Maandamano ya CHADEMA Arusha: Mabomu yarindima, raia wauawa na viongozi wakamatwa

OMBI LANGU KWA WATAKAOKUWEPO KWENYE MAANDAMANO:

Kama utafika hapo na itakuwa vema viongozi wa CHADEMA wakaambiwa kabisa kuwa lazima ziwepo Camera, Video camera za kutosha kupiga picha kila tukio la ajabu. Pia watu waandae kabisa simu zao tayari kupiga picha.

Wasiwasi wangu mie ni kuwa isijetokea baadhi wa ya wapinzani wa Chadema, wakaanza kurusha mawe kwenye nyumba za watu au biashara zao au mali nk nk na hapo ije isemwe ni Chadema.

Pia kama itatokea FFU au POLISI au hata jeshi wanaanza kupiga watu, basi matukio yote yawe yamerekodiwa kwa wingi na hapo miaka ya mbeleni yaje yatumike kuwapandisha hawa akina Charles Taylor wa Tanzania.
Uko sahihi mkuu, vielelezo hivyo vitamsaidia sana Ocampo kama itabidi hapo baadae maana naona viongozi wetu wanataka wafungiwe The Hague kwa kukiuka haki za binadamu na sio Ukonga kwa ufisadi mwaka 2015. Wamegundua jela za huko zina nafuu kuliko hizi wanazoziendesha wao sasa.
 
Mimi nakerwa na hii hali ya hapa Tz, kila siku tunaambiwa tutaandamana kupinga ongezeko la bei ya umeme. Cha kushangaza mpaka sasa hatujaambiwa maandamano yanaanzia wapi na tutaandamana mpaka wapi.

Kwa kuwa huu ni mpango wa nchi nzima basi tupewe modality...kila wilaya tunaandamana namna gani na tunapokelewa na nani baada ya hayo maandamano. Mimi mpaka sasa chaji na hasira iko juu....please anybody give me the modality....we can not tolerate this rubbish thing going on!!!!

Naamini mtaweka mawazo yenu kuhusu ni wapi tunaanzia..

Kwa Arusha leo ni Centrifugal Strategy Mzee ndio tunakanyaga nayo mbele kwa mbele bila shida!!
 
Kwa arusha maandamano yanaanzia soko la mbauda kwenda town.watu 2jitokeze kwa wingi jaman,atakuwepo dr slaa kama kiongoz pamoja na wabunge we2 wote 48,aluta kontnua,karbuni 2onyeshe dunia kuwa peoples powers inawezekana tanzania.umoja ni nguvu......mungu ibarki arusha mungu ibarki tanzania
 
CHAKAZA unalosema ni la kweli maana imezuka tabia. Vyama vya upinzani CUF,CDM nk. vikifanya maandamano huwa na watu wamepandikizwa na chama cha kupindua ili wafanye fujo afu ijeonekana kwamba wafuasi wa vyama hivi vya upinzani ndio wahusika wakuu! Mimi naunga kwa asilimia 100 hilo wazo la kuwa na KAMERA! hii itawakamata wengi!
 
NILISIKIA KAMA POLISI IMEPIGA MARUFUKU HAYO MAANDAMANO NA KUWA IMERUHUSU TU MKUTANO! wadau mna taarifa hii?
 
Ningekuwa Arusha, saa moja asbh ningekuwa barabarabi na familia yangu kuandamana mpaka ifike saa ya mkutano wa hadhara. Kila mwanafamilia ningemtengezea bango.
 
kwa wale memba wa jf waliopo Arusha tunaomba mtujulishe yanayojiri ndani ya jiji la Arusha kwa sasa tuweze kujua yanayoendelea. Je maandamano yamefanyika au kauli ya IGP Mwema imezingatiwa!
 
...tunakopelekwa na Polisi siko! nafikiri mwisho wa duluma hii haupo mbali. Kwa nini Polisi inakuwa hivi kwa wapinzani wa kweli wa CCM? RPC anakubali, IGP anakataa!!! Hapana, we must do something to end this!!!
 
habarini za asubuhi! PEOPLE POWER wa Arusha 2peni habari kinachoendelea hapo town mpango mzima wa maandamano
 
nmc watu wamesha anza kuingia na mh lema anaongoza zoezi la kuwafunga vitambaa vyeupe huku kila kona polisi wamejaa wakiwa tayari kuzuia maandamano kama yatafanyika
 
nmc watu wamesha anza kuingia na mh lema anaongoza zoezi la kuwafunga vitambaa vyeupe huku kila kona polisi wamejaa wakiwa tayari kuzuia maandamano kama yatafanyika

inamaana hawarusiwi kuandamana?
 
Katika kitu ambacho nimekishuhudia leo hapa Arusha asubuhi hii ni kua kwenye kila raia wawili kuna askari watatu pamoja na magari ya polisi yakiwa na askari waliovalia kivita kama vile tuko Afganistar! yoote haya ni kua Chadema wameruhusiwa kufanya mkutano lakini hakuna kuandamana kwaajili ya kwenda kuwapokea viongozi wao wakitaifa. Katika ujio huo wa viongozi hao yupo katibu mkuu Dr.Wilbrod Slaa/Tindu Lisu/Freema Mbowe na na viongozi wengine wa Chadema. Kweli mwaka huu wanachadema sijui itakuaje:A S 39:
 
Maandamano ni noma! maana vifaa vilivyopita hapa(uhuru road) kwa ajili ya kuzuia maadamano vinatisha!
 
Baada ya polisi kupiga maandamano ya Chadema na sasa hivi Chadema wanataka kuandamana kwa lazima hali sio nzuri ni vurugu kati ya Polisi na raia. Polisi ni wengi wengine wameazimwa kutoka CCP na wilaya za jirani. Ni kelele za ving'ora mji mzima.
 
Ni ujinga wa Anden'genye . Kama ni mapinduzi ya ukweli Arusha iko juu na hata wafanye nini hawawezi badilisha tena fikra za watu. Hao askari , magari n.k hayatazuia kufikisha ujumbe .
 
Back
Top Bottom