Maandamano ya Amani - 23/08/2008

LazyDog

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
2,473
189
shalom, are you around? Tarehe saba mwezi huu Shalom aliweka bandiko humu JF: Tuandamane mpaka ikulu


Kuna copy inatembea mtaani nimeona ni vyema kuiweka hapa.
Nimei-type, kwahiyo huenda kuna makosa ya uchapaji.




Maandamano ya Amani

Ndugu, Watanzania wote tunaoitakia maendeleo, amani na utulivu wa kudumu nchi yetu. Tunaombwa kushiriki maandamano ya amani yaliyopangwa kufanyika tarehe 23/08/2008 Saa 4:00 asubuhi yatakayo anzia viwanja vya mnazi mmoja na kumalizikia Ikulu, Mjini Dar es Salaam.

Madhumini ya maandamano haya ni:

  1. Kuiomba serikali itoe ripoti ya kamati ya EPA na kutangaza hadharani majina ya watuhumiwa waliobainika kuchota fedha za EPA.
  • Serikali ifuate sheria kanuni na taratibu tulizojiwekea katika kuwashughulikia watuhumiwa hao.


Ndugu Watanzania hii ni nafasi pekee ya kuonyesha jinsi unavyoipenda na kuithamini nchi yako lakini pia ni njia nzuri ya kuonyesha jinsi unavyo uchukia ufisadi badala ya kuongea tu ndani ya madaladala, vijuweni, ofisini, nk sasa tuunganishe nguvu pamoja na tutashinda.

Tumetoa muda ili kuviwezesha vyombo vya usalama kujipanga kuimarisha ulinzi sehemu zote tutakazo pita ili kufanikisha maandamano hayo.
Kabla ya kuanza kwa maandamano hayo kutakuwepo na sala, dua, maombi, toka dini na madhehebu tofauti.


Muhimu:
  • Maandamano hayo hayahusiani na vyama vya siasa na wanasiasa
  • Asiwepo mtu yeyote atakayebeba silaha ikiwa ni pamoja na fimbo
  • Kubeba vitambaa vyeupe ni muhimu
  • Kufanikiwa kwa maandamano haya ni mwanzo wa Tanzania mpya tunayoitarajia, timiza wajibu wako (njooni kwa wingi)
  • Kutoshiriki maandamano haya ni kuunga mkono ufisadi
  • Maandamano haya yatafanyika nchi nzima kwa awamu
  • Kuwa na uchungu na nchi yako kwa kuisaidia kamati ya kueneza taarifa hizi au toa kopi ya tangazo hili na uzisambaze

Kny Kamati ya kutetea maslahi ya taifa

<SAHIHI>

Rafael Mikaya Luvakubusa
Mtendaji Mkuu
Wasiliana na mtendaji mkuu TEL: 0783 679-079




Tafadhali, pamoja na kutoa maoni yako kuhusu bandiko hili, zingatia kuainisha maboresho ambayo ungependa yafanywe na waandaaji wengine next time.


Amani iwe nanyi!
Lazydog



.
 
count me in, come 30/08/08 nitakuwa mtaani na shuka langu kubwa jeupe, hatua nzuri sana ktk kuleta mabadiliko, kuhusu maboresho mimi sina ila kama kuna watu wengine waliokuwa na mawazo kama hayo ni heri kuunganisha nguvu ili kuleta msisitizo zaidi, nisingependa kuona watu wachache wakijitokeza, lakini nisingependa pia kuona watu wenye nia zenye vurugu katika maandamano hayo. Naomba Mungu atusaidie yawe ya amani nami nitahamasisha watu kujitokeza kwa wingi.
 
Hongera sana. Safi kabisa, nitakuwepo. Je matangazo yamewekwa sehemu zingine kwenye Redio, Tv, au magazeti, kuna mtu anafahamu? Nitajaribu kuomba msaada huo kwenye hivyo vituo pia. Mapambano yanashika moto sasa. Tuko pamoja.
 
Hongera sana. Safi kabisa, nitakuwepo. Je matangazo yamewekwa sehemu zingine kwenye Redio, Tv, au magazeti, kuna mtu anafahamu? Nitajaribu kuomba msaada huo kwenye hivyo vituo pia. Mapambano yanashika moto sasa. Tuko pamoja.


Sifahamu, na nimekuwa najiuliza hayo maswali pia.

Hapa JF tuna nafasi nzuri sana kupeana taarifa, kuhamasisha na zaidi sana kupima effectiveness ya jitihada zinazoanzishwa na wanaJAMII wenzetu, hata kuboresha kwa kushauriana na kujipanga vizuri.


Mbio ndo zimeanza hivyo, na tupokezane kijiti sasa!



.
 
count me in, come 30/08/08 nitakuwa mtaani na shuka langu kubwa jeupe, hatua nzuri sana ktk kuleta mabadiliko, kuhusu maboresho mimi sina ila kama kuna watu wengine waliokuwa na mawazo kama hayo ni heri kuunganisha nguvu ili kuleta msisitizo zaidi, nisingependa kuona watu wachache wakijitokeza, lakini nisingependa pia kuona watu wenye nia zenye vurugu katika maandamano hayo. Naomba Mungu atusaidie yawe ya amani nami nitahamasisha watu kujitokeza kwa wingi.



Tarehe 23, tofauti kidogo na iliyokuwa imependekezwa na Shalom.



.
 
Count me in
Nitakuwepo kama kawa
Haya ndio yanayotakiwa na ndio mwanzo wa Tanzania ya maisha bora kwa kila mtanzania

Siwezi kosekana nitakuwa na bendera nyeupe na magwanda ya Kimgambo! nionane na wakeleketwa wa mabadiliko Tanzania...
 
Huwezi kuandika asieshiriki maandamano hayo anaunga mkono ufisadi ni bora ikatumika lugha nyingine katika kuwashawishi watu au wananchi na nategemea maandamano mengine ni kuidai Tanganyika Huru kuwaunga mkono waliozindua harakati hizo akina Jakaya Kikwete na kundi lake la G55.
 
Maandamano kama haya ni moja ya vitu vilivyomfanya Lech Walesa kuwaangusha wakomunisti huko Poland, mshikamano kama huu wa maandamano ya amani ni moja ya mapigo yaliyomsaidia Mohandas Gandhi kuung'oa utawala wa kifalme wa Uingereza huko India, mandamano kama haya yalikuwa ni moja ya mihimili iliyosababisha vuguvugu la "Civil Rights" chini ya Mchungaji Martin Luther King Jr. kufanikiwa kwa watu weusi.

Ningependa kuona vibali vyote vinavyoweza kuhitajika vinatafutwa na kupatikana kwanza kabla ya kuvipa vyombo vya "usalama" sababu yoyote ya kuingilia matakwa ya watu.when civil measures are not acknowledged for being so, civil disobedience is warranted.

Ningependa kuwepo na organization ya huduma za afya ikia pamoja na ambulances, first aid kits, nursing assistance etc kama zitahitajika.

Ningependa kuona organisation ya maandamano inawasiliana na vikundi vinavyofahamika na kuheshimika duniani katika mambo ya haki za binadamu, vikundi kama "Human Rights Watch" na "Amnesty International" ili kuyapa maandamano exposure na effect ya kutosha hata kimataifa na kuweza kupata msaada inapobidi.Let's face it si kila mtu atafurahia maandamano haya, hususan mafisadi na team zao zilizojaa kila sehemu serikalini mpaka kwenye vyombo vya usalama vilivyo na wajibu wa kulinda haki na usalama wa wananchi.

Ni muhimu kuwajulisha waandamanaji mipaka na malengo ya maandamano.Ni muhimu kwa waandalizi wa maandamano kuhakikisha kuwa watakuwa na control ya maandamano katika muda wote wa maandamano, hata kama msaada wa vyombo vya dola itabidi utumike.Kwa maneno mengine, waandalizi inawabidi waseme wazi kuwa ukivuka mipaka hii na polisi wakikudaka tutakuwa hatuwezi kukutetea. Mara zote kuna chance ya waandamanaji fulani kuanza kuvunja vioo vya magari ya "mafisadi" etc. Rejea issue ya maandamano ya Mtikila na kuvunjwa vioo kwa magari ya "magabacholi. Kwa msingi huu pia ni muhimu kuwasiliana na Traffic police kufunga njia fulani kwa nyakati fulani kuruhusu maandamano yaendelee bila taabu.

Ni muhimu kuvihusisha vyombo vya habari vya kutosha ili kupata maximum exposure.
 
Huu ni mwanzo wa mapambazuko ya kudai na kutafuta haki kwa watanzania wote. Mungu atutangulie katika maandamano hayo ya kweli na amani.
 
Waliotafuna pesa ya EPA naona hawatalala sasa. Lakini ndio tatizo letu hilo iweje mwizi wa kuku afungwe lakini mwizi wa ng'ombe anaachiwa na kuendelea kuiba?

Mzee Mwanakijiji Kasungura alikoacha EL bado kapo?
 
Wazo zuri sana, mwanzo mzuri, tujitokeze kwa wingi kufanikisha umoja wa wapinga mafisadi na kudai mzizi wa fitna ung'olewe, ONCE AND FOR ALL.
 
Maandamano kama haya ni moja ya vitu vilivyomfanya Lech Walesa kuwaangusha wakomunisti huko Poland, mshikamano kama huu wa maandamano ya amani ni moja ya mapigo yaliyomsaidia Mohandas Gandhi kuung'oa utawala wa kifalme wa Uingereza huko India, mandamano kama haya yalikuwa ni moja ya mihimili iliyosababisha vuguvugu la "Civil Rights" chini ya Mchungaji Martin Luther King Jr. kufanikiwa kwa watu weusi.

Ningependa kuona vibali vyote vinavyoweza kuhitajika vinatafutwa na kupatikana kwanza kabla ya kuvipa vyombo vya "usalama" sababu yoyote ya kuingilia matakwa ya watu.when civil measures are not acknowledged for being so, civil disobedience is warranted.

Ningependa kuwepo na organization ya huduma za afya ikia pamoja na ambulances, first aid kits, nursing assistance etc kama zitahitajika.

Ningependa kuona organisation ya maandamano inawasiliana na vikundi vinavyofahamika na kuheshimika duniani katika mambo ya haki za binadamu, vikundi kama "Human Rights Watch" na "Amnesty International" ili kuyapa maandamano exposure na effect ya kutosha hata kimataifa na kuweza kupata msaada inapobidi.Let's face it si kila mtu atafurahia maandamano haya, hususan mafisadi na team zao zilizojaa kila sehemu serikalini mpaka kwenye vyombo vya usalama vilivyo na wajibu wa kulinda haki na usalama wa wananchi.

Ni muhimu kuwajulisha waandamanaji mipaka na malengo ya maandamano.Ni muhimu kwa waandalizi wa maandamano kuhakikisha kuwa watakuwa na control ya maandamano katika muda wote wa maandamano, hata kama msaada wa vyombo vya dola itabidi utumike.Kwa maneno mengine, waandalizi inawabidi waseme wazi kuwa ukivuka mipaka hii na polisi wakikudaka tutakuwa hatuwezi kukutetea. Mara zote kuna chance ya waandamanaji fulani kuanza kuvunja vioo vya magari ya "mafisadi" etc. Rejea issue ya maandamano ya Mtikila na kuvunjwa vioo kwa magari ya "magabacholi. Kwa msingi huu pia ni muhimu kuwasiliana na Traffic police kufunga njia fulani kwa nyakati fulani kuruhusu maandamano yaendelee bila taabu.

Ni muhimu kuvihusisha vyombo vya habari vya kutosha ili kupata maximum exposure.



Agreed 100%.
I'm glad you took time to write this Pundit. Asante sana!





.
 
Nimepiga hiyo namba ya Rafael. Maandamano yatatangazwa kwenye vyombo vya habari na kwamba kufanyika kwake itategemea Raisi atachukua hatua gani kesho kutwa (tarehe 21).




.
 
Nimepiga hiyo namba ya Rafael. Maandamano yatatangazwa kwenye vyombo vya habari na kwamba kufanyika kwake itategemea Raisi atachukua hatua gani kesho kutwa (tarehe 21).




.

Nilitakujua itakuje kama Rais atatoa msimamo kuhusu EPA, ila nashukuru maana nina nusu jibu.
 
Na huku kwetu Mara tutayaanza lini jamani? Naomba mkiyamaliza huko Dar tunaomba myaratibu huku mkoani Mara.
 
Huwezi kuandika asieshiriki maandamano hayo anaunga mkono ufisadi ni bora ikatumika lugha nyingine katika kuwashawishi watu au wananchi na nategemea maandamano mengine ni kuidai Tanganyika Huru kuwaunga mkono waliozindua harakati hizo akina Jakaya Kikwete na kundi lake la G55.


Agreed!
However, I did not fully understand the rest of your message.



.
 
isu hapa siyo maandamano kunahitajika mjadala wa kitaifa juu wa muelekeo wa govt.
 
...its time sasa maana bila vitu kama hivi hakuna chochote kitabadilika,ila kama Pundit alivyo suggest ni vizuri kuwa smart ili kuwanyima usalama na media za CCM sababu za kuharibu hii issue!
 
Back
Top Bottom