Maandiko haya mbona kama yana ukakasi na mashaka makubwa?

Habarini wana JF,

Tuanze,

(A) Ukisoma MWANZO 19:30—38 kuna ukakasi mkubwa na mashaka makubwa juu ya hiyo Aya. Acha niinukuu.

MWANZO 19:30—38
Mwanzo 19:30-38 ( Lutu akapanda kutoka Soari akakaa mlimani, na binti zake wawili pamoja naye, kwa sababu aliogopa kukaa katika Soari. Akakaa katika pango, yeye na binti zake wawili.
Yule mkubwa akamwambia mdogo, Baba yetu ni mzee, wala hakuna mtu mume katika nchi atuingilie kama ilivyo desturi ya dunia yote.

Haya, na tumnyweshe baba yetu mvinyo, tukalale naye, ili tumhifadhie baba yetu uzao.

Wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka huyo mkubwa akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

Ikawa siku ya pili, mkubwa akamwambia mdogo, Tazama, nimelala jana na baba yangu, tumnyweshe mvinyo tena usiku huu, ukaingie ukalale naye.

Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.
Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo.

Na yule mdogo naye akazaa mwana akamwita jina lake Benami; huyo ndiye baba wa Waamoni hata leo.)

Ukisoma hiyo aya kuna mashaka Makubwa ya Nabii Lutu kudhalilishwa kiasi hicho, inawezekanaje Nabii Lutu katembea na Binti zake ndani ya Biblia na kuwapa Mimba? Tena alinyeshwa mvinyo(POMBE) kwa siku mbili mfululizo na kuwatombaz binti zake na kuzaa nao. Hii nadhani ni laana na hiki kizazi ni cha laana. Sasa sijui Bible nzima itakuwa na Laana au itakuwaje!!!

Kuna watu humu walikuwa wanamkashifu Mtume Wetu kwa kumuoa Bi Aisha, tena alimuoa kwa Ndoa kabisa. Na miaka hiyo Bi Aisha alikuwa ameshabalehe tayari.

MASAWLI

(1) JE, NI SAHIHI NABII LUTU KUTEMBEA NA BINTI ZAKE?

(2) HUYU NABII LUTU(NDUGU YAKE NA NABII IBRAHIMU) HAMUONI KAMA AMEDHALILISHWA NDANI YA BIBLIA?

(3) KWANI SIKU YA KWANZA KATEMBEA NA MKUBWA NA HAKUSHTUKA NA KESHO YAKE SIKU YA PILI AKATEMBEA NA MDOGO?

(4) MTUME MUHAMADI KUMUOA BI AISHA NA NABII LUTU KUTEMBEA NA BINTI ZAKE NANIVYUKO SAHIHI?

(5) SWALI LA NYONGEZA:
MTU AKIWA AMELEWA KIASI KWAMBA HAJITAMBUI, ANAWEZAJE KUSIMAMISHA MASHINE NA KUSHIRIKI TENDO?

(B) Pia ukisoma 1 WAKORINTHO 1:25 utakutana na ukakasi mkubwa wa MWENYEZI MUNGU kufananishwa na UPUMBAVU au tuseme MWENYEZI MUNGU ameitwa MPUMBAVU KABISAAAA ndani ya BIBLE. Acha niinukuu Aya.

1 WAKORINTHO 1:25
1 Wakorintho 1:25 (Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.)

Kwa upande wangu huo ni udhalilishaji Mkubwa wa Mungu ndani ya Biblia kwa kuambiwa Mpumbavu na pia kuambiwa ni Mdhaifu.

Chukulia uko Sebuleni na Baba yako Mzazi, alafu ghafla wakati mnaongea Mwambie hivi:-

“Unajua Baba wewe ni Mpumbavu ila upumbavu wako sio sawa na huyo jirani yetu Muuza duka hapo nje”

Alafu baada ya hapo msikilizie Baba yako atakavyokasirika, Sasa chukulia ndio anaambiwa Mungu katika hilo andiko hasira zake na gadhabu zitakuwa mara ngapi ya Baba yako na huo Moto wake siku ya Mwisho sijui itakuwaje.

MASWALI

(6) NI SAHIHI MUNGU KUFANANISHWA NA UPUMBAVU?

(7) JE KWELI MUGU NI MPUMBAVU NA NI DHAIFU?

Naombeni Majibu,
Nawasilisha.
Tafuta pesa hutapata muda wa kujadili mambo yasiyo na tija.
 
Back
Top Bottom