Maaskofu chonde; hubirini habari njema za ufalme wa Mungu na sio ufalme wa dunia hii

Maaskofu, Yesu alihubiri habari za ufalme usio onekana, ufalme wa milele. Yesu hakuhubiri habari za ufalme wa dunia hii unao onekana kwa macho.

Kama mkifanya hivyo mnaifanya injili ionekane kama ni nyepesi sana.

Acheni kuhubiri injili za siasa, hizo injili za siasa acheni kuzihubiri.

Hubirini juu ya ufalme wa Mungu. Ndani ya ufalme wa Mungu kuna kila kitu, vyote vilivyomo duniani vimo ndani ya ufalme wa Mungu.

Chochonde achaneni na mambo ya ufalme unaonekana. Hubiri habari za Yesu kurudi mara ya pili. Wahubirie watanzania waache uzinzi, waache kuchepuka, wahubirie wachawi waache uchawi, wahubirie walevi waache ulevi mara moja, wahubirie waongo waache uongo, wahubirie wezi waache uwizi, wahubirie Watanzania waokoke, wapongeze walio amua kuokoka na kumrudia Yesu Kristo, wapongeze wanyenyekevu, wahubirie watu waokoke.

Wahubirie walogaji waache kuloga, wahubirie wauaji waache kuua, wahubirie waasherati waache maramoja. Wahubirie wanaotembea na wake za watu watubu, wahubirieni wanaokwenda kwa waganga waache, wahubirieni wanaologa ndugu zao ili wapate mali waache, wahubirie wanaologa wenzao makazini waache, wahubirieni habari hizo, wahubirie wanaoiba fedha za serikali na kula rushwa waache,
Wahubirie waingie kwenye ufalme wa Mungu.

Achana na mambo ya siasa Hubiri injili ya kweli. Hubiri injili ndani ya injili kuna kila kitu amani, haki, na vitu vyote vilivyomo duniani.

Ndani ya ufalme wa Mungu kuna amani, upendo, kuna huruma, kuna haki, kuna kila kitu, kuna utajiri. Tukiwa na viongozi waliokoka nchi itakua na amani, itakua tajiri, itakua na huruma, tutaoneana huruma, viongozi wetu wakiwa ni watu waliokoka hawata kula rushwa, hawatafanya ufisadi, hawatarogana ili wang'ang'anie vyeo, viongozi watakuwa waaminifu na upendo na umoja vitajengwa ndani ya taifa, rasilimali zetu zitatumika kwaajili ya kujenga taifa bora lenye watu bora.

Nashangaa sanaa maasikofu mkisimama majukwaani na kuanza kuhubiri habari za siasa. Inasikitisha sana mnasahau kazi mnazotakiwa kufanya.
Wewe dogo, huwezi kutenganisha Imani na Siasa!
Maaskofu, Mapdre na Wachungaji wanahubiria waumini wao wanaoishi katika dunia hii hii iliyotamalaki siasa.
Waumini hawaishi katika sayari ya Pluto!
Hata Mtume Yohana (the Revelator) alifungwa na Wanasiasa kunako gereza la Patmos, unajua kwanini?
 
Maaskofu, Yesu alihubiri habari za ufalme usio onekana, ufalme wa milele. Yesu hakuhubiri habari za ufalme wa dunia hii unao onekana kwa macho.

Kama mkifanya hivyo mnaifanya injili ionekane kama ni nyepesi sana.

Acheni kuhubiri injili za siasa, hizo injili za siasa acheni kuzihubiri.

Hubirini juu ya ufalme wa Mungu. Ndani ya ufalme wa Mungu kuna kila kitu, vyote vilivyomo duniani vimo ndani ya ufalme wa Mungu.

Chochonde achaneni na mambo ya ufalme unaonekana. Hubiri habari za Yesu kurudi mara ya pili. Wahubirie watanzania waache uzinzi, waache kuchepuka, wahubirie wachawi waache uchawi, wahubirie walevi waache ulevi mara moja, wahubirie waongo waache uongo, wahubirie wezi waache uwizi, wahubirie Watanzania waokoke, wapongeze walio amua kuokoka na kumrudia Yesu Kristo, wapongeze wanyenyekevu, wahubirie watu waokoke.

Wahubirie walogaji waache kuloga, wahubirie wauaji waache kuua, wahubirie waasherati waache maramoja. Wahubirie wanaotembea na wake za watu watubu, wahubirieni wanaokwenda kwa waganga waache, wahubirieni wanaologa ndugu zao ili wapate mali waache, wahubirie wanaologa wenzao makazini waache, wahubirieni habari hizo, wahubirie wanaoiba fedha za serikali na kula rushwa waache,
Wahubirie waingie kwenye ufalme wa Mungu.

Achana na mambo ya siasa Hubiri injili ya kweli. Hubiri injili ndani ya injili kuna kila kitu amani, haki, na vitu vyote vilivyomo duniani.

Ndani ya ufalme wa Mungu kuna amani, upendo, kuna huruma, kuna haki, kuna kila kitu, kuna utajiri. Tukiwa na viongozi waliokoka nchi itakua na amani, itakua tajiri, itakua na huruma, tutaoneana huruma, viongozi wetu wakiwa ni watu waliokoka hawata kula rushwa, hawatafanya ufisadi, hawatarogana ili wang'ang'anie vyeo, viongozi watakuwa waaminifu na upendo na umoja vitajengwa ndani ya taifa, rasilimali zetu zitatumika kwaajili ya kujenga taifa bora lenye watu bora.

Nashangaa sanaa maasikofu mkisimama majukwaani na kuanza kuhubiri habari za siasa. Inasikitisha sana mnasahau kazi mnazotakiwa kufanya.

Ufalme gan tena? Huo ufalme wa Mungu ni wakufikilika ila wa dunia tunauona na kuujua waache wahbir mambo ya duniani tunayoyaona kuliko hayo abstract hata hatuna uhakika nayo kama yapo
 
Back
Top Bottom