Maandamano ya mabucha ya Nguruwe 1993

Maswali
1. Je waliwatoa hao masheikh siku hiyo?

2. Sheikh Kassim ilikuaje akakosekana kwenye maandamano aliyoyanzisha akawa arusha akielekea Nairobi "kwenye matibabu"?


Mwaka wa 1993 ulikuwa mwaka mzuri sana kwangu kwani katika miezi 12 nilikuwa nimesafiri mara tatu tena ukichukulia kuwa mwaka wa 1991/92 nilikuwa Uingereza.

Nilikwenda Harare na ulikuwa mwezi wa Ramadhani.

Nilikaa Harare kwa majuma matatu na nikafika hadi Bulawayo.

Nikaenda Lusaka Zambia.

Niliporudi nikaenda Ufaransa nikawa Le Havre na Paris na safari ya kurudi nikapita London nikasali Eid Kubwa Regent Park Mosque hapo London kisha nikaenda Cardiff nikarudi Dar es Salaam.

Wakati huo Bunge liko Karimjee linaunguruma na sakata la Rais Mwinyi kuruhusu Zanzibar kuingia Organisation of Islamic Conference (OIC) na aliyehusika alikuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Ahmed Hassan Diria.

Barua za Kiuchungaji zinashambulia serikali ya Rais Mwinyi pamoja na magazeti yote hata yale ya Chama na Serikali.

Rais Mwinyi akajikuta hana wa kumtetea ila Sheikh Kassim bin Juma Imam Mkuu wa Msikiti wa Mtoro Mwinyi Mangara na ndani ya serikali akifarajiwa na Prof. Kighoma Ali Malima.

Hotuba za Ijumaa za Sheikh Kassim kwenye membar ya Mtoro zilitikisa nyoyo za Waislam na serikali nzima.

Siku ya Ijumaa msikiti unajaa hadi nje kufikia Mtaa wa Livingstone.

Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamu Waziri Mkuu alikuwa Augustine Mrema.

Kulikuwa na makaratasi ya "uchochezi," yakimwagwa misikiti yote ya Dar es Salaam yaliyokuwa yakiandikwa na "waandishi wasiojulikana," yakijibu Barua za Kiuchungaji.

Wachina wana msemo, "May you live in interesting times."

Hizi nyakati zilikuwa za kipekee kabisa hazikupata kutokea hata wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii safari yangu ya Ufaransa ilikuwa imenifanya nipitwe na mengi ya mjini.

Niliporudi nikaenda Zanzibar kushughulikia mambo fulani kuhusu OIC mimi na mwenzangu mmoja.

Tulipokuwa ndani ya chombo tunarejea ndiyo tukapata taarifa kuwa Waislam wamevunja mabucha ya nguruwe baada ya sala ya Ijumaa.

Rais Mwinyi kwa hofu akasema wale waliovunja mabucha ya nguruwe "nguvu za dola ziwaangukie."

Hiki ndicho kilichokuwa kinasubiriwa.

Usiku mmoja hadi kufika asubuhi masheikh na wahadhiri wa Kiislam wakakamatwa.

Waislam wakahamaki taarifa ikatoka kuwa wakutane Msikiti wa Mtoro kujadili kuwatoa masheikh walipokuwa wamewekwa rumande Central Police.

Katika kikao kile cha Mtoro siku ya Jumapili asubuhi msikiti ulijaa vijana hakuna sheikh hata mmoja aliyehudhuria.

Allah amenijaalia kuona kwa macho yangu matukio makubwa katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Mjadala ulikuwa mkali vijana ndani ya msikiti wakidai kuwa uamuzi wowote utakaofikiwa siku ile utoke kwenye Qur'an na Sunna hapatakiwi rai ya mtu binafsi.

Kikao hiki bila kuuma maneno kilikuwa kikao cha vita.

Sijapata kuona hamaki kwa Waislam kama niliyoshuhudia siku ile.

Ndipo Sheikh Waziri Ramadhani akasimama na kusema, "Ndugu zangu Allah leo ametuletea mtihani kutuangalia kama tunaweza kusimama kuipigania dini yake.

Kama dhulma tumeshafanyiwa sana ifike mahali tuseme basi kwa kukamatwa viongozi wa Waislam ni dharau ya juu kabisa dhidi yetu.

Kila unachokiona duniani kinamtumikia Allah basi ndugu zangu tutokeni twendeni Central Police tukawatoe masheikh zetu."

Hapo ndipo yalipotokea maandamano ya kwanza ya Waislam na yalipofika Mnazi Mmoja katika hali ya jua kali ghafla wingu likatanda na mvua ikaanza kunyesha.

Maandamano yalipofika Clock Tower askari wa FFU walikuwa wanawasubiri waandamanaji hapo mapambano yakaanza.

Mabomu mengi yaliyopigwa pale moshi wake ulipeperushwa na ule upepo wa mvua.

Milango ya Central Police ambayo daima haifungwi ikafungwa kwa kuhofu ule umma ungeweza kuingia hadi ndani ya selo za polisi.

Waislam wengi walikamatwa na kufunguliwa mashtaka.

Nahitimisha kwa kusema kuwa wakati haya yanatendeka Sheikh Kassim alikuwa Arusha akielekea Nairobi kwenye matibabu.

Hii ilikuwa "turning point," katika maisha yake kwani yeye alikuwa karibu sana na serikali na iliwashangaza wengi kumuona ameigeukia.

Kama si yeye kufanya vile na kusimamia haki Sheikh Kassim Jums angepita dunia hii kama walivyopita masheikh wengi wengine kabla yake.

Ndugu zanguni msimuone ndugu yenu kakataa kuitambua haki na akawa upande wa dhulma mkamkatia tamaa.

Muombeeni dua.

Kile kibri chake cha yeye kuwa upande wa wenye mamlaka na nguvu kisituvunje moyo.

Picha ambayo hainitoki kichwani mwangu ni picha ya Sheikh Kassim Juma mwaka wa 1979 anamkaribisha Nyerere ndani ya Msikiti wa Mtoro kwenye khitma ya aliyekuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.
 
Huyu Rashid Idd Athuman Njeja alikuja kuokoka na kuanza kuhubiri akiukosoa Uislamu namfahamu. Hakika ni zamani yenye mafunzo.


Mhenga mwenzangu umeeleza vizuri sana, naomba kuongezea kidogo sana ili nisiharibu uliyasema; Sheikh Kasim alikua member wa Balkuta na hata kile kikundi kilichokua kinasema Yesu sio mwana wa Mungu nadhani na chenyewe kilikua ni zao la hao hao Balkuta, kiliwahi kumsilimisha kijana mmoja wa Kiluteli ambaye wao walikua wanamwita "askofu Mwaipopo", huyo dogo aliishiwaga ada ya shule alikua akisoma siminari moja kule Tukuyu; anyway back to the topic; baada ya hilo tukio, vijana kadhaa waliongoza uvunjaji wa mabucha yale walikamatwa na kuwekwa lock up, kesi ikawa inaunguruma Kisutu, wakili wao alikua Musa Kwikima (nadhani kafariki mwaka hu mwezi April, habari zake zipo humu jukwaani ). Namkumbuka kijana mmoja (ki umri nadhani alikua ananizidi mimi so ni makosa kumwita kijana ) anaitwa Rashid Idd Athuman Njeja, vijana wa sheikh Kassimu aliyehitimu elimu nyingi za dini, huyu "dogo" ndiye aliyeongoza hasa uvunjaji ule wa yale mabucha. Kwasasa wengi wa hao watu ni RIP. Well, kilikua kipindi kigumu sana kwa Tanzania hasa jiji la Dar kama ulivyo sema.
 
Umeandika kwa ufupi kaka Mohamed.

Wito na hamasa ya kwenda "kuyafunga" mabucha ya nyama ya nguruwe Mbokomu pale Manzese yalitolewa na baadhi ya wahadhir baada ya mtoto wa kiislamu kutumwa nyama na mzazi wake na akajikuta anauziwa nyama ya nguruwe! Mzazi alipofatilia kutaka arudishiwe pesa akakataliwa na wauzaji na yeye akalipeleka public

Katika madai yao Waislamu walisema njia zote za kisheria walizotumia kuhakikisha kunakua na mipaka/kutengwa kati ya maduka ya kuuzia nyama za nguruwe na wanyama wengine kama ng'ombe na mbuzi, sio tu zilishindikana bali pia walikua wanaambulia kauli za kashfa na kebehi kutoka kwa watendaji wa Wilaya/Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Dar. Walikua wanadai sheria za kuzuia mabucha ya nguruwe kwenye maeneo ya mchanganyiko zipo lakini kwa makusudi na kwa kuwadharau Waislamu zilikua hazifuatwi

Baada ya sakata lile la kuvamia mabucha ya Mbokomu Pork Centre pale Manzese ili kuondoa "munkari" kwa mkono basi ndipo crackdown ya Masheikh ikafuata. Walisombwa waliohusika na wasio husika. Kama alivyosema mletaa uzi, miongoni mwao alikua Sheikh Kassim Bin Jumaa Bin Khamis, Imamu wa Msikiti wa Mtoro aliyekua safarini Arusha!

Kabda ya hapo kulikua na fukuto la hali ya kutoridhika kwa Waislamu kutokana na kuhisi walikua wanatendewa na serikali kama raia wa daraja la pili. Kuna vijana wanaharakati wa dini ya Kiislamu miongoni mwao ni marehemu Mtengwa Buruhani, marehemu Mdidi Musa, Mjeja na wengineo walikua "wamewaamsha" sana Waislamu na lile kundi lao la WARSHA ya waandishi wa Kiislamu katikati ya miaka ya 1980s kuelekea miaka ya mwanzo ya 1990s

Hii ilichukuliwa kama ni uamsho (renaissance) ya harakati za Waislamu na ni kwenye kipindi hiki (1992) Waislamu walipoamua kuichukua BAKWATA iwe mikononi mwao kwa mapinduzi ili iwe kwa faida yao kabda ya move hiyo kuzuiwa na Rais Mwinyi na baadae Augustine Mrema kuja kuendesha harambee ya pesa kutoka kwa viongozi wa kikristo ili kuiwezesha BAKWATA ifanye mkutano wake mkuu ambao walishindwa kuuitisha kwa muda mrefu kutoka na ukata pamoja na kua na rasilimali lukuki hapa nchini

Kuna watu humu wameandika kuhusu BALUKTA kwamba ilikua inamilikiwa na Sheik Kasim Bin Jumaa. Ukweli ni kwamba BALUKTA (Baraza la Kuendeleza Usomaji Kur an Tanzania) ilikua ni taasisi iliyoasisiwa na kuendeshwa na marehemu Sheikh Yahya Hussein. Taasisi hii ni miongoni mwa taasisi zilizokuja kupigwa marufuku na serikali(nadhani ilifutiwa usajili) katika kile kinachodhaniwa ni kuendelea kuipa BAKWATA nguvu ya kupumua baada ya Waislamu kuipuuzilia mbali

Kaka yangu Mohamed Said sina hadhi wala uwezo wa japo kukusogelea kwa tafiti na uandishi wako ila nime tabaruku katika kile kidoogo sana nikijuacho kutokana na kadhia ile ya mabucha ya nguruwe ambayo yalipelekea kufungwa jela kina Habibu Mazinge na wenzake japo kulikua na very strong "alibi" kwamba baadhi yao hawakuwepo kabisaaa Manzese wakati watu "wakiondoa munkari" kwa mkono

Thank you. This is a very balance narration in my opinion. Na inaleta hamasa kusoma.
Kama mtu anauziwa nyama ambayo sio aliyoagiza na anakataliwa kurudishiwa hela yake, that is a problem. Muuza bucha kutoka Mbokumu, Kule Moshi hakusoma alama za nyakati
 
Rashid Njeja anasema kuwa wao walimtuma mtoto makusudi akanunue nyama ya Nguruwe ili kutafuta chokochoko walimtuma then wakawa wanasubiria aje walianzishe. Wanasema lengo lilikuwa ni hilo kutafuta ugomvi na wasio waislamu. Na wakapata chanzo. Anayezungumza haya ni mwislamu mwenzi aliyeshiriki kadhia hiyo na baadaye akaacha uislamu.

Umeandika kwa ufupi kaka Mohamed.

Wito na hamasa ya kwenda "kuyafunga" mabucha ya nyama ya nguruwe Mbokomu pale Manzese yalitolewa na baadhi ya wahadhir baada ya mtoto wa kiislamu kutumwa nyama na mzazi wake na akajikuta anauziwa nyama ya nguruwe! Mzazi alipofatilia kutaka arudishiwe pesa akakataliwa na wauzaji na yeye akalipeleka public

Katika madai yao Waislamu walisema njia zote za kisheria walizotumia kuhakikisha kunakua na mipaka/kutengwa kati ya maduka ya kuuzia nyama za nguruwe na wanyama wengine kama ng'ombe na mbuzi, sio tu zilishindikana bali pia walikua wanaambulia kauli za kashfa na kebehi kutoka kwa watendaji wa Wilaya/Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Dar. Walikua wanadai sheria za kuzuia mabucha ya nguruwe kwenye maeneo ya mchanganyiko zipo lakini kwa makusudi na kwa kuwadharau Waislamu zilikua hazifuatwi

Baada ya sakata lile la kuvamia mabucha ya Mbokomu Pork Centre pale Manzese ili kuondoa "munkari" kwa mkono basi ndipo crackdown ya Masheikh ikafuata. Walisombwa waliohusika na wasio husika. Kama alivyosema mletaa uzi, miongoni mwao alikua Sheikh Kassim Bin Jumaa Bin Khamis, Imamu wa Msikiti wa Mtoro aliyekua safarini Arusha!

Kabda ya hapo kulikua na fukuto la hali ya kutoridhika kwa Waislamu kutokana na kuhisi walikua wanatendewa na serikali kama raia wa daraja la pili. Kuna vijana wanaharakati wa dini ya Kiislamu miongoni mwao ni marehemu Mtengwa Buruhani, marehemu Mdidi Musa, Mjeja na wengineo walikua "wamewaamsha" sana Waislamu na lile kundi lao la WARSHA ya waandishi wa Kiislamu katikati ya miaka ya 1980s kuelekea miaka ya mwanzo ya 1990s

Hii ilichukuliwa kama ni uamsho (renaissance) ya harakati za Waislamu na ni kwenye kipindi hiki (1992) Waislamu walipoamua kuichukua BAKWATA iwe mikononi mwao kwa mapinduzi ili iwe kwa faida yao kabda ya move hiyo kuzuiwa na Rais Mwinyi na baadae Augustine Mrema kuja kuendesha harambee ya pesa kutoka kwa viongozi wa kikristo ili kuiwezesha BAKWATA ifanye mkutano wake mkuu ambao walishindwa kuuitisha kwa muda mrefu kutoka na ukata pamoja na kua na rasilimali lukuki hapa nchini

Kuna watu humu wameandika kuhusu BALUKTA kwamba ilikua inamilikiwa na Sheik Kasim Bin Jumaa. Ukweli ni kwamba BALUKTA (Baraza la Kuendeleza Usomaji Kur an Tanzania) ilikua ni taasisi iliyoasisiwa na kuendeshwa na marehemu Sheikh Yahya Hussein. Taasisi hii ni miongoni mwa taasisi zilizokuja kupigwa marufuku na serikali(nadhani ilifutiwa usajili) katika kile kinachodhaniwa ni kuendelea kuipa BAKWATA nguvu ya kupumua baada ya Waislamu kuipuuzilia mbali

Kaka yangu Mohamed Said sina hadhi wala uwezo wa japo kukusogelea kwa tafiti na uandishi wako ila nime tabaruku katika kile kidoogo sana nikijuacho kutokana na kadhia ile ya mabucha ya nguruwe ambayo yalipelekea kufungwa jela kina Habibu Mazinge na wenzake japo kulikua na very strong "alibi" kwamba baadhi yao hawakuwepo kabisaaa Manzese wakati watu "wakiondoa munkari" kwa mkono
 
Rashid Njeja anasema kuwa wao walimtuma mtoto makusudi akanunue nyama ya Nguruwe ili kutafuta chokochoko walimtuma then wakawa wanasubiria aje walianzishe. Wanasema lengo lilikuwa ni hilo kutafuta ugomvi na wasio waislamu. Na wakapata chanzo. Anayezungumza haya ni mwislamu mwenzi aliyeshiriki kadhia hiyo na baadaye akaacha uislamu.
Chizi,
Umenipa taarifa ambazo sikuwa nazijua.
Ahsante sana.
 
Huyu Mzee ni lini ataacha kuandika maboko...

Ati Sheikh asishangawe kwa kutoisimamia haki? Yaani nae aunge mkono kuvunja Mabucha ya Watu wa Dini tofauti katika nchi inayosimamia haki kwa kila mtu na Serikali isiyo na dini afuate mihemka ya imani ya dini yake si ataumia na kisha umcheke tu.
 
...Ndipo Sheikh Waziri Ramadhani akasimama na kusema, "Ndugu zangu Allah leo ametuletea mtihani kutuangalia kama tunaweza kusimama kuipigania dini yake.
Kwa ufupi, uisilamu ni uwanaharakati, sidhani kama ni dini
 
Mwaka wa 1993 ulikuwa mwaka mzuri sana kwangu kwani katika miezi 12 nilikuwa nimesafiri mara tatu tena ukichukulia kuwa mwaka wa 1991/92 nilikuwa Uingereza.

Nilikwenda Harare na ulikuwa mwezi wa Ramadhani.

Nilikaa Harare kwa majuma matatu na nikafika hadi Bulawayo.

Nikaenda Lusaka Zambia.

Niliporudi nikaenda Ufaransa nikawa Le Havre na Paris na safari ya kurudi nikapita London nikasali Eid Kubwa Regent Park Mosque hapo London kisha nikaenda Cardiff nikarudi Dar es Salaam.

Wakati huo Bunge liko Karimjee linaunguruma na sakata la Rais Mwinyi kuruhusu Zanzibar kuingia Organisation of Islamic Conference (OIC) na aliyehusika alikuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Ahmed Hassan Diria.

Barua za Kiuchungaji zinashambulia serikali ya Rais Mwinyi pamoja na magazeti yote hata yale ya Chama na Serikali.

Rais Mwinyi akajikuta hana wa kumtetea ila Sheikh Kassim bin Juma Imam Mkuu wa Msikiti wa Mtoro Mwinyi Mangara na ndani ya serikali akifarajiwa na Prof. Kighoma Ali Malima.

Hotuba za Ijumaa za Sheikh Kassim kwenye membar ya Mtoro zilitikisa nyoyo za Waislam na serikali nzima.

Siku ya Ijumaa msikiti unajaa hadi nje kufikia Mtaa wa Livingstone.

Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamu Waziri Mkuu alikuwa Augustine Mrema.

Kulikuwa na makaratasi ya "uchochezi," yakimwagwa misikiti yote ya Dar es Salaam yaliyokuwa yakiandikwa na "waandishi wasiojulikana," yakijibu Barua za Kiuchungaji.

Wachina wana msemo, "May you live in interesting times."

Hizi nyakati zilikuwa za kipekee kabisa hazikupata kutokea hata wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii safari yangu ya Ufaransa ilikuwa imenifanya nipitwe na mengi ya mjini.

Niliporudi nikaenda Zanzibar kushughulikia mambo fulani kuhusu OIC mimi na mwenzangu mmoja.

Tulipokuwa ndani ya chombo tunarejea ndiyo tukapata taarifa kuwa Waislam wamevunja mabucha ya nguruwe baada ya sala ya Ijumaa.

Rais Mwinyi kwa hofu akasema wale waliovunja mabucha ya nguruwe "nguvu za dola ziwaangukie."

Hiki ndicho kilichokuwa kinasubiriwa.

Usiku mmoja hadi kufika asubuhi masheikh na wahadhiri wa Kiislam wakakamatwa.

Waislam wakahamaki taarifa ikatoka kuwa wakutane Msikiti wa Mtoro kujadili kuwatoa masheikh walipokuwa wamewekwa rumande Central Police.

Katika kikao kile cha Mtoro siku ya Jumapili asubuhi msikiti ulijaa vijana hakuna sheikh hata mmoja aliyehudhuria.

Allah amenijaalia kuona kwa macho yangu matukio makubwa katika historia ya Waislam wa Tanganyika.

Mjadala ulikuwa mkali vijana ndani ya msikiti wakidai kuwa uamuzi wowote utakaofikiwa siku ile utoke kwenye Qur'an na Sunna hapatakiwi rai ya mtu binafsi.

Kikao hiki bila kuuma maneno kilikuwa kikao cha vita.

Sijapata kuona hamaki kwa Waislam kama niliyoshuhudia siku ile.

Ndipo Sheikh Waziri Ramadhani akasimama na kusema, "Ndugu zangu Allah leo ametuletea mtihani kutuangalia kama tunaweza kusimama kuipigania dini yake.

Kama dhulma tumeshafanyiwa sana ifike mahali tuseme basi kwa kukamatwa viongozi wa Waislam ni dharau ya juu kabisa dhidi yetu.

Kila unachokiona duniani kinamtumikia Allah basi ndugu zangu tutokeni twendeni Central Police tukawatoe masheikh zetu."

Hapo ndipo yalipotokea maandamano ya kwanza ya Waislam na yalipofika Mnazi Mmoja katika hali ya jua kali ghafla wingu likatanda na mvua ikaanza kunyesha.

Maandamano yalipofika Clock Tower askari wa FFU walikuwa wanawasubiri waandamanaji hapo mapambano yakaanza.

Mabomu mengi yaliyopigwa pale moshi wake ulipeperushwa na ule upepo wa mvua.

Milango ya Central Police ambayo daima haifungwi ikafungwa kwa kuhofu ule umma ungeweza kuingia hadi ndani ya selo za polisi.

Waislam wengi walikamatwa na kufunguliwa mashtaka.

Nahitimisha kwa kusema kuwa wakati haya yanatendeka Sheikh Kassim alikuwa Arusha akielekea Nairobi kwenye matibabu.

Hii ilikuwa "turning point," katika maisha yake kwani yeye alikuwa karibu sana na serikali na iliwashangaza wengi kumuona ameigeukia.

Kama si yeye kufanya vile na kusimamia haki Sheikh Kassim Jums angepita dunia hii kama walivyopita masheikh wengi wengine kabla yake.

Ndugu zanguni msimuone ndugu yenu kakataa kuitambua haki na akawa upande wa dhulma mkamkatia tamaa.

Muombeeni dua.

Kile kibri chake cha yeye kuwa upande wa wenye mamlaka na nguvu kisituvunje moyo.

Picha ambayo hainitoki kichwani mwangu ni picha ya Sheikh Kassim Juma mwaka wa 1979 anamkaribisha Nyerere ndani ya Msikiti wa Mtoro kwenye khitma ya aliyekuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.

Umepita nchi zote nguruwe ulikuta TZ tu.kwa kuwa sio nchi yako
Hapa kichwa cha habari na story nimeshindwa kuelewa kwa hiyo sisi nguruwe huo mwaka
 
Thank you. This is a very balance narration in my opinion. Na inaleta hamasa kusoma.
Kama mtu anauziwa nyama ambayo sio aliyoagiza na anakataliwa kurudishiwa hela yake, that is a problem. Muuza bucha kutoka Mbokumu, Kule Moshi hakusoma alama za nyakati
sio balanced kama unavyodhani , huyu kasimulia ili kuwafanya waislam waonekane ni 'good guys' kwenye huo mgogoro, Waislam ni watu wanaotaka imani yao kuwa ndio iwe sheria ya kutolea maamuzi kwenye mambo yote ya kijamii, na kwenye hili nina uhakika hawawezi kuwa innocent kama huyu jamaa alivyosimulia japo kuna uwezekano wa Serikali kufanya makosa pia

tafuta msimulizi mwingine wa upande wa Serikali au wa wauzaji wa Bucha wasimulie na wao ndipo utajua hasa ni yupi mchokozi
 
Picha ambayo hainitoki kichwani mwangu ni picha ya Sheikh Kassim Juma mwaka wa 1979 anamkaribisha Nyerere ndani ya Msikiti wa Mtoro kwenye khitma ya aliyekuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.


MZEE HIYO HAPO JUU INAHUSIANA NINI NA KICHWA CHA HABARI?
 
Siri ya kukosa uvumilivu


View: https://m.youtube.com/watch?v=oiVFGmCKEAA
Dr. Robert Spencer mwanazuoni na mtafiti nguli wa religious studies aliyeandika kitabu - 'Ukweli Kuhusu Muhammad: Mwanzilishi wa Dini Isiyo Na Uvumilivu Zaidi Ulimwenguni', Spencer anajadili vyanzo vya mwanzo kabisa vya Kiislamu kuhusu maisha ya Muhammad nabii wa Uislamu, na anaonyesha jinsi ghasia, kutovumiliana, na ukandamizaji ambao umeashiria utamaduni wa Kiislamu si ukiukwaji. ya kanuni za Kiislamu, lakini zimekita mizizi katika mafundisho na mfano wa muasisi wa Uislamu.

Religious Studies ni nini : Masomo ya kidini, ambayo pia hujulikana kama utafiti wa dini, ni uwanja wa kitaaluma unaojitolea kufanya utafiti wa imani za kidini, tabia na taasisi. Inafafanua, inalinganisha, inafasiri, na inafafanua dini, ikisisitiza mitazamo ya utaratibu, yenye msingi wa kihistoria, na ya tamaduni mbalimbali.
1703513087892.png
 
Picha ambayo hainitoki kichwani mwangu ni picha ya Sheikh Kassim Juma mwaka wa 1979 anamkaribisha Nyerere ndani ya Msikiti wa Mtoro kwenye khitma ya aliyekuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.


MZEE HIYO HAPO JUU INAHUSIANA NINI NA KICHWA CHA HABARI?
Uzalendo,
Mufti Sheikh Hassan bin Ameir alimkaribisha Nyerere katika TAA akiwa mjumbe wa TAA Political Subcommittee tokea 1950.

Wajumbe wengine katika kamati hiyo walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Mshauri wa kamati hii alikuwa Earle Seaton.

Hii ndiyo kamati ndani ya TAA iliyoshughulika na siasa.

Nyerere katika kuivunja EAMWS akatoa amri Mufti Sheikh Hassan bin Ameir akamatwe na arudishwe kwao Zanzibar.

Hii ni sawa na Rais Mwinyi atoe amri Kadinali Pengo akamatwe na kurejeshwa kijijini kwao.

Uhusiano wa hayo maneno ni kule Nyerere kualikwa na masheikh wa BAKWATA kuhudhuria khitma ya Sheikh Hassan bin Ameir kiongozi wa Waislam aliyemfukuza nchini kwa kuwa alikuwa akiwaongoza Waislam kujenga Chuo Kikuu.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom