Elections 2015 Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio!

UHAROOO! Unafikiri kwa ma.... Tangu lini machinga wakapiga kura! Jidanganyeni tu. CCM haiwezi kung'olewa na mtu mmoja mwenye kupania kwenda IKULU kwa gharama yoyote
 
Mwalimu amkatae asimkatae kumbuka kuwa lengo ni kuing'oa ccm, jambo linalowatoa kijasho chembamba, pia usisahau Mwalimu alisema upinzani wa kweli utatoka ndani ya ccm, Kwa hiyo usikariri mistari, isome halafu changanya Na zako, ukizingatia wakati

Lukansola
Tutafutieni Dr Slaa popote alipo tafadhali habari imebadilika huyo mtu wenu kaleta balaa uliona wapi Mwenyekiti anafanya kazi za Katibu kuna nini?
 
Chadema kilikuwa chama cha Ukombozi mpaka alipoingia Lowasa sasa kimekuwa Chama cha Matumaini! Kwa chama cha matumaini, ni vizuri wahamie kwenye magorofa marefu kule Samora ndo kwao. Wawaachie wakombozi ufipa yao!

Mkuu utaimba sana ngonjera na mashahiri ila ukweli utabakia palepale
 
Kwani ruzuku zilikuwa zinatolewa kujenga majengo au kujenga chama?
Itakuwa na maana gani kuwa na jengo la kisasa ilihali chama kikiwa kipo jijini Dar Es Salaam tu waliopo wakina Pasco wanaoenda kunusa habar?

Mkuu watu wa ccm ni kawaida yao
 
Pascal, unashangaza sana. Kipaumbele hakiwezi kuwekwa kwenye majengo na hali mtandao wa wanachama ni mdogo. Vyama vya kisiasa ni kwanza wanachama na watu wengine wanaokiunga mkono. Hata ccm hapo lumumba ni pafinyu. Chama kisichojua vipaumbele ni wazi kitalipoteza taifa endapo kitaingia au kibakia madarakani. Tafakari.
 
Sawa, ruzuku ingetosha kujenga makao makuu, lakini je hizo shughuli nyingine zinazokufanya kila kukicha uijadili chadema zingefanyikaje?
 
Wanasiasa wa kitanzania hawana malengo maalumu ya kushinda uchanguzi.Wakenya walifanikiwa baada ya kungundua "KANU ILIANZA KUWA DHAIFU KWA KUONDOKEWA NA WANACHAMA WAKE MUHIMU".Hapa Tanzania ni ajabu sana....mnamtenga silaha kama Lowassa?. Kwanza mshukuru sana ccm kumkata huyu bwana...Lowassa kama angepitishwa na ccm hakika Upinzani/ukawa msinge muweza hata kidogo.Unganisheni nguvu muondoe ccm.Lengo kuu iwe ni kuondoa ccm bila kuangalia unadhifu wa askari.

Faida ya LOWASSA KUJA UKAWA NI KUBWA SANA.AU mnagombea vyeo?kwanza unganisheni nguvu mshinde.

Wito wangu kwa DR.SLAA TOKA ULIPO NA SEMA LOWASSA TOSHA....TWENDE MBELE.
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom