu".

P
 
Pasco,
Kama huelewi kitu ni bora kuuliza, we ni mwandishi mkongwe, FYI makao makuu ya CHADEMA si nyumba za kupaga, hizo ni mali za CHAMA toka 2012.

Na pia hakuna mpango wa kuhama, lengo ni kuitoa CCM madaraka si kuwa na HQ ya kifahari
Habari wakuu,
Leo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Amesema Makao Makuu ya CHADEMA Wamepanga na hawalipi Kodi hivyo, Mwenye nyumba kila siku anashinda Ofisini kwake kuomba amsaidie kudai deni la Nyumba. Alimwambia nikiwadai wataingiza mambo ya Siasa.
View attachment 1297449
Mkuu Emanuel Ntobi, ukweli ni upi?.
Kiukweli hii ni aibu!.
P
 
P. akiona Uzi huu anaingia chumbani analiaaaa akimaliza anafuta machozi na kuja JF kushusha nondo za "kwa naslahi ya taifa".
Kwa nini analia? Anakumbuka wakati huo alikuwa na ndoto ya kuwa mkurugenzi wa Gerson wa magogoni
 
Mkuu Emanuel Ntobi, ukweli ni upi?.
Kiukweli hii ni aibu!.
P
Mkuu majengo mawili yamechukuliwa eneo moja.... Moja liliuzwa toka hiyo 2012 hilo jingine halikuuzwa sababu mmiliki aligoma kuuza. Sasa usichanganye issue ya jengo B na Jengo kuu yaani A ukaconclude kuwa yamepangishwa

NB: Wewe kama muandishi ''credible'' unapaswa uwe unatafiti kabisa kwa kufika ufipa na kurudi na majibu sio na wewe unakuja na propaganda kuuliza humu wakati ww ndio unapaswa kuhabarisha umma sio kuja kuuliza tena.

Ni lini Tanzania tutakuwa na waandishi serious kama wa KTN na NTV??
 
Nafanya tuu a quick compare and contrast ujio wa Lowassa kujiunga Chadema na yale mafuriko ya watu wake, na kupima alileta nini na sasa ameondoka ameacha nini, na kulinganisha huu ujio wa Maalim Seif ACT, amekuja na nini, ili kuwaanda kisaikolojia Wana ACT original, wasishangilie sana na kujisahau, mgeni apokelewe kwa mikono miwili, na zawadi zake zipokelewe, ukiwemo ule mswala mzuri wenye nakshi nakshi, wa kuswalia, ila nawashauri ile mbachao yao wanayoiswalia siku zote wasiitupe jumla kwa kanuni ya "usiache mbachao kwa mswala upitao" siku mgeni akiondoka, atabeba na mswala wake, hivyo kulazimika, kuirudia mbachao yao.
Na hata kwa kulinganisha utamu wa embe dodo na dafu, kiukweli embe ni tamu zaidi, lakini ni muhimu "usidharau dafu, embe tunda la msimu".

P
Chaguzi za Tz bado sio kipimo halisi cha nguvu ya Lowassa na Seif kwa obvious reasons. Ila kwa kilichotangazwa na NEC ilikua faida kwa CHADEMA maana iliweza ongeza kura maeneo mengi maana kiukweli Magufuli was a strong candidate na bila Lowassa wangeweza pata shida sana kueleweka.

Kuhusu ACT irrespective Maalim atafanyeje post 2020.... Ila ACT itafaidika itapata wabunge 25+ kutoka zenji na kura za Urais pia watazoa zoa kutoka huko hivyo wataweza unda KUB na hapo ongezea viti maalim na ruzuku kupaa. So watafaidika

ACT and CHADEMA had nothing to lose...
So walifaidika na watafaidika kuja kwa Lowassa na Maalim.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom