Paw
Content Manager
- Nov 14, 2010
- 2,110
- 1,360
Kwa hivyo huyo mama mdogo ndo mtuhumiwa??JESHI la Polisi Mkoani Mara jana lililazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya wananchi wa Bunda mkoani Mara ambao walikuwa wamechukua jeneza la mtu ambaye alidaiwa kufa kwenye mazingira ya kutatanisha.
Tukio hilo limetokea jana jioni mkoani humo. Wananchi wa eneo hilo, kwa nyakati tofauti, walidai kuwa baada ya kuifunua maiti hiyo iliyokuwa ndani ya jeneza walikuta ikitoa machozi, hali ambayo ilizua hofu kwa waombolezaji na kudai kuwa kuna mkono wa mtu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, maiti hiyo ilianza kutoa machozi mara baada ya mama mdogo wa marehemu huyo kufika eneo hilo na kuanza kuiangalia na ndipo ilipoanza kudondosha machozi.
Kutokana na kitendo hicho, ndugu wa marehemu hawakukubaliana nacho ndipo walipotaka hatua za kisheria zifuatwe ili wamfahamu aliyehusika na tukio hilo.
Hali hiyo ilisababisha baadhi ya waombolezaji kufanya maandamano huku wakiwa wamebeba maiti yao kwenye mkokoteni hadi kituo cha polisi kwa ajili ya hatua zaidi.
Polisi baada ya kuona umati wa watu umezingira katika kituo chao huku wakileta vurugu walilazimika kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya machozi.
Hata hivyo, haikuweza kufahamika mara moja mama mdogo huyo alitoweka katika mazingira gani.
NCHI hii bana ina mambo.............